Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 5,369
- 5,512
Hii sasa ni total desperation. Mkapa anakumbukwa kwa "mema"? Hakuna mtu asiye na mema kabisa hapa duniani. Hata Mobutu, Idd Amin na Hitler walikuwa na mema yao. Vigezo pekee vya kumkumbuka rais mstaafu ni uongozi thabiti (sio udikteta), uadilifu, uzalendo na kusimamia katiba na haki za binadamu kikamilifu. Muhimu zaidi ni rais ambaye akiondoka anaiacha nchi ikiwa kwenye mwelekeo bora wa maendeleo.
Hakuna rais anayeweza kuwa na sifa hizo huku akisimamia mfumo wa kifisadi unaozingatiwa kikamilifu na chama chake cha siasa. Mkapa ni mwana-CCM kamili na hana tatizo kabisa na jinsi chama hicho kilivyo. Yeye ndiye muumin mkuu wa mwenendo wa kuukabidhi uchumi kwa wawekezaji wa nje kama ndiyo mkakati pekee wa maendeleo. Dharau yake kwa wazawa ilikuwa wazi kabisa bila hata ya kujaribu kuonyesha ni jinsi gani anavyoweza kubadili huo "uduni" wa wananchi wake wawe na uwezo zaidi wa kufikiri na kutenda.
Kwa mtu aliyesimamia ufisadi mkubwa wa rasilimali za taifa na kutishia waliojaribu kuhoji na kisha kurithisha mwenendo huo kwa aliyemfuatia sioni haja ya kumkumbuka kwa chochote; labda waliofadhiliwa kibinafsi wakumbuke. Kwamba aliyefuatia ndio ovyo zaidi si hoja ya maana ya kumkumbuka aliyetangulia katika uozo huohuo. Fisadi ni fisadi tu. You may hate JK, but BM is just another side of the same coin. They play the same game in differing styles.
Hakuna rais anayeweza kuwa na sifa hizo huku akisimamia mfumo wa kifisadi unaozingatiwa kikamilifu na chama chake cha siasa. Mkapa ni mwana-CCM kamili na hana tatizo kabisa na jinsi chama hicho kilivyo. Yeye ndiye muumin mkuu wa mwenendo wa kuukabidhi uchumi kwa wawekezaji wa nje kama ndiyo mkakati pekee wa maendeleo. Dharau yake kwa wazawa ilikuwa wazi kabisa bila hata ya kujaribu kuonyesha ni jinsi gani anavyoweza kubadili huo "uduni" wa wananchi wake wawe na uwezo zaidi wa kufikiri na kutenda.
Kwa mtu aliyesimamia ufisadi mkubwa wa rasilimali za taifa na kutishia waliojaribu kuhoji na kisha kurithisha mwenendo huo kwa aliyemfuatia sioni haja ya kumkumbuka kwa chochote; labda waliofadhiliwa kibinafsi wakumbuke. Kwamba aliyefuatia ndio ovyo zaidi si hoja ya maana ya kumkumbuka aliyetangulia katika uozo huohuo. Fisadi ni fisadi tu. You may hate JK, but BM is just another side of the same coin. They play the same game in differing styles.