Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Ndiyo nauliza mkuu maana wewe ndio umesoma na kuelewa,hayo matope ni ya wapi na hayajakauka hadi leo?
maneno ya mungu wa israel yanakauka
nilifikiri maneno ya mungu ni timeless,kama mungu wa israel anabadili mawazo hanifai mimi,of course huo mzimu wa palestina haunihusu mimi
 
maneno ya mungu wa israel yanakauka
nilifikiri maneno ya mungu ni timeless,kama mungu wa israel anabadili mawazo hanifai mimi,of course huo mzimu wa palestina haunihusu mimi
Ulimaliza kusoma vitabu vyao vyote ?
 
Dini inaingiaje hapa?? Tujikite kwenye hoja kwamba JF wafia dini mbadilike mfungue akili yenu na mkubali maarifa kutoka vyanzo tofauti sio kila hoja mpaka bible

Anyway nimeweka hapo maswali labda tusaidiane kujadili hayo tupate majibu
Ni ngumu mno kwa uzi wako usihusishwe na dini wakati references zako umezitoa kwenye Bible.........jiandae kwa uzi wako kuwa na mlengo wa ki dini na vile vile jiandae kuhamishiwa kwenye jukwaa la dini.
 
maneno ya mungu wa israel yanakauka
nilifikiri maneno ya mungu ni timeless,kama mungu wa israel anabadili mawazo hanifai mimi,of course huo mzimu wa palestina haunihusu mimi
Mbona unaniacha kwenye mataa tena mkuu? wewe ndio umekuja kusema Qur'an inasema jua linazama kwenye matope,yani jua likizama kumbe huwa linazama kwenye matope hivyo ndio Qur'an inavyofundisha. Sasa nimetaka ufafanuzi juu ya hilo matokeo yake unasema hayakuhusu wakati wewe ndio umeleta suala hili.

Usibanie elimu mkuuu,nijuze hayo matope ya wapi na hayakauki?
 
Wewe unacho hicho kidayari/ki diary?? Ni hoja ipi uliijenga kupitia hivyo vitabu ikakataliwa,,,je unajua unakosea kuviita vya kipagani??au unataka hata ukijenga hoja kwa vitabu visivyo na muunganiko na ukristo ukubaliwe tu usipingwe??? Hayo ni mambo yanayowezekana kwenye physics math na bios,,sio dini ya ukristo
Umeielewa hoja yake? Hakuna sehemu aliyosema asipingwe ila anaomba sababu ya kumpinga wakati hivyo vitabu ambavyo ninyi mnaviita vya kipagani vimetumika kama reference kwenye biblia. Unapata wapi uhalali wa kupinga hoja inayotolewa katika hivyo vitabu wakati biblia yenyewe imetutaka kuvisoma kwa ajili ya reference?
 
Mkuu nafikiri bado kuna kitu tunakiacha.... Unaposema biblia ilitaka tufaham hicho tu ila mafundisho mengine yana walakini hapo unaniacha njiapanda mfano

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

Hapa Bible iko clear kabisa kwamba YOTE ALIYOFANYA.... YALIYOSALIA.... Ikimaanisha story ya solomon in depth imekuwa referred kwenye hicho kitabu kizima na sio part ya hicho kitabu. Same kwa story ya daudi na rehoboam. Sasa basi kama kitabu kizima kimekuwa referred hapa je ina maana tukigundua hicho kitabu kina incosistency na kitabu cha wafalme (Maana bible haikuwepo bado) tuchukue msimamo wa kitabu gani?? Wafalme au acts of solomon,Book of Gad etc???

Na ndio hapo narudi kwenye swali la msingi kwamba kama manabii walikuwa huru kurefer biblical stories kwa vitabu ambavyo havitambuliki na Biblia ya sasa je na sisi tukifanya itakuwa kosa?? Na kama ni kosa why kwa manabii haikuwa kosa wakifanya hivyo??

Pia kuhusu credibility ya kama hivyo vitabu ndio hivi vilivyopo nafkiri huo ni mjadala mwingine sababu wanatheolojia wengi leo wanakiri hata barua za paulo hakuandika zote yeye as yeye na badhi ya tafiti zinaonyesha barua hizo ziliandikwa kuwa kwenye mfumo wa ''kitabu'' miaka mingi baada ya paulo kufa kwahiyo tukijikita kwenye hoja hii itabidi hata tuwekee mashaka baadhi ya vitabu vya bible juu ya uandishi wake.

Lakini pia kama hivyo quoted vitabu vitakuwa vimechezewa kama unavyohisi labda niulize je nini hatma ya maneno ya Mungu kama yanaweza kuchezewa na wahuni wachache??ina maana mwanadamu anaweza pambana na maneno ya Mungu hadi afanikiwe?

Mkuu embu tuwekane sawa hapo
Mkuu zitto Junior nimekupata vizuri tuu. Ukiutazama ukristo unajitosheleza kupitia biblia. Hilo la kusema au kutaja vitabu vingine halifanyi biblia isijitosheleze nafkiri hapa tuko pamoja.
Kuhusu vitabu vya upagani naungana na mdau hapo juu. Nilitoa mfano wa masimulizi ya vifo vya mitume kuonesha kuwa vitabu nje ya biblia vinaweza kuwa sawa na vikamjenga mtu kiimani lakini viwe au visiwepo haviwezi kumzuia mtu kwenda mbinguni.
 
Kwa kukusaidia vilivyoandikwa kwenye Bible ni vile tu vilivyokuwa tested na kuthibitika kweli, yale yasiyo na uhakika japo yaweza kuwa kweli yakatupwa nje.
Mambo yanayohusu imani yanakuwa tested kwa namna gani? Imetumika kanuni ipi kutest hayo mambo? Nadhani jambo hilo lingekuwa linawezekana mngekuwa mmeisha test uwepo wa mungu ili kuwadhibitishia atheists
 
Mkuu, kwenye hizo reference ulizotoa, wapi umeona "VITABU VYA KIPAGANI!?" Katika kitabu cha Yohana (Injili) kuna sehemu imeandikwa hivi, "..yapo na mambo mengine ambayo YESU aliyafanya na hayakuandikwa katika kitabu hiki, laity kama kila kitu kingeandikwa then vitabu visingetosha..." Nataka kuonesha, yes yapo mambo mengi tu ya manabii, wafalme, makuhani nk ambayo yalifanywa, kutenda au hata kufundisha lakini hayana reference ndani ya Biblia, swali langu, hapo vitabu vya kipagani we umetoa wapi!?
Kwa mfano leo mtu akiwa anafundisha kanisani, aka fanya reference kwenye nyimbo za tenzi za rohoni, injili, mwimbieni Bwana, nyimbo za wokovu nk. Hizo reference sio za Kibiblia but again huwezi kusema hivyo vitabu ni vya kipagani! Hebu njoo tena na uthibitisho wako kwamba Biblia imeruhusu kufanya reference kwenye vitabu vya kipagani, otherwise mi umeniacha njiapanda, sijaelewa!
 
Sasa kama mtu ana maandiko kwanini mnayakataa kisa hayapo kwenye Biblia ilihali Biblia yenyewe inatuambia habari za Daudi kwa upana wake tutavikuta kwenye vitabu vya Gadi,Nathan n.k ilihali vitabu hivyo vinahesabika ni vya kipagani kwa kanisa???

Yaani kwanini kuna double standards mkuu
Hebu jiridhishe uhusiano wa hao watu na Mungu ndio utajua maandishi yao yanaweza kua na SIFA ya KIPAGANI! Hao ni miongoni mwa manabii wa Mungu, mfano huyo Nathan ndiye aliyekwenda kumuonya mfalme Daudi baada ya kuanguka dhambini kwa kuzini na mke wa mmoja ya askari wake. Au labda neno UPAGANI ndio labda hatuelewani maana yake.
 
Umeielewa hoja yake? Hakuna sehemu aliyosema asipingwe ila anaomba sababu ya kumpinga wakati hivyo vitabu ambavyo ninyi mnaviita vya kipagani vimetumika kama reference kwenye biblia. Unapata wapi uhalali wa kupinga hoja inayotolewa katika hivyo vitabu wakati biblia yenyewe imetutaka kuvisoma kwa ajili ya reference?
Labda angefanya hivi, aeleze kwenye hivyo vitabu vinavyo elezwa hapo sehemu inayosomeka kwamba Daudi aliwahi kuishi kindoa na mtu wa jinsia yake (ya kiume)
 
Hebu jiridhishe uhusiano wa hao watu na Mungu ndio utajua maandishi yao yanaweza kua na SIFA ya KIPAGANI! Hao ni miongoni mwa manabii wa Mungu, mfano huyo Nathan ndiye aliyekwenda kumuonya mfalme Daudi baada ya kuanguka dhambini kwa kuzini na mke wa mmoja ya askari wake. Au labda neon UPAGANI ndio labda hatuelewani maana yake.

Kitu kimoja ambacho najaribu kuwafunda watu wa kidini kila siku na kuwaasa

Ni kwamba mjifunze kumpenda shetani mliye simuliwa toka Enzi za utoto wenu kuwa ni adui yenu

Mkiweza hilo mtabadilika

Na ndiyo Tuzo ya kuwa Anunaki aliyekamilika
 
Una maana gani kuleta hiki kifungu hapa?? Unafkiri kuhoji ndio hatufahamu Biblia?? Na hii ndio shida ya JF mtu akihoji tu masuala ya imani anaonekana shetani na hii ndio inafanya reasoning zetu hazikui

Sasa mfano mtu anaambiwa mnara wa babeli ulijengwa kufikia mbinguni.... Hivi kwani mbingu iko mawinguni?? Hilo nalo ukihoji dhambi?? Je akitokea mpagani unamhubiria akakuuliza hilo swali ukishindwa kujibu unategemea ataokoka??

Narudia tena tupende kuhoji ili tufunguke zaidi.... Na mmi tangu nianze hii mijadala yangu humu mimi binafsi nmejikuta nasoma sana maandiko ya dini zote sio Quran sio Biblia sio Talmud ya wayahudi na nyie mjijengee huo utaratibu wa kujihoji maswali ili mchimbue maandiko sio kutoa kejeli tu hazisaidii ndio maana mkikutana na waislam ni rahisi kuwaangusha kwenye mijadala ya maandiko.
Exactly brother niliwahi kuhoji swala la yuda kurejea kitabu cha henoko ilihali wahusika wanadai cha kipagani nilipata majibu ambayo dhahiri yanaonesha watu wameanishwa vibaya sana na kazi iliyofanyika Constantinople mnamo mwaka 325
 
Ningeomba Moderator wote wa JamiiForums msihamishe uzi huu kupeleka jukwaa la dini maana message najibu mada ya JF intelligence hivyo ningependa ujumbe uwafikie walengwa, natanguliza shukrani kwa ushirikiano wenu

Cc Paw Invisible
vitabu vipi vya kipagani?tambua vipo vitabu vingi na magombo mbalimbali ya manabii wa kale vimepotea,ving havikujumuishwa kwenye bibilia,kumbuka bibili ni mkusnyiko wa vitabu mbalimbali vilivvyoandikwa na watu tofauttoafauti kwa vpindi tofauti vya karne.
 
vitabu vipi vya kipagani?tambua vipo vitabu vingi na magombo mbalimbali ya manabii wa kale vimepotea,ving havikujumuishwa kwenye bibilia,kumbuka bibili ni mkusnyiko wa vitabu mbalimbali vilivvyoandikwa na watu tofauttoafauti kwa vpindi tofauti vya karne.
Sio vitabu vingi Tu

Na hakutakuwa na mwisho wa uandishi

Ukiwa zezeta utakesha Maktaba Unarundikiwa kila aina inayoitwa ujuzi... Mpaka mpagawe
 
Mbona unaniacha kwenye mataa tena mkuu? wewe ndio umekuja kusema Qur'an inasema jua linazama kwenye matope,yani jua likizama kumbe huwa linazama kwenye matope hivyo ndio Qur'an inavyofundisha. Sasa nimetaka ufafanuzi juu ya hilo matokeo yake unasema hayakuhusu wakati wewe ndio umeleta suala hili.

Usibanie elimu mkuuu,nijuze hayo matope ya wapi na hayakauki?
ok,nafikiri ungewauliza waislam au allah kuhusu hilo sababu kisayansi jua kuzama kwenye bwawa la maji ya mmatope ni upuuzi usiomithilika
 
Back
Top Bottom