BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tisa

Mzee Msangi alikuwa amechanganyikiwa sana, sigara aliyokuwa anaivuta ilikuwa ni sigara ya kumi na tatu tangu Imma Ogbo amtoroshe Dr Luis kitalu B. Alikuwa anazunguka meza ya ofisi yake huku akiteketeza sigara isivyo kawaida. Kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana, lakini jambo kuu ilikuwa ni kutoroshwa kwa Dr Luis na Imma Ogbo.

Wakati akiwa katika mzunguko wake mwengine wa meza, mara simu yake iliita. Aliitoa simu yake mfukoni na kuiangalia. Alikuwa rais Mgaya..
Akaipokea.

"Hallo Mheshimiwa rais" Alisema simuni.

"Mzee Msangi mnafanya kitu gani? Mbona umekuwa mpuuzi kiasi hiki safari hii?" Rais Mgaya alisema kwa hasira.

"Kuna nini mheshimiwa rais? Msako wa Dr Luis unaendelea vizuri. Namsubiri Mark hapa tukaanze msako. Tutatampata tu hakuna tatizo. Au kuna tatizo gani tena?" Mzee Msangi aliuliza.

"Mzee Msangi mnafanyaje kazi ninyi? Kikosi cha B1 kimegundua mahali alipofichwa Dr Luis, na sasa kipo njiani wanakuja Kitalu B!" Rais Mgaya alisema.

"Wamepagundua Kitalu B? Kivipi? Hii ni nyumba ya siri na tunafanya mambo yetu kwa siri sana, ni ngumu sana kupagundua hapa jinsi palivyo. Sasa Bi wamepangunduaje?" Mzee Msangi aliuliza.

"Huu sio muda wa kuulizana maswali. Huu ni muda wa utekelezaji. Ripua kwa Bomu hiyo nyumba haraka sana!!. Nanyi mhamie kitalu C haraka iwezekenavyo. Mtafanya kazi hii kutokea kitalu C" Rais Mgaya alisema.

"Sawa mheshimiwa nimekuelewa" Mzee Msangi alisema.
Simu ikakatwa.

Msafara wa Mark the sniper ulikuwa unakaribia katika makazi yao, kitalu B kama walipozoea kupaita. Mara walianza kuona moshi mkali ukiwa juu ya anga.

"Motooo!!" Mark aliropoka.

"Kitalu B kinaungua" Mwenzie aliyekuwa pembeni alisema.

"Afanalek!!, nani kachoma moto kitalu B?" Mark aliuliza swali ambalo hakukuwa mwenye majibu.

"Tusiende pale, ni hatari!" Jamaa aliyekaa siti ya pembeni mwa dereva alisema.

"Lazima twende Elia ! Pale tuliacha wenzetu wapo katika hali gani?" Mark alisema.

"Ni hatari Mark.." Yule jamaa aliyekuwa pembeni alikatishwa na simu ya Mark. Mzee Msangi alikuwa anapiga.

"Mark tukutane kitalu C sasahivi" Mzee Msangi alisema harakaharaka na kukata simu.

"Amenipigia mzee Msangi" Mark aliwaambia wenzake.

"Kasemaje?" Wote waliuliza kwa pamoja.

"Twende kitalu C sasahivi" Mark alisema.

"Huu moto ni wa kupangwa. Its our bomb!" Elia alisema.

"Elia, unataka kuniambia kuna watu waligundua makazi yetu?" Mark aliuliza.

"Itakuwa hivyo. Mzee Msangi hawezi kuruhusu kitalu B kiteketezwe kwa Bomu. Ni nyumba ya gharama sana ile. Kuna vitu vingi sana vya thamani" Elia alisema.

"Inawezekana wamekusudia kuteketeza kitalu B. Twendeni kitalu C kama tulivyoagizwa" Mark alisema huku akigeuza gari kwa kasi. Kwakuwa waligeuza gari ghafla wakina Daniel hawakujipanga kwa hilo. Wao hawakuweza kukata kona. Walipishana na gari la wakina Daniel.

Kwakuwa Mark alishusha kioo kidogo, Adrian alimwona Mark.
Alipigwa na mshangao. Lakini Mark hakumwona Adrian kutoka na giza la kioo.

"Mark!!" Adrian aling'aka

"Vipi unamjua yule dereva?" Daniel aliuliza.

"Nilijua tu siku hii itafika, huyu ndiye aliyejifanya mwanamke aliyevaa baibui kule Rombo hoteli. Ndiye mwenye ile harufu ya uturi uliounusa katika bunduki ya mdunguaji kule juu ya ghorofa katika hoteli ya Rombo. Ndio, ulikuwa ni Uturi wa Mark" Adrian alisema.

"Ndio maana ulisema unamjua Mdunguaji tulivyokuwa kule juu katika hoteli ya Rombo? Who is the Mark?" Daniel aliuliza.

"Mark the sniper. Alikuwa mwenzetu lakini katika mafunzo huko Cuba, lakini alihasi pindi tu tulipomaliza mafunzo. Hakujulikana alienda wapi?

Baadae ikatoka taarifa kwamba Mark amefariki kwa ajiri ya gari huko nchini Nigeria. Lakini mimi haikuniingia akilini hata kidogo. Sikuamini katu. Nilihisi ni ajari ya kutengeneza.

Ulipita mwezi tu tangu taarifa ya kufariki kwa Mark ndipo rais wa nchi ya Sokonja aliuwawa kwa risasi. Kwa jinsi alivyodunguliwa niliamini hisia zangu. Ulikuwa aina ya udunguaji wa Mark the sniper. Nchi ya Sokonja walimtafuta mtu aliyemuua rais wao bila mafanikio..." Adrian alisema wakati akigeuza gari kulifata tena gari la kina Mark. Hakukata kona ghafla ili kuwapoteza maboya wakina Mark.

Gari lilivyokaa sawa Adrian aliendelea kuongea "Miezi miwili baadae rais wa Konjana naye alidunguliwa kwa risasi. Alidunguliwa kwa namna ileile aliyodunguliwa rais wa Sokonja. Si unajua rais wa Sokonja na Konjani walikuwa maadui kutokana na mzozo wao wa mipaka.
Dunia mzima hawakujua nani mdunguaji wa marais hao? Ingawa wengi waliamini nchi ya Sokonja walilipiza kisasi kutokana na kuuwawa kwa rais wao.

Umoja wa Afrika ukatuma wapelelezi wao kuchunguza undani wa vifo hivyo. Baada ya kutokea mzozo mkubwa kila nchi ikikataa wapepelezi wa mwenzake kuimgia nchini mwao.

Mimi, niliteuliwa kuungana na wapelelezi wanne. Mmoja alikuwa anatoka nchini Nigeria, mwengine nchini Zambia, kuna wa Misri na Afrika ya kusini. Lengo ni kufanya uchunguzi wa siri juu ya vifo hivyo. Tilisafiri hadi nchi ya Sokonja nikiwa na wenzangu, kisha tukaenda Konjani. Majibu tuliyoyapata kwamba ile ilikuwa kazi ya Mark.

Kamera za uwanja wa ndege wa nchi zote hizo zilinasa sura ya Mark akiwasili wiki moja kabla ya hayo matukio kutokea. Mark alitumia pasi zenye majina tofauti kuingia katika nchi hizo mbili. Tulipeleka taarifa yetu katika baraza la usalama la umoja wa Afrika. Lakini hakuna aliyetuamini, wote walitudharau na kuamini Mark alikuwa amekufa katika ajari ya gari huko Nigeria!
Nilirudi nchini baada ya kazi hiyo iliyoisha kwa kudharauriwa, lakini moyoni mwangu niliamini Mark the sniper yu hai. Na ndiye aliyewauwa hao marais...Ingawa sikujua kiini cha kuwauwa marais wale" Adrian alisema.

"Daah huyu mtu inaonesha ni hatari sana.." David alisema.

"Mark sio tu ni mtu hatari sana. Mark ni zaidi ya hilo neno hatari linavyomaanisha. Nakumbuka tukiwa mafunzoni hakuwahi kukosa kulenga shabaha. Alikuwa ni namba moja katika udunguaji. Wapo waliokuwa wanaamini Mark alikuwa anatumia uchawi ndio maana alikuwa Mdunguaji mzuri. Waliamini uturi wa Mark ni uchawi aliyopewa na mganga huko Nigeria ambao unamsaidia katika ulengaji wa shabaha. Maana Mark hawezi kufanya udunguaji bila kujipaka uturi. Na inasemekana kwamba Mark hawezi kabisa kulenga shabaha ikiwa hajapaka uturi. Ingawa hilo halijathibitishwa" Adrian alisema.

"Daah Adrian hizo habari mpya kabisa. Sijawahi kusikia mtu wa aina hii tangu niingie katika taaluma hii. Sasa Mark yupo Tanzania, ni nini hasa kitakuwa kimemleta hapa nchini?" Daniel aliuliza.

"Hakuna anayejua ni nini kilichomleta hapa nchini zaidi ya Mark mwenyewe. Lazima tumpate Mark atujibu nini kimemleta hapa? Na pia atuambia kwanini aliwauwa marais wa Sonjani na Sokonja? Na alikuwa wapi baada tu ya kumaliza mafunzo kule Cuba?" Adrian alisema.

"Atatujibu tu soon" Daniel alisema.

Kipindi hiko walikuwa katika chuo cha uhasibu. Gari la kina Mark lilikuwa limekata kushoto, likielekea upande wa Mbagala. Gari la sita nyuma lilikuwa ni gari la kina Daniel Mwaseba.

Hapo ndipo kikatokea kitu cha kushangaza sana....

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tisa

Mzee Msangi alikuwa amechanganyikiwa sana, sigara aliyokuwa anaivuta ilikuwa ni sigara ya kumi na tatu tangu Imma Ogbo amtoroshe Dr Luis kitalu B. Alikuwa anazunguka meza ya ofisi yake huku akiteketeza sigara isivyo kawaida. Kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana, lakini jambo kuu ilikuwa ni kutoroshwa kwa Dr Luis na Imma Ogbo.

Wakati akiwa katika mzunguko wake mwengine wa meza, mara simu yake iliita. Aliitoa simu yake mfukoni na kuiangalia. Alikuwa rais Mgaya..
Akaipokea.

"Hallo Mheshimiwa rais" Alisema simuni.

"Mzee Msangi mnafanya kitu gani? Mbona umekuwa mpuuzi kiasi hiki safari hii?" Rais Mgaya alisema kwa hasira.

"Kuna nini mheshimiwa rais? Msako wa Dr Luis unaendelea vizuri. Namsubiri Mark hapa tukaanze msako. Tutatampata tu hakuna tatizo. Au kuna tatizo gani tena?" Mzee Msangi aliuliza.

"Mzee Msangi mnafanyaje kazi ninyi? Kikosi cha B1 kimegundua mahali alipofichwa Dr Luis, na sasa kipo njiani wanakuja Kitalu B!" Rais Mgaya alisema.

"Wamepagundua Kitalu B? Kivipi? Hii ni nyumba ya siri na tunafanya mambo yetu kwa siri sana, ni ngumu sana kupagundua hapa jinsi palivyo. Sasa Bi wamepangunduaje?" Mzee Msangi aliuliza.

"Huu sio muda wa kuulizana maswali. Huu ni muda wa utekelezaji. Ripua kwa Bomu hiyo nyumba haraka sana!!. Nanyi mhamie kitalu C haraka iwezekenavyo. Mtafanya kazi hii kutokea kitalu C" Rais Mgaya alisema.

"Sawa mheshimiwa nimekuelewa" Mzee Msangi alisema.
Simu ikakatwa.

Msafara wa Mark the sniper ulikuwa unakaribia katika makazi yao, kitalu B kama walipozoea kupaita. Mara walianza kuona moshi mkali ukiwa juu ya anga.

"Motooo!!" Mark aliropoka.

"Kitalu B kinaungua" Mwenzie aliyekuwa pembeni alisema.

"Afanalek!!, nani kachoma moto kitalu B?" Mark aliuliza swali ambalo hakukuwa mwenye majibu.

"Tusiende pale, ni hatari!" Jamaa aliyekaa siti ya pembeni mwa dereva alisema.

"Lazima twende Elia ! Pale tuliacha wenzetu wapo katika hali gani?" Mark alisema.

"Ni hatari Mark.." Yule jamaa aliyekuwa pembeni alikatishwa na simu ya Mark. Mzee Msangi alikuwa anapiga.

"Mark tukutane kitalu C sasahivi" Mzee Msangi alisema harakaharaka na kukata simu.

"Amenipigia mzee Msangi" Mark aliwaambia wenzake.

"Kasemaje?" Wote waliuliza kwa pamoja.

"Twende kitalu C sasahivi" Mark alisema.

"Huu moto ni wa kupangwa. Its our bomb!" Elia alisema.

"Elia, unataka kuniambia kuna watu waligundua makazi yetu?" Mark aliuliza.

"Itakuwa hivyo. Mzee Msangi hawezi kuruhusu kitalu B kiteketezwe kwa Bomu. Ni nyumba ya gharama sana ile. Kuna vitu vingi sana vya thamani" Elia alisema.

"Inawezekana wamekusudia kuteketeza kitalu B. Twendeni kitalu C kama tulivyoagizwa" Mark alisema huku akigeuza gari kwa kasi. Kwakuwa waligeuza gari ghafla wakina Daniel hawakujipanga kwa hilo. Wao hawakuweza kukata kona. Walipishana na gari la wakina Daniel.

Kwakuwa Mark alishusha kioo kidogo, Adrian alimwona Mark.
Alipigwa na mshangao. Lakini Mark hakumwona Adrian kutoka na giza la kioo.

"Mark!!" Adrian aling'aka

"Vipi unamjua yule dereva?" Daniel aliuliza.

"Nilijua tu siku hii itafika, huyu ndiye aliyejifanya mwanamke aliyevaa baibui kule Rombo hoteli. Ndiye mwenye ile harufu ya uturi uliounusa katika bunduki ya mdunguaji kule juu ya ghorofa katika hoteli ya Rombo. Ndio, ulikuwa ni Uturi wa Mark" Adrian alisema.

"Ndio maana ulisema unamjua Mdunguaji tulivyokuwa kule juu katika hoteli ya Rombo? Who is the Mark?" Daniel aliuliza.

"Mark the sniper. Alikuwa mwenzetu lakini katika mafunzo huko Cuba, lakini alihasi pindi tu tulipomaliza mafunzo. Hakujulikana alienda wapi?

Baadae ikatoka taarifa kwamba Mark amefariki kwa ajiri ya gari huko nchini Nigeria. Lakini mimi haikuniingia akilini hata kidogo. Sikuamini katu. Nilihisi ni ajari ya kutengeneza.

Ulipita mwezi tu tangu taarifa ya kufariki kwa Mark ndipo rais wa nchi ya Sokonja aliuwawa kwa risasi. Kwa jinsi alivyodunguliwa niliamini hisia zangu. Ulikuwa aina ya udunguaji wa Mark the sniper. Nchi ya Sokonja walimtafuta mtu aliyemuua rais wao bila mafanikio..." Adrian alisema wakati akigeuza gari kulifata tena gari la kina Mark. Hakukata kona ghafla ili kuwapoteza maboya wakina Mark.

Gari lilivyokaa sawa Adrian aliendelea kuongea "Miezi miwili baadae rais wa Konjana naye alidunguliwa kwa risasi. Alidunguliwa kwa namna ileile aliyodunguliwa rais wa Sokonja. Si unajua rais wa Sokonja na Konjani walikuwa maadui kutokana na mzozo wao wa mipaka.
Dunia mzima hawakujua nani mdunguaji wa marais hao? Ingawa wengi waliamini nchi ya Sokonja walilipiza kisasi kutokana na kuuwawa kwa rais wao.

Umoja wa Afrika ukatuma wapelelezi wao kuchunguza undani wa vifo hivyo. Baada ya kutokea mzozo mkubwa kila nchi ikikataa wapepelezi wa mwenzake kuimgia nchini mwao.

Mimi, niliteuliwa kuungana na wapelelezi wanne. Mmoja alikuwa anatoka nchini Nigeria, mwengine nchini Zambia, kuna wa Misri na Afrika ya kusini. Lengo ni kufanya uchunguzi wa siri juu ya vifo hivyo. Tilisafiri hadi nchi ya Sokonja nikiwa na wenzangu, kisha tukaenda Konjani. Majibu tuliyoyapata kwamba ile ilikuwa kazi ya Mark.

Kamera za uwanja wa ndege wa nchi zote hizo zilinasa sura ya Mark akiwasili wiki moja kabla ya hayo matukio kutokea. Mark alitumia pasi zenye majina tofauti kuingia katika nchi hizo mbili. Tulipeleka taarifa yetu katika baraza la usalama la umoja wa Afrika. Lakini hakuna aliyetuamini, wote walitudharau na kuamini Mark alikuwa amekufa katika ajari ya gari huko Nigeria!
Nilirudi nchini baada ya kazi hiyo iliyoisha kwa kudharauriwa, lakini moyoni mwangu niliamini Mark the sniper yu hai. Na ndiye aliyewauwa hao marais...Ingawa sikujua kiini cha kuwauwa marais wale" Adrian alisema.

"Daah huyu mtu inaonesha ni hatari sana.." David alisema.

"Mark sio tu ni mtu hatari sana. Mark ni zaidi ya hilo neno hatari linavyomaanisha. Nakumbuka tukiwa mafunzoni hakuwahi kukosa kulenga shabaha. Alikuwa ni namba moja katika udunguaji. Wapo waliokuwa wanaamini Mark alikuwa anatumia uchawi ndio maana alikuwa Mdunguaji mzuri. Waliamini uturi wa Mark ni uchawi aliyopewa na mganga huko Nigeria ambao unamsaidia katika ulengaji wa shabaha. Maana Mark hawezi kufanya udunguaji bila kujipaka uturi. Na inasemekana kwamba Mark hawezi kabisa kulenga shabaha ikiwa hajapaka uturi. Ingawa hilo halijathibitishwa" Adrian alisema.

"Daah Adrian hizo habari mpya kabisa. Sijawahi kusikia mtu wa aina hii tangu niingie katika taaluma hii. Sasa Mark yupo Tanzania, ni nini hasa kitakuwa kimemleta hapa nchini?" Daniel aliuliza.

"Hakuna anayejua ni nini kilichomleta hapa nchini zaidi ya Mark mwenyewe. Lazima tumpate Mark atujibu nini kimemleta hapa? Na pia atuambia kwanini aliwauwa marais wa Sonjani na Sokonja? Na alikuwa wapi baada tu ya kumaliza mafunzo kule Cuba?" Adrian alisema.

"Atatujibu tu soon" Daniel alisema.

Kipindi hiko walikuwa katika chuo cha uhasibu. Gari la kina Mark lilikuwa limekata kushoto, likielekea upande wa Mbagala. Gari la sita nyuma lilikuwa ni gari la kina Daniel Mwaseba.

Hapo ndipo kikatokea kitu cha kushangaza sana....

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..
Asanteee man
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tisa

Mzee Msangi alikuwa amechanganyikiwa sana, sigara aliyokuwa anaivuta ilikuwa ni sigara ya kumi na tatu tangu Imma Ogbo amtoroshe Dr Luis kitalu B. Alikuwa anazunguka meza ya ofisi yake huku akiteketeza sigara isivyo kawaida. Kichwa chake kilikuwa na mambo mengi sana, lakini jambo kuu ilikuwa ni kutoroshwa kwa Dr Luis na Imma Ogbo.

Wakati akiwa katika mzunguko wake mwengine wa meza, mara simu yake iliita. Aliitoa simu yake mfukoni na kuiangalia. Alikuwa rais Mgaya..
Akaipokea.

"Hallo Mheshimiwa rais" Alisema simuni.

"Mzee Msangi mnafanya kitu gani? Mbona umekuwa mpuuzi kiasi hiki safari hii?" Rais Mgaya alisema kwa hasira.

"Kuna nini mheshimiwa rais? Msako wa Dr Luis unaendelea vizuri. Namsubiri Mark hapa tukaanze msako. Tutatampata tu hakuna tatizo. Au kuna tatizo gani tena?" Mzee Msangi aliuliza.

"Mzee Msangi mnafanyaje kazi ninyi? Kikosi cha B1 kimegundua mahali alipofichwa Dr Luis, na sasa kipo njiani wanakuja Kitalu B!" Rais Mgaya alisema.

"Wamepagundua Kitalu B? Kivipi? Hii ni nyumba ya siri na tunafanya mambo yetu kwa siri sana, ni ngumu sana kupagundua hapa jinsi palivyo. Sasa Bi wamepangunduaje?" Mzee Msangi aliuliza.

"Huu sio muda wa kuulizana maswali. Huu ni muda wa utekelezaji. Ripua kwa Bomu hiyo nyumba haraka sana!!. Nanyi mhamie kitalu C haraka iwezekenavyo. Mtafanya kazi hii kutokea kitalu C" Rais Mgaya alisema.

"Sawa mheshimiwa nimekuelewa" Mzee Msangi alisema.
Simu ikakatwa.

Msafara wa Mark the sniper ulikuwa unakaribia katika makazi yao, kitalu B kama walipozoea kupaita. Mara walianza kuona moshi mkali ukiwa juu ya anga.

"Motooo!!" Mark aliropoka.

"Kitalu B kinaungua" Mwenzie aliyekuwa pembeni alisema.

"Afanalek!!, nani kachoma moto kitalu B?" Mark aliuliza swali ambalo hakukuwa mwenye majibu.

"Tusiende pale, ni hatari!" Jamaa aliyekaa siti ya pembeni mwa dereva alisema.

"Lazima twende Elia ! Pale tuliacha wenzetu wapo katika hali gani?" Mark alisema.

"Ni hatari Mark.." Yule jamaa aliyekuwa pembeni alikatishwa na simu ya Mark. Mzee Msangi alikuwa anapiga.

"Mark tukutane kitalu C sasahivi" Mzee Msangi alisema harakaharaka na kukata simu.

"Amenipigia mzee Msangi" Mark aliwaambia wenzake.

"Kasemaje?" Wote waliuliza kwa pamoja.

"Twende kitalu C sasahivi" Mark alisema.

"Huu moto ni wa kupangwa. Its our bomb!" Elia alisema.

"Elia, unataka kuniambia kuna watu waligundua makazi yetu?" Mark aliuliza.

"Itakuwa hivyo. Mzee Msangi hawezi kuruhusu kitalu B kiteketezwe kwa Bomu. Ni nyumba ya gharama sana ile. Kuna vitu vingi sana vya thamani" Elia alisema.

"Inawezekana wamekusudia kuteketeza kitalu B. Twendeni kitalu C kama tulivyoagizwa" Mark alisema huku akigeuza gari kwa kasi. Kwakuwa waligeuza gari ghafla wakina Daniel hawakujipanga kwa hilo. Wao hawakuweza kukata kona. Walipishana na gari la wakina Daniel.

Kwakuwa Mark alishusha kioo kidogo, Adrian alimwona Mark.
Alipigwa na mshangao. Lakini Mark hakumwona Adrian kutoka na giza la kioo.

"Mark!!" Adrian aling'aka

"Vipi unamjua yule dereva?" Daniel aliuliza.

"Nilijua tu siku hii itafika, huyu ndiye aliyejifanya mwanamke aliyevaa baibui kule Rombo hoteli. Ndiye mwenye ile harufu ya uturi uliounusa katika bunduki ya mdunguaji kule juu ya ghorofa katika hoteli ya Rombo. Ndio, ulikuwa ni Uturi wa Mark" Adrian alisema.

"Ndio maana ulisema unamjua Mdunguaji tulivyokuwa kule juu katika hoteli ya Rombo? Who is the Mark?" Daniel aliuliza.

"Mark the sniper. Alikuwa mwenzetu lakini katika mafunzo huko Cuba, lakini alihasi pindi tu tulipomaliza mafunzo. Hakujulikana alienda wapi?

Baadae ikatoka taarifa kwamba Mark amefariki kwa ajiri ya gari huko nchini Nigeria. Lakini mimi haikuniingia akilini hata kidogo. Sikuamini katu. Nilihisi ni ajari ya kutengeneza.

Ulipita mwezi tu tangu taarifa ya kufariki kwa Mark ndipo rais wa nchi ya Sokonja aliuwawa kwa risasi. Kwa jinsi alivyodunguliwa niliamini hisia zangu. Ulikuwa aina ya udunguaji wa Mark the sniper. Nchi ya Sokonja walimtafuta mtu aliyemuua rais wao bila mafanikio..." Adrian alisema wakati akigeuza gari kulifata tena gari la kina Mark. Hakukata kona ghafla ili kuwapoteza maboya wakina Mark.

Gari lilivyokaa sawa Adrian aliendelea kuongea "Miezi miwili baadae rais wa Konjana naye alidunguliwa kwa risasi. Alidunguliwa kwa namna ileile aliyodunguliwa rais wa Sokonja. Si unajua rais wa Sokonja na Konjani walikuwa maadui kutokana na mzozo wao wa mipaka.
Dunia mzima hawakujua nani mdunguaji wa marais hao? Ingawa wengi waliamini nchi ya Sokonja walilipiza kisasi kutokana na kuuwawa kwa rais wao.

Umoja wa Afrika ukatuma wapelelezi wao kuchunguza undani wa vifo hivyo. Baada ya kutokea mzozo mkubwa kila nchi ikikataa wapepelezi wa mwenzake kuimgia nchini mwao.

Mimi, niliteuliwa kuungana na wapelelezi wanne. Mmoja alikuwa anatoka nchini Nigeria, mwengine nchini Zambia, kuna wa Misri na Afrika ya kusini. Lengo ni kufanya uchunguzi wa siri juu ya vifo hivyo. Tilisafiri hadi nchi ya Sokonja nikiwa na wenzangu, kisha tukaenda Konjani. Majibu tuliyoyapata kwamba ile ilikuwa kazi ya Mark.

Kamera za uwanja wa ndege wa nchi zote hizo zilinasa sura ya Mark akiwasili wiki moja kabla ya hayo matukio kutokea. Mark alitumia pasi zenye majina tofauti kuingia katika nchi hizo mbili. Tulipeleka taarifa yetu katika baraza la usalama la umoja wa Afrika. Lakini hakuna aliyetuamini, wote walitudharau na kuamini Mark alikuwa amekufa katika ajari ya gari huko Nigeria!
Nilirudi nchini baada ya kazi hiyo iliyoisha kwa kudharauriwa, lakini moyoni mwangu niliamini Mark the sniper yu hai. Na ndiye aliyewauwa hao marais...Ingawa sikujua kiini cha kuwauwa marais wale" Adrian alisema.

"Daah huyu mtu inaonesha ni hatari sana.." David alisema.

"Mark sio tu ni mtu hatari sana. Mark ni zaidi ya hilo neno hatari linavyomaanisha. Nakumbuka tukiwa mafunzoni hakuwahi kukosa kulenga shabaha. Alikuwa ni namba moja katika udunguaji. Wapo waliokuwa wanaamini Mark alikuwa anatumia uchawi ndio maana alikuwa Mdunguaji mzuri. Waliamini uturi wa Mark ni uchawi aliyopewa na mganga huko Nigeria ambao unamsaidia katika ulengaji wa shabaha. Maana Mark hawezi kufanya udunguaji bila kujipaka uturi. Na inasemekana kwamba Mark hawezi kabisa kulenga shabaha ikiwa hajapaka uturi. Ingawa hilo halijathibitishwa" Adrian alisema.

"Daah Adrian hizo habari mpya kabisa. Sijawahi kusikia mtu wa aina hii tangu niingie katika taaluma hii. Sasa Mark yupo Tanzania, ni nini hasa kitakuwa kimemleta hapa nchini?" Daniel aliuliza.

"Hakuna anayejua ni nini kilichomleta hapa nchini zaidi ya Mark mwenyewe. Lazima tumpate Mark atujibu nini kimemleta hapa? Na pia atuambia kwanini aliwauwa marais wa Sonjani na Sokonja? Na alikuwa wapi baada tu ya kumaliza mafunzo kule Cuba?" Adrian alisema.

"Atatujibu tu soon" Daniel alisema.

Kipindi hiko walikuwa katika chuo cha uhasibu. Gari la kina Mark lilikuwa limekata kushoto, likielekea upande wa Mbagala. Gari la sita nyuma lilikuwa ni gari la kina Daniel Mwaseba.

Hapo ndipo kikatokea kitu cha kushangaza sana....

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..
Six man Tuma vitu
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Ishirini.


Walipokuwa hatua chache usawa wa chuo cha Uhasibu, simu ya Adrian iliita. Adrian akaitoa mfukoni simu yake, huku mokono mwengine ukibaki kaushikia usukani. Simu ambayo iliwafumbua baadadhi ya vitu wakina Daniel Mwaseba.

"Mwanasheria mlevi anapiga" Adrian alisema huku akimpa simu Daniel.

Daniel akaipokea simu kutoka kwa Adrian , kisha akaipokea.

"Daniel" Sauti ya Mwanasheria mlevi ilisikika simuni.

"Nambie Mwanasheria?" Daniel alisema.

"Hii namba uliyonipa niichunguze umeitoa wapi?" Mwanasheria mlevi aliuliza.

"Kuna kimeo tunakifatilia. Sasa katika harakati za uchunguzi tukakutana na hiyo namba" Daniel alisema.

"Kaka hii namba ya ajabu sana. Sidhani kama kuna mtu angeweza kugundua mawasiliano ya namba hii zaidi ya sisi, usalama wa taifa. Namba imefichwa katika code ngumu sana. Ni namba ya mtandao wa simu wa Telecom lakini mawasiliano yake hayapo katika database za Telecom " Mwanasheria mlevi alisema.

"Daah mambo ya kushangaza sana. Lakini umefanikiwa?" Daniel aliuliza kwa wahka mkubwa.

"Swali gani hilo Daniel? Sasa kwani imewahi kushindikana kitu kwangu. Program waliyoitumia ni ya kitoto sana ukilinganisha na programs zetu. Mwanaume nimegundua kila kitu" Mwanasheria mlevi alisema kwa majigambo.

"Eeh nambie hiyo namba inamilikiwa na nani?" Daniel aliuliza kwa shauku.

"Namba imesajiliwa kwa jina la Elia Kilasi" Mwanasheria mlevi alisema.

"Elia Kilasi?" Daniel alirudia jina huku akiwatazama kwa zamu Adrian na David, wote walikataa kwa kichwa kuwa hawamfahamu mtu mwenye jina hilo.

"Elia Kilasi, Tutamtafuta mtu mwenye jina hilo. Eeh hiyo namba inawasiliana zaidi na namba gani?" Daniel aliuliza.

"Hapo ndipo penye utata mkubwa sana Daniel" Mwanasheria mlevi alisema.

"Utata gani?"

"Hii namba imewasiliana na namba tano tu tangu isajiliwe" Mwanasheria mlevi alisema.

"Ni namba zipi hizo?" Daniel aliuliza.

"Namba nne zipo katika uficho. Inahitajika program ya juu zaidi ili kuzigundua. Nimezituma namba hizo kwa rafiki yangu, yupo katika kitengo cha ujasusi cha CIA Marekani. Muda mfupi ujao tutakuwa na majibu ya namba hizo nne ni za kina nani?. Lakini namba moja ambayo nimeigundua ni ya Mohammed Msangi" Mwanasheria mlevi alisema.

"Mohammed Msangi!!" Daniel aling'aka kwa nguvu.

"Ndiyo, Mohammed Msangi. Aliyekuwa mkuu wa usalama wa Taifa" Mwanasheria mlevi alisema.

"Nimestushwa sana na kitu ulichokigundua mwanasheria mlevi. Mzee Msangi ni mmoja wa viongozi makini sana kuwahi kutokea katika idara ya usalama wa taifa. Alistaafu bila makandokando yoyote yale. Na hiyo ilimfanya awe rafiki sana na rais aliyepita na hata huyu wa sasa. Namba yake kukutwa katika orodha ya Elia Kilasi ambaye ndiye alikuwa anampa amri David ni jambo la kushangaza sana" Daniel alisema.

"Hivi unajua hujanambia unachunguza nini Daniel? Na huyo David ni nani?" Mwanasheria mlevi aliuliza.

"Haya mambo si ya kuongea kwenye simu. Yatupasa tukutane ana kwa ana. Nahitaji pia mchango wako katika uchunguzi wangu, pia naihitaji sana idara yako katika kazi hii ambayo wewe ni mkuu" Daniel alisema.

"Nihesabu nipo ndani ya misheni yako. Dakika yoyote ukinihitaji au kutaka msaada wangu wowote nipo tayari.."

"Nitakucheck Mwanasheria, simu yangu inaita" Daniel alisema.

Mwanasheria mlevi alikata simu, Daniel akapokea simu iliyokuwa inapigwa. Alikuwa ni Martin Hisia.

"Daniel mbona umeniweka tu hapa Mlimani city?" Martin aliuliza pindi tu simu yake ilipopokelewa.

"Mambo mengi Martin. Kuna jamaa walituteka wakati nakuja kwako. Nilipofanikiwa kuwatoka ikatokea dharura ya haraka, nikasahau kabisa kuhusu miadi yetu" Daniel alisema.

"Pole sana Daniel"

"Ndio kazi zetu. Kutekwa ni njia ya kuwafahamu wahalifu. Mara nyingi ukitekwa wanakupeleka katika makazi yao, hivyo ukifanikiwa kutoka unakuwa umepiga hatua kubwa sana" Daniel alisema.

"Ni kweli Daniel. Upo wapi kwasasa ?" Martin aliuliza.

"Nipo mitaa ya Aziz Ally kwa sasa, kuna kimeo nakifukuzia hapa" Daniel alisema.

"Nipo njiani nakuja pande hizo. Siwezi kukaa tu hapa wakati mwenzangu upo kazini" Martin alisema.

"Njoo haina shida. Tutawasiliana maana mwelekeo wangu ni uelekeo wa hawa jamaa" Daniel alisema.

"Sawa Daniel" Martin aliitikia.

Dakika hiyohiyo Martin Hisia alikodi teksi na kuelekea uelekeo wa Mbagala, kuwafuata wakina Daniel Mwaseba.

***

Imma Ogbo alikuwa katika nyumba ya kulala wageni huko pembeni kidogo ya kijiji cha Vikindu. Alikuwa amekaa huku akimwangalia Dr Luis aliyekuwa amelala kitandani. Haikuwa rahisi kutoka na Dr Luis Kigamboni hadi Vikindu. Imma ilimpasa atumie mbinu za kijasusi hasa, hadi ikafikia hatua ya kumtoa fahamu Dr Luis ili ijulikane kwamba alikuwa anampeleka mgonjwa hospitalini.

Baada ya vikwazo vingi njiani ndipo alipofanikiwa kufika katika nyumba ya kulala wageni ya Platnumz. Nyumba ya kulala wageni iliyopo nje kidogo ya kijiji cha Vikindu.

Utulivu wa nyumba hiyo ya kulala wageni, na umbali wake kutoka kijiji cha Vikindu ndicho kilichomfanya Imma Ogbo aamini kwamba pale palikuwa ni sehemu sahihi.

"Nimefanikisha hii misheni kwa awamu ya kwanza. Awamu ya kumtorosha Dr Luis mikononi mwa wale jamaa. Sasa yanipasa kwenda awamu ya pili na ngumu zaidi. Kumtoa Dr Luis Tanzania!!
Lazima niwasiliane na rais Abayo tuone jinsi ya kumsafirisha Dr Luis hadi Nigeria. Najua itakuwa kazi ngumu sana, lakini kwa msaada wa rais Abayo lazima tumpeleke huyu mtu nchini Nigeria. Hatuwezi kuruhusu Dr Luis akauwawa hivihivi, ametusaidia sana katika misheni ngumu na za siri katika nchi mbalimbali Duniani.." Wakati Imma Ogbo anawaza simu yake ikaita.

Alikuwa Felisia.

"Umefika wapi Felisia?" Imma Ogbo aliuliza alipopokea simu.

"Nipo Mwandege hapa" Felisia alisema baada ya kumuuliza dereva teksi.

"Mwambie akushushe hapohapo" Imma alisema.

"Sawa Imma" Felisia alisema

Baada ya Felisia kumlipa yule dereva teksi, alishuka. Akiiruhusu ile teksi irejee ilipotoka. Baada ya kama dakika tano Imma Ogbo alipiga simu.

"Felisia, tafuta dereva teksi hapo mwambie akupeleke Kongowe" Imma Ogbo alisema. "Wakati ukienda Kongowe kuwa makini, hakikisha hakuna mtu yeyote anayekufatilia"

"Usiwaze Imma" Felisia alisema na kukata simu.

Felisia alifanya kama alivyoambiwa. Alikodi teksi hadi Kongowe. Alipofika Kongowe alimpigia tena simu Imma. Imma akamwambia akodi bodaboda amreheshe Mwandege tena, kisha ashuke, apande daladala hadi Vikindu. Wakati huo Imma Ogbo alitoka katika ile nyumba ya kulala wageni, alikuwa Vikindu stendi kwenye duka kubwa la dawa. Alikuwa anaangalia usalama wa pale stendi. Aliridhishwa nao. Felisia alipowasili pale stendi, alimpokea na kuelekea mahali ilipo nyumba ya kulala wageni ya Platnumz.
Bado walimkuta Dr Luis amelala kitandani, hajarejewa na fahamu.

"Imma umenizungusha sana. Kumbe mahali penyewe ni hapa" Felisia alisema.

"Ilikuwa ni lazima nifanye vile, kama itatokea mtu wa kufuata nyayo zako iwe ngumu kukufikia" Imma Ogbo alisema.

"Upo sahihi Imma. Eeh nambie kilitokea nini kule kitalu B hadi ikafikia hatua ya kutoelewana na kina Mzee Msangi na kumtorosha Dr Luis?" Felisia aliuliza.

"Felisia wewe ni rafiki yangu wa siku nyingi sana. Tumefanya misheni nyingi sana na wewe na kufanikiwa kwa kiwango cha juu. Sitaki kukudanganya chochote kwa kuwa ninakuhitaji sana katika misheni hii" Imma Ogbo alisema wakati Felisia alikuwa anamsikiliza kwa umakini mkubwa.

"Felisia, mimi nimetumwa na rais Abayo kwenye misheni hii"

"Umetumwa na rais Abayo?" Felisia alishangaa.

"Ndio, nimetumwa na rais Abayo kuja kumtoa mikononi mwa wale jamaa Dr Luis na kumrejesha nchini Nigeria" Imma alisema.

"Rais Abayo anamtaka wa nini Dr Luis?" Felisia aliuliza.

"Kuna vitu vingi bado haujavifahamu kuhusu Dr Luis. Kwanza inatakiwa ujue Dr Luis ni Jasusi mkubwa sana wa Nigeria!!!" Imma alisema.

"Unajua sikuelewi Imma. Hebu niweke wazi nikuelewe. Hapa unanichanganya tu"

"Kama nilivyokwambia Felisia. Dr Luis ni jasusi wa Nigeria. Alikuja hapa nchini kwa kazi maalum. Dr Luis amefanya kazi kubwa sana na kufanikiwa, hata mikataba waliosaini juzi kati ya rais Abayo na rais Mgaya ni kazi ya Dr Luis. Ndani ya mikataba ile kuna siri kubwa sana ambayo wananchi hawajui. Rais Mgaya hajasaini mikataba ile kwa kupenda, kuna shinikizo nyuma yake, na shinikizo hilo limeletwa na huyu kiumbe aliyepoteza fahamu hapa" Imma alisema.

"Imma umenieleza mambo makubwa sana, ingawa hujataka kunifafanulia. Nilikuwa sijui kitu kuhusu Dr Luis, wala kuijua kwa undani misheni hii. Lakini kwanini umenieleza mimi yote hayo?" Felisia aliuliza.

"Kwa sababu nataka unisaidie"

"Nikusaidie nini Imma?"

"Kama ujuavyo, kuna ulinzi mkali sana katika viwanja vyote vya ndege na mipakani. Lakini mimi ninataka kumtorosha Dr Luis na kumrejesha nyumbani. Najua kwasasa itakuwa ngumu sana kwakuwa Dr Luis anasakwa usiku na mchana. Lakini yanipasa kumtoa Dr Luis hapa nchini kwa namna yoyote ile. Na katika kazi hiyo ngumu nimekuteua wewe Felisia unisaidie kumtoa Dr Luis hapa nchini kwenu. Nikuahidi tu kazi hiyo ina malipo makubwa sana. Tukifanikisha kazi hii unaenda kuwa bilionea Felisia. Na pengine kuwa mwanamke wa kwanza tajiri hapa nchini kwenu" Imma alisema.

"Imma wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu sana. Tumefanya misheni nyingi za kifo na wewe. Katika kazi hii unayonipa huna haja ya kunitangazia pesa. Ninakuahidi ushirikiano na kuhakikisha Dr Luis anarejea Nigeria salama. Lakini naomba nijue baadhi ya vitu kama hautojari" Felisia alisema.

"Uliza chochote kile, kama kipo ndani ya uwezo wangu nitakujibu"

"Kwanza nataka kumjua zaidi Dr Luis. Na kama hautajari nambie nini hasa kilimleta hapa nchini ambacho kwa sasa kinasabanisha atake kuuwawa?. Na ni nani hasa ambaye yupo nyuma ya mipango ya kuuwawa kwa Dr Luis?"

Imma Ogbo aliinamisha kichwa chini "Felisia kauliza maswali magumu sana. Namwamini sana Felisia lakini sipo tayari kumueleza juu ya hayo aliyouliza. Hizo ni siri ya nchi yetu, kumueleza Felisia ni jambo la hatari sana. Ni sawa na kumvua nguo rais Abayo.."

"Imma Ogbo" Felisia aliita wakati Imma Ogbo akiwa katikati ya mawazo.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
Mwandishi; Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Moja

"Nikuombe kitu kimoja Felisia" Imma Ogbo alisema.

"Nakusikiliza Imma" Felisia alisema huku akimwangalia Imma kwa chati.

"Naomba nisikujibu maswali yako kwasasa. Naomba hayo maelezo niliyokupa yatoshe. Lakini nikuahidi tu siku ambayo mpango wa kumtoa Dr Luis hapa Tanzania utafanikiwa ndio siku ambayo nitakueleza kila kitu" Imma Ogbo alisema.

Falisia aliinama chini, kisha akasema kwa unyonge
" Sawa".

"Najua Felisia hajaridhika na majibu yangu. Lakini sipaswi kumwambia kila kitu Felisia. Katika hizi kazi usimwamini mtu kwa asilimia mia moja. Muda wowote anaweza kukugeuka. Ingawa sina mashaka hata kidogo na Felisia. Nimemfahamu kitambo sana. Hawezi kuwa double agent lakini pia sipaswi kufunguka kila kitu kwake" Imma Ogbo aliwaza.

"Sasa Imma umepangaje ili kuhakikisha Dr Luis anatoka nje ya mipaka ya Tanzania?" Felisia aliuliza.

"Kama nilivyosema awali. Kwa kutumia njia ya ndege za abiria ama kumtorosha kupitia mipaka itakuwa ni kazi ngumu sana. Kuna kitu nimewaza. Ila ninahitaji sana ushirikiano wako ili kuweza kukifanikisha" Imma alisema.

"Kitu gani hiko ulichowaza?" Felisia aliuliza.

"Nataka kupoteza tension ya vyombo vya ulinzi. Unajua kwasasa vyombo vya ulinzi vyote vimejiandaa katika msako wa Dr Luis. Sasa mimi ninataka niwabadilishe uwelekeo wao" Imma alisema.

Felisia alibaki kimya, akisikiliza.

"Nataka tufanye tukio ambalo litabadilisha uelekeo wa vyombo vyote vya usalama hapa Tanzania" Imma Ogbo alisema.

"Unataka tufanye tukio gani Imma?"

"Nataka tuulipue ubalozi wa Uganda hapa Tanzania!!" Imma alisema.

"Imma Ogbo!!" Felisia aliita kwa sauti.

"Felisia, hiyo ndiyo njia pekee itakayotuwezesha kumtoa Dr Luis nje ya nchi. Tukiulipua ubalozi wa Uganda hapa nchini, macho na masikio ya nchi yataelekea katika tukio hilo, na kusahau kuhusu habari za Dr Luis. Hapo ndipo tutakapopata nafasi ya kwenda Nigeria" Imma Ogbo alisema.

"Inawezakana kuna ukweli katika maneno yako. Lakini sio rahisi kama usemavyo. Hilo ni jambo kubwa na la hatari sana. Na ni jambo ambalo linaweza kuleta mtafaruku mkubwa kati ya Uganda na Tanzania, na jumuia ya Afrika Mashariki kwa ujumla" Felisia alisema.

"Come on Felisia. Lengo letu kuu ni kuhakikisha Dr Luis anatoka hapa Tanzania kwa namna yoyote ile. Mambo ya mtafaruku sijui hatari ni out of our business" Imma Ogbo alisema.

"Imma, huo sio mpango wa kufanywa na watu wawili. Unajua jinsi balozi zinavyolindwa, suala kwenda kulipua ubalozi si la kitoto" Felisia alisema.

"Hatupo wawili. Tupo watu watatu mahiri sana. Sisi ni jeshi. Sisi sio tu tunaweza kuulipua ubalozi wa Uganda, tunauwezo wa kulipua hata dunia mzima tukitaka. Mimi, wewe na Mark the sniper tunaweza kufanya chochote kile. Suala ni kukubaliana tu na kuanza mpango wetu. Hiyo ndio njia pekee ya kumtoa Dr Luis Tanzania" Imma Ogbo alisema.

"Ina maana na Mark yupo upande wetu?" Felisia alishangaa.

"Mimi na Mark tupo katika misheni moja. Wote tumeletwa na rais Abayo kwa lengo la kumsaidia Dr Luis, na kuhakikisha anarudi salama Nigeria" Imma Ogbo alisema.

Felisia aliinama chini kufikiri " Ni kweli Imma Ogbo ni rafiki yangu sana. Tumesaisaidiana katika misheni mbalimbali kama ndugu. Lakini hii misheni ya sasa ni ngumu sana kwangu. Kuungana na Imma katika misheni hii ni kuisaliti nchi yangu na kuiunga mkono nchi ya Nigeria. Hii ni misheni yangu ya kwanza ngumu kuamua..."

"Felisia" Imma Ogbo aliita na kumtoa Felisia mawazoni.

Felisia alinyanyua kichwa chake. Alikutana na Dr Luis akiwa kafumbua macho.

"Dr Luis ameamka!!" Felisia alishangaa.

"Nilimnusisha dawa ambayo ilimtoa duniani kwa saa mbili" Imma Ogbo alisema.

Dr Luis alipiga chafya mara tatu mfululizo.

Na akarejea tena duniani.

***

Hannan Halfani bado alikuwa ametekwa katika nyumba moja huko Tegeta. Watekaji walijitahidi kumtibu Hannan ili atengemae. Waliamini kwamba Hannan ni silaha ambayo wanaweza kuitumia hapo baadae.

Hannan mwenyewe afya yake ilikuwa nzuri kidogo ingawa alijifanya bado anaumwa ili asiwape nafasi wale watekaji kufanya walichotaka kufanya. Kila sekunde alikuwa anawafikiria wakina Daniel na misheni yao. Alijilaumu kwa kukamatwa kijinga kule hospitali.

"Wameniteka kama kuku hawa wajinga. Hii ni kwasababu sipo sawa kiafya. Waache waniweke hapa ipo siku watajuta kwa kitendo chao cha kukaa na nyoka nyumba moja. Nitawashangaza. Nashukuru wananihudumia vizuri, na hii inanifanya nizidi kuwa imara kila sekunde. Lakini hawa watu ni kina nani? Ingekuwa ni majambazi wasingeniweka hapa na kunihudumia vizuri namna hii. Jinsi walivyoniteka kule hospitali inaonesha ni watu wenye mafunzo maalum. Kwakuwa afya yangu inaanza kuwa imara lazima nianze kuwapeleleza kuanzia usiku wa leo" Hannan alikuwa anawaza akiwa katika chumba chake. Mara mlango ulifunguliwa. Aliingia msichana ambaye alikuwa anamuhudumia tangu aingizwe katika ile nyumba.
Yule msichana alienda hadi mezani na kuanza kutoa vyombo vya chakula ambavyo alishavitumia.

"Uliniambia unaitwa nani vile?" Hannan aliuliza.

Yule msichana aliacha kutoa vyombo na kumwangalia Hannan.

"Naitwa Anna"

"Anna. Samahani ninaomba unisaidie kitu" Hannan alisema.

"Nikusaidie nini dada?"

"Kwani hapa ni wapi Anna?" Felisia aliuliza.

"Hapa ni Tegeta" Anna alijibu wakati huku akianza tena kukusanya vyombo.

"Mdogo wangu naomba unisaidie simu. Mama yangu mgonjwa sana, nataka nimjulie hali" Felisia alitupa karata yake.

"Dada ombi lako haliwezi kufanikiwa. Mtu yoyote anayeingizwa katika chumba hiki hatakiwi kuwa na mawasiliano yoyote yale na nje" Anna alisema.

"Kwani ninyi ni kina nani?" Felisia aliuliza.

"Felisia, nimeshangaa sana wewe kuletwa hapa. Wewe ni msichana mdogo sana, na unaonekana ni innocent. Na hii ndo sababu iliyonifanya nifungue mdomo wangu kuzungumza na wewe. Hii nyumba wanaletwa magaidi na watu walioshindikana, na wakiingia tu humu ndani watafunguka kila kitu. Sasa wewe sijui umefanya jambo gani la kuhatarisha usalama wa nchi hadi ukaletwa hapa" Anna alisema.

"Kwani ninyi ni askari?" Felisia aliuliza.

"Sisi ni zaidi ya askari. Akija Ayoub Ndondo atakueleza kila kitu kuhusu sisi. Na nikushauri tu usilete ujuaji mbele ya Ayoub Ndondo, atakuchakaza!!. ayoub hana huruma. Mjibu kila atakachokuuliza, tena umwambie ukweli mtupu!" Anna alisema.

Felisia alimwangalia Anna kisha akasema " Kwahiyo huwezi kunisaidia nilichokuomba? Unachoweza wewe ni kunitisha tu!" Felisia alisema.

"Msubiri Ayoub Ndondo!!" Anna alisema kwa mkato na kutoka nje na vyombo vya chakula.

Imma Ogbo anapanga kuulipua ubalozi wa Uganda, je watafanikiwa? Wakati Hannan anaambiwa akisubiri kiumbe kinachoitwa Ayoub Ndondo, je ni nani huyo Ayoub? Endelea kuisoma Bomu upate majibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom