Bei ya gesi huko Ulaya inazidi kupanda na kufikia rekodi mpya, hali ambayo inaziletea nchi za Ulaya wasiwasi mkubwa kuhusu uhaba wa nishati.
Ufaransa imeweka mpango wa kubana matumizi ya nishati kote nchini, na kutoa wito kwa wananchi wapunguze muda wa kuoga, na kuzima kabisa vifaa vya kielektroniki wakati wa usiku.
Uingereza inapanga kufungua maeneo ya umma yenye vifaa vya kupasha joto kama vile maktaba kwa wananchi kuepuka baridi.
Huko Italia, familia nyingi zimeanza kukusanya kuni ili kuepuka baridi kali.