Bei ya Cement yapanda

Bei ya Cement yapanda

Tuendelee kuandamana nyuma ya KEYBOARD wakuu...sisi ni zaidi ya mazuzu... maneno mengi nyuma ya keyboard, action ni 0.
 
Kumbe ni buku tuu,sawa tuliambiwa hivyo Bungeni
Ukiangalia katika perspective hiyo utaona buku ni ndogo! Buku ninkwaa kila kilo 50 ya cement, dangote anazalisha tani zaidi ya 5000 kwa siku.
 
Wanatuonyesha njia ya kufanya mageuzi ila tumelala kama pono, inakera, tozo kodi na hupati huduma kamilifu umeme kero, maji kero duh

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuwaamsha vijana wa Nchi hii kazi sana, wangezaliwa kabla ya uhuru sidhani kama wangepambana kutuletea Uhuru.

Wameshindwa hata na Kinjikitile wa kule kusini ndani ndani alihamasisha vijana wenzake kupigana Vita ya Maji Maji

Au hata Mangi Meli, Mchaga mfanyabiashara kupigana na Wajerumani kule Kilimanjaro.

Ama mtoto wa Mkulima Mkwawa kupigana na Wajerumani kule Iringa

Hawa Vijana wao waambie Kubet, kushindana kunywa beer, kuvuta mashisha, kushikishwa Ukuta ili wapewe hela wakauze Sura Tiktok/Instagram ndicho wanachoweza. Poor them 😢
 
Nimeona pia taarifa ya Mbeya cement, nayo imeonesha hilo ongezeko la shilingi 1,000 kwa kila mfuko wa saruji.

Yaani pamoja na ugumu huu wa maisha wameamua ku impose mzigo mwingine wa kodi kwa Raia wake

=======
Ingekuwa Nchi nyingine zinazoejielewa mfumko huu wa maisha ingekuwa tiketi ya Viongozi hao wakuu na Serikali yao kuondoshwa madarakani
Tuko na mchumi No 1. asiyejua athari za kuziia watu lujenga nyumba bora
 
Wanachosahau wanasiasa wanapoamua kuongeza Kodi,Anaeumia Ni mtumiaji sio mfanyabiashara

Angalia Apo dangote kaweka wazi kua itaongezeka buku kila mfuko

Maana ake hiyo Tsh 20 kila kilo inalipwa moja kwa moja na mlalahoi

KWA tafsiri hiyo
Hii tuite Ni TOZO YA CEMENT, sio kodi
 
Ukichunguza hili suala kwa jicho la 3

Utagundua serikali nayo imeamua KUFANYA biashara ya cement kwa mlango wa nyuma.

Kwa maana,
Hata Iyo buku wanochukua kila mfuko wa cement, inazidi faida ya mfanyabiashara husika anayeuza cement na kulipia tena Kodi tra
 
Back
Top Bottom