Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

Hivi katika post zote mbili,wana jf mnapata onnection ya moja kwa moja ya zitto na usaliti anaousema ben???
Ben hakuna sehemu aliyomuonesha zitto akiuwa na kundi hili zaidi ya bla bla za maneno yake.lakini ni wapi zittto anaingia kwenye hizi shutuma?

Taswira:Soon utaanzisha uzi wako na true ID yako.Endelea kupaka rangi upepo.Tumeshawaelewa wote kwa rangi zenu endeleeni kujipambanua pamoja kitumbua kuingia mchanga bado mnaendelea na vikao kujibu ujinga?
 
Wazee wenyewe wamekaa kimya..tunaangalia.

Na bora mkae kimya mje kuibuka kila kitu kimeeleweka na mashudu yamenyooshwa.CHADEMA haiwezi kwenda mbele bila kumaliza hiki kitimtim, kimekuwepo kwa muda mrefu so kuteketezwa kwake ndiyo safari njema ya chama hiki kinachomulikwa kama tumaini la watanzania mafukara
 
There are currently 320 users browsing this thread. (144 members and 176 guests)

 
Endeleeni na michezo yenu zitabaki sufuria na vikombe tu.

vp zile sku tisini za kuogopana bado ngapi? Huku si tunachanana tu, chama ni uma sio mtu kama mnavoishi chama lenu magamba
 
Ukitafakari kwa makini utaona both BAVICHA & UVCCM have one thing in common - wanatumika.

Halafu wanatuambia mtu anayefaa kuwa rais awe amezaliwa baada ya 1961! Wengine wanataka kubadili katiba kabisa ili watuwekee haya mayenu!
 
Toa takataka yako hii uliyoandika isiyoeleweka peleka kwenu huko ulikuwa wapi siku zote kusema haya mpaka umengojea Ben Saanane kutiririka mambo yote na wewe ndiyo unakurupuka na story za kiabunuwasi zisizo kuwa na kichwa wala miguu na subirini tu ushahidi utazidi kupatikana tu CDM kilianza na Mungu na mambo yote mabaya juu yake yatamalizwa na Mungu
 
Ben amefanya kazi ya uspy na amefanikiwa, maelezo ya Ben yanaonesha ukweli ila watuhumiwa kama Mchange wameshikwa pabaya, hawajitetei wao binafsi bila kumsifia na kumpamba Zitto, hii inaonesha kuna uhusiano mkubwa kati yao.Kweli inaonesha Ben alikua msaliti ama iwe kwa kutaka kuwafahamu maadui wa chama au kwa maslahi yake binafsi ,ila amekiri na kuamua jitoa jambo ambalo wenzake kama mtuma post hii imewaudhi.Namshauri Ben awasilishe ushahidi wake kunako husika na wale wanaopinga pia wawasilishe ushaidi wa kujitetea

uchambuzi nimefanya baada ya kusoma post ya Mamuya, Zitto, Ben Saa nane ,Mchange na Juliana Shonza.
 
Mchange, Zitto, Juliana Shonza, Mtela Mwampamba ni wanafiki wakubwa kwa hoja 2 kuu;

1. Mchange, hii story umetunga na kuiunga unga tuu, haiwezekani mtu anayetaka kukua kwa ajali ya gari afungue tairi ya nyuma ya gari wakati anajua kwa kufanya hivyo huwezi kupata ajari mbaya inayoweza sababisha kifo. Umeandika hivyo kwa sababu HUJUI NA NI LIMBUKENI wa magari so hukujua unachokiandika.

2. Mdogo wangu MWAMPAMBA alitusaliti kule jimboni kwetu baada ya kumpigia kura za yeye kua mbunge but kwa roho yake ya unafiki akauza matokeo kwa CCM (Mh. Zambi) hivyo inanifanya niamini kuwa hata siku moja kunguru hawezi kuruka pamoja na njiwa. Japo kabla sijathibitisha kua anaweeza akawa mnafiki nilifanya kazi kubwa sana ya kumtetea jimboni kuwa namfahamu vizuri asingeweza kuuza matokeo ila naijutia nafsi yangu.

mchange ni maskini sana ndio kwanza katoka kumaliza chuo amesomeshwa kwa mkopo, ndo mana ukimtoa out lazma bill yote ulipie wewe,. Saiz kajiliwa na zitto kubeba tunguri zake msameheni jamani, ni ufukara wake sio yeye
 
Last edited by a moderator:
Mchange Juliana Shonza na Mtela Mwampamba kwanini mlikuwa mnatumia ID ya Tuntemkeke JF kuwatukana viongozi wa chama? Pia yale matusi mliokuwa mkitukana fcbk nayo pia mlitumwa na Ben? Pia yale matishirt yalioandikuwa MOVEMENT 4 CHAGAS mliyoyatengeneza kwa msaada wa mwigulu je nayo Ben aliwatuma?

Inahitaji akili ya maiti kuwaelewa.
 
Last edited by a moderator:
SAA NANE, Waislam wanasema sifa za mnafiki tatu (ayatul munafiq tharasa).
1. akiongea huongea uwongo..
2..akiaminiwa hajiaminishi/hudhiaki..na ..
3..akiahidi hatimizi..

A salalee........hii mbona inamgusa 100% Baba Mdogo wa Taifa?
 
Vijana wa CDM hakuna lolote. Tuwaachie wenye umri wa makamo na wazee waendelee kugombea uongozi (ukiwamo na ubunge), sisi vijana tuwe wapiga kura tu!

hilo zengwe lote limepangwa na mzee.huyo ben alitumika tu ili kuwaingiza mkenge vijana afu baadae awaexpose waonekane hawafai target hasa ikiwa ni zito na lengo ikiwa ni kumfanya aonekane hafai kugombea urais kupitia chadema.FOLLOW THE MONEY TRAIL,hizo pesa za kufacilitate vikao vyao lilikua ni fungu anapewa huyo ben na huyo mzee ili awakamate vizuri hao kina machage.
Anaporudi kusema kuwa anakiri kuwa alikua akisaliti chama wakati ndo yeye alianzisha kundi hilo hapo ndo anapowapiga changa la macho wasiopembua masuala .hii inaonyesha chadema walivyo na kiu kubwa ya madaraka hasa huyo mzee.
Tulidhani kina lowasa ndo vinara wa hayo mambo kumbe humo chadema ndo wako more advanced hasa huyo mzee.
 
Toa takataka yako hii uliyoandika isiyoeleweka peleka kwenu huko ulikuwa wapi siku zote kusema haya mpaka umengojea Ben Saanane kutiririka mambo yote na wewe ndiyo unakurupuka na story za kiabunuwasi zisizo kuwa na kichwa wala miguu na subirini tu ushahidi utazidi kupatikana tu CDM kilianza na Mungu na mambo yote mabaya juu yake yatamalizwa na Mungu
umeshachagua upande na wewe..ulitaka aanze nani?..mbona SAA NANE haukumuuliza kuwa alikuwa wapi kabla hajakanwa na zitto?..think critically
 
lakini mbona wanaotuhumiwa wanaokihujumu chama wote sio wachaga ? kunanini hapa ?
 
Tatizo la hiki chama hakuna adabu, na hiyo ndio inatofautisha CCM na CDM, pamoja na udhaifu wao ccm is well organised n more disciplined, hawaropoki ovyo ovyo tu kama hawa cdm yaani kila mtu anaropoka tuu, ovyo hakuna staha wala kujua nini cha kuongea mbele za watu na nini cha kuhifadhi twende kikaoni, ukiangalia hapa yupo mtu anaitwa Mchange, sijui juliana sasa hawa wote kwanini wasisemane kwenye vikao..nadhani hawa wanaojita vijana ni wavulana na wasichana sio vijana na sasa wanatumika kwa njaa njaa zao..

I can simply say you guys HAMTOSHI KABISA...
 
umeshachagua upande na wewe..ulitaka aanze nani?..mbona SAA NANE haukumuuliza kuwa alikuwa wapi kabla hajakanwa na zitto?..think critically

There we go! Kama mtu hakufahamu ATAKUKANAJE????
 
Back
Top Bottom