Bila tija mshahara usiongezwe serikalini

Bila tija mshahara usiongezwe serikalini


Nadhani umekosea kuni-quote,maana kama kuajiriwa nina miaka lundo naupiga mpunga wa serikali.
 
Kwanza, sikatai mishahara ipande kutokana na productivity ya mtu, lakini serikalini mtu unaweza wekwa sehemu bila kupewa ABC na unatakiwa kuperform mwisho wa siku, serikalini mtu hadi kuelewa mambo/kazi nje ndani struggle lake sio la kitoto.
Pili, evaluation system za serikalini naona magumashi tu. Unaweza fanya kazi kwa bidii sana na kwa moyo wote lakini mwisho wa siku unakalia kuti kavu tu.
Tatu, career-wise the future is quite uncertain though job security is high. Kufukuza mtu serikalini ni ishu ila kuna uwezekano mkubwa sana wa ku-stuck in career developmemt.
Ndio maana tunalilia increment zetu za jumla jumla (za wote) ili tutoke wote angalau.
Ata private naamin mapungufu yapo lakini sio kwa kiasi sawa na serikalini.
Pia mleta maada ujue kwamba, uko ulipo wewe ambapo your hardwork is easly noticed and appreciated sio sawa na huku.
 
We jamaa sijui unatumia sehemu gani ya mwili wako kufikiri!!
Kwa hali hii ya uchumi,mfumuko wa bei, unatarajia tija ndio mshahara uongezwe?
Acheni kutafuta nafasi serikalini kwa kujipendekeza kwa Mkuu kwa mawazo mgando kiasi hiki,mshaurini mkuu ainusuru nji hii kwa kuongeza mishahara angalau kwa 50%,ili wajomba zako na mashangazi warejeshewe uhai
Anatumia makalio
 
mtoa post kasha pima uwezo wa reasoning capacity ya wafanyakazi,kwa nch zenye wafanyakaz wanaojitambua kama Kenya asingetoa uzi huu wa zarau kwa wafanyakaz wa kitanzania ktk hat tete iliyowakumba,ila kwasababu amegundua hlo na Rais wake amelitambua hlo ameona aweze waambia kwa njia ya mafumbo! kwa nch zenye wafanyakaz nirudie kama ya Kenya nadhan mpaka sasa dalili ya mawingu ya mvua ya el nino ingesha jionesha lkn sasa kwa wafanyakaz wa Tanzania jins walivyojengewa mising ya woga ndo kwanza wanafanyakaz kwa kas huku mioyo na nafsi zikinung'unika na kila mwisho wa mwez wakiwa wanauliza vp hakuna kanyongeza safar hii huku muda ukienda na mambo yakienda mubashara! raha sana kumwongoza mpumbav na lofa na sio kumwongoza mjinga na mjanja! Magu kamua ng'ombe wako mpaka watoke damu make hawajitambui wamejawa woga! hongera mtoa post kwa kuwafumbua wafanyakaz wa serikal ya Tanzania ingawa hawata tambua logc ya andiko lako! MEI MOC hyo wkt TUCTA washa kula mlungula na watawaletea porojo 2 cku hyo!
 
Acha waongezewe mkuu.
Maisha ni magum sana mpaka kero.
 
Jina lako na mahali unapojisitiri please!
Unajua akili na elimu ni vitu viwili tofauti, that's why ukiipima IQ ya mtu unaweza ikuta around 50, halafu akakuambia nina bachelor degree.
Swali dogo tu kwako:2015 June 1kg ya sembe ilikuwa 1000-1200/= ,sasa Aprili 2017 ,1kg ya unga 2200. Unapata somo gani hapo?.
Leo nimeamka vizuri,ningekutukana mpaka ulie.
 
hawa ndo wanakaa kwenye vijiwe vya kahawa kazi yao umbea kusema watu na viongozi wa serikali kujifanya wanajua maisha ya watu ukiangalia maisha yao ni ushuzi mtupu[emoji53]
 
Hakuna nyongeza mpaka wafanyakazi wamenyeke sawa sawa.
 
Pole kwa kukosa ajira serikalini, tambua kuwa huwezi kufanikiwa ktk maisha yako kwa kuwa na wivu wa kipumbavu dhidi ya binadamu wenzako.
 
Kuna umaskini wa roho na umaskini wa kipato. nauogopa sana umaskni wa roho. mtoa post (kwa mtazamo wangu, ana umaskini wa kipato). ni aina zile za watu ambao, anatamani watu wakose kitu fulani hata kama kukosa kwao yeye hakutamuongezea chochote. mshahara kupanda kila Julai (ambayo ni January ya kiserikali) ni suala la kisheria kutokana na ukweli kwamba gharama za maisha zinaendelea kupanda maana hapa unamaanisha mtumishi wa serikali alipwe shs 200 aliyokuwa analipwa mtumishi mwenzake eg mwaka 1977. Sina shaka kwamba mtoa post sio mwajiriwa wa serikali na nahisi alijaribu sana kupata hiyo fursa akakosa au ni mhanga wa vyeti feki. FYI: kabla ya kuajiriwa rasmi, mtu anakuwa chini ya uangalizi maalum (Probation) kwa miezi 6 hadi 12 na lengo la huu uangalizi limefafanuliwa kwenye Kifungu D.41 cha Standing Order,2009 version na anafanyiwa tathmini na mkuu wake wa idara/kitengo (immediate supervisor) kama kifungu D.42 kinavyofafanua. Kwa kipindi chote cha ajira yake (eg 40 years au 32 years etc), mtumishi huyu atajifanyia na atafanyiwa tathmini ya utendaji wake kazi katika mfumo unaoitwa OPRAS kama Public Service Act, Cap 298 na Public Service Regulation,2003 zinavyoelekeza. Tathmini ya utendaji kazi ya mtumishi wa umma imefafanuliwa vyema pia kwenye kifungu D.62 cha Standing Order. Kwa maelezo haya mafupi ni kwamba basically na legally hakuna mtumishi wa umma mzembe na mvivu maana wazembe na wavivu wanapatikana kwenye OPRAS na taratibu zingine za adhabu za kitumishi na wanaondolewa. Wengi wenu mnaosaka huduma kwenye ofisi za umma mnataka mkifika mpate huduma zenu ndani ya muda mfupi mnaojiwekea ndani ya fikra zenu kumbe wakati mwingine taratibu za kazi haziruhusu. Kwa hiyo nyongeza ya mshahara ya kila Julai ni takwa la kisheria so JPM kwa kutoongeza mshahara Julai 2016 alikuwa amevunja sheria. Labda useme nyongeza ya mshahara itokanayo na kupanda daraja inaweza isiwepo kila mwaka kwa kuzuia kupanda madaraja mwaka husika. Jifunze kutoshabikia magumu kwa mwanadamu mwenzio
 
Back
Top Bottom