Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

There are currently 2662 users browsing this thread. (76 members and 2586 guests).
Naamini watu wa usalama mnasoma sana humu JF. Tangu hii thread imeanzishwa hapa leo ninaamini wamepita wasomaji wengi na members wengi sana kwa siku ya leo, JF wana statistics. Hii inaonesha jinsi ambavyo watanzania wengi hawafurahishwi na jinsi mambo yanavyoendeshwa. Tukumbuke kuwa watu wengi sasa hivi wameelimika na si rahisi kukubali mambo ya danganya toto. Tafakarini!!! Sipati picha.
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA
logo_tpf.jpg
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA MAENDELEO YA UPELELEZI WA TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI JIJINI ARUSHA LILILOTOKEA TAREHE 05/05/2013
Ndugu wanahabari, mtakumbuka kwamba mara ya mwisho nilipokutana nanyi niliwaahidi kwamba nitaendelea kuwapa mara kwa mara taarifa juu ta maendeleo ya upelelezi wa tukio la mlipuko wa bomu lililotokea katika kanisa katoliki la mtakatifu joseph mfanyakazi parokia ya olasiti tarehe 05/05/2013 na kusababisha vifo vya watu watatu(3) na wengine kudhaa kujeruhiwa.Kama nilivyowaeleza hapo awali, baada ya tukio hilo jumla ya watuhumiwa tisa(9) walikamatwa na kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani. Watuhumiwa haoa ni victor Ambros Kalist, (20), dereva wa bodaboda na mkazi wa kwa Morombo; Yusuph Lomayani Josee (18) mwendesha bodaboda mkazi wa kwa Morombo na George Bathlomeo Silayo (23) mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti.Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni raia watatu toka nchi za falme za kiaruabu (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme za kiarabu, Fouad Saleem Ahmed Al Hareez Al Mahri (29) mfanyakazi wa kikosi cha zimamoto katika Falme za Kiarabu, Saeed Abdulla Saad (28) askali polisikitengo cha traffic katika falme za Kiarabu, pamoja na raia mmoja wa Saudi Arabia Al-Mahri Saeed Mohseens (29)Rai hao wa kigeni walikamatwa pamoja na wenyeji wao wawili ambao ni raia wa tanzania wenye asili ya Yemen. Majina ya watanzania hao ni Mohamed Suleiman Saad, (38) mkazi wa ilala jijini Dar es Salaam na Jasm Mubarak (29) mkaazi wa mtaa wa Bondeni jijini Arusha.Uchunguzi wa kina uliofanywa na timu ya upelelezi ukihusisha taaasis nyingine za upelelezi FBI pamoja na INTERPOL kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani umebaini kuwa raia hao wanne wa kigeni hawakuhusika katika shambulio hilo. Baada ya jalada la tukio hilo kufikishwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Arusha – divisheni ya mashtaka imeelekeza kuwa watuhumiwa hao wakabidhiwe ofisi za idara ya uhamiaji mkoa wa arusha ili kuona kama kuna taratibu zozote za kiuhamiaji ziikiukwa na wageni hao wakati walipoingia nchini ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa dhidi yao. Pia ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali imeandaa mashitaka dhidi ya victor S/O Ambros kalisti na amefikishwa mahakamani leo kwa tuhuma za mauaji na kujaribu kuua. Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa waliosalia unaendelea kwa sasa tunao wataalamu kutoka kenye na Uganda ambao tunashirikiana nao katika upelelezi wa shauri hilo.Aidha, hadi sasa idadi ya majeruhi wa tukio hilo la mlipuko wa bomu wanaoendelea kupata matatibabu katika hospitali mbalimbali ni 31 ambao kati yao 19 wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mount Meru arusha, 4 katika hospitali ya St. Elizabeth arusha na wengine 8 katika hospitali ya taifa muhimbili jijini dar es salaam na taarifa zinaonyesha hali zao zinaendelea kuimarika.Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine wanaohusishwa na tukio hilo ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani pia jeshi la polisi linaendelea kuwaomba wananchi au raiayeyote mwenye taarifa zitakazowezesha kubaini mtandao wa kigaidi nawatuhumiwa wengine wanaohusika na tukio hilo wajitokeze na kuwasilisha taarifa hizo; tayari mkuu wa jeshi la polisi (IGP) amekwishaahidi zawadi nono ya Tshs. 50,000,000/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa hizo za siri kwa kukamatwa kwa watu hao. ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA
LIBERATUSI SABAS – ACP
TAREHE 13/05/2013.
 
KIKWETE DHAIFU, HATUWEZI KUFIKA KWA MTINDO HUU.Wanawaogopa hao wa Saudia kwani watashindwa kuwasaidia waislamu wa Tanzania kuanzisha mahakama ya kadhi:argue::drum:

inaelekea uanaamini kila muarabu ni muislamu na kila muislamu ana asili ya uarabu, vipi na Ambrrose ni Mwarabu au muislamu?
 
Ni hatari sana kuhusisha LIWALO NA LIWE project na medani za kimataifa...
 
Udini hautaisha mpaka tutakapoitoa CCM madarakani.Kinara wa udini Nchini ni M/Kiti wa CCM Dr Jakaya Kikwete.by G.Lema.

NANI ASIYEJUA KUWA CDM NDIO WAASIS WA UDINI MPAKA MWENYEKITI WAO PADRI......SASA LABDA KAMA UMEPEWA NUSU KAPUTI HUNA FAHAMU NDIO UTAAMINI HIZO PROPAGANDA. PILI KAMA CCM NI WADINI NA MPAKA WATOLEWE BASI UDINI HUO HAUTAKWISHA MAANA PAMOJA NA PROPAGANDA ZENU ZOTE MITANDAONI CDM INAZIDI KUSHUKA HADHI.........tumegundua ndio wadini na wakabila wakuuu ni janga kwa taifa.
 
Inaelezwa wazi kuwa hao waarabu walikuwa at the wrong place at the wrong time.......cardinal pengo amesema anaushahidi kutoka kwawatu wakaribu yake na anao waamini kuwa sio shambulio la kidini kwa makusudi tu mnataka kupindisha ukweli, ambrose atamtaja tu aliemtuma nyie mnataka kupotosha si ajabu mnaujua ukweli. Maana arusha ndio makao yenu makuu.
 
...if the 3 Emiratis were released by TZ police....then how about those Tanzanians???...or does TZ police force want us to believe that all those Tanzanians held are guilty???....how about the guy who carried the bomber unknowingly??...

...why is diplomacy involved in matters of terrorism and security to the country???......

Since when did the TZ government lost its awareness that most terror attacks in Eastafrica (TZ inclusive)were coordinated from outside these countries??...

If TZ has released the foreigners...then this tells us citizens that this was a local religious attack....something this very government has been against...even Hon. Lema told them about this(and they ridiculed him).....now we are back to squire one.

I wonder how will the archbishop Pengo be feeling now!!! ....when he sees people being released before even being thoroughly investigated...just because they are foreigners...this is only in TZ....
 
Inawezekana kweli huyo Victor akapanga mpango wote yeye mwenyewe? Hii ni dhuluma kwa kweli
 
Bombing: Tanzania frees 3 Emiratis

2013-05-13 10:57

8b0d522b58b0486c96281c25914d1b53.jpg


Dubai - Three Emiratis arrested in Tanzania after a deadly attack on a church there a week ago have been freed and are back home, the Al-Khaleej daily reported on Monday.

Tanzanian authorities had arrested them "because they happened, by chance, to be at the site of the attack", the paper said, citing tweets of the United Arab Emirates foreign ministry.

The trio were released with the foreign ministry's help following "co-ordination between the UAE embassy and Tanzania", it said.

The report quoted "informed sources" as saying that the three Emiratis had returned home.

Saudi Arabia's foreign ministry announced Sunday that a Saudi citizen who had been arrested at the same time as the UAE nationals had been freed without charge.

The Saudi and the three Emiratis were arrested along with five Tanzanians after last Sunday's bombing, described by Tanzanian President Jakaya Kikwete as "an act of terrorism".

It was one of the worst such incidents to hit the east African country in years.

In addition to the three people killed in the blast, more than 60 people were injured when attackers hurled a bomb into the compound of the newly built Saint Joseph's Roman Catholic church.

The church was celebrating its inaugural mass at the time and was filled with worshippers.

- AFP

Movie nyengine hiyooooooooo,kama nchi nyengnie serikali inabidi iwalipe hao waliokamatwa bila hatia na kuachiwa ,hawa polisi wa Tanzania wana umbumbu gani hata wamkamate mtu,wamdhanie mtu kafanya kitu kwasababu tu wanatoka nchi fulani,kwanini wasifanye uchunguzi kabla hawajaamua kuwaweka ndani
 
Ni bora wamewaachia manake kuwashikilia watu bila kuwa na hatia ni kadhia kubwa. Ni vyema hata watanzania wenzetu walioshikiliwa waachiwe huru endapo kuna wasiohusika.

Ni imani yetu kuwa kila asiyehusika na tukio hilo ataachiwa huru mapema na wahusika wote wasakwe na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

Mungu ibariki Tz!
 
Huyo aliyeua padre huko Zanzibar ona tu JINSI anavyochekacheka ovyo mahakamani na anaongea kwa kiburi maana anajua hatafanyiwa chochote,Ilunga mmemficha wapi? ameongea maneno ya uchochezi weee badala ya kukamatwa akafichwa,Tatizo sio watz ni CCM na Serikali yake ambao waliwahi kuweka ahadi za kuwatimizia waislamu mpaka kwenye Ilani ya CHAMA chao,sasa CCM inahangaika na kujitahidi ku-BALANCE EQUITION,matokeo yake waislamu wachache walioamua kuwa MAGAIDI wanavuruga AMANI na Mshikamano wetu huku Viongozi wetu kwa kuwa ni Dhaifu wanaona yote hayo ni mema.
 
Chezea Mkulu kuahirisha ziara wewe???
 
:A S 103::argue:ACHENI KUJIFANYA HAMJUI KINACHOENDELEA, PENGO KASHASEMA ANAWAFAHAMU WALIPUAJI KWA MUJIBU WA TAARIFA ALIZOPEWA NA WATU WAKE WA ITELEGENSIA. HIVYO SUBIRINI IPO SIKU ATAWATAJA HADHARANI,:whoo:
 
Na bado kabisa hapo kwani Tanzania inatakiwa kuomba msamaha kwa kuchafua nchi hizo na raia wake lakin pia kulipa gharama zote za raia hao waliowekwa kizuizini bila kuwa na ushahidi wa kutosha ikiwa pamoja na kulipa gharama zote za kuchafua majina yao.

msifikiri huyo ni Shehe Ponda na watu wake wanawekwa ndani kunyimwa dhamana lakin hawana kosa bali ni mfumo tu wa nchi yenu unaowaendesha.
 
Tatizo wengi hawajui sharia wanafikiria UDINI tu.

Kumbukeni mahakama inataka ushahidi pasi na shaka ndio mtu anatiwa hatiani na sio bla bla za kidini au siasa inaweza kumfunga mtu.

kama mna ushahidi dhwahiri kuhusu watu hao pelekeni ili sharia ichukue mkondo wake.

Poleni sana kwa kusukumwa na UDINI katika haki za watu.
 
Mi nawashangaa wana jf.. just because ni waarabu basi ni lazima wawe magaidi na wafungwe..

Mlilia FBI wamekwenda na.Nina uhakika wameridhika hao jamaa hawakuhusika bado mnabwabwaja kulaumu serikali..

Kwa.standard za JF muendesha.bodaboda mkristo bwana Victor haiwezekani akahusika..

AMA kweli now days jf imejaa ma low thinkers ..
 
Mi nawashangaa wana jf.. just because ni waarabu basi ni lazima wawe magaidi na wafungwe..

Mlilia FBI wamekwenda na.Nina uhakika wameridhika hao jamaa hawakuhusika bado mnabwabwaja kulaumu serikali..

Kwa.standard za JF muendesha.bodaboda mkristo bwana Victor haiwezekani akahusika..

AMA kweli now days jf imejaa ma low thinkers ..
Hawa walikuwa ni watalii waliotoka ktk majeshi mbali mbali, zimamoto, trafiki na jeshi. Waliingia Tz kwa ndege ya Quartar tarehe 4 May, kisha wakamaliza utalii wao mara baada ya bomu kulipuka Olasiti. Waliamua kuondoka kwa barabara kupitia Kenya kurudi kwao Emirates. Mtu asiwasumbue wala kuwafikiri vibaya Waarabu wa watu. Hongera polisi kwa upelelezi wa kina.
 
ndugu zangu wanajamvi kwanza tujipeni pole kwa janga lililotukuta majuzi kanisani Arusha kwa kuwapoteza ndugu zetu pamoja na wengine kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili.Sasa niongelee hii aibu iliyolikumba taifa kwa ujumla wake, Polisi wetu ambao wanalipwa pesa kutokana na kodi zetu wamekuwa wazembe kupindukia kwa kufanya kazi kwa kukurupuka, kukamata watu bila ya kuwa na weledi wa wanachokifanya na kututangazia kwenye vyombo vya habari wamewakamata waarabu .leo wamewachia je?hiyo si aibu kwetu
 
Back
Top Bottom