Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Hivyo vitabu nilivyoweka hapo hata kimoja umesoma?? Je ukikuta kinakinzana na Biblia uko tayari kuwajibika??

Ingia humu uvipakue alafu ukisoma ndio urudi kusema kama vina uhalali au lah... Utakaposoma kuwa Nuhu hakujenga safina wala Paharaoh hakufa majini na gharika halikuja sababu ya dhambi ilihali Biblia haisemi hivyo nafikiri ndio utanielewa kwanini naviita vya kipagani!!

Pseudepigrapha, Apocrypha and Sacred Writings
Ukweli sijakisoma na wala hata sijui vinakopatikana though bado ninashawishika kuamini kua "haviwezi kua vya kipagani" kwasababu ya waandishi wake! Hapa na refer vitabu ulivyo vitaja, sina hakika na vingine ambavyo either sivifahamu au ambavyo hujavitaja kwenye UZI wako!
 
Mkuu Quran na Talmud na Biblia vyote vinadai ni maneno ya Mungu lakini ukisoma unakuta vinapingana sasa cha kujiuliza je Mungu anaweza kujipinga mwenyewe?? Na kama hawezi kujipinga sasa kivipi viwepo vitabu 3 vya dini kuu za Abrahamic alafu vijipinge??

Huoni hapo mmoja ndio yuko sahihi wengine wamefoji maandiko kama anavyosema mkuu nyabhingi ?? Sasa swali linabaki je ni nani huyo ambaye ndio amefoji maneno ya Mungu??
Kwa mtazamo wangu (najua Wakristo wengi, sio wote watakubaliana na mimi). Quran na Biblia havijatokana na source moja; Hakuna Mkristo wa kweli anae amini kwamba Quran ni kitabu cha Mungu wa mbinguni aliyeziumba mbingu na nchi, siwezi zungumzia msimamo wa Uislamu kuhusu Biblia, hilo wao ndio wanaweza kusema and this is why, huwezi kumkuta Mkristo anafanya reference ya Mungu through Quran ingawa wapo Waislam wengi hufanya reference ya mambo ya Mungu kupitia Biblia. Kwenye hili tunaweza kufungua UZI tofauti na hu na tukaendeleza mjadara huko na mimi nina ahidi kutokashfu IMANI ya yeyote
 
Ok Yuda kafanya reference ya kitabu cha Henoko ambacho nimeshakiweka humu JF kinapingana kabisa na baadhi ya mafundisho ya Biblia mfano wakati Biblia inasema dhambi ndio zilisababisha gharika yeye Henoko anasema malaika walivyozini na wanadamu ndio ikasababisha gharika maana Mungu alikwazika pia Biblia inasema Nuhu ndio alijenga safina ila Henoko anasema malaika ndio waliojenga hiyo meli..... lakini licha ya ukinzano huu kuna mistari zaidi ya 12 agano jipya ambayo ni direct copy kutoka book of Enoch ndio sasa nauliza je kitabu cha Henoko sio cha kipagani?? Na kama sio cha kipagani nani mkweli kati ya Henoko au Biblia??? Nisaidie hapa

2. Yoshua na timotheo tunaona wanavitaja kabisa na kunakili kitabu cha Yasheri..... Sasa kitabu cha Yasheri sura ya 81 kinasema pharaoh hakufa kwenye bahari ya shamu na alisalia peke yake na akamfuata Mungu wa Israel lakini ukisoma zaburi inasema Pharaoh aliteketezwa na jeshi lake baharini..... Sasa je Yasheri kukinzana na Biblia ni kosa nikikiita cha kipagani?? maana wote tunaamini maneno ya Mungu hayakinzani ikimaanisha Yasheri sio maneno ya Mungu automatically kinakuwa cha KIPAGANI si ndio maana yake

Sasa baada ya kukubaliana kuwa ni vya KIPAGANI je ni halali Biblia kuvinakili vitabu hivi ili kujengea hoja?? Na kama ni halali je na mimi nikivinakili kujengea hoja ntakuwa nakosea

Hapa ndio mzizi wa hoja wakuu
Mkuu Zitto Jr, kwanza niseme wazi, nimependa jinsi unavyo dadavua, hushindani bali unajenga HOJA, something which I also like. Wakristo wanao bisha hapo kwenye Bold, waende wakasome kwenye Biblia tena kitabu cha Mwanzo sura ya 6 kama sikosei, inasema the same thing na alicho kisema Henoko, na hapo kwenye italic, again sioni kama ni tofauti na Biblia, the issue is, hivi kwa mfano leo hi wanajeshi wote wa JMT (police, wanajeshi, mgambo, TISS, magereza etc) wote wauawe kwenye battle (nasema battle na sio vita) na amiri jeshi mkuu ndio awe amewatuma, tafsiri yake kwa mkuu wa nchi hapo ni ipi kama sio KUFA tu!? Nasema kafa kwasababu hawezi tena kutamba kwa lolote maanake hana security (kauri kama, ningeanza na shangazi zao hawezi tena kuzitamka zaidi tu ya kwenda kupiga magoti kwa huyo aliye ua hao askari wake) Remember Biblia inasema, nguvu ya mfalme ni watu wake, hivi kwa sisi tusio jua kutumia bunduki tunawezaje kua "nguvu ya mfalme?" But again, Kibiblia kuna namna 3 ya mtu kufa! Ya kwanza ni hiki kifo mtu anakufa na tunakwenda kumzika, ya pili ni mtu wa Mungu kumuacha Mungu na kurudia DHAMBI, hicho nacho ni KIFO na aina ya tatu ni hiki, mtu aliyekua MPAGANI (with this case is Pharao) na kumrudia Mungu, huyu nae amekufa, yaani matendo yake ya mwili yamekufa na kule kubatizwa ndio anazikwa na kufufuka na kua mwili mpya. SO bado sijaona tofauti ya Henoko na Biblia (ingawa hicho kitabu sijakisoma)
 
Wakijibu hili swali na mimi nachangia kwa hoja na ufanisi mkubwa ili jamii itambue umuhimu wa kuficha vitabu kadhaaa katika biblia na kuifanya jamii kushindwa kuconnect dots ili kupata mtiririko mzuri wa jinsi ulimwengu wa mwanadamu ulivyopata kuwa..


Pia kuna vitabu kama the Gospel of Mary Magdalena havipo kwenye biblia ya leo..

The Gospal of Thomas pia inakosekana katika edition mpya kitu ambacho ukimtolea reference mtu aliyebase na edition ya sasa hivi mtabishana mpaka kunakucha..

The Gospal of the lost twins kinakosekana kwenye edition ya bible iliyopo...

Yan wakati hivyo vitabu ndo vinajaribu kuwa na source at least ya kuweza kupata walau moja mbili tatu juu ya ukweli wote..

The last Super inaelezewa vizuri tena kwa mfumo mkubwa sana wa itifaki lakini kinakosa nafasi ya kuingizwa kwenye biblia iliyopo..

Mpaka hapo nachoka kwa uchovu mkubwa sana juu ya bibl kuwa kama source pekee ya kila kitu kinachohujiwa ndani...


The bible can not be the source of informations and at the same time stands as a reference point to explain the inside mentioned issues.
Hakuna wakujibu hilo swali

Ila tunaomba ututoshelezee tamaa yetu ya kuunga Doti

Mwagika mkuu....
 
Kumbe kila kitabu nje ya Biblia ni cha kipagani?? Na kama vitabu ulivyoorodhesha hapo vipo, ungetoa ushahidi kama mfno!
 
nimerekebisha,wanasema linazama kwenye bwawa la maji
jua linazama kwenye bwawa tokea lini?
Wanaosema hivyo nani? mbona nishakwambia sijawahi kusikia waislamu kufundishana kuwa jua huwa linazama kwenye matope wala kwenye bwawa la maji,Ni wewe ndio nakusikia ukisema hayo.
 
labda nikwambie kwamba hawakupata tabu sana,wali-plagiarize maandiko yaliyokuwepo kabla mfano maandiko ya wamisri kwenye kitabu kinachoitwa the papayrus of ani
Hayo maandiko yalikuwepo kabla ya nini?
 
Mtume hakuwahi andika Quran, alikuwa anateremsha maneno kwa imla (anapandwa na mzuka/anawehuka kwa kiswahili kibovu).
Kwani ndugu yangu huwezi kujadili kwa lugha ya staha? Au ni hasira kwakishindwa kumjibu Zito junior?
 
Kwa mtazamo wangu (najua Wakristo wengi, sio wote watakubaliana na mimi). Quran na Biblia havijatokana na source moja; Hakuna Mkristo wa kweli anae amini kwamba Quran ni kitabu cha Mungu wa mbinguni aliyeziumba mbingu na nchi, siwezi zungumzia msimamo wa Uislamu kuhusu Biblia, hilo wao ndio wanaweza kusema and this is why, huwezi kumkuta Mkristo anafanya reference ya Mungu through Quran ingawa wapo Waislam wengi hufanya reference ya mambo ya Mungu kupitia Biblia. Kwenye hili tunaweza kufungua UZI tofauti na hu na tukaendeleza mjadara huko na mimi nina ahidi kutokashfu IMANI ya yeyote

Judaism has as its holy book the Hebraic Bible. This differs from the Old Testament of
the Christians in that the latter have included several books which did not exist in Hebrew.
In practice, this divergence hardly makes any difference to the doctrine. Judaism does not
however admit any revelation subsequent to its own.
 
Kwani ndugu yangu huwezi kujadili kwa lugha ya staha? Au ni hasira kwakishindwa kumjibu Zito junior?
zitto junior ni jamaa yangu sana humu JF 🙂.
Kuna manabii kama Daniel walikuwa wanapewa ufunuo kupitia ndoto, yani mpaka walale ndio wanaoteshwa then asubuhi wanakuja ongea walichoota!. (Ni simple kuelezea hili tendo eeehh!?).
Sasa kuna huyu Mtume Muhammad yeye alikuwa halali kuelezea taarifa anazopewa!. Nikuombe unisaidie kuielezea hiyo hali 'kwa lugha ya staha' unayoielewa wewe babu na mjukuu ila kumbuka kuweka hii hoja "mtoa taarifa hakuwa anajua kusoma wala kuandika!".
Sijashindwa kumjibu zitto junior sababu hoja zake zilibase kwa watu mnaotaka referance za kwenye bible pekee!. Ukiiifatiria michango yangu humu Intelligence Forum utajua nipo upande upi wa story!.
 
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
Lutu alilala na binti yake kwa kupenda mwenyewe!
 
Wewe unajua kabisa kuwa kulikuwa na mitume na walikuwa na vitabu,sasa hoja ingekuwa kipi kimepotoshwa na yapi yameongezwa katika hayo mafundisho yaliyo kwenye hivyo vitabu?
Ila waliotangulia ni wayahudi as wayahudi kupitia Tanakh/Torah ambayo Biblia pia imeazima na kutumia kwenye agano la kale lakini kuanzia agano la jipya maandiko ya wayahudi na wakristo yanakinzana then baadae wanakuja waislam nao wanakinzana na both jews and christians hivyo kama hoja ni kwamba wa kwanza ndio mkweli basi dini ya wayahudi ambayo haimtambui Yesu kama messiah ndio inayosema ukweli if at all tutachukua definition yako kwamba wa kwanza kuandika ndio mkweli.
 
Upo sawa kabisa but ungerekebisha hilo neon,UPAGANI cause reference uliofanyia kwenye vitabu vyako nje ya Biblia bado waandishi wake ni watu wa Mungu, Manabii so vitabu vyao haviwezi kua vya KIPAGANI, hiyo ni kwa mtazamo wangu, sina hakika na hao wengine
Nimeviita vya kipagani sababu vinapingana na Biblia ndio maana nikakuhoji kama sio vya kipagani ina maana Book of enoch ni sahihi licha ya kupigana na Biblia?? Je ina maana Book of Jasher ni sahihi licha ya kupingana na Biblia

Kwa mtazamo wako maneno ya Mungu yanaweza kukinzana?? Kama hayawezi niyaitaje hayo maandiko yanayopinga Biblia bila kujali ni ya Nabii gani??

Naomba unisaidie jina la kutumia ili mods waedit kichwa cha habari
 
Ukweli sijakisoma na wala hata sijui vinakopatikana though bado ninashawishika kuamini kua "haviwezi kua vya kipagani" kwasababu ya waandishi wake! Hapa na refer vitabu ulivyo vitaja, sina hakika na vingine ambavyo either sivifahamu au ambavyo hujavitaja kwenye UZI wako!
Nimekuwekea link ukavisome na hivyo jasher na enock sijavitaja ila nimesummarise kuwa viko zaidi ya 20 vingine..... Ndio hivi viwili vinaingia ingawa na vyenyewe vinakinzana na Bible hivyo unaposema sio vya kipagani unaniacha na maswali mengi sana kwamba je maneno ya Mungu yanakinzana??

Alafu kwanini tunatishika na majina?? Ina maana leo mwakasege akisema HAKUNA MBINGU hutomuita ni mpagani kisa ni "mtumishi" wa Mungu

Upagani hatuangalii status ya mtu bali tunajali KAZI yake.... Hivyo haijalishi kama Enoko/Gad/Nathan alikuwa ana status gani ila kwa wakristo wanaamini as long as anakinzana na Biblia basi anageuka MPAGANI by his writings.

I hope tunaelewana hapa
 
Ikiwa akili haina sifa timilifu
Hata kama watakusanyika watu wote,Bado sifa itabaki pale pale,nayo ni kutotimia asilimia 100
Unapomuoma mtu,anakuwa na jeuri na nguvu bandia,mpaka kumjadili Muumba mbingu na ardhi au kuwajadili Manabii wa Mola
Basi,sifa yake ya upunguani,ndio inajidhihirisha kidogo kidogo
atafika sehemu
atamkana mpaka Mama yake mzazi,na kukana haki zake
atakuja kumuoa Mama yake,huku akiuliza
Ni nani ameweka sheria hizi?!!
atamuoa mpaka Dada yake tumbo moja
huku akijiona kuwa yupo sawa

Tunamshukuru Muumba mbingu na ardhi,kwa kutupa mwangaza sahihi wa kumtumia yeye tu
Hakuna Mola apasae kuabudiwa kwa Haki,isipokuwa Mola mmoja tu,na Mohammad ni Mtume wake
Shukran
 
Mkuu mitale na midimu nimekuelewa hoja yako ila labda nigusie mambo machache

1. Unaposema kuwa hakatazwi mtu kuquote "nje ya Biblia"as long as unaangalia context..... Je ni wakati gani ambapo manabii walijua Biblia inasema A na wao wakaandika B ilihali mpaka Yesu anakuja hakukuwa na standard bible?? Nachojua ni kwamba baada ya wote kuandika ndio wakatokea watu miaka 300 baadae wakasema huyu anakinzana na huyu ndio maana vikatolewa na vingine vikaachwa Ndio kina Enock na Mwandishi wa Jasher na vitabu vingine vya kufanana wakawa victims wa hilo tokea mwanzo kabisa.

Kuhusu kuquote nachojiuliza sio tu kwa kuangalia muktadha ila Biblia mfano kwa story ya Daudi inasema historia ya Daudi MWANZO MWISHO na hata Rehoboam MWANZO MWISHO vimeandikwa kwenye kitabu cha Gadi n.k sasa je hapo nikienda kusoma na nikagundua inconsistency juu ya story ya daudi katika kitabu cha samweli/wafalme na kitabu cha gadi/Nathan je ntakuwa nina makosa kushikilia msimamo wa kitabu hicho???

2. Mkuu wanaosema vimepotea sio mimi ni hao hao waliocompile Biblia kuna apokrifa zilikuwa termed as LOST BOOKS yaani vilipotea katika uso wa dunia mfano kitabu cha shemaya kipo katika kundi hilo na ushahidi wote wa kiachiolojia unaonyesha manuscript zake zilishapotea kitambo unless una ushahidi mwingine kuwa Manuscript za book of shemaya,Gadi na Nathan bado vipo unaweza kutusaidia mkuu.

3. Mkuu kuhusu uandishi hilo jambo halipo kwenye Book of Enock pekee hata Wimbo ulio bora au barua kama 7 za paulo ni pseudepigrapha yaani havina ushahidi kuwa viliandikwa na paulo au paulo maana vimeandikwa vingi baada ya kifo cha paulo..... Mfano waebrania ni pseudepigrapha ila kwenye bible kipo hivyo sidhani kama hoja hii ya uandishi au backdating ya apokeifa ina mashiko tena hasa ukizingatia backdating/auhtorship crisis hata ndani ya Bible vipo according to theologians.

Ubarikiwe
1: Hadi Yesu anakuja Standard bible ilikuwepo. Walikuwa hawasomi kila kitu mwenye masinagogi kama maandiko matakatifu.
Hicho kilichokuwepo kwenye Hekalu na masinagogi ambacho hata Yesu alikisoma na akasema kinamuelezea yeye ndio bibilia ya wakati huo.
Kama nilivykupa mfano wa jinsi yalivyohifadhiwa. Ndio maana Yesu alisema '' Mwayachunguza maandiko'' alikuwa hazungumzii vitabu vya kufikirika kila andiko lililokuwepo. na hivyo unavyosema sijawahi kujifunza popote kuwa enzi za Yesu vulikuwa ni maandiko matakatifu na Yesu hakuwahi kuviquote au kuviendorse.

Bibilia inasema maneno ya manabii huwatii manabii ikitokea kuna ukinzani hapo kuna sababu ya kujiuliza kwa nini. Ila ikiwa maelezo na mafunzo ya samweli yanaumana na waandishi wenzake wa bibilia ila yanakinzana na huyo Gadi. Muamini Samweli. Kuhusu daudi kutenda dhambi haijalishi ziliandikwa zote au kadhaa, ikiwa alitembea katika mwili alikuwa prone kufanya kila aina ya uovu. Ila ukweli ni kwamba alimrudia Mungu, na Mungu akasema hakuna mtu aliyenipenda na kunitii kama Daudi kuonyesha Mungu anasemehe na kutupilia mbali makosa ya kale.
Katika maandishi ya kiyahudi ambayo yalitambuliwa kama Maandiko matakatifu kwa Uongozi wa Mungu, Unaushahidi wowote kuwa walikuwa wanakitabu CHA GADI, au tukienda kwenye masinagogi yao Tutaambiwa hilo? kama sio Basi Kitabu cha Gadi kitabaki kuwa kitabu ambacho sio Maandiko matakatifu. Ukiambiwa habari za mkwawa utazikuta kwa mchawi mkuu wake haimaanishi kila kilichoandikwa na mchawi huyo ni sahihi.

2: Wakinanani hao, unaweza kufunguka zaidi. maana compilation ya bibilia inamambo mengi ya kuzungumzia.

3: Licha ya hiyo changamoto. Kikubwa ambacho nakisisitiza ni doctrinal consistence ya hivyo vitabu 66 ya bibilia. Fact kuu ni kuwa hakuna og mauscript
hivyo ushahidi wa kuungana mkono kwa vitabu hivyo, Lakini pia magombo mengi ya kale yanayovumbuliwa yanaonyesha kuwepo kwa barua nyingi zilizokuwa zikisambaa katika makanisa ya awali na ufanano wa kimafundisho na misistizo ambayo inaungana kama mnyororo kuanzia mwanzo hadi ufunuo. Usadikisho wa Lengo kuu la Mungu kwa mwanadamu mdambi unapatikana katika vitabu vyote. Ila hivyo unavyotaka viingizwe kama authority sawa na bibilia ambavyo havina idadi na vingine licha ya kuwa na sehemu chache zinazungana na bibilia tunayoiamini vina mavitu mengi ya ajabu yasiokidhi viwango vya kuingia katika mnyororo wa Mwanzo hadi Ufunuo. Yaani anguko la mwanadamu, Wokovu kupitia Yesu.
 
Back
Top Bottom