Ben Saanane awatoa Mafichoni Zitto na wenzake

Ben Saanane awatoa Mafichoni Zitto na wenzake

Status
Not open for further replies.
1.Zitto zuberi kabwe,
naibu katibu mkuu,,,,,,,, M4C hajawahi kushiriki hata moja!
2. Dr slaa kama hayupo na zitto yupo, mnyika anakaimu karibu mkuu.
Nilikuwa najiuliza kwanini? Kumbe kikosi cha ukachero chadema kilishajua
nyendo zake. Kwa kweli Dr slaa na Mbowe mnastahili sifa.

Ha ha ha ha haaa, mkuu hata mi nlikuwa nashangaa sana kwa nini inakuwa hivyo???.

Kumbe Joka lishajulikana zamani sana anasubiriwa tu anase mwenyewe.
Bravo CDM.
 
Hii hapa chini ni quotation ya ujumbe mzito wa Ben sanane ktk fcbk wall yake muda huu

"Chama kitakapowashughulikia masalia PM7/, watakaoathirika zaidi ni CCM- Trust me!"

my outlok:
Naona kuna haja ya chama kukaa chini na kijana huyu jasiri ili kudadavua mchakato mzima wa kuwashughulikia PM7 masalia kwani naamin kwa kazi aliyofanya Ben na kwa ujumbe huu anaoutoa Ben ni wazi kwamba ana muono mkubwa sana juu ya kazi za hili kundi na CCM pia yupo ver familiar na impact zake baada ya chama kuwashughulikia.
 
Hawa jamaa wamekamatika vizuri sana.

Ni Kama nyoka walioibuka kwa kuchomewa matairi kwenye mashimo yao ya maficho
 
hivi kuna watu wana laana eh?hivi saiv Kaborou cjui nan yule wa Kigoma yuko wap?Zito bado hajabalehe nahc..
 
Hapana, Ben Saa8 hakuwa msaliti bali amefanya kazi nzuri sana. Kazi aliyotumwa ameimaliza. Hoja kwamba haonekani kwenye ujenzi wa Chama kwenye majukwaa ni dhaifu kwani kazi hii aliyoifanya ni moja ya kazi za ujenzi wa Chama.

Hongera Ben Saa8 na Mamuya mmefanya kazi nzuri.

Maana Watu wangejitolea kujenga chama huku wengine wako bize kubomoa.

Fire them all, Zitto,et al!

Kazi hii katumwa na nani? Hiki chama kinaanza kupoteza matumaini ya baadhi ya wananchi, hasa mimi. BTW mwanasiasa ni mwanasiasa tu.

Zitto ajiondoe au afukuzwe kwenye chama ili chama kianze mwanzo kabisa (2015 tuisahau kama hili likitokea), na Zitto hatakaa awe rais wa hii nchi kupitia CDM kwa sababu:-

1. Ni mdini (sio mkristo);
2. Ana tamaa;
3. Ana dharau;
4. Anatoka Kigoma na kajitangazia uchawi tayari;
5. Ni fisadi;
6. Hana uvumilivu; na
7. Anaropoka ovyo.

Nina uhakika kwa yanayotokea sasa ni kutuonyesha pande zote za huyu Bwana, nina uhakika watanzania hatuko tayari tena kurudia kosa, hii miaka kumi inatutosha, "Birds of the same feathers fly together".
 
Ben saanane ni kijana shujaa sana nampongeza sana na Nina amini ametutoa pabaya kwani sasa majibu tumeyapata ya maswali tuliyokuwa tunajiuliza mfano.

1-kwanini zito haonekani kwenye harakati?
2-kwa nini zito amekuwa akipingana na wenzake pale wanaposhinikiza serikali?
3- kwanini Zitto amekuwa akipingana na kukejeli safari za JK wakati yeye kila kukicha ni pipa?
4-kwanini zito hapokei ushauri wa wazee wa cdm?
5-kwanini ajione yeye ndio anayefaa Kuwa raisi ndani ya cdm na sio mwingine?

Hapo ndio nadhibitisha Kuwa alikuwa anavuruga cdm badala ya kuijenga. Asante sana Ben Saanane kwa ujasiri wako.

Nakuunga mkono Zitto siku hizi haonekani kwenye harakati na maranyingi amekuwa akipingana na viongozi wake. HUYU JAMAA NI YUDA
 
Nimefuatilia kwa ukaribu na kwa umakini sana hili sakata, Ben Saanane ni kijana shujaa na Chadema inapaswa kumuweka kwenye vitabu vya kumbukumbu, wale wapuuzi wa Zitto Kabwe wote sasa wamekimbia hapa JF na wanatapatapa tu, Zitto avuliwe uanachama sasa na si vinginevyo.
 
Last edited by a moderator:
Zitto hafai kuwa rais nia yake ni mbaya

Nimeshangazwa na maneno ya ZZK alivyosema "........ mimi nimetoka kwetu Kigoma NIMEAGA......... kama atatokea mtu wa kutoa uhai wangu, ifahamike kuwa nyumbani kwa mtu huyo hakitasalia chochote hadi panya" Haya ni maneno ya mtu anaejipambanua kugombea urais 2015. Naomba Zitto aichapishe nukuu yake hii katika ilani yake endapo atamsimama kugombea uraisi kwa tiketi ya chama chochote au mgombea binafsi ili atueleze umuhimu wa kuwa na Raisi mshirikina.
 
Tatizo lenu wadau munakomenti kwa kuendeshwa na hisia na sio uhalisia.laiti kama mungepewa kutoa hukumu kama majaji basi mungewahukumu watu bila kuzingatia uhalisia.
Someni kwa makini facts,angalieni history background ya tatizo,wahusika na ushahidi walio nao,mutapata ukweli ninani mtuhumiwa sahihi wakuhukumiwa!
 
Simpongezi Ben Saanane kwa sababu alikua pamoja nao na bila kutokea kutoelewana asingeyasema hayo. Nae ni mnafiki ingawa amesaidia kujua tatizo linalowakabili vijana na lengo lao kuu ambalo kimsingi ni tofauti kabisa na lengo la chama. Wahusika wote wamekichafua chama kwa namna moja ama nyingine na hivyo wanastahili karipio kali na kuwekwa sawa ili kujenga chama, kuwafukuza uanachama haitakua suluhisho ama njia ya kujenga chama bali kubomoa.
 
Kwanini Mh.Zitto a.k.a kiboko ya mapanya yaliyoshindikana asilisaidie taifa na panya wanaokula viazi na mihogo mashambani kwetu shy vijini,badala yake analeta unafiki na usaliti wa kitoto na kijinga?-ajiuzuru tu,au ahamie Yanga tu.Hafai kuwa rais.
 
😕 "Wanafunzi wanaopata Mimba ni kwa sababu ya kiherehere chao" JK 2010🙄.
:A S angry:" Uwepo wa foleni dar es salaam ni dalili za maendeleo":target:
 
6. Kwa nini Zito atangaze nia ya kugombea Urais 2010 wakati akijua Chadema inamgombea ambaye alikuwa ni Dr. Slaa?
7. Kwa nini Zito atangaze kugombea urais mapema namna hii (2012) wakati wenzake wapo kwenye harakati za kujenga Chama?
8. Kwa nini Zito awe karibu kiasi kile na Usalama wa Taifa wanaoshughulikia siasa?
9. Kwa nini ......

Kwa nini Zitto asiheshemu ridhaa aliyopewa na wananchi wake kuwatumikia kwa uadilifu?
Kwa nini Zitto anatusaliti......................
 
Na kwa nini ashinikize umri wa wagombea Uraisi upunguzweeeeeeeeee..................... ????????????????????

Halafu kuna kauli ya kijinga inatolew kuwa eti wazee waliozaliwa kabla ya uhuru hawafai kutuongoza! aibu sana kwa huyu kijana !
 
kwanza anayemchagua na kumpa zitto uraisi nani? mwanga huyo anayelala kwa sangoma usiku na mchana
mmh! kwahiyo na kujifanya kote anataka kugombea uraisi eti kisa sangoma kamuahidi ushindi?! lol kabwe! labda kama Mungu aliyeziumba mbingu na nchi hayupo utapata huo urais lakn km yupo basi ndoto zako za uraisi sahau. nyzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz akah!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom