Heshima sana wakuu,
Issue ya Bwana Lema Mkurugenzi wa kampuni ya NEWL & Elerai Construction katika hii kesi nadhani ipo kishinikizo zaidi kuliko kisheria.
Bwana Lema alikuwa akifanya biashara na Mohamed Mustafa kwa muda mrefu kidogo.Mohamed Mustafa alikuwa akimuuzia Lema bidhaa mbali mbali kupitia kampuni zake alizosajili nyingi zikiwa za uongo (fake campany) zikiwa na TIN & VRN ambazo zote zinatolewa na TRA usajili wa kampuni unafanywa na BRELA.Baadhi ya bidhaa amabazo Mohamed aliuzia NEWL ni pamoja na filter za generators zilizoko kwenye minara ya simu cement na nondo aliuza Elerai amabayo ilikuwa na tender ya kujenga ofisi za mkuu wa mkoa Manyara na ofisi nyingi za serekali hasa wilaya na mikoa mipya.
Kwa upeo wangu sidhani kama ilikuwa sahihi kumuunganisha Bwana Lema na kampuni fake za Mohamed kwasababu zifuatazo.
Kampuni za Lema yaani Elerai & NEWL zilikuwa zikinunua huduma / bidhaa kutoka kwa kampuni za Mohamed baadhi zilikuwa na usajili na nyingine zilikuwa na usajili wa magumashi lakini zote zilikuwa na VRN,TIN,Clearance Certificates,Certificate of Incorporation na leseni za biashara.Mwisho wa mwezi wahasibu walikuwa wakitumia invoices za kampuni za Moahamed to claims VAT utshangaa wakiingiza VRN kwenye system inakubaliwa ?.
Hivi ukienda dukani kununua bidhaa ukakuta leseni fake,tin fake.... kosa linakuwa kwa mnunuzi au muuzaji ?.Nadhani mnunuzi hayuko katika nafasi nzuri ya kugundua iwapo sehemu anayonunua bidhaa au huduma kuna tatizo la kisheria.
Nadhani vyombo vyetu vya sheria vingi vinafanya kazi kwa hofu,kujionyesha..... lakini mwisho wa siku wakienda mbele ya sheria wanajikuta wanashindwa kwakuwa mara nyngi hawafanyi utafiti wa kutosha na kujiridhisha kabla ya kupeleka kesi mahakamani.