Bingwa wa Kutuma salamu?

Bingwa wa Kutuma salamu?

James Kasonda

Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
84
Reaction score
49
Zamani sana kabla teknolojia haijasonga kama ilivyo leo, kumtumia mtu salamu ilikuwa kazi kweli kweli. Aidha uandike barua (ambayo itachukua wiki nzima kumfikia mlengwa), au utume salamu kwa njia ya simu ya mezani (wenye nazo walikuwa wachache kweli kweli) au utume salamu kwa njia ya Redio na wakati huo kulikuwa na kituo kimoja tu cha Redio.
Sasa hivi kumtumia mtu salamu hata dakika haipiti. Ninachoshangaa ni kwamba bado kuna watu wanapata tabu sana kutuma sms au kupiga simu kwenye vituo vya Redio eti kutumia salamu rafiki zao. Swali ni kwamba wanataka kutuma salamu kweli au wanataka wasikike tu hewani? Mtu anahangaika saa nzima kutafuta line!! Kwa nini asipige tu simu moja kwa moja kwa hao rafiki zake? Naomba kutoa hoja.
 
sioni tatizo lolote kwa watu kutuma salamu kwa njia ya redio, kwanza ni ishara ya mshikamano kama taifa,amani, kujenga upendo na utani,pia ni njia moja ya kueneza lugha, ni utamaduni mzuri

pia mtoa kioja kumbuka watuma salamu wa redioni si lazima mfahamiene ila mnaweza kutumiana salamu mkafahamiana na kujenga fursa za maisha nje ya salamu
 
kabisa wanakera sana afu haya mambo ya kutumiana salamu radioni yapo afrika tu! huu m_bara wetu bhana dah! sjui nani kaanzisha huu utoto
 
Si kila mtu anamiliki smartphone au ana uwezo wa kuwa na salio daily.

Binafsi sins tatizo na kutuma au kutumiwa salami redioni. Hata kama salami hizo hazinihusu.

Huwa inasaidia kuleta ukaribu,kufahamiana, na kuongeza ushawishi wa kuwakumbuka watu wako.

I think it' s a matter of attitude.
 
hahahhhaa Don nakuunga mkonyo kabisa. ni ushamba na kuppoteza muda tu.mi sisikilizagi redio sasa ukintumia salamu halafu hainifikii maana ake nini?
 
Si kila mtu anamiliki smartphone au ana uwezo wa kuwa na salio daily.

Binafsi sins tatizo na kutuma au kutumiwa salami redioni. Hata kama salami hizo hazinihusu.

Huwa inasaidia kuleta ukaribu,kufahamiana, na kuongeza ushawishi wa kuwakumbuka watu wako.

I think it' s a matter of attitude.
kwaio mkuu unaweza kaaga kwenye redio all day long kusubiri uskie ukisalimiwa?
 
Hivi ni kwanini usimtumiane hizo salamu kwa SMS au whatsapp..?
Kila jambo lina wakati wake mkuu...
Kipindi kile hiyo ndio ilikua fashion, na ili kuonekana mjanja kwenye jamii inayo kuzunguka kwamba umesikika redioni.
Siku zile watu wengi hawakua na simu pia teknolojia haikua juu kama leo hii.
Wewe unaona kama ni ushamba kwakua tu, umebahatika kukua kipindi ambacho teknolojia ime tamalaki.
 
kabisa wanakera sana afu haya mambo ya kutumiana salamu radioni yapo afrika tu! huu m_bara wetu bhana dah! sjui nani kaanzisha huu utoto
Utoto huo ndo unauona Leo!!
Sisi waafrika, bado kuna vitu vya kipekee kwetu ambavyo vitaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia hii.
Kutuma salamu redioni ni moja ya desturi zetu waafrika tangu enzi na enzi.
 
Back
Top Bottom