Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Sio logic unayozungumza Quran ni living miracle kila kizazi kitaon na kugundua yake yapo mwngi ambayo quran umeyasema ambayi sayans bado haijayafikia mafano Quran imesema kuna sayari nyingine tofauti na ya kwetu na kuna misha nje ya sayari yetu so yapo mambo kwa kizazi kile ilikiwa ngumu kuyaelewa hata ungwalelezea vip yalisubiri ili sience ikia advance yagundulike na iww ishara kwa mwanadamu kuwa yupo aliyeyapanga unajua kadri mwanadamu anavyopiga hatua kiteknolojia ndio anakuwa haoni sababu ya kuamin uwepo au ujitaji wa Mungu so wataendelea kugundua na na iww ishara ya Mungu kwao kuwa yakieandaliwa haya yote na yeue Muumba..!

Hatukuwepo wakati mussa anavusha watu hatujaona Yesu akifufua watu maana hiiyo kizazi hiki hakishuhudia miujiza kikubwa Ya Allha ioa kutuelea Quran ambayo kila kadri sayan inavyoendelea Quran haija achwa nyuma so kutokulewa kweny sio mpaungufu ya Quran..!
Ndugu yangu Quran imetengenezwa karne nyingi sana baada hata ya mitume wa Yesu kufa.kwa kitabu cha namna hiyo lazima kuwepo na advancements kisayansi,kijamii,kitamaduni na kisiasa.Mambo ambayo hayakuongelewa na vitabu vingine haina maana hayakuwepo au hayana maana You should keep that in mind.Quran imeendelea kuwa ilivyo kwa sababu inalindwa na upanga na namna yeyote ya kuitafsiri manake ni kifo,rejea kesi ya Salman Rushdie na wengine.Siku mkitoa uhuru wa watu kuexpress views zao middle east hakutakuwa na muislam.Jiulize kwa nini kwenye nchi nyingi za sheria hamtaki hata mtu kuabudu waziwazi au kuhubiri waziwazi.The Quran has remained unchanged due to socio political and sociocultural aspects.Lakini siku msipotanguliza adhabu ya kifo kwa apostates na wahubiri wengine mtashangaa!

Hebu nipe sababu zinazoifanya quran kuwa miracle
 
Kila siku kwa makadirio vinandikwa vitabu viwili au article kuuoinga uislam na muhhamad sasa kama ukisoma hivyo ku justfy iman yako ndio ulipozid kupotea hiyo artcle nimeisoma sana hata mimi najua zipo arrtcle za kuupinga ukrssto na hata kuwepo kwa Yesu lakin why niziamin na wakati najua zina uzushi mwingi nazisima tu kuongeza maarif...sijui kama umeahi kusikia injil ya maria magdalena imasema yesu alioa akaza na watoto na maria magdalena so inabidi uwe smart angalau kuwa posstive tafuta vtnazo sahihi ili uwe judge mzuri usotafite habari ambazo utapenda kuzisikia au kuziona against islama halfu ukiznshikia bando utaumbuka mbele sababu hazina mashiko ya kiushahidi
Hujakisoma hicho kitabu usiseme uongo.Naomba utafute muda ukisome kina pages zaidi ya mia tisa.
 
Habari za jioni wana JF natumaini wote humu ni wazima.
View attachment 885770
Nlipokuwa naipitia uzi huu Mjue Yoabu - Jenerali Mkuu wa Mfalme Daudi, Katili na asiyeogopa chochote! - JamiiForums

Mkuu Elungata aliibua hoja kuhusu Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja na nathan ila muanzisha uzi alipotaka ushahidi aliuwekea condition hii.




Baada ya kusoma hii comment nilisikitika sana na nilijiuliza sana kwamba inakuaje kila story ya watu waliotajwa kwenye bible watu wanataka reference kutoka ndani ya Biblia pekee as if Biblia imeandika kila kitu?? Kwanini tunapenda kujifunga akili kiasi hicho?


Baada ya kuona mentality hiyo imeanza kukua humu JF intelligence nikaona nilete mada jinsi Biblia yenyewe imetutuma tukasome vitabu vingine nje ya Biblia ili tuongeze ufahamu kuhusu baadhi ya watu na matukio ambayo Bibila yenyewe haikuandika yote kwa upana wake, hivyo nia ya uzi huu ni kwa wale waliojifunga kwenye kusoma maandiko pekee wabadilike na kuwa na fikra huru na kuruhusu maarifa kutoka kona zote kwa mithiri ya kujifunza zaidi na kupanua uelewa wa mambo.
View attachment 885772
Kwa kuanzia tu labda nitumie nafasi hii kumjibu mkuu wangu maishapopote kuwa hata biblia yenyewe inakiri kuwa maisha yote ya Daudi yameelezewa vizuri zaidi nje ya Biblia hivyo imetutuma tukasome vitabu hivyo mnavyoita vya kipagani ili tujifunze kwa ufanisi zaidi

1 NYAKATI 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

Vitabu vilivyotajwa hapa ni Book of Gad the seer,Book of Nathan the prophet, Book of Samuel the seer (Sio samuel 1&2) ambavyo kwenye biblia havikuwekwa . Sasa kama Biblia inakiri kuwa sio kila story yake imeongelewa kwa upana wake katika biblia je kwanini siku hizi watu wakijengea hoja kuhusu personality za biblia mnalazimisha reference iwe ndani ya bible pekee??? Ina maana waandishi wa Biblia ni wajinga hadi watutume tukasome hivyo vitabu vingine ambavyo mnaviita vya kipagani??

MAANDIKO
Hapa chini nimeambatanisha vifungu vya Biblia hivyo ningeomba tuisome kwa makini kabla ya kuchangia hoja. Neno Tarehe kwenye maandiko haya kwa kiswahili rahisi inamaanisha Nyaraka/rekodi/kitabu au kwa kizungu book/journal/Annal.
View attachment 885773

1. Kitabu cha Yehu

2 Nyakati 20:34
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

2. Kitabu cha Nabii Gadi muonaji/ Kitabu cha shemaya

2 Nyakati 13:22
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

2 Nyakati 12:15
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

1 Nyakati 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

3. Kitabu cha mfalme Ahasuero

Nehemiah 12:23
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu

Pia kinatajwa Esther 10:2, 2:23, 6:1

4. Matendo ya Mfalme suleiman

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

5. Nyakati za wafalme wa Israel & Yuda

1 wafalme 14:19
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.(chronichles of the kings of israel/Judah)

6. Kitabu cha Hozai

2 Nyakati 33:19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.

Hivi ni kwa uchache tu ila kuna vitabu vingine zaidi ya 20 vinatajwa kama reference point kwenye biblia ilihali havipo kwenye Biblia na wala havitambuliki na kanisa lakini leo hii akijengea mtu hoja anaonekana shetani!!
View attachment 885774

HITIMISHO
Baada ya uzi huu nisingetegemea tena kusikia wana JF wakitaka reference kutoka kwenye biblia pekee ilihali Biblia yenyewe inataka tukarefer kwenye vitabu vingine ambavyo vingi ni vya kipagani tu ili tupate uelewa zaidi ya watu muhimu kwenye bible.

However ningependa tujiulize maswali haya ili kupanua fikra zaidi

1. Kwanini vitabu hivi ambavyo Biblia inaturefer tukasome ili kuelewa baadhi ya matukio havikuwekwa kwenye biblia??

2. Na kama havikuwekwa kwa sababu yeyote ile je ina maana ni vya kipagani??

3. Na kama ni vya kipagani ni kwanini vimekuwa referred kwenye bible?

4. Kuna vitabu vingine ambavyo vimenakiliwa hapa ni halali kabisa katika kanisa la kale lakini kwa sasa viko categorized kama vitabu vilivyopotea.... Je nini hatma ya Biblia kama maneno ya Mungu ilihali yanaweza kupotea??

5. Na kama yamepotea je ina maana biblia haijakamilika sababu sehemu ya stori yake imepotea??

Naomba kuwasilisha

Cc: Wana JF intelligence wote bila kuwasahau kina Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler monde arabe mtu watu
Nani kaviita vya kipagani,au unajaribu kukoleza stori,si kweli kuwa kitabu au nyaraka au habari kutokuwa ndani ya biblia inamaana ni ya kipagani,
 
Yaani kitabu cha reference kiandikwe na mtu mwenye kupakwa mafuta ya kipekee kama Nabii Samuel,,au nabii Gadi au nabii Elisha watu wenye roho ya tofauti ndani yao na wewe uite vitabu vyao kuwa vya kipagani??? Mtu wa kawaida kama wewe mwandishi Unaweza kuhoji credibility ya kitabu kilichoandikwa na Nabii mwenye permanent connection na mbingu?? Uwezo wako ungehoji credibility ya vitabu vya Charles Darwin,,au da Vinci.
Ndo haswaaa nililokuwa nafikiria
 
Ningeomba Moderator wote wa JamiiForums msihamishe uzi huu kupeleka jukwaa la dini maana message najibu mada ya JF intelligence hivyo ningependa ujumbe uwafikie walengwa, natanguliza shukrani kwa ushirikiano wenu

Cc Paw Invisible
Asante sana kwa angalizo hili muhimu ,hii tabia ni kama inaota mizizi sasa na hata ukiwasiliana nao hakuna respond yoyote toka kwao...nakwazika sometimes....
 
Soma vizuri mada...... Huyo Nabii Gadi au Nabii Nathan vitabu vyao HAVIPO kwenye Biblia maana kanisa limeviterm vitabu vyao kama Pseudepigrapha/Apocrypha hivyo havitambuliki kwenye Bible na vinahesabika ni vya kipagani tu.

Sasa nikuhoji wwe... Je kwanini basi Biblia inatoa reference kutoka vitabu vya kipagani?? Ila sisi wana JF tukitoa reference kutoka vitabu vya nje ya bible mnakataa hoja zetu??

Tuanzie hapo kwanza
Nani kavihesabu vya kipagani?,nisaidie kunipa mahali vitabu hivi ulivyoviorodhesha vimeitwa vya kipagani?
 
Ukiona kitabu chenye hayo maelezo basi ndio Unatakiwa uhoji uhalisia wake..Lutu kulala na wanawe sio kigezo cha Daudi kumpiga miti mwanaume mwenzie.Ni dharau iliopita heshima ya mtu
Wanaoyawaza haya ni wanaoyatenda ama kuyatamani ama walipatikana kihivyo
 
Nadhani kwa maoni yangu tunajaribu kuigeuza Bibilia kitabu cha kubishania badala ya Kitabu cha mahusiano kati ya Mungu na wanadamu.
Picha kubwa ya biblia ambayo kila mtu anapaswa kuiona ni
1:Mungu aliumba Dunia na Wanadamu wakamilifu.
2:Adam na hawa wakachagua kumsikiliza shetani badala ya kauli ya Mungu na kutuingiza wanadamu wote katika shida japo Wapo kama wakina henoko na Abraham walitembea kwa Imani Mungu akawatukuza.
3:Mungu aliandaa mpango wa Wokovu, Kupitia Yesu Kila amwaminie na kumtii apate uzima wa milele na raha wenda zaidi ya ile ya adam na hawa bustanini baada ya hukumu ya Haki.

Picha kubwa kati ya Pambano la Wema na uovu na hitimisho lake Haipaswi kuhafifishwa na story nyingine yoyote.
Hii inaitoa Bibilia kwenye level ya Kitabu cha Kisomi na kukifanya Kitabu kinachomtambulisha Mungu muumbaji kwa kiumbe chake kilichopotea. Bibilia ni kitabu chenye lengo la kuleta mahusiano kati ya Mwanadamu na Mungu. Hii ndiyo inatakiwa kuwa output ya mtu kusoma bibilia. ie Daily connection with God until restoration.

Kuchimbua mambo ili kuhalalisha au kuharamisha mawazo flani ni kutoka nje ya BIG PICTURE YA KWA NINI BIBILIA.
Barikiwa sana mkuu
 
Ndugu yangu Quran imetengenezwa karne nyingi sana baada hata ya mitume wa Yesu kufa.kwa kitabu cha namna hiyo lazima kuwepo na advancements kisayansi,kijamii,kitamaduni na kisiasa.Mambo ambayo hayakuongelewa na vitabu vingine haina maana hayakuwepo au hayana maana You should keep that in mind.Quran imeendelea kuwa ilivyo kwa sababu inalindwa na upanga na namna yeyote ya kuitafsiri manake ni kifo,rejea kesi ya Salman Rushdie na wengine.Siku mkitoa uhuru wa watu kuexpress views zao middle east hakutakuwa na muislam.Jiulize kwa nini kwenye nchi nyingi za sheria hamtaki hata mtu kuabudu waziwazi au kuhubiri waziwazi.The Quran has remained unchanged due to socio political and sociocultural aspects.Lakini siku msipotanguliza adhabu ya kifo kwa apostates na wahubiri wengine mtashangaa!

Hebu nipe sababu zinazoifanya quran kuwa miracle
Uislam sasa ndio din inayoenea kwa kasi america na ulaya kuliko dini yoyote ile makanisa yanafungwa mengine yanabadilishwa kuwa msikiti kuna upanga gani unaotumika au wapi ulisoma Quran au din ilisambazwa kwa upanga...unavijua vita vya msalaba Crusade War??? Had Pope aliomba radh miaka ya juz kati

Hata sayans unayosema ime advance bado isingekuwa rahisi kwanadamu wa zama zile kuzifahamu kwa mfano Quran inazungumzia hatua za ukiwaji wa binadamu ndani ya tumbo la mama yake tena imeanza kwa kusema "mwenyez Mungu anakuumben atakavyo ndani ya viza vitatu amnavyo kisayansi wanasema ni three phases zilizopo kwenye kuta za tumbo la uzazi kisha ikasema unaanza kuwa manii kisha pande dam kisha nyama na kufanyika umbo kala taa, kisha mifupa na mifupa inavikwa nyama na kisha kupukiziwa roho..

Mgunduz wa hatua hiz prof Keeth moore wa chuo cha colorado ambae ndio bingwa embriology alifatwa na waislam wakamuuliza kama hatua zilozoelezwa ndani ya Quran zina ukweli akasema " yapo nakubaliana nayo yapo bado yanahitaji uchunguzi ila kwa haya niliyo yaona ungeniuliza miaka 30 nyuma ninsingekuwa na majibu"
Baada ya hapo akarud maabara kwa msaada wa facts zilizopo kwemye Quran akatoa kitabu kingine ambacho kilishinda tuzo ya kuwa kitabu bora cha embriology ndipo akasema " Ufafanuzi juu ya Hatua za ukuaji wa mwanadamu ndani ya Quran ni far superior kuliko sisi tuliweza kufafanua kwa kuangalia kwa msaada wa microscope hakuna shaka Quran ni devine revelation na Muhammad ni Mtume wa Mungu"

Jop prof hakuwakujulikana alibadili ama vip ila mwenzake alitania akasema huenda Muhaamad alikuwa anawapsua wanawake tumboni na kuangalia akasema hatua za ukuaji wa binadamu huwez kuziona kwa macho yetu had msaada wa vifaa kama micro scope..!

"This is our book and we will guard it against any Curroption" "indeed the promise of Allah is true"
 
Jambo la kwanza mwandishi unapaswa kufahamu nini maana halisi ya neno Biblia, Basi kama maana yake ni mkusanyiko wa vitabu ambavyo vimefanyika kuwa kitabu kimoja chenye vitabu vingi vyenye kuzungumzia matendo na ukuu wa Mungu aliyehai. Basi fahamu kuwa enzi za kale hakuwako mwandishi mmoja mwenye kuandika habari za Mungu ila zile ambazo zilipatikana katika ukusanyaji zikiwa zimekamilika ndizo zilizohifadhiwa kwa pamoja huku kila nakala ikiwa na mwandishi wake, Ndio maana utakuta waandishi wa injili wote waliandika habari ya mtu mmoja kwa kadri ambavyo kila mmoja alivyoipata kwa undani wake kutokana na nafasi yake aliyopata katika shuhuda alizopata kuziona kwa wakati fulani, Kuna wengine waliandika kutokana na kupewa ufunuo na Mungu mfano Yohana aliyeandika "Ufunuo wa Yohana” alipokuwa patmo.
Waandishi walikuwa ni wengi walioandika habari za mtukio ya watu ambao walikuwa maarufu na wenye nguvu katika empire zao ambapo waliwezeshwa na Mungu na sababu zao katika kuanguka, Hivyo katika saula la reference sijaona shida sababu huyo mwaandishi anataka kuthibitisha ukweli wa habari ya matukio kupitia kwenye vitabu vya waandishi wengine ambapo yamkini vitabu vyao vilipotea ama havikukamilika katika nakala za kale ambazo zilipatika hata kukusanywa na kuhifadhiwa pamoja hata leo tunaita Biblia.
Pia ufahamu kuwa kulikuwa upinzani na upotoshaji katika uandishi uliotokana na waandishi hao kutokubaliana na ukweli wa Mungu na matendo aliyoyafanya hivyo kulikuwa na uandishi wa kiitikadi kati ya wapagani na wale wamwabuduo Yehova kabla ya Kristo hivyo kukatokea kupindisha habari na hata kutunga habari za kupotosha ukweli ndipo utakuja kuona hata leo Biblia ya kiroma kuna waandishi ambao wameweka habari zao na ukweli ni kwamba baadhi ya waandishi hao walikuwa ni wapagani wasiojua taratibu za Mungu aliyehai nini anavyopaswa kuabudiwa ila ziliweka ili kushinikiza mambo ambayo hayapo ndio hivyo vitabu vya Mapokeo ya ibada za kipagani.
 
Mkuu Nakuomba ufanye tena Utafiti mwingine juu ya haya ninayotaka kusema hapa!

Kwanza Uislam haukuwepo kabisa kabla ya mwaka 570 AD. Ingawaje Waislam wanadai Uislam ulikuwepo kwa nguvu za kulazimisha tu! Historia ya Mashariki ya kati inakataa (Secular history of the Middle East).
Lakini pia Mohamed(S.A.W) alipoanza huduma ya utume kwa maelezo ya Quran na Hadith alipambana na Makafiri na watu wengine waliokataa na waliopinga sana Ujumbe wa Mja huyu wa Allah;Je Kama Uislam Ulikwepo toka Mwanzo Mohamed alikuja kutangaza nini? Historia inaenda mbali zaidi kueleza jinsi Waarabu walivyokuwa magwiji wa ibada za Sanamu za mawe na Ushirikina.

Pili Habari za Yesu Kristo ambaye kwa madai ya Waislam ni Issa Bin Mariam; ambaye habari zake zinapatikana sana katika Quran Surat Mariam,Surat Al-Imran,Surat Al-Nisa. Habari hizi za Yesu na Issa haziko sawa!
Yesu alizaliwa Kwenye Holi la Ng'ombe wakati Issa alizaliwa chini ya Mtende na kuongea akiwa bado mchanga.
Yesu alikufa na Kufufuka! Issa hakufa bali alibadilishwa asipatikane na Madhara.
Je? KKitabu kipi kinasema kweli? Biblia iliyokuwepo wakati ule au Quran ilikuja kuandikwa baadae?

Tatu Je? JE? UISLAM ambao umekuja baada ya uwepo wa imani nyingi tu duniani kama vile Judaism,Buddhism,Hinduism na Zoroastrianism Umeleta kanuni gani Mpya (mpya kabisa) ambazo hazikuwepo kabla yake? Ubora upi ambao haulinganishwi na Imani zingine?
(Rejea nguzo tano za Uislam kama Nuru ya kujua haya yalikuwepo ama la?)

Mwisho Hujanijibu Swali la Injili,Zaburi na Torati kama na vyewewe vilishushwa na kama vilishushwa vilishushwa lini na wapi?
Wasalam.
Nimekupata na una hoja nzuri kwanza lazima uelewe maana ya uislama ili uweze kuelewa ulikuwepo tangu lini...neno ISLAM linatokana na na mizizi neno ya kiarabu mawili salim lenye maana ya kujisalimisha au kunyenyekea na neno mzizi lingine ni salam maana ya amani ambayo ni sifa moja wapo ya Allah...na ndio maana tunaposalimiana kwa lugha ya kiarabu tunaambianaba asalam aleiku au ki aramec au kiebrania wanasema shalom elechim maana yake aman ya Mungu iwe juu yako..!..so kitendo cha kujisalimisha na kunyenyea mbele ya Mungu kwa kiarabu ndio kinaitwa ISLAM.!

Sasa ukiangalia mafundisho ya mitume wote kuanzia Adam had Noah kama.mtume wa kwanza kutumwa kwa watu wote walikuja na ujumbe mmoja wa watu kujisalimisha nakumtegemea Mungu pekee ambayo ndio kiarabu inatwa islam, din zingine zilitokea kwa baada ya mitume wale kuondoka na watu wakiofata kupotosha wa watu kuamua kuchukua mrengo ambao hawakufundishwa kwa mfano Mussa alitumwa kwa wana wa israel hakufundisha Din ya uyahudi wala hajawahi kusema hicho kitu ila wana wa israel kwa ujeuri wao wakaifanya ikawa dini ya kikabila yaan wewe huwez kuwa dini ya kiyahudi kama wewe sio myahud na hayo ni baada ya Musa kuondoka kwa hiyo uyahud chimbuko lake ni kabila la judas..japo Mussa alifundisha juu ya Mungu mmoja amri kumi za Mungu ila mafundisho ya makihab wengine ndio yalileta hata sababu za kumkataa yesu na Muhamam sababu ilikuwa kila mtume alipokaribia kuondoka aliwapa habari juu ya mtume atakae kuja na juu ya habari ya mtume wa mwisho.!

Au ukija kwenye ukristo ( hapa naomba msini judge kiiman muangalie fact) maana iman zetu sometime zinatufunika kuuona ukweli...neno KRISTIOS ni neno la kigiriki maana ya asili ya neni hili masseh au masih ambalo ndio jina la Yesu kutoka mbinguni kwa mujibu wa Quran inasema marym aliambiwa atapata mtoto jina lake masih ila bible inasema jina lake ataitwa Emmanuel ila uliza mtu yoyote wapi yesu alitumia au aliitwa emmanuel kama jina lake? Ila aliitwa masih ambayo Tafsri ya yake kigiriki ndio KRISTOS na kingereza ikatafsriwa kama Crist..so jina cristians wa wakristo litokana na wayahud kuwaita wafuasi wa yesu wakrsisto kwa kiyahud jina nimelisahu ila kiarabu wanaitwa Nasara ambayo Tafsri yake ni hiyo waktisto...ila wakati wa Yesu alipokuweoo hakuwahi kuhubiri ukristo wala hajawahi kutamka iman ya ukristo sababu kimsingi kristo ni jina lake na asingehubiri jina lake na wakati yeye ametumwa tu...alichohubiri ni watu kumtambua Mungu mmoja na wala hakujiita yeye mungu na wala hakusema watu wamuabudu na wala hakusema ametoka kwenye utatu mtakatifu..ila amesema " baba angu ni mkubwa kuliko wote,au baba angu ni mkubwa mimi na pia akasema " mimi mwenyewe siwez kufanya chochote ninachokisikia ndio ninachokiamua sio kwa matakwa yangu ila kwa baba aliyenituma" na pia akasem "Enyi israel Mungu wangu na Mungu wenu ni Mungu mmoja" kauli hii pia mussa aliwaambia wana israel so Yesu alihubiri ukubwa wa Mungu na watu wajusalimishe mbele ya Mungu na akapewa uwez wa kufanya miujiza mikubwa ili kudhihirisha ili watu wapate kumuamin alichokifundisha yesu kiarabu kinaitwa islam.!

Muhhamad amekuja na Muhuri na ndio mtume wa mwisho ametabiri kwenye vitabu vyote vya dini vilivyotangulia na mitume wote walikuja kabla yake amekuja na mfumo wa maisha unaokidh dunia ya leo had mwisho wa dunia kuanzia ngazi ya familia mtu mmoja mmoja had kitaifa na kidunia uislam umekuja mifumo ya kupambana unaguzi wa aina yoyote,ustawi wa jamii,masuala ya kiuchumi,uhuru na usawa wa kibinadamu,masuala ya ndoa,mirath, mambo ambayo hakuna mtume before alinyanyua mdomo kuyasema walikuja na kaz moja tu kutangaza ukubwa wa Mungu na pili mitume wote walitumwa kwa ajili ya watu fulan na kwa kipind fulan mtume muhammad S.W.A amesema walitumwa mitume 124,000 kabla yangu kila mmoja kwa watu fulan na kipind hata Yesu alikuja kwa ajili ya wana wa israel tu na alisema "sikutumwa ila kwa kondoo walipotea wa nyumba ya israel" ila muhammad alitumwa kwa ajili ya ulimwengu mzima amekuja ku seal utume hata yesu atakapokuja mara ya pili hatakuja na maagizo mapya au kitabu kipya Muhammad anasema atakapokuja tena issa dunia nzima itaamin dini ya Mungu mmoja..!so muhamad ni seal kwenye series ya mitume wote waliotumwa na Mungu na ukifatilia utauona mtiririko ila ukifatilia sijui kiagano kuna sehem utaona kuna disconection kama ilivyo kwa wahayahud nikipata muda nitawaketa ushahid wa muhammda mdani ya agano la kale na agano jipya

Zaburi,torat na injili navyo vilishushwa kama Quran alikiwa akiwasilisha maagizoi hayo ya mwenziMungu na mitume ni malaika Jibril (Gabriel) au roho mtakatifu ila mtu muhammad anasema "torat iliteremka ikiwa imeshandikwa ndio kitabu kilicho andikwa na Allah kwa mkono wake wenyewe..!..ila kitokana na.muda kupitia watu waliingilia maandiko hayo na kwa kujibu wa wanazuoni wa kikristo wanathinbitisha hilo kuwa kuna mambo mengi yameongezwa nahayakiwepo kwenye original na mengine yamepotea...ila.Quran Allah aliahaidi kuilinda na akailinda had leo ipo vile vile hakuna alie ongeza waka.kupunguza japo watu wanajitahidi kupotosha ila kuna fact ukizjua utajua hii ni devine revelation.'!
 
Uislam sasa ndio din inayoenea kwa kasi america na ulaya kuliko dini yoyote ile makanisa yanafungwa mengine yanabadilishwa kuwa msikiti kuna upanga gani unaotumika au wapi ulisoma Quran au din ilisambazwa kwa upanga...unavijua vita vya msalaba Crusade War??? Had Pope aliomba radh miaka ya juz kati

Hata sayans unayosema ime advance bado isingekuwa rahisi kwanadamu wa zama zile kuzifahamu kwa mfano Quran inazungumzia hatua za ukiwaji wa binadamu ndani ya tumbo la mama yake tena imeanza kwa kusema "mwenyez Mungu anakuumben atakavyo ndani ya viza vitatu amnavyo kisayansi wanasema ni three phases zilizopo kwenye kuta za tumbo la uzazi kisha ikasema unaanza kuwa manii kisha pande dam kisha nyama na kufanyika umbo kala taa, kisha mifupa na mifupa inavikwa nyama na kisha kupukiziwa roho..

Mgunduz wa hatua hiz prof Keeth moore wa chuo cha colorado ambae ndio bingwa embriology alifatwa na waislam wakamuuliza kama hatua zilozoelezwa ndani ya Quran zina ukweli akasema " yapo nakubaliana nayo yapo bado yanahitaji uchunguzi ila kwa haya niliyo yaona ungeniuliza miaka 30 nyuma ninsingekuwa na majibu"
Baada ya hapo akarud maabara kwa msaada wa facts zilizopo kwemye Quran akatoa kitabu kingine ambacho kilishinda tuzo ya kuwa kitabu bora cha embriology ndipo akasema " Ufafanuzi juu ya Hatua za ukuaji wa mwanadamu ndani ya Quran ni far superior kuliko sisi tuliweza kufafanua kwa kuangalia kwa msaada wa microscope hakuna shaka Quran ni devine revelation na Muhammad ni Mtume wa Mungu"

Jop prof hakuwakujulikana alibadili ama vip ila mwenzake alitania akasema huenda Muhaamad alikuwa anawapsua wanawake tumboni na kuangalia akasema hatua za ukuaji wa binadamu huwez kuziona kwa macho yetu had msaada wa vifaa kama micro scope..!

"This is our book and we will guard it against any Curroption" "indeed the promise of Allah is true"
Shida yangu ni source za hzo tafiti.Uislamu unakua Ulaya kama ambavyo ukristu unavyokua Africa hiyo siyo sababu ya kuifanya Quran kutokuwa na makosa.Na hiyo ulaya unayoiongelea ni Ufaransa na Ujerumani tu refer demography ya nchi hizo mbili na sababu zinazopelekea.
i am glad umejibu vyema sana kuhusu kuiprotect quran,na hicho ndicho nilichomaanisha ila wewe hukunielewa vzr.Methodology ya protection ya quran ni upanga and not otherwise.Sijaongelea kuhusu spread kupitia upanga japo huwez kutumia crusade kama base ya usambazaji wa christianity.Katika mitume wote wa Yesu hakuna aliyetumia upanga kusambaza dini lkn mtume na maswahaba wake walitumia upanga kwa ahadi ya kubikiri wanawake watamu.
 
Nani kaviita vya kipagani,au unajaribu kukoleza stori,si kweli kuwa kitabu au nyaraka au habari kutokuwa ndani ya biblia inamaana ni ya kipagani,
Okay naviita vya kipagani kwa sababu kati ya vitabu vilivyokuwa referred kuna Book of jasher na Book of Enoch

Sasa book of Enock inasema malaika ndio walijenga safina ilihali Biblia inasema ni Nuhu.... Pia Henoko anadai malaika kuzaa na binadamu ndio kulimuudhi Mungu kuleta gharika ilihali Biblia inasema DHAMBI ndio zilisababisha?? Sasa nikikiita kitabu cha Enock ni cha kipagani nakosea au wwe unakiona sio cha kipagani ilihali kinapingana na Biblia?? Hapo sijaongelea ukinzano uliofanywa na Book of Jasher kuwa Pharaoh hakufia baharini na Musa hakuenda Midian n.k je ww vitabu hivi utaviitaje??

Karibu tueleweshane
 
Wakuu nimeweka hii mada tujadili hayo maswali yangu ila sikuwa na matarajio uzi huu utageuka wa kushambuliana kidini mara Quran hivi mara Biblia hivi.... Ningeomba tubaki kwenye hoja

Cc Half Genious Nantahulila
 
Jambo la kwanza mwandishi unapaswa kufahamu nini maana halisi ya neno Biblia, Basi kama maana yake ni mkusanyiko wa vitabu ambavyo vimefanyika kuwa kitabu kimoja chenye vitabu vingi vyenye kuzungumzia matendo na ukuu wa Mungu aliyehai. Basi fahamu kuwa enzi za kale hakuwako mwandishi mmoja mwenye kuandika habari za Mungu ila zile ambazo zilipatikana katika ukusanyaji zikiwa zimekamilika ndizo zilizohifadhiwa kwa pamoja huku kila nakala ikiwa na mwandishi wake, Ndio maana utakuta waandishi wa injili wote waliandika habari ya mtu mmoja kwa kadri ambavyo kila mmoja alivyoipata kwa undani wake kutokana na nafasi yake aliyopata katika shuhuda alizopata kuziona kwa wakati fulani, Kuna wengine waliandika kutokana na kupewa ufunuo na Mungu mfano Yohana aliyeandika "Ufunuo wa Yohana” alipokuwa patmo.
Waandishi walikuwa ni wengi walioandika habari za mtukio ya watu ambao walikuwa maarufu na wenye nguvu katika empire zao ambapo waliwezeshwa na Mungu na sababu zao katika kuanguka, Hivyo katika saula la reference sijaona shida sababu huyo mwaandishi anataka kuthibitisha ukweli wa habari ya matukio kupitia kwenye vitabu vya waandishi wengine ambapo yamkini vitabu vyao vilipotea ama havikukamilika katika nakala za kale ambazo zilipatika hata kukusanywa na kuhifadhiwa pamoja hata leo tunaita Biblia.
Pia ufahamu kuwa kulikuwa upinzani na upotoshaji katika uandishi uliotokana na waandishi hao kutokubaliana na ukweli wa Mungu na matendo aliyoyafanya hivyo kulikuwa na uandishi wa kiitikadi kati ya wapagani na wale wamwabuduo Yehova kabla ya Kristo hivyo kukatokea kupindisha habari na hata kutunga habari za kupotosha ukweli ndipo utakuja kuona hata leo Biblia ya kiroma kuna waandishi ambao wameweka habari zao na ukweli ni kwamba baadhi ya waandishi hao walikuwa ni wapagani wasiojua taratibu za Mungu aliyehai nini anavyopaswa kuabudiwa ila ziliweka ili kushinikiza mambo ambayo hayapo ndio hivyo vitabu vya Mapokeo ya ibada za kipagani.
Kumbe hamna shida kunakili vitabu vya pembeni?? Sasa kwanini humu JF na platform nyingine ukijengea hoja ya let's say maisha ya Yesu au Daudi kwa kutumia hivyo vitabu ambavyo hao manabii walivinakiri hoja hizo hupingwa??

Ndio swali langu linakuja hapo...... Yaani kwanini wakiquote manabii hakuna shida ila tukiquote sisi inapingwa kwa hoja kwamba "BIBLIA HAIKUANDIKA HIVYO"

Kingine vitabu hivyo havikuingizwa kwenye Biblia sababu walisema havina uvuvio wa Roho mtakatifu sasa swali kwanini manabii wa Biblia wananakiri vitabu visivyo na uvuvio wa Roho mtakatifu??

Huoni kuna double standards mkuu
 
Shida yangu ni source za hzo tafiti.Uislamu unakua Ulaya kama ambavyo ukristu unavyokua Africa hiyo siyo sababu ya kuifanya Quran kutokuwa na makosa.Na hiyo ulaya unayoiongelea ni Ufaransa na Ujerumani tu refer demography ya nchi hizo mbili na sababu zinazopelekea.
i am glad umejibu vyema sana kuhusu kuiprotect quran,na hicho ndicho nilichomaanisha ila wewe hukunielewa vzr.Methodology ya protection ya quran ni upanga and not otherwise.Sijaongelea kuhusu spread kupitia upanga japo huwez kutumia crusade kama base ya usambazaji wa christianity.Katika mitume wote wa Yesu hakuna aliyetumia upanga kusambaza dini lkn mtume na maswahaba wake walitumia upanga kwa ahadi ya kubikiri wanawake watamu.
Daud hakupiga vita?joshua hakupigana vita? nitajie vita ambavyo muhammad alienda kuvamia aidha mji au eneeo ili watu waukubali uislam vita zote alizopigana Muhamamad ni vita vya kujihami dhid ya uvamiz na ndio kasome surati Tawba utaona masharti ya vita vya jihad...neno UPANGA halipo kwenye Quran nzima lakin lipo kwenye biblia mara 200...hakuna mtume alieneza neno la Mungu kwa upanga ilanwajihami hata Yesu alikuwa kwa lolote maaana aliwaambiwa wanfunzi asiekuwa na UPANGA akauze makoti yao wanunue upanga na hata wanafunzi wake walimwambia tutakulinda kwa panga hiz tulizonazo ili tukio la kusulubishwa lisitokee na akawaambia wazitunze panga zao na Yuda alipoenda kumsaliti bible inasema alikatwa sikio na mmoja wa wanafunzi wa Yesu ndio kilichotokea kwa mitume wote bahari ya muhamad alifanikiwa kama kija DAUD,SULEIMAN walifanikiwa had kuunda majeshi lakin yote yalikiwa katikana kujihami na kujilinda muhhamad hajafanya uvamiz popote na aliishi madina na wayahud na had anakufa sio watu wote walikuwa ni waislam pale makka...

Fact nilizokupa za spread of islam zipo hata google zipo hata cnn walikuwa na wanajadili huli suala sababu baada ya 9/11 pale newyork kulisababisha watu wengi kuanza kuufantilia uislama lakin ndio kipindi uislam kasi ya kushambukiwa iliongezeka mara 100 lakin watu wakakuta matarial walikuwa wanapewa na propaganda za kwemye media sio za kweli utamaduni wao wakufanya utafiti unawasaidia kujua ukweli wa mambo mengi africa ni rahisi ukristo kuoenea sababu waafrica muda wa utafiti hamna ilia mrad tukisahaletewa miujiza iwe ya ukweli au ya uwongo tunakwenda na maji haya maandiko waafrica tunayaogopabhata kuyahoji kwa kusema ni maneno ya Mungu yasiguswe Kumbe Mungu anataka umtafute atakuonesha njia..!


Kama pepon, hakuna wanawake wazuri,mito ya maziwa na asali yaana niende tu kuimba mapambio na kusifu bora nibaki duniani milele kuna starehe zaid..!
 
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
Sasa kama lutu alilala nawawe na biblia imeandika ivyo,mbona kwa daudi haikuandika kuwa alilala na Jonathan I?
 
Back
Top Bottom