Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

sitakaa nikaamini kwamba victor pekee ndiye aliyekula njama, akaagiza bomu, na kulipua kanisa bila kumshirikisha mtu au watu wengine.

na sitaki kuanini kwamba vyombi cyetu vya ulinzi kwa zaidi ya wiki vimeshindwa kubaini waluoshirikiana na victor hata kama ni mapadre au masista

naelekea kuamini kwamba waliohusika wanajulikana na hawakamatwi na hawatakamatwa kwa kuwa vyombo " vimezuiwa" kufanya kazi yake.

sasa wajue hii ni mbaya ni kutoa nafasi ya kila mtu kuwaza lake na kama tutaendelea hivi kuna 'vichaa' wanaweza kuamua kuchukua sheria mikonon
 
Kuna kesi nyingi sana zimefunguliwa na baadaye huko mahakamani ikaonekana mtu hana hatia, akaachiliwa. Lwakatare aliwekwa ndani kwa 'kubambikiwa' kesi lakini ilichukua muda mrefu sana mpaka kufutiwa kesi ya ugaidi, na mpaka leo hii bado yuko ndani kwa shitaka moja.

Shitaka la ugaidi ni kubwa sana kutegemea ya kuwa ndani ya wiki moja serikali itakuwa imekusanya ushahidi wa kutosha kiasi cha 'kuwafungulia' waarabu hao. Ikumbukwe ya kwamba Tanzania ilipata mikikimikiki ya ugaidi wakati Ubalozi wa Marekani ulipolipuliwa na bomu mwezi Agosti 1998. Wakati dunia nzima inahangaika kutunga sheria za kupambana na matukio ya kigaidi, sisi mpaka leo hii hatuna sheria kali za uhakika isipokuwa za 'kusuka mikanda ya video'. Kushutumiwa kwa kesi ya ugaidi kungewezesha serikali kuwaweka ndani kwa muda mrefu ili kukusanya ushahidi wa kutosha, na kutoa fursa kwa vyombo vya sheria kuangalia uzito wa kesi yenyewe kwa upana wake. Sioni sahihi kama watanzania huhusan dereva wa 'bajaj' au bodaboda wanaendelea kushikiliwa huku raia wa kigeni wameachiwa 'eti kwa kukosekana ushahidi'. Kwa nini basi na hao watanzania wasiachiwe wote? Suala zima linaleta harufu ya kuwasafisha wenye pesa wageni (wafadhili) na kuwabambikizia kesi wazawa kwa kuwa uwezo wao kipesa ni mdogo.

Enzi za Mwalimu kulikuwa na Presidential Detention Act iliyokuwa inampa mamlaka Rais kumweka ndani mtuhumiwa kwa muda mrefu bila ya kumfungulia mashitaka ikiwa anashukiwa kuhatarisha usalama wa Taifa, ama kwa kuhujumu uchumi, siku hizi tunaita kufisadi. Sheria kama hii ingeweza kutungwa na kutumika kwenye masuala nyeti kama haya. Si lazima iwe kama ilivyokuwa mwanzoni, kwamba rais ndiye awe mwenye mamlaka, lakini hata mahakama ingeweza kupewa mamlaka ya kumweka ndani mtu anayeshukiwa kwa ugaidi kwa muda mrefu zaidi na kuendelea kutafuta ushahidi (kama upo).

Haiingii akilini mwangu kabisa... tunataka yatokee mangapi ndiyo tujue wabaya wetu ni kina nani? Kama ni kuwaachia basi wawaachie wote, tujue hatuna serikali wala jeshi la polisi la kutulinda sisi wanyonge!

uzi mreeefu kumbe pumba
 
Juzi kuna uzi humu ulituhabarisha ati kuna wasomi fulani waki inteligensia ati bomu lilirushwa na cia!

Kweli sometimes dini za kigeni zinatusababishia utaahila!
 
KIKWETE DHAIFU, HATUWEZI KUFIKA KWA MTINDO HUU.Wanawaogopa hao wa Saudia kwani watashindwa kuwasaidia waislamu wa Tanzania kuanzisha mahakama ya kadhi:argue::drum:
Ungemshukuru Kikwete na wanadiplomasia wake!

Jamaa wamekubali kutoa official version kuwa raia wao walikuwa karibu na tukio kinyume na ukweli kuwa wamekamatwa mpakani kitu ambacho kingeifanya Tanzania ionekana kuwa ni wabaguzi dhidi ya Waarabu na Waislamu na matokeo yake yasingekuwa mazuri kwa Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA MAENDELEO YA UPELELEZI WA TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI JIJINI ARUSHA LILILOTOKEA TAREHE 05/05/2013

Ndugu wanahabari, mtakumbuka kwamba mara ya mwisho nilipokutana nanyi niliwaahidi kwamba nitaendelea kuwapa mara kwa mara taarifa juu ta maendeleo ya upelelezi wa tukio la mlipuko wa bomu lililotokea katika kanisa katoliki la mtakatifu joseph mfanyakazi parokia ya olasiti tarehe 05/05/2013 na kusababisha vifo vya watu watatu(3) na wengine kudhaa kujeruhiwa.




Kama nilivyowaeleza hapo awali, baada ya tukio hilo jumla ya watuhumiwa tisa(9) walikamatwa na kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani. Watuhumiwa haoa ni victor Ambros Kalist, (20), dereva wa bodaboda na mkazi wa kwa Morombo; Yusuph Lomayani Josee (18) mwendesha bodaboda mkazi wa kwa Morombo na George Bathlomeo Silayo (23) mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti.




Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni raia watatu toka nchi za falme za kiaruabu (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme za kiarabu, Fouad Saleem Ahmed Al Hareez Al Mahri (29) mfanyakazi wa kikosi cha zimamoto katika Falme za Kiarabu, Saeed Abdulla Saad (28) askali polisikitengo cha traffic katika falme za Kiarabu, pamoja na raia mmoja wa Saudi Arabia Al-Mahri Saeed Mohseens (29)




Rai hao wa kigeni walikamatwa pamoja na wenyeji wao wawili ambao ni raia wa tanzania wenye asili ya Yemen. Majina ya watanzania hao ni Mohamed Suleiman Saad, (38) mkazi wa ilala jijini Dar es Salaam na Jasm Mubarak (29) mkaazi wa mtaa wa Bondeni jijini Arusha.


Uchunguzi wa kina uliofanywa na timu ya upelelezi ukihusisha taaasis nyingine za upelelezi FBI pamoja na INTERPOL kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani umebaini kuwa raia hao wanne wa kigeni hawakuhusika katika shambulio hilo.




Baada ya jalada la tukio hilo kufikishwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Arusha – divisheni ya mashtaka imeelekeza kuwa watuhumiwa hao wakabidhiwe ofisi za idara ya uhamiaji mkoa wa arusha ili kuona kama kuna taratibu zozote za kiuhamiaji ziikiukwa na wageni hao wakati walipoingia nchini ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa dhidi yao.




Pia ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali imeandaa mashitaka dhidi ya victor S/O Ambros kalisti na amefikishwa mahakamani leo kwa tuhuma za mauaji na kujaribu kuua. Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa waliosalia unaendelea kwa sasa tunao wataalamu kutoka kenya na Uganda ambao tunashirikiana nao katika upelelezi wa shauri hilo.




Aidha, hadi sasa idadi ya majeruhi wa tukio hilo la mlipuko wa bomu wanaoendelea kupata matatibabu katika hospitali mbalimbali ni 31 ambao kati yao 19 wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mount Meru arusha, 4 katika hospitali ya St. Elizabeth arusha na wengine 8 katika hospitali ya taifa muhimbili jijini dar es salaam na taarifa zinaonyesha hali zao zinaendelea kuimarika.




Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine wanaohusishwa na tukio hilo ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani pia jeshi la polisi linaendelea kuwaomba wananchi au raiayeyote mwenye taarifa zitakazowezesha kubaini mtandao wa kigaidi nawatuhumiwa wengine wanaohusika na tukio hilo wajitokeze na kuwasilisha taarifa hizo; tayari mkuu wa jeshi la polisi (IGP) amekwishaahidi zawadi nono ya Tshs. 50,000,000/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa hizo za siri kwa kukamatwa kwa watu hao.


ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA
LIBERATUSI SABAS – ACP
TAREHE 13/05/2013.


Nnaona jeshi la polisi na usalama wa nchi hii kwa ujumla MMEAMUA KUMTOA KAFARA VICTOR AMROS,kumbukeni maisha yake hayatapotea hivihivi lazima yatalipwa.
 
unategemea nini kama rais hakai na nchi zote ameshazitembelea imebaki za uarabuni lazima wangeachwa tu ili aende huko.

Mkuu usisahau kuwa hii nchi ya mazuzu so inaongozwa kizuzu ndio maana tumeuzwa pamoja na Twiga wetu.
 
Diversions za kisiasa..yeyote mwenye akili timamu alipaswa kujua tangu awali kwamba bomu halikua ugaidi wala udini..
YES Mdau...it was an Inside job! wamelipua wao wenyewe ili ajenda zao zizidi kuboreshwa! Mfumo.......at work. Waliomuua Padre Mushi wametangazwa mpaka sasa? Yes was an Inside job too! hizi si vurugu za kiimani... mfumo...at work. Nchi haitatawalika by Dr Slaa
 
Nchi haitatawalika yupo kazini na yatima Ambrose ndio Daraja lake.Au CCM wanataka kutawala milele.Moja kati ya haya mawili ni sahihi.
 
Aisee tumasubiri mtuambie alie husika, maana hatusikii Kama Victor mwendesha Bodaboda nae kaachiiwa. ndio aachiwe kwani na Yeye ilitokea tu akambeba abiria hadi kwenye eneo la tukio.

Victor wamempeleka Mahakamani na kumfungulia mashitaka 21 na ndiyo Mshtakiwa No.1, kwa hali hii tunakazi sana watanzania ya kujilinda wenyewe, Inatakiwa tujiulize ndani ya Nchi hii na huko Arusha kuna waarabu wangapi wageni? na je kwa nini walikamatwa hao tu na kama walikuwa ni washukiwa mbona wameachiwa mapema sana wakati tukio lililotokea ni kubwa?. KWA HALI ILIVYO SASA WATANZANIA UHAI WETU UNAUZWA KWA RASILIMALI ZETU
 
Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

2013-05-13 10:57

8b0d522b58b0486c96281c25914d1b53.jpg


Dubai - Three Emiratis arrested in Tanzania after a deadly attack on a church there a week ago have been freed and are back home, the Al-Khaleej daily reported on Monday.

Tanzanian authorities had arrested them "because they happened, by chance, to be at the site of the attack", the paper said, citing tweets of the United Arab Emirates foreign ministry.

The trio were released with the foreign ministry's help following "co-ordination between the UAE embassy and Tanzania", it said.

The report quoted "informed sources" as saying that the three Emiratis had returned home.

Saudi Arabia's foreign ministry announced Sunday that a Saudi citizen who had been arrested at the same time as the UAE nationals had been freed without charge.

The Saudi and the three Emiratis were arrested along with five Tanzanians after last Sunday's bombing, described by Tanzanian President Jakaya Kikwete as "an act of terrorism".

It was one of the worst such incidents to hit the east African country in years.

In addition to the three people killed in the blast, more than 60 people were injured when attackers hurled a bomb into the compound of the newly built Saint Joseph's Roman Catholic church.

The church was celebrating its inaugural mass at the time and was filled with worshippers.

- AFP

Mkuu hiyo picha ya JK uliyoiweka hapo juu kwa sisi watu wa kudadavua mambo inatupa ujumbe fulani juu ya kuachiwa hao jamaa na isitoshe juzi tu alikuwa kwa hao jamaa.
 
Diversions za kisiasa..yeyote mwenye akili timamu alipaswa kujua tangu awali kwamba bomu halikua ugaidi wala udini..

Hakika kaka, Gambaz zinatengeneza "Katiba mpya". Wanaofatilia mambo kwa mtindo wa "vikosi vya uzimaji moto" hawawezi ona hii janja.
 
Kwa kifupi ni kwamba wahusika wa bomu la Arusha walikakamatwa lakini order ikatoka ikulu wakaachiwa!!!!
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA MAENDELEO YA UPELELEZI WA TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI JIJINI ARUSHA LILILOTOKEA TAREHE 05/05/2013

Ndugu wanahabari, mtakumbuka kwamba mara ya mwisho nilipokutana nanyi niliwaahidi kwamba nitaendelea kuwapa mara kwa mara taarifa juu ta maendeleo ya upelelezi wa tukio la mlipuko wa bomu lililotokea katika kanisa katoliki la mtakatifu joseph mfanyakazi parokia ya olasiti tarehe 05/05/2013 na kusababisha vifo vya watu watatu(3) na wengine kudhaa kujeruhiwa.

Kama nilivyowaeleza hapo awali, baada ya tukio hilo jumla ya watuhumiwa tisa(9) walikamatwa na kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani. Watuhumiwa haoa ni victor Ambros Kalist, (20), dereva wa bodaboda na mkazi wa kwa Morombo; Yusuph Lomayani Josee (18) mwendesha bodaboda mkazi wa kwa Morombo na George Bathlomeo Silayo (23) mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti.

Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni raia watatu toka nchi za falme za kiaruabu (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme za kiarabu, Fouad Saleem Ahmed Al Hareez Al Mahri (29) mfanyakazi wa kikosi cha zimamoto katika Falme za Kiarabu, Saeed Abdulla Saad (28) askali polisikitengo cha traffic katika falme za Kiarabu, pamoja na raia mmoja wa Saudi Arabia Al-Mahri Saeed Mohseens (29)

Rai hao wa kigeni walikamatwa pamoja na wenyeji wao wawili ambao ni raia wa tanzania wenye asili ya Yemen. Majina ya watanzania hao ni Mohamed Suleiman Saad, (38) mkazi wa ilala jijini Dar es Salaam na Jasm Mubarak (29) mkaazi wa mtaa wa Bondeni jijini Arusha.

Uchunguzi wa kina uliofanywa na timu ya upelelezi ukihusisha taaasis nyingine za upelelezi FBI pamoja na INTERPOL kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani umebaini kuwa raia hao wanne wa kigeni hawakuhusika katika shambulio hilo.

Baada ya jalada la tukio hilo kufikishwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Arusha – divisheni ya mashtaka imeelekeza kuwa watuhumiwa hao wakabidhiwe ofisi za idara ya uhamiaji mkoa wa arusha ili kuona kama kuna taratibu zozote za kiuhamiaji ziikiukwa na wageni hao wakati walipoingia nchini ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Pia ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali imeandaa mashitaka dhidi ya victor S/O Ambros kalisti na amefikishwa mahakamani leo kwa tuhuma za mauaji na kujaribu kuua. Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa waliosalia unaendelea kwa sasa tunao wataalamu kutoka kenya na Uganda ambao tunashirikiana nao katika upelelezi wa shauri hilo.

Aidha, hadi sasa idadi ya majeruhi wa tukio hilo la mlipuko wa bomu wanaoendelea kupata matatibabu katika hospitali mbalimbali ni 31 ambao kati yao 19 wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mount Meru arusha, 4 katika hospitali ya St. Elizabeth arusha na wengine 8 katika hospitali ya taifa muhimbili jijini dar es salaam na taarifa zinaonyesha hali zao zinaendelea kuimarika.

Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine wanaohusishwa na tukio hilo ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani pia jeshi la polisi linaendelea kuwaomba wananchi au raiayeyote mwenye taarifa zitakazowezesha kubaini mtandao wa kigaidi nawatuhumiwa wengine wanaohusika na tukio hilo wajitokeze na kuwasilisha taarifa hizo; tayari mkuu wa jeshi la polisi (IGP) amekwishaahidi zawadi nono ya Tshs. 50,000,000/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa hizo za siri kwa kukamatwa kwa watu hao.


ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA
LIBERATUSI SABAS – ACP
TAREHE 13/05/2013.
 
Ngoma. Mzito but they aim to show efforts

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
kuna habari nilisoma sijui kama ilifika humu jamvini inasomeka kwamba balozi wa saudi nchini agoma kurudi Dar aamua kuweka kambi arusha mpaka ahakikishe watu wake wanaachiwa-naona yametimia

Hivyo ndivyo mabalozi wa nchi za wenzetu wanavyofanya kutetea raia wa nchi zao. Sasa wewe leo kamatwa nchi za nje kwa kosa la kusingiziwa halafu uone balozi wako kutoka tanzania atakavyokuruka na kukuacha unyanyaswe.
 
Jioni njema hutokea kukamata randomly; Mwezi jana kwenye tokeo la Boston Marathon bomu, Tangazo la kwanza kabisa wamerekaniUS na taaluma zote za kiintelijensia baada ya mripuko tu walitangaza eti Msaudi ndo mhusika na ni kijana mwanafunzi tumemkaribia kumweka nguvuni !! (hapo boston peke kuna wanafunzi zaidi ya elfu5 wa kisaudia) Looh,
Wakuu hao baadaye kupeleleza waka geuza kibao na kuomba radhi na kutoa taarifa ingine kuwa walotenda ni wa CHECHENIA/warussi. eti wanafanana, Sasa mambo kama haya yanatokea kukamata mtu katika " WRONG PLACE and WRONG TIME"...
Lakini tusubiri reporti ya FBI hao mababa riwaya yao ni nini? Hakuna siri itakayo fichwa milele!!
good luck.
unaweza kutuwekea hiyo ripoti inayoonyesha waliomba radhi?
 
Back
Top Bottom