Beki wa Manchester City, Kyle Walker, ameiomba radhi familia yake kwa kufanya uamuzi wa ovyo kufuatia wiki kadhaa za tetesi kuhusu usaliti kwenye ndoa yake.
Mchezaji huyo ameliambia gazeti la the Sun, kuhusu uhusiano wa kimapenzi [mchepuko] na Lauryn Goodman, mtangazaji wa TV.
“Nilichokifanya ni kibaya mno,” alisema, huku akimuomba radhi mke wake Annie Kilner, ambaye ni mjamzito, na ambaye tayari wana watoto watatu pamoja.
“Matendo yangu yamesababisha maumivu makubwa kwa watu wengi. Naomba radhi kwa sababu kama mtu wa familia, hili halitakiwi kutokea.”
The Sun limeripoti kuwa Walker alipata watoto wawili na Goodman, wakati akiwa kwenye ndoa na mkewe Annie.
Nini maoni yako?
Source -The sun
Written by Mjanja M1