Bila tija mshahara usiongezwe serikalini

Bila tija mshahara usiongezwe serikalini

Nina mashka na elimu yako na uwezo wako wa kufikiri...ukijua vitu vinavyochangia utendaji kazi wenye tija wala usingeandika upuuzi huu
 
Watumishi wa umma ni wavivu, wamekosa ubunifu na bado wanalilia mshahara uongezwe Mei Mosi. Nashauri pasiongezwe hata senti mpaka pathibitishwe kuongezeka kwa tija, tuwapime mpaka 2019 labda.


Huu uandishi sio wa bwana yule kweli?
 
nia yako ni kumchonganisha mkulu na wafanyakazi kitu ambacho ni hatarikwa ustawi wa ccm 2020
 
hiyo pesa badala ya kuwaongezea watumishi tutawapelekea hao walala hoi direct .....watumishi hawa hawa mwisho wa mwezi wakipata mishahara wanashinda bar kunywa pombe?
Kwanini ulitoroka mirembe? Leo umetumia dawa?
 
We jamaa sijui unatumia sehemu gani ya mwili wako kufikiri!!
Kwa hali hii ya uchumi,mfumuko wa bei, unatarajia tija ndio mshahara uongezwe?
Acheni kutafuta nafasi serikalini kwa kujipendekeza kwa Mkuu kwa mawazo mgando kiasi hiki,mshaurini mkuu ainusuru nji hii kwa kuongeza mishahara angalau kwa 50%,ili wajomba zako na mashangazi warejeshewe uhai
Anatumia papuchi Mkuu
 
Jamaa yangu unanifurahisha sana uzuri wewe umesoma social issues tena kwa kiwango kizuri tu cha *******,management pia uliyo soma inakusaidiaje jamaa yangu *****ry?? Swala la utumishi lina mambo mengi sana ,ubora wa kazi una mambo mengi sana tena sana ukiachilia mbali kazi za kitumwa ambazo ni za lazima ufanye hata bila malipo, nadhan ungeanza na kutoa maelezo vizuri kwa utaalamu wako kitaalamu maana hapo hicho ulicho andika inaonekana kama umeandika kisiasa na kutafuta kuungwa mkono na watu wa upande wa sifa na kusifiwa.
Mbona unammbembeleza huyu mtoro wa mirembe na hata alichoandika ndio mwisho wake wa kufikiri. Usitegemee makubwa
 
Ni Kweli huyu ana chuki binafsi na watumishi wa umma kwani mtumishi SAA nane zote anakua kazini kwa kungoja alipwe mwisho wa mwezi tofauti na mfanyabiashara au wengineo. Pili mshahara ukiongezeka hata mzunguko wa hela huongezeka.
 
Kuna umaskini wa roho na umaskini wa kipato. nauogopa sana umaskni wa roho. mtoa post (kwa mtazamo wangu, ana umaskini wa kipato). ni aina zile za watu ambao, anatamani watu wakose kitu fulani hata kama kukosa kwao yeye hakutamuongezea chochote. mshahara kupanda kila Julai (ambayo ni January ya kiserikali) ni suala la kisheria kutokana na ukweli kwamba gharama za maisha zinaendelea kupanda maana hapa unamaanisha mtumishi wa serikali alipwe shs 200 aliyokuwa analipwa mtumishi mwenzake eg mwaka 1977. Sina shaka kwamba mtoa post sio mwajiriwa wa serikali na nahisi alijaribu sana kupata hiyo fursa akakosa au ni mhanga wa vyeti feki. FYI: kabla ya kuajiriwa rasmi, mtu anakuwa chini ya uangalizi maalum (Probation) kwa miezi 6 hadi 12 na lengo la huu uangalizi limefafanuliwa kwenye Kifungu D.41 cha Standing Order,2009 version na anafanyiwa tathmini na mkuu wake wa idara/kitengo (immediate supervisor) kama kifungu D.42 kinavyofafanua. Kwa kipindi chote cha ajira yake (eg 40 years au 32 years etc), mtumishi huyu atajifanyia na atafanyiwa tathmini ya utendaji wake kazi katika mfumo unaoitwa OPRAS kama Public Service Act, Cap 298 na Public Service Regulation,2003 zinavyoelekeza. Tathmini ya utendaji kazi ya mtumishi wa umma imefafanuliwa vyema pia kwenye kifungu D.62 cha Standing Order. Kwa maelezo haya mafupi ni kwamba basically na legally hakuna mtumishi wa umma mzembe na mvivu maana wazembe na wavivu wanapatikana kwenye OPRAS na taratibu zingine za adhabu za kitumishi na wanaondolewa. Wengi wenu mnaosaka huduma kwenye ofisi za umma mnataka mkifika mpate huduma zenu ndani ya muda mfupi mnaojiwekea ndani ya fikra zenu kumbe wakati mwingine taratibu za kazi haziruhusu. Kwa hiyo nyongeza ya mshahara ya kila Julai ni takwa la kisheria so JPM kwa kutoongeza mshahara Julai 2016 alikuwa amevunja sheria. Labda useme nyongeza ya mshahara itokanayo na kupanda daraja inaweza isiwepo kila mwaka kwa kuzuia kupanda madaraja mwaka husika. Jifunze kutoshabikia magumu kwa mwanadamu mwenzio
Makala hii nimeipenda !!!huyo ni fungu LA kukosa
 
  • Thanks
Reactions: reg
Mimi niliajiriwa zamani serikalini kwa kuona maslahi yasiyoniridhisha nikaamua Kuondoka na kwenza sekta binafsi, huko nilijifunza ili ulipwe ni uzalishaji wako wa tija tu unaamua mshahara na daraja kupanda tofauti kubwa na sekta ya umma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
uko sahihi sana

lazima KPI iwe introduced kwa wafanyakazi wa serikali

wengi wavivu, hawajielewi, hawajiamini, hawajui procedures, sio wabunifu, hawana kipya yaani....
Hii inaashiria serikali iliyo madarakani ineshindwa kusimamia wafanyakazi wake

Mtueleze lini basi serikali itaweza kuwafanya wafanyakazi wake kuwa na tija.
?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watumishi wa umma ni wavivu, wamekosa ubunifu na bado wanalilia mshahara uongezwe Mei Mosi. Nashauri pasiongezwe hata senti mpaka pathibitishwe kuongezeka kwa tija, tuwapime mpaka 2019 labda.
Nafasi za kazi zimetangazwa huko nenda ukaombe acha kukohoa kohoa hapa kama una sifa.

Wakati wengine wanasoma ninyi mlikuwa mnakimbilia kuvuta bangi,

Maana kwa mtu mwenye kazi na biashara yake hawezi andika haya dhidi yake na wateja wake

Wewe ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa na maisha magumu na kuishi kwa shemeji

Shemeji yako mwenyewe mfanya kazi akikusikia huna pa kulala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watumishi wa umma ni wavivu, wamekosa ubunifu na bado wanalilia mshahara uongezwe Mei Mosi. Nashauri pasiongezwe hata senti mpaka pathibitishwe kuongezeka kwa tija, tuwapime mpaka 2019 labda.




nadhani utakuwa na shida kidogo, mtumishi wa umma hapimwi kwa namna hiyo unavyodhani, ufanisi wa mtumishi wa umma hutokana na motivation au motisha, motisha ya kwanza ya mtumishi ni mshahara wake wa mwezi, pia katika mshahara huo kuna nyongeza za kisheria ambazo ziko kwenye mkataba wake na mwajiri, sasa nakushangaa unaposema watumishi wasipewe nyongeza ya mshahara... sikuelewi unatumia sheria ipi, taaratibu zipi na kanuni ipi? na unaposema kwamba mpaka 2019 unatumia kanuni ipi? au ninyi ndio mnaoteketeza dira ya Tanzania ya viwanda.
 
Back
Top Bottom