HALFANI SUDY katika BOMU
Mawasiliano; 0652 212391
Sehemu ya Ishirini na Nane
"Adrian umeongea jambo zuri sana. Sijui muda wote huu hatujawaza hivyo. Hili sulala lilipofikia lazima tumfahamishe mheshimiwa rais. Uhusika wa rais Abayo katika suala hili ni jambo zito sana!. Lazima rais ajue nani adui wake mkuu kwasasa.
Lakini tatizo Ikulu si mahali unapoweza kuingia kiurahisi. Lazima uwe na jambo muhimu na zito, pia uwe na mtu anayeweza kufanikisha ukaingie ndani ya jumba hilo tukufu. Ngoja niwasiliane na Chifu ili atutafutie namna ya kuonana na Mheshimiwa rais. Tukimueleza kuwa tuna jambo zito la kumwambia rais juu ya kutekwa nyara kwa Dr Louis lazima tutaipata hiyo nafasi. Bila shaka yeye atatupa namna sahihi ya kulimaliza hili suala" Daniel alisadiki maneno ya Adrian.
Suala la michirizi ya damu liliishia pale. Kilibaki ni kitendawili juu mahali walipoelekea wakina Imma Ogbo. Wote wanne walitoka eneo lile na kuelekea mahali ambapo walikuwa wamepaki gari yao. Wakajitosa ndani ya gari na kurudi katika maskani yao.
Nyumbani kwa Daniel Mwaseba.
"Kipindi hiki ambacho tunasubiri kukubaliwa ombi letu la kuonana na Mheshimiwa rais mnaonaje tukaenda kuwasaka watu wetu waliotekwa?" Adrian aliuliza.
"Umeongea jambo zuri sana Adrian. Unajua mwanzoni tulikuwa tumeweka nguvu kubwa sana ya kumsaka Dr Louis. Lengo ni kumkomboa kabla hajapatwa na madhara makubwa zaidi. Lakini kwakuwa tumegundua Dr Louis yupo na watu wake, itakuwa vizuri tukaitumia nafasi hii kuwasaka watu wetu, Hannan na familia ya David" Daniel aliunga mkono hoja.
"Tutaanzia wapi sasa kuwasaka? Maana hadi sasa sidhani kama tumepata sehemu sahihi pa kuanzia msako wetu.." David aliuliza, huku akionekana kabisa furaha ilikuwa imechanua usoni kwake.
"David, tunapo pa kuanzia msako wetu!" Daniel alisema kwa uhakiks huku akichukua simu ya Adrian.
Moja kwa moja akampigia mshkaji wake, Mwanasheria mlevi..
"Hallo Mwanasheria mlevi?" Daniel alisema pindi tu simu yake ilipopokelewa upande wa pili.
"Eeh nambie Daniel Mwaseba. Nimeona kimya sana, vipi mlifanikiwa kuwapata wale majamaa?" Mwanasheria alisema.
Daniel alivuta pumzi kidogo.
"Hatujafanikiwa kuwapata Mwanasheria, ingawa tupo katika mwelekeo mzuri sana. Unajua mambo yale tuliyoyagundua baada ya kutumiwa ujumbe na Felisia ni mazito sana. Tumeona kwa uzito wake kuna umuhimu wa kumshirikisha Rais" Daniel alisema.
"Sidhani kama ni sahihi kumweleza Mheshimiwa rais kwasasa. Unajua yale ni mamho mazito sana. Yanahusisha nchi nyingine. Kwanini msimalizie uchunguzi wenu hadi mwisho na kisha mumueleze rais mkiwa ushahidi uliokamilika?" Mwanasheria mlevi alipinga wazo la Daniel.
"Umesema vyema Mwanasheria, lakini tumewaza sana na wenzangu hapa. Tumeona umuhimu wa kumueleza Mgeshimiwa rais sasa kabla maji hayajakorogeka. Hatujui rais ana mpango gani na nchi ya Nigeria, lazima tuhakikishe anasimamisha uhusiano wake na nchi hiyo". Daniel alisema.
"Sawa Daniel. Ni kutofautiana tu maoni na mawazo, lakini kama mnahisi hiyo ni njia sahihi, basi tupo pamoja. Mimi nitawaunga mkono kwa kadri ya uwezo wangu"
"Upo sahihi Mwanasheria, wote tunajenga nyumba moja, na sisi ni watoto wa mama mmoja. Mama Tanzania.
Vipi, bado upo ofisini?" Daniel aliuliza.
"Ndio bado nipo ofisini. Mambo yamekuwa mengi sana hapa ofisini. Vipi ulikuwa unataka nije nini, nami nivae jezi tuingie wote uwanjani?" Mwanashetia aliuliza kimas'hara.
"Hapana kijana, kuna kitu kidogo nilikuwa ninataka unisaidie" Daniel alisema.
"Nitakusaidie kitu chochote kile, kama kipo ndani ya uwezo wangu basi hesabu kitu hiko kmekwisha!" Mwanasheria alisema kwa uhakika.
"Ninakuamini jamaa yangu. basi nipe dakika moja ninakutumia ujumbe mfupi" Daniel alisema.
Simu ikakatwa.
Daniel aliangalia ile namba ya simu aliyoitumia Hannan kupiga na kisha kumwambia akiwa Rombo hoteli. Aliandika pembeni katika karatasi ndogo, akaandika pamoja na muda simu hiyo ilipopigwa.
Akaandika katika simu yake, kisha akamtumia meseji Mwanasheria mlevi.
Alivyohakikisha ujumbe umefika kwa Mwanasheria mlevi. Akasindikiza na meseji ya pili iliyokuwa inasomeka.
"Nipe location yake"
Zilipita kama dakika mbili, majibu yalirudi kutoka kwa Mwanasheria mlevi. Ilikuwa ni meseji yenye eneo na namba ya nyumba aliyokuwepo Hannan.
"Tunaelekea Tegeta sasahivi" Daniel alisema kwa sauti iliyosikiwa na wote.
***
Taa mbalimbali zilikuwa zinawaka ndani ya Ikulu ya Tanzania, iliyopo maeneo ya Posta, jijini Dar es salaam. Walinzi maalum wa rais, wenye silaha za kisasa walikuwa wanazunguka eneo hilo kuhakikisha usalama unaendelea kudumishwa ndani ya jengo.
Nje nako kulikuwa kumejaa walinzi lukuki wenye bunduki. Wakihakikisha kila kitu kinakaa mahali pake.
Katika chumba cha faragha cha Mheshimiwa rais, kulikuwa na watu wawili. Walinzi na wahudumu walitolewa nje, wakiwaacha watu wawili tu ndani ya chumba hiko.
Kilikuwa ni chumba kidogo chenye kila kitu ndani yake. Samani za ghali na za kisasa, friji ndogo pembeni iliyojaa matunda na kila aina ya sharubati, kompyuta ya bei, kutoka kampuni ya Apple mezani, air condition ikiyotoa hewa mujarab ukutani huku kabati dogo lililojaa mafaili mbalimbali likiwa pembeni konani mwa chumba hiko. Kilikuwa chumba kidogo lakini kilichopangiliwa vizuri sana. Chumba hiko kizuri kwasasa, sofa zake ghali na za kisasa zilikaliwa zimekaliwa na watu wawili tu..
Mheshimiwa Rais Mgaya na Mohammed Msangi.
"Safari hii mzee Msangi umeniangusha sana. Sikutegemea suala la kumpata Dr Louis litakuwa gumu na kuchukua muda mrefu namna hii?" Rais Mgaya alisema baada ya kusafisha koo lake kwa sharubati ya embe.
" Niombe tena msamaha kwa hilo Mheshimiwa Rais. Hili suala limekuwa tata na gumu. Yaani sijui hata nisemeje. Kama nilivyokwambia awali, Tulifanikiwa kumtia mikononi mwetu Dr Louis lakini yule kijana uliyetuletea kutoka kwa rais Abayo ndiye aliyeharibu kila kitu, alimteka Dr Louis na hadi sasa hatujui wapi amempeleka. Lakini sisi bado hatujakata tamaa, tunaendelea kumsaka Dr Louis hadi apatikane" Mzee Msangi alisema.
"Kusema kweli nimesikitishwa sana na kitendo alichokifanya huyo kijana. Nimemweleza Rais Abayo juu ya kitendo alichokifanya kijana wake. Naye amesikitishwa sana, na amesema atatusaidia kwa namna yoyote ile kuhakikisha tunampata Dr Louis pamoja na huyo kijana" Rais Mgaya alisema.
"Kwakuwa umemwambia rais Abayo haina shida, lakini nikuhakikishie tu sisi wenyewe tumejipanga vizuri, na nakuahidi tutampata Dr Louis" Mzee Msangi alisema kwa uhakika.
"Nakuamini sana Mzee Msangi. Ila kuchelewa kwenu kumpata Dr Louis ndo kunanipa mashaka. Sikudhami kama suala hili litachukua muda mrefu namna hii. Nimewaagiza wakuu wa usalama wafunge mipaka yote ya nchi kuhakikisha mnawakamata watu hao lakini bado majibu na yaleyale, bado bado!!.." Rais Mgaya alisema huku akigonga meza.
"Mheshimiwa rais usiwe na shaka. Hii ni ahadi yangu ya mwisho kwako. Nakuahidi nakuletea Dr Louis hapa" Mzee Msangi akameza mate. Kisha akauliza.
"Kwani kuna kitu gani cha siri kati yenu kinachokufanya umsake sana Dr Louis? Mimi ni mshirika wako na sidhani kama kutakuwa na ubaya wowote nikifahamu. Pengine itachochea msako wake" Mzee Msangi aliuliza swali.
Rais Mgaya alikaa kimya. Alimwangalia Mzee Msangi huku uso wake ukionesha hajapendezwa na swali hilo.
"Bila shaka kuna siri kubwa sana kati ya rais na Dr Louis. Na siri hiyo nikiijua kwangu itakuwa ni hela. Lazima nimsake Dr Louis kwa nguvu kubwa sana ili niitie mikononi mwangu siri hiyo! Siri ya kutengeneza mabilioni!" Dr Louis alijisemea kifuani.
"Mzee Msangi, sidhani kama sasahivi ni wakati sahihi wa kukwambia kwanini ninamsaka sana Dr Louis. Ipo siku nitakwambia sababu, na siku hiyo ni utakayoniletea Dr Louis mbele yangu" Rais Mgaya alisema.
Rais Mgaya na mzee Msangi waliongea kama muda wa robo saa, kisha wakaagana.
Mzee Msangi alipotoka tu nje, alimpigia simu Antony Kyando..
Je kuna siri gani kati ya Rais na Dr Louis?
Wakina Daniel watafanikiwa kumuokoa hannan?
Antony Kyando ni nani?