Nimesoma hizi post tangu Juzi usiku ile ya
Exaud Mamuya na jana ya
Ben Saanane na leo hii nimesoma hii yako. Nilikuwa sijachangia lolote.
Baada ya kusoma pia na mjibu ya
Zitto ya juzi usiku kwa Mamuya, nahisi kuna uvundo mkubwa kati yako na Zitto et al!
Sipendi migogoro na sipendi kushabikia Migogoro, lakini majibu yako yanafanana kwa kiasi kikubwa sana na alichokiandika Zitto kwa Mamuya Juzi. It seems you have something in Common with him.
Hujajibu hoja zozote za Ben Saanane so far, Ulichokifanya ni ku-revenge. Hebu jibu kile alichokieleza kwenye post yake ili tujue nani mkweli na nani muongo. Kumshambulia badala ya kujibu hoja zake kama alivyofanya Zitto juzi kushambulia badala ya kujibu MNAKOSEA!
Anyway nawatakieni mema kwenye chama chenu maana mie sio mwanachama wa chama chochote duniani. Lakini kiukweli, Zitto, wewe, akina Chagulani, Juliana Shonza na wengineo mlioko 'Masalia' mnayoibadili jina na kuiita PM7 leo mnatukatisha tamaa sisi vijana tunaohitaji mabadiliko.
Mzikubali kuongozwa na uchu wa madaraka kiasi hicho, msikubali kuongozwa na utumwa wa akili kiasi hicho na kumwabudu Zitto kama Mungu, msikubali kuingiza ushetani na kwenda kwa waganga katika mambo ya msingi kama haya. Unapokubaliana na Zitto kuwa ameaga kwao nazidi kuthibitisha kile alichosema Saanane kuwa mnaabudu ushirikina sana. Kijana anapokuwa mshirikina, mzee kama Kingunge afanye nini??? Shame on You!
Nimeongea kwa hasira kidogo sababu umeniudhi kushindwa kujibu hoja na badala yake unashambulia kama njia yako ya kujibu mapigo. Vijana huwa tunashindana kwa hoja ambapo hoja lazima ijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo.
Nimeona post za Shonza Facebook akimtaka Zitto akae kimya na kuonyesha kuwa yeye ni kiongozi. Sawa, wewe inaonekana umetumwa na Zitto kujibu kwa niaba yake maana muda wote wa mchana ulikuwa wapi kujibu au tangu juzi alipotuma thread Mamuya na badala yake umeibuka saa saba hii usiku???
Ngoja niishie hapa kwanza naenda kulala nitarejea asubuhi kuona kama utakuwa umejibu hoja alizozisema Mamuya na Saanane dhidi yako wewe na Masalia wenzako plus bosi wenu Zitto.
Asalam Aleykum