Kwa hali nchi ilipofikishwa na Jk ikulu kufanywa pango la wanyang'anyi.Sehemu yakufanyia biashara ya uwaziri nalazimika kukumbuka kauli ya Mzee Mkapa kwamba tutamkumbuka.
Japokuwa Mh.Mkapa alikuwa na mapungufu yake lkn hakuwa dhaifu kama huu.
Mkapa alipokea nchi kutoka kwa dhaifu wa kukusanya kodi na alipokuwa anatoka akamwachia dhaifu wa kufuja kodi zetu.
Jk hakumbuki kuwa Mh. Mkapa alituambia tufunge mikanda na akasahau kutuambia tuifungue mpaka leo.
Tulikubali kufunga mkanda akajenga barabara, bunge la kisasa ambalo wassira na komba wanachapa usingizi,uwanja wa mpira wa kisasa,majengo pacha ya benki kuu, jk airport,ndege ya rais,rada,daraja la Mkapa n.k
Alirudisha heshima ya mfanyakazi iliyokuwa imepotea kipindi cha ruksa
Leo hii ni MAJANGA. Sio serikalini sio chamani kote kumekuwa kama familia ya MAPANYA .baba mwizi, mama,watoto,shangazi, mjomba,wajukuu wote wezi.
kwa shingo upande nalazimika kumkumbuka Mzee Mkapa pamoja na madhaifu yake.
teeh teeh, kaka nimecheka hadi nimejamba. Kweli nchi hii mwinyi aliiuguza, Mkapa akaitibisha na ikapona, Kikwete ameibebenda na afya ya nchi imezorota kama mtoto mwenye kwashiorkor, imedumaa na huenda ikafariki kabisa.