Basi la New Force lapata ajali leo asubuhi

Basi la New Force lapata ajali leo asubuhi

Kampuni za wazawa zimeamua kuwalia collabo hawa wageni. Ila nao siwahurumii maana wamezidi, wanataka kuwekeza kwenye kila kitu? Sisi tule wapi sasa na kwao hatuwezi kwenda kuwekeza?
Point yako sijaielewa Mkuu,kumaanisha ni figisu za kampuni za nyumbani kwa wageni?! Na kwa namna gani wanafanya izo figisu wakat sababu za ajali zinafahamika?!
 
Hiki ndicho hutokea mamlaka husika ya usimamizi inapokuwa legelege.
Acha tuendelee kupunguza Trafiki barabarani,tupunguze faini maana zinawatesa madereva na wamiliki wa magari, hawa abiria hata wakifa kwa uzembe wa madereva na uzembe wa mamlaka zinazohusika hakuna hasara yeyote,maana tulishaamua iwe hivyo,
 
Acha wivu wa kijinga sauli toka ameanza biashara ya usafirishaji haijawahi kuua

Kwahiyo kwa kuwa haiui ndio iachwe ifanye upuuzi barabarani. Gari zinakimbizwa hovyo hovyo, overtaking za hovyo hovyo n.k Pumbavu kabisa wewe.
 
Baada ya juzi kupata ajali mbaya na kuua watanzania wengi japo Serikal imeficha ukwl na kusema ni abiria watano

Leo tena kampuni ya newforce imepAta ajali maeneo ya Kibaha

Hii itakua ajali ya 6 ndani ya siku 21

Chanzo kikuu cha ajali hizo ni kile kile mwendokasi na kufanya overtaking za ovyo

Sasa ni wakati wa Serikal kuipiga Rungu kampuni hii ya mwekezaji kama ilivyofnya kwa kampuni za wazawa


View attachment 2666040
Kampuni hii ifungiwe, ni kampuni ya machinjio
 
Msijali mabasi mapya yanayo kuja yatapewa jina la Golden Deer kupunguza taharuki
 
New force pamoja na magumu wanayo pitia nikampuni iliyo saidia Sana kuondoa mabasi mabovu kwenye ruti nyingi hapa Tanzania Hao jamaa Kila baada ya miezi 6 wanaleta mabasi mapya yasiyo pungua 20 kwa Hilo nawakubali sana
Nakazia.
 
Nimeenda kusoma comments kwa page zao mitandaoni.... huwezi amini wasafiri ndio wanaohamasisha na kusifia mwendo.
KUna comment wanataka gari za saa9 alfajiri lunch wakale mbeya na kugeuza kurudi Dar [emoji1][emoji1]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Na wanajua ratiba zote za gari??
Wapo humo wanawajua hadi madereva wa gari hizo na kuwasifia [emoji1][emoji1]
Kuna mmoja anaitwa Tito hadi wafuasi anao humo
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
nilipanda haya magari aisee ni hatari yanakimbia sijapata ona ,picha limeanza hilo basi lilitoka tunduma limeingia iringa mjini saa 4 kamili mimi nilipandia hapo kuja dar huko njiani ni balaa na tuliyapita ma bus yote yaliyotoka iringa asubuhi na dar tuliingia saa 12 jion.Sikushangaa niliposikia ajali za haya ma busi
 
Kufa watano tu ni kidogo sana serikali Huwa inapenda wafe basi Zima ndio hatua zinachukuliwa sasa.
 
Back
Top Bottom