Tuzifahamu hizo hoteli njia zote kuanzia dar to moshi/arusha, dar to mwanza, musoma, bukoba, dar to iringa, mbeya, maana asubuhi umepata chai lazima ubanwe na mkojo kukojoa ni korogwe au mombo kama unaenda moshi/arusha. Unakojoa morogoro mpaka shinyanga kama unaenda mwanza. Ukitoka moshi kukojoa/kunya ni babati. Safari usiwe makulakula sana utapata shida ya kujisaidia kituo na kituo na umbali mrefu sana. Unakula chakula ghali safarini halafu unaishia kufedheheka pindi ukibanwa na haja zote mbili. Kumekuwa na visa vingi sana vya abiria kufedheheka kwa kutokwa na haja bila kutaka. Kuficha aibu wengine huzingizia ni wagonjwa baada ya haja kuwatoka kwa kushindwa kujikaza hadi wafike kituo cha kujisaidia chooni