Binti afia gesti,Kinondoni!!!

Binti afia gesti,Kinondoni!!!

mhhh inauma.polisi kama wakitumia forensic evidence watampata tu hana ujanja,kama gest zingekuwa na CCTV ingekuwa poa zaidi,wadada msikubali kupelekwa uchochoroni na mtu ambae humwamini.
 
Niltaka kwenda ghouse kumbe yanayojiri haya wala ht cendi tena nimegairi roho yangu icje acha mwili.cku hz ht wanawake wanatoa za wanaume
 
"..Oh Lord please help me to forgive those who SIN differently than I.."

RIP Young Lady...
 
Hatua za kufanya

1) Kwanza achunguzwe kama ana jeraha lolote mwilini
2) Pili apimwe alitumia chakula/kinywaji gani mara ya mwisho
3) Kitambuliwe chochote alichoacha mwanaume kabla ya kuondoka (vitumike kumtambua mwanaume na kwanini alidanganya kwamba anaenda kununua chakula)
4) Kitambulisho kitumike kujua anapokaa na anaposoma then kujua alikutana na nani mara ya mwisho mbali na mwanaume



Katika ideal situation, ndivyo inavyotakiwa. Lakini na mapolisi wetu, na rais, mfano hao wa gesti, si ajabu wamekwisha haribu evidence za hapo.

R.I.P Dada Mwanafunzi
 
Bongo kila aina ya tukio utalisikia; MAUAJI YA ALBINO, VICHANGA KADHAA VYAFUKIWA KWENYE SHIMO LA TAKA, VIKONGWE WAUAWA, MABOMU YALIPUKA NA KUUA/KUJERUHI KADHAA, BINTI AFIA GUEST HOUSE, POLISI WAPIGA RISASI WAANDAMANAJI, VIBAKA WAVAMIA RAIA, MGAWO WA UMEME USIOKUWA NA MWISHO........ na mengineyo mengi

Kama yote haya yanatokea ndani ya Nchi yetu, mbona kila siku viongozi wetu wanaimba kuwa Tanzania ni kisiwa cha amani?
 
OMG.
So sorry to her boyfriend ambae wenda hakuwa anajua Mpenziwe alipo, Parents, Kwa Taifa kupoteza msomi, kwa watanzania walipa kodi....................Dah
 
RIP

But ningependa kuwaasa kizazi cha sasa (wale ambao bado mnatongozwa) Si kila mtongozaji anania njema na wewe.........wengine vibaka, wengine washirikina wametumwa nyweke ya mwanamke ili wapate utajiri, wengine maserial kilaz so be careful

Well said MJ1,
RIP
 
Maskinini msichana wa watu amefariki kwa aibu sijui ndugu zake watakuwa wanamkumbuka kwa hilo au watamkumbuka kwa mema pia aliyoyafanya. historia mbaya sana
 
arest inpeace... Ila papara zetu zinatuponza..
 
Jaman hizi nyumba za wenyeji nazo. poleni wafiwa
 
Dah! Hali ni mbaya.
Watu wana roho mbaya utafikiri wanakaanga sumu.
RIP binti.
 
Bado namfikiria huyu binti maskini?? sijui anasoma wapi
 
Hapo Benjamin Mkapa Tower, kuna msichana alirushwa na Mzungu , lakini Mzungu akahonga wahudumu wa hotel ya paradise ,ikaonekana haijulikani huyo demu alifikaje humo hotelini, ilasemekana demua likuwa na huyo mzungu na alitaka kumuibia hela mzungu ndio akagundua na kumrusha dirishani.

Police wamekaa kimya hadi leo.

R.I.P
 
Hapo Benjamin Mkapa Tower, kuna msichana alirushwa na Mzungu , lakini Mzungu akahonga wahudumu wa hotel ya paradise ,ikaonekana haijulikani huyo demu alifikaje humo hotelini,ilasemekana demua likuwa na huyo mzungu na alitaka kumuibia hela mzungu ndio akagundua na kumrusha dirishani.Police wamekaa kimya hadi leo.

R.I.P

Duh kumbe haya mambo yapo na yanaendelea kutokea kwa sana
 
nakumbuka kuna siku mchungaji wangu alinifundisha somo liitwalo " tambua hila za adui shetani" moja wapo ni usinzi, vijana inabidi tubadilike, for real inahuzunisha sana, tena kwa kifo alichokufa na mahali alipofia!!

Mungu ilaze roho ya Amina mahali pema peponi!! Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe!!
 
Msichana mmoja [Jina tunalihifadhi] mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Ubungo Islamic amekutwa amefariki ndani ya gesti jijini Dar es Salaam.
Msichana huyo jina kapuni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Ubungo Islamic alikutwa amefariki ndani ya gesti ya Mkomboni iliyopo kata ya Hananasif, Kinondoni.

Kwa mujibu wa wahudumu wa gesti hiyo, msichana huyo aliingia ndani ya gesti hiyo akiwa na mwanaume ambaye siku tatu zilizopita aliingiza wanawake wawili tofauti ndani ya gesti hiyo.

Mmoja wa wahudumu akimuelezea mwanaume aliyekuwa na mwanafunzi huyo alisema kuwa mwanaume huyo siku tatu zilizopita alikuja na mwanamke mmoja katika gesti hiyo na kuchukua chumba namba 4, baada ya lisaa limoja mwanamke huyo alisikika akilia kwa uchungu huku akidai kurudisha pesa zake.

Siku iliyofuatia mwanaume huyo alikuja na mwanamke mwingine tofauti na kuchukua chumba namba 6 na ndani ya masaa mawili mwanamke huyo alitoka huku akilia akisema mwanaume huyo kamfanyia kitu kibaya ndio maana kaamua kumkimbia.

Jana mwanaume huyo ndipo alipotinga tena kwenye gesti hiyo akiwa na mwanafunzi huyo wa kike kwenye majira ya saa tisa mchana.

"Kwenye majira ya saa kumi tulisikia mlio kwa ndani lakini hatukufuatilia
kwa sababu tulijua ni mambo ya mapenzi lakini kadri muda ulivyozidi ndipo sauti ile ilikuwa ikipotea baadaye yule jamaa alitoka na kuondoka sisi tukijua kuwa labda wameondoka wote tulivyo kwenda kutaka kufanya usafi tulimkuta binti huyo kalala kama amekufa", alisema mmoja wa wahudumu wa gesti hiyo.

Mhudumu huyo alitoa taarifa katika kituo cha polisi cha Oysterbay na walipofika walimkagua na kukuta vitambulisho vya binti huyo lakini katika mkoba wake hakukuwa na simu wala pesa.

Taarifa zilizopatikana baadae zilidai kuwa mwanafunzi huyo ameiaga dunia.
picha zaidi gonga hapa chini
NIFAHAMISHE .: PHOTO GALLERY :.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom