Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 254
- 892
- Thread starter
- #81
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Kumi na Tisa
Mzee Msangi alikuwa amechanganyikiwa sana, sigara aliyokuwa anaivuta ilikuwa ni sigara ya kumi na tatu tangu Imma Ogbo amtoroshe Dr Luis kitalu B. Alikuwa anazunguka meza ya ofisi yake huku akiteketeza sigara isivyo kawaida. Kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana, lakini jambo kuu ilikuwa ni kutoroshwa kwa Dr Luis na Imma Ogbo.
Wakati akiwa katika mzunguko wake mwengine wa meza, mara simu yake iliita. Aliitoa simu yake mfukoni na kuiangalia. Alikuwa rais Mgaya..
Akaipokea.
"Hallo Mheshimiwa rais" Alisema simuni.
"Mzee Msangi mnafanya kitu gani? Mbona umekuwa mpuuzi kiasi hiki safari hii?" Rais Mgaya alisema kwa hasira.
"Kuna nini mheshimiwa rais? Msako wa Dr Luis unaendelea vizuri. Namsubiri Mark hapa tukaanze msako. Tutatampata tu hakuna tatizo. Au kuna tatizo gani tena?" Mzee Msangi aliuliza.
"Mzee Msangi mnafanyaje kazi ninyi? Kikosi cha B1 kimegundua mahali alipofichwa Dr Luis, na sasa kipo njiani wanakuja Kitalu B!" Rais Mgaya alisema.
"Wamepagundua Kitalu B? Kivipi? Hii ni nyumba ya siri na tunafanya mambo yetu kwa siri sana, ni ngumu sana kupagundua hapa jinsi palivyo. Sasa Bi wamepangunduaje?" Mzee Msangi aliuliza.
"Huu sio muda wa kuulizana maswali. Huu ni muda wa utekelezaji. Ripua kwa Bomu hiyo nyumba haraka sana!!. Nanyi mhamie kitalu C haraka iwezekenavyo. Mtafanya kazi hii kutokea kitalu C" Rais Mgaya alisema.
"Sawa mheshimiwa nimekuelewa" Mzee Msangi alisema.
Simu ikakatwa.
Msafara wa Mark the sniper ulikuwa unakaribia katika makazi yao, kitalu B kama walipozoea kupaita. Mara walianza kuona moshi mkali ukiwa juu ya anga.
"Motooo!!" Mark aliropoka.
"Kitalu B kinaungua" Mwenzie aliyekuwa pembeni alisema.
"Afanalek!!, nani kachoma moto kitalu B?" Mark aliuliza swali ambalo hakukuwa mwenye majibu.
"Tusiende pale, ni hatari!" Jamaa aliyekaa siti ya pembeni mwa dereva alisema.
"Lazima twende Elia ! Pale tuliacha wenzetu wapo katika hali gani?" Mark alisema.
"Ni hatari Mark.." Yule jamaa aliyekuwa pembeni alikatishwa na simu ya Mark. Mzee Msangi alikuwa anapiga.
"Mark tukutane kitalu C sasahivi" Mzee Msangi alisema harakaharaka na kukata simu.
"Amenipigia mzee Msangi" Mark aliwaambia wenzake.
"Kasemaje?" Wote waliuliza kwa pamoja.
"Twende kitalu C sasahivi" Mark alisema.
"Huu moto ni wa kupangwa. Its our bomb!" Elia alisema.
"Elia, unataka kuniambia kuna watu waligundua makazi yetu?" Mark aliuliza.
"Itakuwa hivyo. Mzee Msangi hawezi kuruhusu kitalu B kiteketezwe kwa Bomu. Ni nyumba ya gharama sana ile. Kuna vitu vingi sana vya thamani" Elia alisema.
"Inawezekana wamekusudia kuteketeza kitalu B. Twendeni kitalu C kama tulivyoagizwa" Mark alisema huku akigeuza gari kwa kasi. Kwakuwa waligeuza gari ghafla wakina Daniel hawakujipanga kwa hilo. Wao hawakuweza kukata kona. Walipishana na gari la wakina Daniel.
Kwakuwa Mark alishusha kioo kidogo, Adrian alimwona Mark.
Alipigwa na mshangao. Lakini Mark hakumwona Adrian kutoka na giza la kioo.
"Mark!!" Adrian aling'aka
"Vipi unamjua yule dereva?" Daniel aliuliza.
"Nilijua tu siku hii itafika, huyu ndiye aliyejifanya mwanamke aliyevaa baibui kule Rombo hoteli. Ndiye mwenye ile harufu ya uturi uliounusa katika bunduki ya mdunguaji kule juu ya ghorofa katika hoteli ya Rombo. Ndio, ulikuwa ni Uturi wa Mark" Adrian alisema.
"Ndio maana ulisema unamjua Mdunguaji tulivyokuwa kule juu katika hoteli ya Rombo? Who is the Mark?" Daniel aliuliza.
"Mark the sniper. Alikuwa mwenzetu lakini katika mafunzo huko Cuba, lakini alihasi pindi tu tulipomaliza mafunzo. Hakujulikana alienda wapi?
Baadae ikatoka taarifa kwamba Mark amefariki kwa ajiri ya gari huko nchini Nigeria. Lakini mimi haikuniingia akilini hata kidogo. Sikuamini katu. Nilihisi ni ajari ya kutengeneza.
Ulipita mwezi tu tangu taarifa ya kufariki kwa Mark ndipo rais wa nchi ya Sokonja aliuwawa kwa risasi. Kwa jinsi alivyodunguliwa niliamini hisia zangu. Ulikuwa aina ya udunguaji wa Mark the sniper. Nchi ya Sokonja walimtafuta mtu aliyemuua rais wao bila mafanikio..." Adrian alisema wakati akigeuza gari kulifata tena gari la kina Mark. Hakukata kona ghafla ili kuwapoteza maboya wakina Mark.
Gari lilivyokaa sawa Adrian aliendelea kuongea "Miezi miwili baadae rais wa Konjana naye alidunguliwa kwa risasi. Alidunguliwa kwa namna ileile aliyodunguliwa rais wa Sokonja. Si unajua rais wa Sokonja na Konjani walikuwa maadui kutokana na mzozo wao wa mipaka.
Dunia mzima hawakujua nani mdunguaji wa marais hao? Ingawa wengi waliamini nchi ya Sokonja walilipiza kisasi kutokana na kuuwawa kwa rais wao.
Umoja wa Afrika ukatuma wapelelezi wao kuchunguza undani wa vifo hivyo. Baada ya kutokea mzozo mkubwa kila nchi ikikataa wapepelezi wa mwenzake kuimgia nchini mwao.
Mimi, niliteuliwa kuungana na wapelelezi wanne. Mmoja alikuwa anatoka nchini Nigeria, mwengine nchini Zambia, kuna wa Misri na Afrika ya kusini. Lengo ni kufanya uchunguzi wa siri juu ya vifo hivyo. Tilisafiri hadi nchi ya Sokonja nikiwa na wenzangu, kisha tukaenda Konjani. Majibu tuliyoyapata kwamba ile ilikuwa kazi ya Mark.
Kamera za uwanja wa ndege wa nchi zote hizo zilinasa sura ya Mark akiwasili wiki moja kabla ya hayo matukio kutokea. Mark alitumia pasi zenye majina tofauti kuingia katika nchi hizo mbili. Tulipeleka taarifa yetu katika baraza la usalama la umoja wa Afrika. Lakini hakuna aliyetuamini, wote walitudharau na kuamini Mark alikuwa amekufa katika ajari ya gari huko Nigeria!
Nilirudi nchini baada ya kazi hiyo iliyoisha kwa kudharauriwa, lakini moyoni mwangu niliamini Mark the sniper yu hai. Na ndiye aliyewauwa hao marais...Ingawa sikujua kiini cha kuwauwa marais wale" Adrian alisema.
"Daah huyu mtu inaonesha ni hatari sana.." David alisema.
"Mark sio tu ni mtu hatari sana. Mark ni zaidi ya hilo neno hatari linavyomaanisha. Nakumbuka tukiwa mafunzoni hakuwahi kukosa kulenga shabaha. Alikuwa ni namba moja katika udunguaji. Wapo waliokuwa wanaamini Mark alikuwa anatumia uchawi ndio maana alikuwa Mdunguaji mzuri. Waliamini uturi wa Mark ni uchawi aliyopewa na mganga huko Nigeria ambao unamsaidia katika ulengaji wa shabaha. Maana Mark hawezi kufanya udunguaji bila kujipaka uturi. Na inasemekana kwamba Mark hawezi kabisa kulenga shabaha ikiwa hajapaka uturi. Ingawa hilo halijathibitishwa" Adrian alisema.
"Daah Adrian hizo habari mpya kabisa. Sijawahi kusikia mtu wa aina hii tangu niingie katika taaluma hii. Sasa Mark yupo Tanzania, ni nini hasa kitakuwa kimemleta hapa nchini?" Daniel aliuliza.
"Hakuna anayejua ni nini kilichomleta hapa nchini zaidi ya Mark mwenyewe. Lazima tumpate Mark atujibu nini kimemleta hapa? Na pia atuambia kwanini aliwauwa marais wa Sonjani na Sokonja? Na alikuwa wapi baada tu ya kumaliza mafunzo kule Cuba?" Adrian alisema.
"Atatujibu tu soon" Daniel alisema.
Kipindi hiko walikuwa katika chuo cha uhasibu. Gari la kina Mark lilikuwa limekata kushoto, likielekea upande wa Mbagala. Gari la sita nyuma lilikuwa ni gari la kina Daniel Mwaseba.
Hapo ndipo kikatokea kitu cha kushangaza sana....
Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Kumi na Tisa
Mzee Msangi alikuwa amechanganyikiwa sana, sigara aliyokuwa anaivuta ilikuwa ni sigara ya kumi na tatu tangu Imma Ogbo amtoroshe Dr Luis kitalu B. Alikuwa anazunguka meza ya ofisi yake huku akiteketeza sigara isivyo kawaida. Kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana, lakini jambo kuu ilikuwa ni kutoroshwa kwa Dr Luis na Imma Ogbo.
Wakati akiwa katika mzunguko wake mwengine wa meza, mara simu yake iliita. Aliitoa simu yake mfukoni na kuiangalia. Alikuwa rais Mgaya..
Akaipokea.
"Hallo Mheshimiwa rais" Alisema simuni.
"Mzee Msangi mnafanya kitu gani? Mbona umekuwa mpuuzi kiasi hiki safari hii?" Rais Mgaya alisema kwa hasira.
"Kuna nini mheshimiwa rais? Msako wa Dr Luis unaendelea vizuri. Namsubiri Mark hapa tukaanze msako. Tutatampata tu hakuna tatizo. Au kuna tatizo gani tena?" Mzee Msangi aliuliza.
"Mzee Msangi mnafanyaje kazi ninyi? Kikosi cha B1 kimegundua mahali alipofichwa Dr Luis, na sasa kipo njiani wanakuja Kitalu B!" Rais Mgaya alisema.
"Wamepagundua Kitalu B? Kivipi? Hii ni nyumba ya siri na tunafanya mambo yetu kwa siri sana, ni ngumu sana kupagundua hapa jinsi palivyo. Sasa Bi wamepangunduaje?" Mzee Msangi aliuliza.
"Huu sio muda wa kuulizana maswali. Huu ni muda wa utekelezaji. Ripua kwa Bomu hiyo nyumba haraka sana!!. Nanyi mhamie kitalu C haraka iwezekenavyo. Mtafanya kazi hii kutokea kitalu C" Rais Mgaya alisema.
"Sawa mheshimiwa nimekuelewa" Mzee Msangi alisema.
Simu ikakatwa.
Msafara wa Mark the sniper ulikuwa unakaribia katika makazi yao, kitalu B kama walipozoea kupaita. Mara walianza kuona moshi mkali ukiwa juu ya anga.
"Motooo!!" Mark aliropoka.
"Kitalu B kinaungua" Mwenzie aliyekuwa pembeni alisema.
"Afanalek!!, nani kachoma moto kitalu B?" Mark aliuliza swali ambalo hakukuwa mwenye majibu.
"Tusiende pale, ni hatari!" Jamaa aliyekaa siti ya pembeni mwa dereva alisema.
"Lazima twende Elia ! Pale tuliacha wenzetu wapo katika hali gani?" Mark alisema.
"Ni hatari Mark.." Yule jamaa aliyekuwa pembeni alikatishwa na simu ya Mark. Mzee Msangi alikuwa anapiga.
"Mark tukutane kitalu C sasahivi" Mzee Msangi alisema harakaharaka na kukata simu.
"Amenipigia mzee Msangi" Mark aliwaambia wenzake.
"Kasemaje?" Wote waliuliza kwa pamoja.
"Twende kitalu C sasahivi" Mark alisema.
"Huu moto ni wa kupangwa. Its our bomb!" Elia alisema.
"Elia, unataka kuniambia kuna watu waligundua makazi yetu?" Mark aliuliza.
"Itakuwa hivyo. Mzee Msangi hawezi kuruhusu kitalu B kiteketezwe kwa Bomu. Ni nyumba ya gharama sana ile. Kuna vitu vingi sana vya thamani" Elia alisema.
"Inawezekana wamekusudia kuteketeza kitalu B. Twendeni kitalu C kama tulivyoagizwa" Mark alisema huku akigeuza gari kwa kasi. Kwakuwa waligeuza gari ghafla wakina Daniel hawakujipanga kwa hilo. Wao hawakuweza kukata kona. Walipishana na gari la wakina Daniel.
Kwakuwa Mark alishusha kioo kidogo, Adrian alimwona Mark.
Alipigwa na mshangao. Lakini Mark hakumwona Adrian kutoka na giza la kioo.
"Mark!!" Adrian aling'aka
"Vipi unamjua yule dereva?" Daniel aliuliza.
"Nilijua tu siku hii itafika, huyu ndiye aliyejifanya mwanamke aliyevaa baibui kule Rombo hoteli. Ndiye mwenye ile harufu ya uturi uliounusa katika bunduki ya mdunguaji kule juu ya ghorofa katika hoteli ya Rombo. Ndio, ulikuwa ni Uturi wa Mark" Adrian alisema.
"Ndio maana ulisema unamjua Mdunguaji tulivyokuwa kule juu katika hoteli ya Rombo? Who is the Mark?" Daniel aliuliza.
"Mark the sniper. Alikuwa mwenzetu lakini katika mafunzo huko Cuba, lakini alihasi pindi tu tulipomaliza mafunzo. Hakujulikana alienda wapi?
Baadae ikatoka taarifa kwamba Mark amefariki kwa ajiri ya gari huko nchini Nigeria. Lakini mimi haikuniingia akilini hata kidogo. Sikuamini katu. Nilihisi ni ajari ya kutengeneza.
Ulipita mwezi tu tangu taarifa ya kufariki kwa Mark ndipo rais wa nchi ya Sokonja aliuwawa kwa risasi. Kwa jinsi alivyodunguliwa niliamini hisia zangu. Ulikuwa aina ya udunguaji wa Mark the sniper. Nchi ya Sokonja walimtafuta mtu aliyemuua rais wao bila mafanikio..." Adrian alisema wakati akigeuza gari kulifata tena gari la kina Mark. Hakukata kona ghafla ili kuwapoteza maboya wakina Mark.
Gari lilivyokaa sawa Adrian aliendelea kuongea "Miezi miwili baadae rais wa Konjana naye alidunguliwa kwa risasi. Alidunguliwa kwa namna ileile aliyodunguliwa rais wa Sokonja. Si unajua rais wa Sokonja na Konjani walikuwa maadui kutokana na mzozo wao wa mipaka.
Dunia mzima hawakujua nani mdunguaji wa marais hao? Ingawa wengi waliamini nchi ya Sokonja walilipiza kisasi kutokana na kuuwawa kwa rais wao.
Umoja wa Afrika ukatuma wapelelezi wao kuchunguza undani wa vifo hivyo. Baada ya kutokea mzozo mkubwa kila nchi ikikataa wapepelezi wa mwenzake kuimgia nchini mwao.
Mimi, niliteuliwa kuungana na wapelelezi wanne. Mmoja alikuwa anatoka nchini Nigeria, mwengine nchini Zambia, kuna wa Misri na Afrika ya kusini. Lengo ni kufanya uchunguzi wa siri juu ya vifo hivyo. Tilisafiri hadi nchi ya Sokonja nikiwa na wenzangu, kisha tukaenda Konjani. Majibu tuliyoyapata kwamba ile ilikuwa kazi ya Mark.
Kamera za uwanja wa ndege wa nchi zote hizo zilinasa sura ya Mark akiwasili wiki moja kabla ya hayo matukio kutokea. Mark alitumia pasi zenye majina tofauti kuingia katika nchi hizo mbili. Tulipeleka taarifa yetu katika baraza la usalama la umoja wa Afrika. Lakini hakuna aliyetuamini, wote walitudharau na kuamini Mark alikuwa amekufa katika ajari ya gari huko Nigeria!
Nilirudi nchini baada ya kazi hiyo iliyoisha kwa kudharauriwa, lakini moyoni mwangu niliamini Mark the sniper yu hai. Na ndiye aliyewauwa hao marais...Ingawa sikujua kiini cha kuwauwa marais wale" Adrian alisema.
"Daah huyu mtu inaonesha ni hatari sana.." David alisema.
"Mark sio tu ni mtu hatari sana. Mark ni zaidi ya hilo neno hatari linavyomaanisha. Nakumbuka tukiwa mafunzoni hakuwahi kukosa kulenga shabaha. Alikuwa ni namba moja katika udunguaji. Wapo waliokuwa wanaamini Mark alikuwa anatumia uchawi ndio maana alikuwa Mdunguaji mzuri. Waliamini uturi wa Mark ni uchawi aliyopewa na mganga huko Nigeria ambao unamsaidia katika ulengaji wa shabaha. Maana Mark hawezi kufanya udunguaji bila kujipaka uturi. Na inasemekana kwamba Mark hawezi kabisa kulenga shabaha ikiwa hajapaka uturi. Ingawa hilo halijathibitishwa" Adrian alisema.
"Daah Adrian hizo habari mpya kabisa. Sijawahi kusikia mtu wa aina hii tangu niingie katika taaluma hii. Sasa Mark yupo Tanzania, ni nini hasa kitakuwa kimemleta hapa nchini?" Daniel aliuliza.
"Hakuna anayejua ni nini kilichomleta hapa nchini zaidi ya Mark mwenyewe. Lazima tumpate Mark atujibu nini kimemleta hapa? Na pia atuambia kwanini aliwauwa marais wa Sonjani na Sokonja? Na alikuwa wapi baada tu ya kumaliza mafunzo kule Cuba?" Adrian alisema.
"Atatujibu tu soon" Daniel alisema.
Kipindi hiko walikuwa katika chuo cha uhasibu. Gari la kina Mark lilikuwa limekata kushoto, likielekea upande wa Mbagala. Gari la sita nyuma lilikuwa ni gari la kina Daniel Mwaseba.
Hapo ndipo kikatokea kitu cha kushangaza sana....
Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..