Bodaboda sio salama kwa watoto wetu wadogo - Mzazi mjali mwanao, ukimpeleka shule mbali mlipie schoolbus au mpeleke na kumchua mwenyewe

mama D

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
19,760
35,205
Pamoja na wazazi wengi kuwasajili watoto wao shule za mbali na wanakoishi ili sababu ya ubora wa hizo shule ukweli ni kwamba wamekua wakiwatesa sana watoto wao.

Fikiria mtoto wa Dar es salaam anaishi pugu, gongo lamboto, kibamba, mbagala, toangoma halafu anasoma bunge primary, diamond au olympio. Huyu mtoto anaamka saa ngapi, anatoka nyumbani saa ngapi, anarudi nyumbani saa ngapi na analala masaa mangapi

Kwa wazazi ambao wanatumia au wameshawahi tumia public transport asubuhi na jioni wanaelewa jinsi vitoto vinavyokuaga vimechoka na kulala mwanzo wa safari hadi mwisho. Hivi kweli hii ina maslahi kwa mtoto au kwa mzazi?

Sasa heri hata hao wanaopanda daladala wakalala..... wapo ambao wanapandishwa bodaboda alfajiri na jioni. Tena bodaboda zenyewe hazipiti vichochoroni bali zinapita highways. Kwani lazima asome huko buana?

Wazazi tuwe na huruma na mapenzi kwa watoto wetu japo kidogo tuu. Ni hatari zaidi ya tunavyodhani jamani. Tuwatetee hawa viumbe wasioweza kujitetea

Msikilize huyu mzazi hapa ukiweza share na watu wako wa karibu wanaosafirisha watoto kwa bodaboda kuwakumbusha hatari iliyo kwa watoto wao.


 
Mafundi welding wanaweza kuitumia hii fursa kutengeneza vitu kama vile viti vya watoto kwenye magari. Hivi vikawa maalum kwa bodaboda tena viwe na mikanda.
 
Pamoja na wazazi wengi kuwasajili watoto wao shule za mbali na wanakoishi ili sababu ya ubora wa hizo shule ukweli ni kwamba wamekua wakiwatesa sana watoto wao.

Fikiria mtoto wa Dar es salaam anaishi pugu, gongo lamboto, kibamba, mbagala, toangoma halafu anasoma bunge primary, diamond au olympio.
Sasa hivi kuna ujinga umeenea wa watu kujifanya kjtafuta shule nzuri kuwapeleka watoto wao wakapate imu bora.

Huu ujinga mimi sifanyi,watu wamesoma shule ya kata wakajua kusoma na kuandika vizuri tu.

Mwanangu atasoma shule ya serikali lakini ataenda akiwa amwpata lishe bora ambayo nitainunua kwa pesa ambazo ningelipia school bus na vinginevyo.

Watoto wetu tuwaboreshee lishe na vitu vingine kama vile miundo mbinu mizuri ya kumkuza kiakili.

Watoto wasome shule za karibu aisee.

Kama una pesa mwanao hawezi kwenda shule na bodaboda,utakuwa ni mwenye pesa mjinga.
 
Mafundi welding wanaweza kuitumia hii fursa kutengeneza vitu kama vile viti vya watoto kwenye magari. Hivi vikawa maalum kwa bodaboda tena viwe na mikanda.
Bado sio salama mkuu.

Kwa nini mtoto asomw kwa tabu wakati kuna mambo mengi ya kumfundisha akiwa karibu na nyumbani.
 
Sasa hivi kuna ujinga umeenea wa watu kujifanya kjtafuta shule nzuri kuwapeleka watoto wao wakapate imu bora.

Huu ujinga mimi sifanyi,watu wamesoma shule ya kata wakajua kusoma na kuandika vizuri tu.

Mwanangu atasoma shule ya serikali lakini ataenda akiwa amwpata lishe bora ambayo nitainunua kwa pesa ambazo ningelipia school bus na vinginevyo.

Watoto wetu tuwaboreshee lishe na vitu vingine kama vile miundo mbinu mizuri ya kumkuza kiakili.

Watoto wasome shule za karibu aisee.

Kama una pesa mwanao hawezi kwenda shule na bodaboda,utakuwa ni mwenye pesa mjinga.

Kutafuta shule nzuri sio tatizo

Kutafuta shule nzuri bila kuzingatia usalama wa mtoto ndio tatizo.

Unapomtaftia mtoto shule ni muhimu kuzingatia umbali na athari zake kwenye muda wa kulala au kuamka kwa mtoto, usafiri wa kwenda na kurudi huko shule, changamoto anazoweza kutana nazo mtoto njiani na hata shuleni

Au mzazi ukiipenda shule sana tafuta nyumba karibu na hiyo shule ili watoto wako wasome kwa furaha
 
Kutafuta shule nzuri sio tatizo

Kutafuta shule nzuri bila kuzingatia usalama wa mtoto ndio tatizo.

Unapomtaftia mtoto shule ni muhimu kuzingatia umbali na athari zake kwenye muda wa kulala au kuamka kwa mtoto, usafiri wa kwenda na kurudi huko shule, changamoto anazoweza kutana nazo mtoto njiani na hata shuleni

Au mzazi ukiipenda shule sana tafuta nyumba karibu na hiyo shule ili watoto wako wasome kwa furaha
Ni sahihi uyasemayo.

Ndio maana nikasema watoto wangu watasoma shule za karibu.

Ishu ni umbali,mimi huwa nikitoka alfajiri msikitini saa kumi na moja alfajiri nakutana na watoto wa primary wanasubiri gari waende shule,wakati huo hapa mtaani kuna shule ya karibu ambayo mtoto wa mtaai kwa muda huo amelala na kuukuza ubongo na mwili wake.

Wabongo tumevamia eli.u
 
Ni sahihi uyasemayo.

Ndio maana nikasema watoto wangu watasoma shule za karibu.

Ishu ni umbali,mimi huwa nikitoka alfajiri msikitini saa kumi na moja alfajiri nakutana na watoto wa primary wanasubiri gari waende shule,wakati huo hapa mtaani kuna shule ya karibu ambayo mtoto wa mtaai kwa muda huo amelala na kuukuza ubongo na mwili wake.

Wabongo tumevamia eli.u

Imagine🤔🤔🤔

Watoto wanateseka hadi unajiuliza hivi ni kweli Mungu aliwabariki wazazi watoto na pesa ili watoto wapokonywe haki zao?
 
Pamoja na wazazi wengi kuwasajili watoto wao shule za mbali na wanakoishi ili sababu ya ubora wa hizo shule ukweli ni kwamba wamekua wakiwatesa sana watoto wao.


View attachment 1962688

Wazazi wenye tabia hii.wote wanatoka uswahilini .

Uswahilini wanapenda sifa wakisikia mwanae sijui yupo muhimbili primary,bunge,olympio au maeneo ambayo yako mbali na makazi.

Mtoto makazi manzese shule ya msingi msimbazi.

Mtoto makazi buguruni shule ya msingi mugabe sinza
 
Hayo yote ni matatizo ya umaskini uliokithiri, baada ya miaka 60 ya uhuru serikali ilipaswa kuhakikisha watoto wote mijini na vijijini wanasoma katika mazingira bora. Wana usafiri mzuri badala ya lifti za bodaboda na daladala.
Pamoja na wazazi wengi kuwasajili watoto wao shule za mbali na wanakoishi ili sababu ya ubora wa hizo shule ukweli ni kwamba wamekua wakiwatesa sana watoto wao.


View attachment 1962688
 
Hayo yote ni matatizo ya umaskini uliokithiri, baada ya miaka 60 ya uhuru serikali ilipaswa kuhakikisha watoto wote mijini na vijijini wanasoma katika mazingira bora. Wana usafiri mzuri badala ya lifti za bodaboda na daladala.

Sijui unaongelea umaskini upi, labda umaskini wa akili ila sio mali wala pesa.

Maskini aliyekithiri hawezi mtoa binti yake Pugu au Mbezi mwisho na bodaboda kwenda kumsomesha bunge primary, diamond, muhimbili au Olympio. Tena pesa ya kutumia mchana anampa elfu3

Mbezi, gongolamboto, pugu, mbagala, tabata sio vijijini na shule zipo nyingi tuu huko kama zile nilizosoma mimi, na wewe kama ulijaliwa

Lift za bodaboda??? Umesoma post vizuri au ndio vile unasomaga bila kuelewa!!?? Yaani dreva wa bodaboda aamke saa11 kwenda kumpa mtoto wa mtu lift!? Tena zaidi ya km10!? Jiongezage buana
 
Back
Top Bottom