BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

HALFANI SUDY katika BOMU
Mawasiliano; 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Saba

Stoo yote aliyokuwepo Felisia ilikuwa imetapakaa damu, na nyingine ikianza kuganda sakafuni.

Maumivu aliyokuwa anayasikia Felisia sehemu mbalimbali katika mwili wake hayakuwa na mfanowe. Alikuwa anasikia maumivu kuanzia utosini hadi nyayoni. Imma Ogbo alimfanyia unyama wa hali ya juu!!

Kama Felisia alikuwa anadhani aliwahi kukutana na mtu katili hapa duniani, basi hiyo itakuwa labda kabla ya kukutana na Imma Ogbo!

Imma Ogbo alikuwa katili na nusu!

Imma Ogbo, mwanaume wa Kinaijeria ambaye aliamini kuwa ni rafiki wa kweli kwake lakini kwasasa haikuwa hivyo. Alikuwa ni adui namba moja kwake.

Na aliapa kumuua kwa mkono wake endapo akipata tu nafasi hiyo!!

Felisia, hakujua kwamba Imma Ogbo hakuwa na urafiki hata kidogo na yeye, alikuwa ni rafiki maslahi. Alikuwa anakuwa rafiki anapokuhitaji, adui asipokuhitaji.

Muda huu, Imma Ogbo, Dr Louis na balozi Agdir walikuwa katika ofisi ndogo ndani ya nyumba hiyo. Walikuwa wanapanga mipango yao kwa umakini mkubwa na kuhakikisha inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

Kuhakikisha kina Imma Ogbo wanatoka Tanzania salama..

"Balozi Agdir tunashukuru sana kwa kuweza kututoa kule porini na kutufikisha hapa. Yaani tulilikuwa tumekwama kabisa. Na tungechelewa kidogo tu tulikuwa tunatiwa mkononi na wale jamaa. Yaani yule malaya ni mshenzi sana. Nilimstukia kwamba alienda kuongea na watu wake kule bafini. Halafu kumuuliza ananiletea ujuaji. Nilikuwa sina namna zaidi ya kumkata kidole!

Lakini bado alijifanya mtukutu...

Akaleta ujanja mpya tulipotoka kule chumbani. Ujanja wa kuchuruzisha damu yake kila tulipokuwa tunapita ili iwe rahisi kwa hao watu wake kutufatilia!

Na hapo ndipo nilipoamua kumtoboa jicho!!" Imma Ogbo alisema kwa hasira.

"Achana na habari za yule malaya. Zawadi uliyompa ya kumtoboa jicho na kumkata kidole nd'o zawadi aliyokuwa anastahili. Na sasa hakuna kingine anachostahili zaidi ya kifo! Hiyo ndio zawadi kuu ya msaliti!" Dr Louis alisema kwa nguvu.

"Imma Ogbo, hamna haja ya kunishukuru mimi hata kidogo. Ni kitu kidogo sana nimekifanya katika kuwaokoa ukilinganisha na mliyoyafanya nyinyi kwa Nigeria. Nyinyi mmefanya kazi kubwa sana katika kuhakikisha mnayalinda maslahi ya nchi yenu. Niwaambie tu nami nilijisikia fahari sana kupokea simu ya rais Abayo ikinitaka kuhakikisha nawatoa kule porini, na kuwasaidia kuhakikisha mnatoka salama hapa Tanzania" Balozi Agdir alisema.

Kikapita kimya kifupi kabla ya Imma Ogbo hajaongea tena.

"Tuyaache hayo. Tu'focus ya mbele, maana kwa sasa mpango wa kuulipua ubalozi wa Uganda bila shaka umefeli. Nimewasiliana na Mark na kunambia mpango huo tayari umeshamfikia Rais. Bila shaka kupitia kwa huyu mwanamke. Sasa sijui tutatumia njia gani tena ya kutuwezesha kutoka nje ya Tanzania?"

"Ni swali zuri sana. Kwanza ule mpango wa kulipua ubalozi wa Uganda ulikuwa mzuri sana. Lakini kwasasa si mpango tena, mpango umeingia kidudu mtu, lazima tutafute njia nyingine ya kutufikisha Nigeria. Na njia hiyo lazima iwe ya haraka sana" Dr Louis alisema.

"Msiwe na shaka, nitaongea na rais Abayo tuone atatupa mbinu gani kututoa nje ya nchi? Yule ni rais hawezi kukosa namna ya kututoa hapa nchini" Balozi Agdir alisema.

Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan, David na Martin Hisia, ambaye aliwasiliana na kina Daniel na kuelekezwa eneo walipo walikuwa wamesimama pale kulipokuwa na kidimbwi cha damu.

Walijaribu kuchanganya akili zao lakini hawakugundua pale kilitokea nini? Ukweli ulibaki uleule, Michirizi ya damu iliishia palepale walipomkuta David na hakukuwa na dalili yoyote ya kuonesha wakina Imma Ogbo walikuwa wamenda wapi?

Walijaribu kutafuta nyayo za miguu, lakini uwepo wa nyasi nyingi eneo hilo zilikwamisha kabisa zoezi hilo. Wakina Daniel wakabaki tena katika sifuri. Wakiwa hawana lolote la kufanya..

Walikuwa wametorokwa kiajabu!!

"Sasa tunafanyaje hapa? Jamaa wameyeyuka hapa kwa mtindo usioeleweka. Si mashariki, si magharibi, si kusini na kaskazini pote hakuna dalili za kuonesha kwamba hawa jamaa walielekea? Sijui walipaa hapa? Tunafanyaje kuhakikisha tunawapata?" Adrian aliwauliza wenzie.

"Hawa jamaa ni wajanja sana. Sijui wametumia mbinu gani kutoroka. Lakini niwaambie tu kwa sasa tupo karibu yao kuliko wakati wowote ule. Na tutawakamata tu hawana ujanja!" David alisema kwa hasira. Zilikuwa ni mchanganyiko wa hasira za kutekwa familia yake.

"Martin Hisia. sijui una mawazo gani mwenzetu? Sisi wote watatu hapa tupo watupu, lakini angalau tumepunguza tishio la kulipuliwa kwa ubalozi wa Uganda baada ya kumtaarifu IGP John Rondo, bila shaka vyombo vyetu vya ulinzi vitahakikisha hilo halitokei. Lakini swali ni tunafanyaje kuwakamata hawa wahalifu wenye nia ovu na nchi yetu?" Daniel aliuliza.

"Felisia, Felisia.." Martin alisema. Na hili ni neno pekee ambalo alilokuwa analitamka tangu afike eneo hilo.
Kuambiwa hali ilivyokuwa kabla ya ujio wake, na kuona damu ambazo kwake yeye aliamini ni za Felisia zilimnyong'onyesha sana. Macho yake yalikuwa mekundu huku yakitoka machozi kila dakika. Midomo ilimtetemeka sambamba na mikono.

Safari hii, alikuwa amepigwa penyewe!

Daniel akaona hakuna msaada kwa kumtegemea Martin Hisia. Hakukuwa na nafasi ya kuzitumia hisia zake. Sasa, Martin alikuwa anaelekea kuwehuka, kupotea kwa Felisia kulimuumiza isivyo kawaida.

"Hapa lazima turudi maskani kwetu tukajipange upya. Ila kiukweli hadi sasa tumepiga hatua kubwa sana. Tumejua ushiriki wa Rais Abayo katika sakata hili. Pia tumejua kwamba Dr Louis anaushirikiano wa karibu na Imma Ogbo. Hii ni hatua kubwa sana ambayo tumepiga kwa leo" Daniel alisema.

Wote walikubali kwa kutikisa kichwa, kasoro Martin Hisia.

"Lakini Daniel, kwanini tusiombe nafasi ya kwenda kuonana na Mheshimiwa Rais Mgaya? Tumueleze mheshimiwa rais juu ya uhusika wa rais Abayo katika upoteaje wa Dr Louis?" Adrian aliuliza akiwa anamwangalia Daniel usoni.

Wakati wakina Imma Ogbo wakipanga kumueleza Rais Abayo awasaodie kutoka nchini, Adrian anatoa wazo nao wamwambie rais Mgaya juu ya uhusika wa rais Abayo katika sakata hili. Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
Mkuu Sixman shukrani
Lakini km ikiwezekana ongeza kidogo
 
HALFANI SUDY katika BOMU
Mawasiliano; 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Nane

"Adrian umeongea jambo zuri sana. Sijui muda wote huu hatujawaza hivyo. Hili sulala lilipofikia lazima tumfahamishe mheshimiwa rais. Uhusika wa rais Abayo katika suala hili ni jambo zito sana!. Lazima rais ajue nani adui wake mkuu kwasasa.

Lakini tatizo Ikulu si mahali unapoweza kuingia kiurahisi. Lazima uwe na jambo muhimu na zito, pia uwe na mtu anayeweza kufanikisha ukaingie ndani ya jumba hilo tukufu. Ngoja niwasiliane na Chifu ili atutafutie namna ya kuonana na Mheshimiwa rais. Tukimueleza kuwa tuna jambo zito la kumwambia rais juu ya kutekwa nyara kwa Dr Louis lazima tutaipata hiyo nafasi. Bila shaka yeye atatupa namna sahihi ya kulimaliza hili suala" Daniel alisadiki maneno ya Adrian.

Suala la michirizi ya damu liliishia pale. Kilibaki ni kitendawili juu mahali walipoelekea wakina Imma Ogbo. Wote wanne walitoka eneo lile na kuelekea mahali ambapo walikuwa wamepaki gari yao. Wakajitosa ndani ya gari na kurudi katika maskani yao.

Nyumbani kwa Daniel Mwaseba.

"Kipindi hiki ambacho tunasubiri kukubaliwa ombi letu la kuonana na Mheshimiwa rais mnaonaje tukaenda kuwasaka watu wetu waliotekwa?" Adrian aliuliza.

"Umeongea jambo zuri sana Adrian. Unajua mwanzoni tulikuwa tumeweka nguvu kubwa sana ya kumsaka Dr Louis. Lengo ni kumkomboa kabla hajapatwa na madhara makubwa zaidi. Lakini kwakuwa tumegundua Dr Louis yupo na watu wake, itakuwa vizuri tukaitumia nafasi hii kuwasaka watu wetu, Hannan na familia ya David" Daniel aliunga mkono hoja.

"Tutaanzia wapi sasa kuwasaka? Maana hadi sasa sidhani kama tumepata sehemu sahihi pa kuanzia msako wetu.." David aliuliza, huku akionekana kabisa furaha ilikuwa imechanua usoni kwake.

"David, tunapo pa kuanzia msako wetu!" Daniel alisema kwa uhakiks huku akichukua simu ya Adrian.

Moja kwa moja akampigia mshkaji wake, Mwanasheria mlevi..

"Hallo Mwanasheria mlevi?" Daniel alisema pindi tu simu yake ilipopokelewa upande wa pili.

"Eeh nambie Daniel Mwaseba. Nimeona kimya sana, vipi mlifanikiwa kuwapata wale majamaa?" Mwanasheria alisema.

Daniel alivuta pumzi kidogo.

"Hatujafanikiwa kuwapata Mwanasheria, ingawa tupo katika mwelekeo mzuri sana. Unajua mambo yale tuliyoyagundua baada ya kutumiwa ujumbe na Felisia ni mazito sana. Tumeona kwa uzito wake kuna umuhimu wa kumshirikisha Rais" Daniel alisema.

"Sidhani kama ni sahihi kumweleza Mheshimiwa rais kwasasa. Unajua yale ni mamho mazito sana. Yanahusisha nchi nyingine. Kwanini msimalizie uchunguzi wenu hadi mwisho na kisha mumueleze rais mkiwa ushahidi uliokamilika?" Mwanasheria mlevi alipinga wazo la Daniel.

"Umesema vyema Mwanasheria, lakini tumewaza sana na wenzangu hapa. Tumeona umuhimu wa kumueleza Mgeshimiwa rais sasa kabla maji hayajakorogeka. Hatujui rais ana mpango gani na nchi ya Nigeria, lazima tuhakikishe anasimamisha uhusiano wake na nchi hiyo". Daniel alisema.

"Sawa Daniel. Ni kutofautiana tu maoni na mawazo, lakini kama mnahisi hiyo ni njia sahihi, basi tupo pamoja. Mimi nitawaunga mkono kwa kadri ya uwezo wangu"

"Upo sahihi Mwanasheria, wote tunajenga nyumba moja, na sisi ni watoto wa mama mmoja. Mama Tanzania.

Vipi, bado upo ofisini?" Daniel aliuliza.

"Ndio bado nipo ofisini. Mambo yamekuwa mengi sana hapa ofisini. Vipi ulikuwa unataka nije nini, nami nivae jezi tuingie wote uwanjani?" Mwanashetia aliuliza kimas'hara.

"Hapana kijana, kuna kitu kidogo nilikuwa ninataka unisaidie" Daniel alisema.

"Nitakusaidie kitu chochote kile, kama kipo ndani ya uwezo wangu basi hesabu kitu hiko kmekwisha!" Mwanasheria alisema kwa uhakika.

"Ninakuamini jamaa yangu. basi nipe dakika moja ninakutumia ujumbe mfupi" Daniel alisema.

Simu ikakatwa.

Daniel aliangalia ile namba ya simu aliyoitumia Hannan kupiga na kisha kumwambia akiwa Rombo hoteli. Aliandika pembeni katika karatasi ndogo, akaandika pamoja na muda simu hiyo ilipopigwa.
Akaandika katika simu yake, kisha akamtumia meseji Mwanasheria mlevi.

Alivyohakikisha ujumbe umefika kwa Mwanasheria mlevi. Akasindikiza na meseji ya pili iliyokuwa inasomeka.

"Nipe location yake"

Zilipita kama dakika mbili, majibu yalirudi kutoka kwa Mwanasheria mlevi. Ilikuwa ni meseji yenye eneo na namba ya nyumba aliyokuwepo Hannan.

"Tunaelekea Tegeta sasahivi" Daniel alisema kwa sauti iliyosikiwa na wote.

***

Taa mbalimbali zilikuwa zinawaka ndani ya Ikulu ya Tanzania, iliyopo maeneo ya Posta, jijini Dar es salaam. Walinzi maalum wa rais, wenye silaha za kisasa walikuwa wanazunguka eneo hilo kuhakikisha usalama unaendelea kudumishwa ndani ya jengo.

Nje nako kulikuwa kumejaa walinzi lukuki wenye bunduki. Wakihakikisha kila kitu kinakaa mahali pake.

Katika chumba cha faragha cha Mheshimiwa rais, kulikuwa na watu wawili. Walinzi na wahudumu walitolewa nje, wakiwaacha watu wawili tu ndani ya chumba hiko.

Kilikuwa ni chumba kidogo chenye kila kitu ndani yake. Samani za ghali na za kisasa, friji ndogo pembeni iliyojaa matunda na kila aina ya sharubati, kompyuta ya bei, kutoka kampuni ya Apple mezani, air condition ikiyotoa hewa mujarab ukutani huku kabati dogo lililojaa mafaili mbalimbali likiwa pembeni konani mwa chumba hiko. Kilikuwa chumba kidogo lakini kilichopangiliwa vizuri sana. Chumba hiko kizuri kwasasa, sofa zake ghali na za kisasa zilikaliwa zimekaliwa na watu wawili tu..

Mheshimiwa Rais Mgaya na Mohammed Msangi.

"Safari hii mzee Msangi umeniangusha sana. Sikutegemea suala la kumpata Dr Louis litakuwa gumu na kuchukua muda mrefu namna hii?" Rais Mgaya alisema baada ya kusafisha koo lake kwa sharubati ya embe.

" Niombe tena msamaha kwa hilo Mheshimiwa Rais. Hili suala limekuwa tata na gumu. Yaani sijui hata nisemeje. Kama nilivyokwambia awali, Tulifanikiwa kumtia mikononi mwetu Dr Louis lakini yule kijana uliyetuletea kutoka kwa rais Abayo ndiye aliyeharibu kila kitu, alimteka Dr Louis na hadi sasa hatujui wapi amempeleka. Lakini sisi bado hatujakata tamaa, tunaendelea kumsaka Dr Louis hadi apatikane" Mzee Msangi alisema.

"Kusema kweli nimesikitishwa sana na kitendo alichokifanya huyo kijana. Nimemweleza Rais Abayo juu ya kitendo alichokifanya kijana wake. Naye amesikitishwa sana, na amesema atatusaidia kwa namna yoyote ile kuhakikisha tunampata Dr Louis pamoja na huyo kijana" Rais Mgaya alisema.

"Kwakuwa umemwambia rais Abayo haina shida, lakini nikuhakikishie tu sisi wenyewe tumejipanga vizuri, na nakuahidi tutampata Dr Louis" Mzee Msangi alisema kwa uhakika.

"Nakuamini sana Mzee Msangi. Ila kuchelewa kwenu kumpata Dr Louis ndo kunanipa mashaka. Sikudhami kama suala hili litachukua muda mrefu namna hii. Nimewaagiza wakuu wa usalama wafunge mipaka yote ya nchi kuhakikisha mnawakamata watu hao lakini bado majibu na yaleyale, bado bado!!.." Rais Mgaya alisema huku akigonga meza.

"Mheshimiwa rais usiwe na shaka. Hii ni ahadi yangu ya mwisho kwako. Nakuahidi nakuletea Dr Louis hapa" Mzee Msangi akameza mate. Kisha akauliza.

"Kwani kuna kitu gani cha siri kati yenu kinachokufanya umsake sana Dr Louis? Mimi ni mshirika wako na sidhani kama kutakuwa na ubaya wowote nikifahamu. Pengine itachochea msako wake" Mzee Msangi aliuliza swali.

Rais Mgaya alikaa kimya. Alimwangalia Mzee Msangi huku uso wake ukionesha hajapendezwa na swali hilo.

"Bila shaka kuna siri kubwa sana kati ya rais na Dr Louis. Na siri hiyo nikiijua kwangu itakuwa ni hela. Lazima nimsake Dr Louis kwa nguvu kubwa sana ili niitie mikononi mwangu siri hiyo! Siri ya kutengeneza mabilioni!" Dr Louis alijisemea kifuani.

"Mzee Msangi, sidhani kama sasahivi ni wakati sahihi wa kukwambia kwanini ninamsaka sana Dr Louis. Ipo siku nitakwambia sababu, na siku hiyo ni utakayoniletea Dr Louis mbele yangu" Rais Mgaya alisema.

Rais Mgaya na mzee Msangi waliongea kama muda wa robo saa, kisha wakaagana.

Mzee Msangi alipotoka tu nje, alimpigia simu Antony Kyando..

Je kuna siri gani kati ya Rais na Dr Louis?

Wakina Daniel watafanikiwa kumuokoa hannan?

Antony Kyando ni nani?
 
HALFANI SUDY katika BOMU
Mawasiliano; 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Nane

"Adrian umeongea jambo zuri sana. Sijui muda wote huu hatujawaza hivyo. Hili sulala lilipofikia lazima tumfahamishe mheshimiwa rais. Uhusika wa rais Abayo katika suala hili ni jambo zito sana!. Lazima rais ajue nani adui wake mkuu kwasasa.

Lakini tatizo Ikulu si mahali unapoweza kuingia kiurahisi. Lazima uwe na jambo muhimu na zito, pia uwe na mtu anayeweza kufanikisha ukaingie ndani ya jumba hilo tukufu. Ngoja niwasiliane na Chifu ili atutafutie namna ya kuonana na Mheshimiwa rais. Tukimueleza kuwa tuna jambo zito la kumwambia rais juu ya kutekwa nyara kwa Dr Louis lazima tutaipata hiyo nafasi. Bila shaka yeye atatupa namna sahihi ya kulimaliza hili suala" Daniel alisadiki maneno ya Adrian.

Suala la michirizi ya damu liliishia pale. Kilibaki ni kitendawili juu mahali walipoelekea wakina Imma Ogbo. Wote wanne walitoka eneo lile na kuelekea mahali ambapo walikuwa wamepaki gari yao. Wakajitosa ndani ya gari na kurudi katika maskani yao.

Nyumbani kwa Daniel Mwaseba.

"Kipindi hiki ambacho tunasubiri kukubaliwa ombi letu la kuonana na Mheshimiwa rais mnaonaje tukaenda kuwasaka watu wetu waliotekwa?" Adrian aliuliza.

"Umeongea jambo zuri sana Adrian. Unajua mwanzoni tulikuwa tumeweka nguvu kubwa sana ya kumsaka Dr Louis. Lengo ni kumkomboa kabla hajapatwa na madhara makubwa zaidi. Lakini kwakuwa tumegundua Dr Louis yupo na watu wake, itakuwa vizuri tukaitumia nafasi hii kuwasaka watu wetu, Hannan na familia ya David" Daniel aliunga mkono hoja.

"Tutaanzia wapi sasa kuwasaka? Maana hadi sasa sidhani kama tumepata sehemu sahihi pa kuanzia msako wetu.." David aliuliza, huku akionekana kabisa furaha ilikuwa imechanua usoni kwake.

"David, tunapo pa kuanzia msako wetu!" Daniel alisema kwa uhakiks huku akichukua simu ya Adrian.

Moja kwa moja akampigia mshkaji wake, Mwanasheria mlevi..

"Hallo Mwanasheria mlevi?" Daniel alisema pindi tu simu yake ilipopokelewa upande wa pili.

"Eeh nambie Daniel Mwaseba. Nimeona kimya sana, vipi mlifanikiwa kuwapata wale majamaa?" Mwanasheria alisema.

Daniel alivuta pumzi kidogo.

"Hatujafanikiwa kuwapata Mwanasheria, ingawa tupo katika mwelekeo mzuri sana. Unajua mambo yale tuliyoyagundua baada ya kutumiwa ujumbe na Felisia ni mazito sana. Tumeona kwa uzito wake kuna umuhimu wa kumshirikisha Rais" Daniel alisema.

"Sidhani kama ni sahihi kumweleza Mheshimiwa rais kwasasa. Unajua yale ni mamho mazito sana. Yanahusisha nchi nyingine. Kwanini msimalizie uchunguzi wenu hadi mwisho na kisha mumueleze rais mkiwa ushahidi uliokamilika?" Mwanasheria mlevi alipinga wazo la Daniel.

"Umesema vyema Mwanasheria, lakini tumewaza sana na wenzangu hapa. Tumeona umuhimu wa kumueleza Mgeshimiwa rais sasa kabla maji hayajakorogeka. Hatujui rais ana mpango gani na nchi ya Nigeria, lazima tuhakikishe anasimamisha uhusiano wake na nchi hiyo". Daniel alisema.

"Sawa Daniel. Ni kutofautiana tu maoni na mawazo, lakini kama mnahisi hiyo ni njia sahihi, basi tupo pamoja. Mimi nitawaunga mkono kwa kadri ya uwezo wangu"

"Upo sahihi Mwanasheria, wote tunajenga nyumba moja, na sisi ni watoto wa mama mmoja. Mama Tanzania.

Vipi, bado upo ofisini?" Daniel aliuliza.

"Ndio bado nipo ofisini. Mambo yamekuwa mengi sana hapa ofisini. Vipi ulikuwa unataka nije nini, nami nivae jezi tuingie wote uwanjani?" Mwanashetia aliuliza kimas'hara.

"Hapana kijana, kuna kitu kidogo nilikuwa ninataka unisaidie" Daniel alisema.

"Nitakusaidie kitu chochote kile, kama kipo ndani ya uwezo wangu basi hesabu kitu hiko kmekwisha!" Mwanasheria alisema kwa uhakika.

"Ninakuamini jamaa yangu. basi nipe dakika moja ninakutumia ujumbe mfupi" Daniel alisema.

Simu ikakatwa.

Daniel aliangalia ile namba ya simu aliyoitumia Hannan kupiga na kisha kumwambia akiwa Rombo hoteli. Aliandika pembeni katika karatasi ndogo, akaandika pamoja na muda simu hiyo ilipopigwa.
Akaandika katika simu yake, kisha akamtumia meseji Mwanasheria mlevi.

Alivyohakikisha ujumbe umefika kwa Mwanasheria mlevi. Akasindikiza na meseji ya pili iliyokuwa inasomeka.

"Nipe location yake"

Zilipita kama dakika mbili, majibu yalirudi kutoka kwa Mwanasheria mlevi. Ilikuwa ni meseji yenye eneo na namba ya nyumba aliyokuwepo Hannan.

"Tunaelekea Tegeta sasahivi" Daniel alisema kwa sauti iliyosikiwa na wote.

***

Taa mbalimbali zilikuwa zinawaka ndani ya Ikulu ya Tanzania, iliyopo maeneo ya Posta, jijini Dar es salaam. Walinzi maalum wa rais, wenye silaha za kisasa walikuwa wanazunguka eneo hilo kuhakikisha usalama unaendelea kudumishwa ndani ya jengo.

Nje nako kulikuwa kumejaa walinzi lukuki wenye bunduki. Wakihakikisha kila kitu kinakaa mahali pake.

Katika chumba cha faragha cha Mheshimiwa rais, kulikuwa na watu wawili. Walinzi na wahudumu walitolewa nje, wakiwaacha watu wawili tu ndani ya chumba hiko.

Kilikuwa ni chumba kidogo chenye kila kitu ndani yake. Samani za ghali na za kisasa, friji ndogo pembeni iliyojaa matunda na kila aina ya sharubati, kompyuta ya bei, kutoka kampuni ya Apple mezani, air condition ikiyotoa hewa mujarab ukutani huku kabati dogo lililojaa mafaili mbalimbali likiwa pembeni konani mwa chumba hiko. Kilikuwa chumba kidogo lakini kilichopangiliwa vizuri sana. Chumba hiko kizuri kwasasa, sofa zake ghali na za kisasa zilikaliwa zimekaliwa na watu wawili tu..

Mheshimiwa Rais Mgaya na Mohammed Msangi.

"Safari hii mzee Msangi umeniangusha sana. Sikutegemea suala la kumpata Dr Louis litakuwa gumu na kuchukua muda mrefu namna hii?" Rais Mgaya alisema baada ya kusafisha koo lake kwa sharubati ya embe.

" Niombe tena msamaha kwa hilo Mheshimiwa Rais. Hili suala limekuwa tata na gumu. Yaani sijui hata nisemeje. Kama nilivyokwambia awali, Tulifanikiwa kumtia mikononi mwetu Dr Louis lakini yule kijana uliyetuletea kutoka kwa rais Abayo ndiye aliyeharibu kila kitu, alimteka Dr Louis na hadi sasa hatujui wapi amempeleka. Lakini sisi bado hatujakata tamaa, tunaendelea kumsaka Dr Louis hadi apatikane" Mzee Msangi alisema.

"Kusema kweli nimesikitishwa sana na kitendo alichokifanya huyo kijana. Nimemweleza Rais Abayo juu ya kitendo alichokifanya kijana wake. Naye amesikitishwa sana, na amesema atatusaidia kwa namna yoyote ile kuhakikisha tunampata Dr Louis pamoja na huyo kijana" Rais Mgaya alisema.

"Kwakuwa umemwambia rais Abayo haina shida, lakini nikuhakikishie tu sisi wenyewe tumejipanga vizuri, na nakuahidi tutampata Dr Louis" Mzee Msangi alisema kwa uhakika.

"Nakuamini sana Mzee Msangi. Ila kuchelewa kwenu kumpata Dr Louis ndo kunanipa mashaka. Sikudhami kama suala hili litachukua muda mrefu namna hii. Nimewaagiza wakuu wa usalama wafunge mipaka yote ya nchi kuhakikisha mnawakamata watu hao lakini bado majibu na yaleyale, bado bado!!.." Rais Mgaya alisema huku akigonga meza.

"Mheshimiwa rais usiwe na shaka. Hii ni ahadi yangu ya mwisho kwako. Nakuahidi nakuletea Dr Louis hapa" Mzee Msangi akameza mate. Kisha akauliza.

"Kwani kuna kitu gani cha siri kati yenu kinachokufanya umsake sana Dr Louis? Mimi ni mshirika wako na sidhani kama kutakuwa na ubaya wowote nikifahamu. Pengine itachochea msako wake" Mzee Msangi aliuliza swali.

Rais Mgaya alikaa kimya. Alimwangalia Mzee Msangi huku uso wake ukionesha hajapendezwa na swali hilo.

"Bila shaka kuna siri kubwa sana kati ya rais na Dr Louis. Na siri hiyo nikiijua kwangu itakuwa ni hela. Lazima nimsake Dr Louis kwa nguvu kubwa sana ili niitie mikononi mwangu siri hiyo! Siri ya kutengeneza mabilioni!" Dr Louis alijisemea kifuani.

"Mzee Msangi, sidhani kama sasahivi ni wakati sahihi wa kukwambia kwanini ninamsaka sana Dr Louis. Ipo siku nitakwambia sababu, na siku hiyo ni utakayoniletea Dr Louis mbele yangu" Rais Mgaya alisema.

Rais Mgaya na mzee Msangi waliongea kama muda wa robo saa, kisha wakaagana.

Mzee Msangi alipotoka tu nje, alimpigia simu Antony Kyando..

Je kuna siri gani kati ya Rais na Dr Louis?

Wakina Daniel watafanikiwa kumuokoa hannan?

Antony Kyando ni nani?
Ahsante sana angalau mchana umepita salama
 
HALFANI SUDY katika BOMU
Mawasiliano; 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Tisa

Wakina Daniel Mwaseba walikuwa wameshawasili Tegeta, au ili tupajue zaidi palikuwa panaitwa Tegeta Nyuki. Gari yao moja kwa moja ilipaki katika nyumba ambayo walielekezwa na Mwanasheria mlevi.

Kwa kutumia miguu, kutoka katika kiduka kidogo, mahali walipopaki gari yao, walifika katika nyumba aliyokuwemo Hannan Halfan. Walitumia dakika tatu kuichunguza nyumba hiyo. Kisha walijipanga vizuri kuvamia, nyumba ambayo walikuwa wameshaichunguza na kuona maeneo yote dhaifu ya kuwawezesha kuwaingiza ndani.

Walinzi wawili wenye silaha za moto walikuwa karibu na geti. Mmoja alikuwa amesimama karibu kabisa na geti huku mwengine alikuwa katiks kibanda kidogo kilichokuwa pembeni ya geti.

Mlinzi wa tatu alikuwa katika mlango wa kuingilia ndani wa nyumba hiyo. Alikuwa anaranda pale mlangoni, huku akiikumbatia bunduki yake.

Mlinzi wa nne alikuwa nyuma ya nyumba hiyo. Naye pia alikuwa na short gun machine mkononi.

Lakini walinzi hao wanne wenye silaha, hawakuwaogopesha hata kidogo wakina Daniel Mwaseba. Ingawa hawakujua ndani ya nyumba hiyo kuna walinzi wangapi.

Hofu ilikuwa maili nyingi sana katika mioyo yao..

Daniel Mwaseba na David walielekea m mbele ya geti la nyumba hiyo. Mahali ambapo waligundua kuwa kulikuwa na walinzi wawili.

Adrian Kaanan alizunguka nyuma ya nyumba hiyo, lengo ni kuhakikisha anaenda kumsambaratisha yule mlinzi mwenye short gun machine mkononi.

Wakati Martin Hisia alibaki ndani ya gari. Kuhakikisha eneo lote la nje linakuwa salama- salmin.

Kutokea upande wa mbele, Daniel Mwaseba aligonga geti kwa kutumia mkono wa kushoto.

Yule mlinzi aliyekuwa karibu na geti, alifungua mlango mdogo wa geti na kutoa kichwa chake kwa nje kumsikiliza mbisha hodi. Huku akiisahau bunduki yake ndani ya geti.

Mwenyewe alikuwa anajiamini, akiamini hakuna kitu kibaya kitakachotokea, lakini nikwambie tu nd'o lilikuwa kosa kubwa sana kuwahi kufanywa katika maisha yake.

Daniel alikuwa tayari amejipanga kwa kitendo hiko. Na pengine zaidi ya kitendo hiko...

Kwa kasi, aliikandamiza ile sura kwa kitambaa cheupe chenye unga mweupe alichokishika mkononi huku akimvutia kwa nje. Mlinzi aliburuzwa bila kupenda.

Yule mlinzi mwengine aliyekuwa katika kibanda karibu kabisa na geti akapatwa na shaka na mwenzake.

Alimshuhudia jinsi alivyoka nje katika namna ya ajabu!
Naye akiwa na silaha yake mkononi alielekea ule upande wa geti.

Wakati huohuo, Adrian Kaanan alikuwa amefanikiwa kwa siri kukwea ukuta mrefu wa ile nyumba na kujitosa ndani ya ile nyumba bila kutoa sauti yoyote ile.

Mlinzi aliyekuwa upande ule alikuwa ameugekia ukuta, akiupisha upepo huku akijarubu kuiwasha sigara yake.

Kwa mwendo wa kunyata, wa taratibu sana. Huku akihakikisha nyayo zake hazitoi ukelele wowote ule, Adrian Kaanan alikuwa anamsogelea yule mlinzi. Alipomkaribia kwa mita chache sana, mlinzi alihisi kitu. Aligeuka kwa kasi na bunduki yake mkononi.

Tayari kwa kumpasua mtu!

Lakini kwa bahati mbaya sana kwake, alikuwa amechelewa. Kisu kikali kilikita upande wake wa kushoto na kumdondosha chini akiisahau bunduki yake kwa muda. Mlinzi alitaka kutoa ukelele wa maumivu, lakini haukotoka.

Utatoka vipi?

Wakati Adrian alikuwa amemuwahi kwa kasi na kuubana kwa nguvu mdomo wa mlinzi kwa mkono wake wa kushoto.

Sauti ya mlinzi ilirudi tumboni kwake mwenyewe...

Kule kwa mbele, David alikumbana katikati ya mlango mdogo wa geti na yule mlinzi mwengine, kipindi ambacho Daniel akimsweka kichochoroni yule mlinzi mwengine aliyemvutisha unga uliomlalisha bila kupenda.

Teke la nguvu na kasi la David liliikwapua bunduki ya yule mlinzi na kuirudisha kule ndani ya geti. Mlinzi alijaribu kujitetea kwa mikono yake lakini ilikuwa ni kazi bure kwa David Ngocho.

Jamaa alikuwa ni mwamba msituni!

Kwanza alimvuta kwa nje kumtoa machoni kwa yule mlinzi aliyekuwa anarandaranda kule mlangoni kwa mbali.

Mpambano ulianza.

David alipangua kwa ustadi mkubwa sana kila pigo la yule mlinzi, aliyekuwa anarusha ngumi na mateke kwa pupa. Na yeye akipiga sehemu muhimu tu kila alipopata nafasi.

Walidumu katika mapigano ndani ya dakika mbili tu kabla ya yule mlinzi kulazwa chini. Damu zikimvuja puani na masikioni.

Alikuwa amekata moto!

Daniel Mwaseba aliungana na David na kujitosa ndani. Walikuwa wanaenda kwa umakini huku wakijificha katika maua mengi yaliyopandwa mle ndani. Hatimaye walifika. Walikuta Adrian ameshazunguka kwa mbele na kumpa pumziko la kudumu yule mlinzi aliyekuwa katika mlango wa mbele.
Sasa walikuwa wamevimaliza vikwazo vyote vya nje. Wakaingia ndani.

Walianza kukagua nyumba yote, huku wakitembea kwa umakini na silaha zao mikononi.

Hakukuwa na mlinzi yoyote yule mle ndani..Katika chumba cha mwisho kabisa upande wa kulia ndipo walipomkuta Hannan baada ya kuvunja mlango. Hannan alikuwa salama kabisa.

Lakini familia ya David haikuwemo mle ndani.

Walimchukua na kuondoka naye.

Hannan anaokolewa na kina Daniel, lakini familia ya David hawajaikuta, je itakuwa ipo wapi?

Wale wanayoitaka simulizi hii yote tuvumiliane kidogo, inarekebishwa ili usome kitu ambacho hutokuja kukisahau.
 
HALFANI SUDY anatusimulia BOMU


Whatsapp 0652 212391

Dakika ishirini na tano baadaye ndipo Anna, mfanyakazi wa nyumba aliyosekwa Hannan alirudi katika makazi yao. Alikuwa amebeba kapu kubwa la rangi ya kahawia mkononi, kapu lenye vitu mbalimbali. Alikuwa ametoka sokoni..

Alipigwa na bumbuwazi tangu akiwa mbali, mita kadhaa kutoka katoka getini, alienda na bumbuwazi lake hadi alipowasili.

Kuona geti la nyumba yao kuwa wazi haikuwa kawaida hata kidogo. Ile, ilikuwa ni nyumba maalum kwa kazi maalum. Umaalum huo haukuruhusu lile geti jeusi liwe wazi zaidi ya dakika tano.

Aliongeza kasi ya kutembea kuelekea getini, alipofika ndio alishuhudia unyama uliotendeka ndani ya nyumba yao.

Hakusubiri hata dakika moja. Ampigia simu Mzee Msangi kumtaarifu kilichotokea.

Wakati huo mzee Msangi alikuwa sebuleni kwa Antony Kyando, mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani hapa nchini, chama cha Tanzania People Party.

"Mambo bado magumu sana Mheshimiwa Mwenyekiti. Hadi sasa hatujafanikiwa kumpata Dr Luis atueleze hiyo siri tuisakayo. Ni Dr Luis pekee ndiye anayeweza kutuambia madhara ya kirusi DH+ baada ya kufanikisha kumpaka rais. Nilifanya jukumu la kumpaka, lakini sielewi kinatokea nini baada ya kumpaka kirusi cha DH+. Na hayo matokeo ndio siri tuitatayo." Mzee Msangi alisema.

"Lakini mzee Msangi, mwanzoni si ulisema mmefanikiwa kumpata Dr Louis na kumficha kitalu B huko Kigamboni? Sasa nini kilitokea huko? Au mlifanya kazi ya rais Mgaya badala ya kufanya kazi yangu?" Mwenyekiti Antony aliuliza huku akimwangalia mzee Msangi.

"Kama nilivyokwambia Mwenyekiti. Ni kweli tulimpata Dr Luis katika hoteli ya Dos Santos, lakini kwa bahati mbaya kuna mwenzetu mmoja alitusaliti kule kitalu B na kutoroka naye. Na nikwambie tu, hadi hivi sasa tupo katika harakati za kumtafuta huyo mwenzetu" Mzee Msangi alijitetea.

"Je, mlivyomkamata ulimdokeza kuhusu kututengeneza hiko kirusi cha DH+?" Antony aliuliza kwa shauku kubwa.

"Kazi ya kumhoji alipewa jasusu mmoja kutoka Nigeria, anaitwa Imma Ogbo. Ni miongoni mwa vijana aliopewa rais Mgaya kutoka kwa rais Abayo. Nilimdokeza Imma Ogbo amuulize Dr Luis kuhusu kirusi cha DH+. Unajua rais Mgaya hakutaka hata kidogo Dr Luis ahojiwe. Agizo lake lilikuwa ni kumteka na kumsubiri yeye arejee kutoka Nigetia. Hivyo ni mimi ndiye niliyefanya Dr Luis ahojiwe, na lengo lilikuwa tujue ana siri gani ya rais Mgaya? Pia tujue kuhusu kirusi DH+. Lakini sasa kabla hatujambana zaidi juu ya hiko kirusi, na kumwomba atutengenezee ndio akatoroshwa na Imma Ogbo baada ya kupishana kauli na mimi.." Mzee Msangi alisema.

Maneno hayo yalipenya katika masiko mawili ya Mwenyekiti Antony Kyando. Mwenyekiti alikaa kimya akitafakari. Huku akichambua kila neno la Mzee Msangi.

"Mwenyekiti, lakini kuna kitu kimoja kinaniumiza sana kichwa" Mzee Msangi alisema wakati Antony Kyando akiwa katika tafakuri.

"Kitu gani hiko?" Mzee Msangi aliuliza harakaharaka. Hakuwa na haja ya kuzama katika tafakuri wakati kulikuwa kuna cha kuuliza.

"Mimi, najua wewe sababu ya kumsaka Dr Luis kwa udi na ubani. Lengo ni kwaajili akutengenezee kirusi cha DH+. Lakini unadhani ni nini sababu ya Rais Mgaya kumsaka Dr Luis namna hii?" Mzee Msangi aliuliza swali ambalo alikuwa na jibu lake.

"Mzee Msangi, wewe ndiye mtu wa karibu sana na Mheshimiwa rais, nadhani mimi nd'o ningekuwa katika nafasi nzuri ya kuuliza hilo swali. Wakati wewe ndiye ungekuwa unajibu" Antony alikwepa kujibu.

"Nimeuliza hivyo kwasababu leo hii, nimejaribu sana kumdadisi Rais Mgaya, lakini hakuwa tayari hata kidogo kunambia siri hiyo" Mzee Msangi alisema.

"Basi hata mimi sifahamu..ninachojua mimi chanzo cha siri hii, ni matokeo ya kirusi cha DH+ uliyompaka akiwa amelala.." Antony alisema.

"Lakini Mwenyekiti, huoni fursa ya kutengeneza pesa nyingi sana kupitia hiyo sababu ya rais kumsaka Dr Luis? Ukimsikiliza kwa umakini mheshimiwa rais anavyoongea inaonesha kuwa kuna siri nzito sana kati yake na Dr Luis. Na siri hiyo tukiigundua inaweza ikawa dili la kupata pesa nyingi sana. Kwanini tusikazanie kuijua siri ya Mheshimiwa rais Mgaya kwake mwenyewe kuliko kupitia kwa Dr Luis ambaye imekuwa ni kitendawili kumkamata?" Mzee Msangi alisema.

Mwenyekiti Antony alikaa kimya. Akitafakari kwa umakini maneno ya mzee msangi.

"Umewaza sana Mzee Msangi. Na niseme tu umewaza kitu kikubwa sana Leo. Umeiona fursa adhimu sana. Lakini pamoja na kuijua hiyo siri ambayo wewe umeigeuza kuwa pesa, mimi ninakitaka kirusi chenyewe, nahitaji DH+ kiwe mikononi mwangu.." Antony alisema kwa hamasa.

"We cha nini kirusi DH+?" Mzee Msangi aliuliza.

Mwenyekiti Antony alikaa kimya. Aliinama chini akifikiri. Huku akicheza vidole vyake vya mkono wa kushoto.

Hakuhangaika hata kidogo kujibu swali la mzee Msangi.

Na hapo ndipo simu ya mzee Msangi iliita.

Simu ilikuwa inatoka kwa mfanyakazi wake, Anna.

***

Wakina Daniel Mwaseba walifika salama salmin wakiwa na Hannan nyumbani kwake Mikocheni.

Hapo ndipo walipopachagua pawe sehemu sahihi ya kupanga mikakati yao.
Ilikuwa ni nyumba kubwa ya kisasa, yenye kila kitu ndaniye.

Walikuwa wamekaa sebuleni. Kama kawaida wakipanga mipango yao. Huku wakimsubiri daktari kwa ajiri ya kuja kuiangalia afya ya Hannan. Ingawa kwa macho ya kawaida alionekana yupo fit.

"Tumefanikiwa kumwokoa Hannan. Zoezi limekuwa rahisi sana. Tumerudi wote salama, tena tukiwa na Hannan. Ni suala la kumshukuru Mungu sana.

Nini kifuatacho sasa?

Sasa ni zamu ya kwenda kuikoa familia ya David popote pale ilipo. Kwa damu au kwa jasho, lazima familia ya David tukaikoe, ili tumrejeshee furaha mwenzetu" Adrian alisema.

"Ni kweli Adrian. Hiyo ni kazi yetu ya pili baada ya kumwokoa Hannan.

Katika kazi hii tuna pa kuanzia pia. David alikuwa anatumiwa meseji na mtekaji wa familia yake. Tunaweza kum'track huyo mtu akiyetuma hizo meseji kwa David. Tukimjua tutajua nini cha kufanya.
David, hebu nipe namba ambazo akiyotumia huyo mtu kukupa maagizo yake" Daniel alisema.

Harakaharaka, David alipekua katika simu yake, na kumpa Daniel simu yake, ikionesha meseji mojawapo ya huyo mtu.

"Safi sana. Hii namba itatusaidia sana kuelekea mahali tunapopataka. Kama mnakumbuka Mwanasheria mlevi alisema namba hii imesajiliwa kwa majina ya Elia Kilasi. Sasa ni lazima tupige hatua nyingine mbele. Tumfamu vizuri huyo Elia Kilasi ni nani haswa?" Daniel alisema.

"Na uzuri leo hapa sebuleni tunaye Hannan. Kwa kiasi kikubwa sana atatusaidia kufumbua fumbo hili tata.

Fumbo la Elia Kilasi!!" Adrian alisema.

Watu wote pale sebuleni wakamwangalia Hannan. Ambaye alikuwa amekaa sofa la mwisho kabisa karibu na runinga. Alikuwa ndani ya suruali ya jeans iliyombana vyema, huku juu akivaa T-shirt ya bluu iliyoandikwa maandishi meusi katikati, neno likisomeka (FORCE).

"Laptop yangu waliichukua wale jamaa. Daniel kama una kompyuta ya ziada humu ndani nipe nianze kazi" Hannan alisema kwa kujiamini sana.

Daniel alitoka pale sebuleni na kwenda chumbani kwake. Alirudi kama baada ya dakika tatu, alikuwa amebeba tarakilishi nyeusi. Kwa nyuma ilisomeka Toshiba. Akamkabidhi Hannan.

sekunde ileile, Hannan aliiwasha ile tarakilishi. Akachomeka 'modem' iliyokuwa juu ya meza pale.

Ndani ya dakika thelathini na tano alizitumia kuingiza programs mbalimbali anazozijua yeye.

Kisha akaiomba ile namba ya Elia Kilasi.

Ukumbi mzima ulikuwa kimya, unamwangalia yeye. Kwa muda huu yeye ndiye alikuwa tumaini lao. Tumaini jipya. Tumaini la pekee.

Hannan aliingiza ile namba katika 'program' anayoijua yeye, tena kwa namna anayoijua yeye.
Akasema.

"Hii namba haipatikani kwa sasa, hivyo itakuwa ngumu kidogo kujua mahali alipo mmiliki wa namba hii.."

David alipiga kite cha ghadhabu.
Tumaini lililofufuka kwa kasi la kuipata familia yake lilipotea tena.

"Usihofu David, tutaiokoa tu familia yako. Hatujawahi kushindwa, siku zote sisi ni washindi" Daniel alisema kwa kujiamini.

"Hannan inamaana hakuna namna nyingine yoyote ya kuweza kupajua mahali alipo huyo Elia Kilasi?" Adrian aliuliza.

"Hivi kwanini tusiangalie uelekeo mwengine. Tumchunguze Mzee Msangi. Maana ni miongoni mwa watu waliowasiliana na Elia Kilasi? Tukimtia mikononi mwetu mzee Msangi atatuambia tu ana uhusiano gani na Elia Kilasi" Daniel alisema.

"Wazo zuri san Daniel, ila sasa changamoto nyingine ni, namba ya mzee Msangi tutaipata wapi?" Adrian aliuliza.

"Hii hapa nimeipata" Hannan alisema. Wote macho yao yakageuka kwa Hannan.

"Ni kweli Elia alikuwa anawasiliana na Mohammed Msangi mara kadhaa. Na hapa ndipo nilipoipata namba yake" Hannan alisema.

"Kazi nzuri sana Hannan, hebu i'track hiyo namba ya mzee Msangi. Tukamsangue" Daniel alisema.

Ukumbi mzima ulikaa kimya. Wote wakimsubiri Hannan afanye mambo yake. Ilikuwa inasikika sauti ya 'laptop' tu wakati ikibonyazwa na Hannan.

Je watampata mzee Msangi?

Riwaya hii itapatikana yote kwa njia ya whatsapp kesho..Gharama ni 3000 tu. Nikwambie tu hapo ni katikati ya riwaya hii ya kusisimua ya Bomu!!.. Mambo bado sana...
 
Simulizi nzuri Sana japo inakuwa fupi sijui ni kutokana na kunogewa Hadi naiona fupi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom