Ndio maana nikasema katika juhudi za kuleta amani au utulivu au kuhukumu mwenye makosa, si kwa sababu ya mtu dini
yake hayo yatekelezwe kwa mtanzania na maslahi ya kitanzania! hata waislam hawapendi kuonekana wao ndio shida, kama wengine mnasema waislam hawajasoma ndio maana lakini yote sio kweli, usishangae ukaona uwiano wa PhD za waislam na wasiokuwa waislam zikawa sawa hapa tanzania, watu wamesoma lakini hawapendi kujionesha au kujigamba Mungu hapendi majivuno!!
Hata mimi sikusema dini ya mtu, nilizungumzia Ponda na UAMSHO.
Namjua Ponda kwa uchochezi wake na si kwa dini yake. Hayo ya dini ya Ponda mimi sijayasema.
Naijua UAMSHO kwa kadhia iliyofanya Zanzibar na sio kwa dini yake.
Wewe umerukia kwenye dini kwa kuwa ndio silaha ya watu wajinga. Facts kwao hazina maana zaidi ya imani. Ukifuata facts utakubaliana na mm kuwa Ponda ni mpumbavu na ndio maana anaamini kuwa haki yake ataipata kwa mnunuzi badala ya aliyeuza.
Kuhusu wasomi, huo ni upuuzi mkubwa mkuu. Jambo lililofanyika haliwezi kamwe kufanywa na mtu mwenye elimu nyingine zaidi ya ile aliyonayo Ponda. Hebu niambie ikiwa unaamini yule Dr. Twalib Ngoma anaweza kwenda na kundi la watu kudai mali ya waislamu ambayo tayari imeshauzwa?
Hata wewe ni mjinga, nitakwambia kwa nini. Kama unadhani kuna wasomi wa imani kama yako, mbona usijiulize kwa nini wao hawashiriki mambo yale aliyofanya Ponda kama si kwa sababu ni mambo ya kijinga?
Wote walioko pale na walioshiriki vurugu hizi ni vijana waliofeli maisha baada ya kuzaliwa wengi kwa mzazi mmoja kiasi resources hazikutosha kuwaendeleza, wamama waliokata tamaa ya maisha na wanazuoni wa madrasa ambao madarsa ya elimu ya magharibi yamewaacha, kama alivyo Ponda mwenyewe.
Sidhani mtu na PhD unayoisema anaweza kuvaa suruali fupi. Atajiuliza tu maswali madogo; nivae suruali ichafuke mguu ubakie safi au nivae fupi isichafuke lkn mguu ujae vumbi.
Mwenye PhD anajua kuwa ukimpa Juma mali akulindie, Juma akaiuza kwa Jabiri basi unayetakiwa kumdai ni Juma na sio kwenda kumfanyia fujo Jabiri.
Kutetea ujinga hakuwezi kufanywa na mtu mwenye akili