Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

BODI YA MAZIWA Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!! Semina elekezi wiki 3 ARGENTINA (tiketi ya ndege=3,500 USD, malazi@200 USDx21days=4200USD , Per Diem x 21 days@420 USD=8820 USD) JUMLA KUU=16520 USD/pp. Hapo sijahesabia ada iliyotumwa moja kwa moja Chuoni/taasisi inayotoa mafunzo huko nje ya nchi. Nchi hii imeliwa haswaaa!!!
Kila lita ya maziwa unayokunywa wenyewe wanapata mgao. Na kuna siku ya maziwa ilizinduliwa kwa mbwembwe nyiiingi na mmoja wa watu mashuhuri na ilinishangaza sana tunaanzisha bodi ya maziwa na wanyama wana mazao mengi, sasa sijui tutaanzisha Bodi ya ngozi, Bodi ya Pembe, Bodi ya Nyama, Bodi ya Kwato na Makongoro, Bodi ya......... Hatari sana
 
Unaweza tafakari kwa nini kuna bodi ya KAHAWA, KOROSHO, PAMBA, SUKARI, nk?

Unajua kwamba maziwa ni zao litokanalo na mifugo na linahitaji kutafutiwa uwekezaji, masoko ya kutosha, na uhamasishaji wa watu kujikita ktk kufuga ng'ombe wa maziwa ili kuongeza uzalishaji ktk kutimiza mahitaji ya soko?

Hivi umewahi jiuliza kwa nini maziwa mengi yaliyosindikwq yanatoka nje ya nchi?

Maziwa kama yalivyo mazao mengine ni zao litokanalo na mifugo ambalo linahitaji uwekezaji mkubwa ili liweze kuzalisha ajira za kutosha. Ili kufikia kusudio hilo lazima kuwe na chombo cha kuratibu na kusimamia zao hilo nacho ni BODI YA MAZIWA

Tafakari kwa kina utaona umuhimu wa bodi kama hizi

Updates

Unafikiri kuna umuhimu wowote wa BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU? kwanini kazi hiyo isifanywe na WIZARA YA FEDHA kushirikiana na TCU na vyuo husika? je nao ni ufujaji wa fedha?

Endelea kutafakari
Je imefanya nn cha kujivunia, ndio tunajua hizo ni kazi zake ila wamefanya nn au ni kulipwa mpunga baasi
 
Hiyo bodi ipo siku nyingi sana, ukiona kitu kinaundiwa bodi ujue kinaulaji, ulishawahi kusikia kuna bodi ya mahindi, mpunga, mihogo, au viazi?
 
Bado Mabonde ya mito sasa... RUBADA, Bonde la mto kilombero, bonde la mto mara, yaani vurugu mechi
 
Bodi hii ama ivunjwe ama Iunganishwe TFDA au Bodi nyingine inayofanana na hiyo
 
Hizo ndizo hoja za kujenga (WAMEFANYA NINI?), lakini siyo kusema hawana umuhimu.
Wanaumuhimu mkubwa sana ila may be hawafanyi Yale yawapasaya kufanya na ndio maana zinaonekana kuwa hazima maana kuwepo ila kumbe tatizo c bodi ila ni watendaji maana km hawajui yawapasaya kufanya
 
Uzushi tu hizo bodi ni za kiupigaji tu
Bodi ya maziwa hiyo imefanya nini cha maana tangia ianzishwe.....
 
Nimestushwa na kukutana na gari STL pembeni imeandikwa BODI YA MAZIWA daah! hivi kweli tumefikia hatua ya kuunda BODI MAALUM Kwa ajili ya MAZIWA (naamini wanamaanisha haya maziwa ya KUNYWA kupitia mdomoni) hapo hapo tuna TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE (TFNC) nao wanapata bajet nenee!!

Mgao wa magari ya kutosha bila kusahau safari za nje ya nchi. Hapo hapo tuna TANZANIA FOOD & DRUGS AUTHORITY (TFDA) nao vile vile tiripu za nje kama kawa, VX za kutosha. Jamani tuoneeni huruma sisi walipa kodi maskini. TUMEROGWA??

Sekta ya maziwa ingekuwa active kwa maana ya uzalishaji Bodi kama regulator ingehitajika sana
 
Nimestushwa na kukutana na gari STL pembeni imeandikwa BODI YA MAZIWA daah! hivi kweli tumefikia hatua ya kuunda BODI MAALUM Kwa ajili ya MAZIWA (naamini wanamaanisha haya maziwa ya KUNYWA kupitia mdomoni) hapo hapo tuna TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE (TFNC) nao wanapata bajet nenee!!

Mgao wa magari ya kutosha bila kusahau safari za nje ya nchi. Hapo hapo tuna TANZANIA FOOD & DRUGS AUTHORITY (TFDA) nao vile vile tiripu za nje kama kawa, VX za kutosha. Jamani tuoneeni huruma sisi walipa kodi maskini. TUMEROGWA??

Sekta ya maziwa ingekuwa active kwa maana ya uzalishaji Bodi kama regulator ingehitajika sana
 
Bodi ya dagaa
Bodi ya nguruka
Bodi ya panadol
Bodi ya .........
Pendekeza bodi gan unataka ianzishwe maana hamna jinsi
 
Back
Top Bottom