Bingwa wa Kutuma salamu?

Bingwa wa Kutuma salamu?

kuna kipindi clouds cha dj elly saa kumi za usiku eti watu wanatuma salamu cha kushangaza wana salimiana wenyewe kwa wenyewe
 
kwaio mkuu unaweza kaaga kwenye redio all day long kusubiri uskie ukisalimiwa?
Hapana, simaanishi hivyo mkuu.
Inapotokea bahati nasikiliza redio na Mara wakatuma salami huwa sisiti kuendelea kusikiliza.

Maana kwa kusikiliza huko hunikumbusha ndugu,jamaa na marafiki zangu ambao hatujaonana au kusalimiana muda mrefu.
 
kabisa wanakera sana afu haya mambo ya kutumiana salamu radioni yapo afrika tu! huu m_bara wetu bhana dah! sjui nani kaanzisha huu utoto
Usipende kuonyesha upumbavu wako kwenye hadhara, kama haujui jambo nibora ukalikalia kimya na upite polepole
 
Binafsi naona sio tatizo.. anaejiona anasimu yenye uwezo asidhani wote wanazo simu za dizai hii..
Hivyo watangazaji wanavyotoa fursa ya kutuma salama
 
-Na wao wanakushangaa kula chakula cha jioni mtaani wakati nyumbani kwako kuna chakula.
-Na wao wanakushangaa kwenda kuangalia mpira baa tena kwa kulipia wakati nyumbani una TV inaonyesha mechi hiyohiyo

**Mambo mengi tunayafanya kwa kujifurahisha ili kuondoa msongo wa mawazo ya kungojea viwanda****
 
Utoto huo ndo unauona Leo!!
Sisi waafrika, bado kuna vitu vya kipekee kwetu ambavyo vitaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia hii.
Kutuma salamu redioni ni moja ya desturi zetu waafrika tangu enzi na enzi.
Huyu mpuuzi haja tembea tu aiseeee......
 
UKISIKILIZA RADIO ONE KUANZIA SAA SABA HADI SAA 12 NDIO UTACHEKA NA WENGI NI KUTOKA KANDA YA ZIWA. KUTUMA SALAMU NI JAMBO JEMA TUU HALINA TATIZO.
 
kuna kipindi clouds cha dj elly saa kumi za usiku eti watu wanatuma salamu cha kushangaza wana salimiana wenyewe kwa wenyewe
Nawe huwasikiliza?
Wa join kwa maana hamna mbaya, ni salamu tu!

Au ulitaka muda huo watangaze taarifa ya habari ya kupanda kwa bei ya sukari.
 
Natuna salamu kwa mods wote wa jf, bila kumsahau bibi wa jf faiza fox. Ujumbe, popote alipo maleria sugu ajue jukwaa la siasa lime mmiss
 
Kila jambo lina wakati wake mkuu...
Kipindi kile hiyo ndio ilikua fashion, na ili kuonekana mjanja kwenye jamii inayo kuzunguka kwamba umesikika redioni.
Siku zile watu wengi hawakua na simu pia teknolojia haikua juu kama leo hii.
Wewe unaona kama ni ushamba kwakua tu, umebahatika kukua kipindi ambacho teknolojia ime tamalaki.
nazan anamanisha kutuma salam kwa kipind iki ambacho meanz za kuwasiliana zipo nying ...masimu kibao bei cheeeee...still mtu anatuma salam na vipind ivyo baadhi ya redio bado vipo
 
natuma salamu kwa shangazi aliyepo hapa nyumbani,pili kwa dada angu tupo nae hapa na tatu kwangu mimi mwenyewe....!!!
 
Nawe huwasikiliza?
Wa join kwa maana hamna mbaya, ni salamu tu!

Au ulitaka muda huo watangaze taarifa ya habari ya kupanda kwa bei ya sukari.
yaani kweli unaamka saa kumi za usiku kucheza kidali poo cha salamu? SMFH
 
Anasema hajasahau kufungua tovuti ya Radio China kimataifa, na habari anazozikuta zimekuwa kama
nyota kwake. Kwa yote anasema hongera kwa CRI. Anasema ana hakika ya kwamba kituo chetu ni kituo pekee, na hadhani kama kuna kituo
kingine kinachotilia maanani haswa
kuwasiliana na wasikilizaji wake kama
ya Radio China kimataifa.
 
hahahhhaa Don nakuunga mkonyo kabisa. ni ushamba na kuppoteza muda tu.mi sisikilizagi redio sasa ukintumia salamu halafu hainifikii maana ake nini?
Ushamba ni nini na umjini ni nini? Sisikilizagi ni Ushamba au ni umjini? Ukintumia ni Ushamba au ni umjini? Bora kuwa mshamba kuliko kuwa limbukeni.
 
kuna kipindi clouds cha dj elly saa kumi za usiku eti watu wanatuma salamu cha kushangaza wana salimiana wenyewe kwa wenyewe
Saa kumi usiku ulikuwa unafanya nini? Ulijuaje usiku huo Kuna kipindi clouds cha dj elly watu wanatumiana salamu.
Wewe kelvin x na dj elly nani mjuzi wa mambo?
 
nazan anamanisha kutuma salam kwa kipind iki ambacho meanz za kuwasiliana zipo nying ...masimu kibao bei cheeeee...still mtu anatuma salam na vipind ivyo baadhi ya redio bado vipo
Radio station zote Kuna vipindi vya salamu.
Zamani radio zilitumia post card na barua. Lakini sasa njia rahisi na haraka ni simu na viunganisho vyake (sms, whatsap nk).
 
Back
Top Bottom