Barua ya Wazi kwa Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Dotto Mashaka Biteko: Waagizaji wa Mafuta watumie Dhahabu kununua Mafuta Nje ya Nchi

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,328
8,243
Barua ya Wazi kwa Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko: Waagizaji wa Mafuta watumie Dhahabu kununua Mafuta Nje ya Nchi

Heshima Mheshimiwa Waziri wa Nishati na naibu waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Doto Mashaka Biteko,

Kabla ya yote napenda kuchukua fursa hii kukupongeza kwa dhati kwa uteuzi wako kuwa Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uteuzi huu unaashiria imani na uwezo wako mkubwa katika kuchangia maendeleo ya nchi yetu, na tunatarajia utaendelea kuongoza kwa ufanisi.

Napenda pia kuchukua fursa hii kuwasilisha maoni yangu kwa njia ya barua hii ya wazi kuhusu tatizo la ukosefu wa mafuta na upungufu wa dola katika nchi yetu. Tunashuhudia changamoto hizi zikisumbua sekta ya nishati na uchumi wetu kwa ujumla, na ningependa kutoa pendekezo ambalo naamini linaweza kutusaidia kupata ufumbuzi wa kudumu kwa matatizo haya.

Tatizo la ukosefu wa mafuta na upungufu wa dola ni jambo ambalo limekuwa likijitokeza mara kwa mara nchini, na lina athari kubwa kwa uchumi wetu na maisha ya wananchi wetu. Kwa kuzingatia hili, napendekeza njia mpya ya kushughulikia suala hili: Waagizaji wa mafuta wanaweza kutumia dhahabu kununua mafuta nje ya nchi.

Pendekezo hili linajikita katika kuokoa biashara ya mafuta nchini mwetu wakati tunakabiliwa na uhaba wa mafuta ya petroli. Napendekeza kuwa taasisi na vyama vinavyohusika na sekta hii, kama vile EWURA, Chama cha Waagizaji na Wasambazaji Mafuta Tanzania, Wizara ya Madini, Chama cha wanunuzi na Wauzaji madini Tanzania (TAMIDA), PBPA, na Wizara ya Nishati washirikiane kwa karibu.

Njia hii inaweza kutekelezwa kwa kufuata hatua zifuatazo:

1. Waagizaji wa mafuta wanaweza kutumia dhahabu kama malipo ya kununua mafuta nje ya nchi kwenye soko la kimataifa.

2. Mafuta yakiuzwa nchini, shillingi zitakazopatikana kutokana na mauzo ya mafuta zinaweza kutumika kununua madini ya dhahabu hapa nchini.

3. Baada ya kununua dhahabu, waagizaji wa mafuta wanaweza kubadilisha dhahabu hiyo na dola kwenye soko la kimataifa.

4. Dola zilizopatikana zinaweza kutumika kununua mafuta ya petroli, dizeli na bidhaa nyingine za mafuta kutoka nje ya nchi kwenye soko la kimataifa.

5. Mafuta yanaweza kuingizwa nchini na kusambazwa kwa njia ya kawaida na kuuzwa kwa shilingi. Fedha zitakazopatikana zitatumika tena kununua dhahabu, ambayo itapelekwa kwenye soko la kimataifa kwa ajili ya kubadilishwa na dola ambazo zitatumika kununulia mafuta.

Kwa kufuata njia hii, waagizaji wa mafuta watakuwa na njia mbadala ya kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini hata kama nchi haina dola za kutosha. Pia, njia hii inaweza kuchochea ukuaji wa biashara ya madini ya dhahabu na kuleta manufaa ya kiuchumi kwa nchi yetu.

Napenda kuhimiza ushirikiano kati ya wizara na taasisi zinazohusika katika utekelezaji wa pendekezo hili. Pia, ni muhimu kuzingatia masuala ya udhibiti na usalama katika utekelezaji wa mpango huu ili kuhakikisha kuwa unatekelezwa kwa ufanisi na kwa faida ya nchi yetu.

Nashukuru kwa kusoma pendekezo hili na natumaini kwamba litazingatiwa kwa umakini. Ndugu Mh. waziri kiukweli bado tuna fursa ya kubadilisha changamoto hii kuwa fursa ya maendeleo na ustawi wa nchi yetu.

Elia Wilinasi
Nawasilisha kwako mheshimiwa
 

Attachments

  • Barua_ya_Wazi_kwa_Waziri_Dkt_Dotto_Biteko.pdf
    96.5 KB · Views: 6
Mkuu tunatoa ni maoni tu.
Mimi kuhusu ishu ya mafuta nawazaga mambo mawili.
1. Serikali ifute kodi kwenye magari ya umeme mapya au used. Na sekta nzima ya magari ya umee kodi iwe chini.


2. Au haya matrillioni wanayotumia kula raha na kununua ma V8 kwa nini wasijilipue kufanya research kuchimba visima vya mafuta na kuwa na oil refinery hata ndogo tu.


Nawaza tu.


NB: serikali inakusanya kodi nyingi kwenye mafuta. Ma trillion ya kutosha kila mwaka. Taarifa ipo the chanzo naona waliipost mitandaoni
 
Mimi kuhusu ishu ya mafuta nawazaga mambo mawili.
1. Serikali ifute kodi kwenye magari ya umeme mapya au used. Na sekta nzima ya magari ya umee kodi iwe chini.


2. Au haya matrillioni wanayotumia kula raha na kununua ma V8 kwa nini wasijilipue kufanya research kuchimba visima vya mafuta na kuwa na oil refinery hata ndogo tu.


Nawaza tu.


NB: serikali inakusanya kodi nyingi kwenye mafuta. Ma trillion ya kutosha kila mwaka. Taarifa ipo the chanzo naona waliipost mitandaoni

Ni mawazo mazuri. Lkn wangetilia mkazo zaidi kwenye matumizi ya gesi asili hali ingekuwa tofauti sana.
 
Mimi kuhusu ishu ya mafuta nawazaga mambo mawili.
1. Serikali ifute kodi kwenye magari ya umeme mapya au used. Na sekta nzima ya magari ya umee kodi iwe chini.


2. Au haya matrillioni wanayotumia kula raha na kununua ma V8 kwa nini wasijilipue kufanya research kuchimba visima vya mafuta na kuwa na oil refinery hata ndogo tu.


Nawaza tu.


NB: serikali inakusanya kodi nyingi kwenye mafuta. Ma trillion ya kutosha kila mwaka. Taarifa ipo the chanzo naona waliipost mitandaoni
Hongera kwa mchango mzuri, lakini ni muhimu kutambua kwamba mawazo yako yanaweza kuwa suluhisho la muda mrefu ambalo linahitaji uwekezaji wa muda mrefu. Kwa mfano, kuchimba visima vya mafuta, kujenga refinery, au kupunguza kodi kwenye magari ya umeme ni miradi mikubwa inayohitaji maandalizi ya kina na uwekezaji wa muda mrefu. Inapaswa kuwa mikakati ya baadaye ili kujenga msingi imara kwa ustawi wa nchi.

Hata hivyo, katika kipindi kifupi ambapo kuna changamoto za haraka za upatikanaji wa mafuta na upungufu wa dola, ni muhimu kuzingatia suluhisho za muda mfupi ili kukabiliana na mahitaji ya sasa ya mafuta. Kwa hiyo, ni muhimu kutathmini njia za kuboresha upatikanaji wa mafuta ya haraka, huku tukizingatia pia miradi ya muda mrefu ili kuhakikisha ustawi wa nchi katika siku za usoni.
 
Upungufu wa mafuta vituoni unahusiana na utaratibu wa kukokotoa bei kila mwisho wa mwezi.
Wafanyabiashara wakijua bei itapanda wanasubiria bila kuchukua na kuuza mzigo ambao tayari wameshanunua kwa bei ya jumla.
Ni vizuri bei iamuliwe na soko, serikali iingilie tu pale inapobidi.
 
Kwa mujibu wa mikataba, dhahabu yetu sio inauzwa nje tu na si humu ndani?

Yaani wawekazaji kwenye migodi ya dhahabu, mikataba yao si inawaruhusu wauze kwa dola moja kwa moja nje na hawalazimika kuleta dola hapa nchini?
 
Ni mawazo mazuri. Lkn wangetilia mkazo zaidi kwenye matumizi ya gesi asili hali ingekuwa tofauti sana.
Nakubaliana nawe kabisa, ni kweli kabisa kwamba matumizi ya gesi asilia kwenye magari ni suluhisho zuri la kupunguza utegemezi wa mafuta ya petroli na dizeli. Sote tunajua kwamba gesi asilia ni rasilimali inayoweza kutumika kama nishati mbadala katika sekta ya usafiri.

Na serikali inaweza kuhamasisha matumizi ya gesi asilia kwa kutoa sera na ruzuku kwa watumiaji wa magari yanayotumia gesi asilia, na pia kwa kujenga miundombinu ya kusambaza gesi asilia, hasa vituo vya kujaza gesi asilia kwenye magari. Hii pia inaweza kuwa njia nzuri ya kupunguza gharama za mafuta.

Lakini ni muhimu kutambua kwamba njia hii pia inahitaji uwekezaji mkubwa na inachukua muda mrefu kuweza kuitekeleza. Hivi sasa tuna vituo viwili tu vya kujaza gesi asilia kwenye magari Tanzania nzima. Sii hivyo tu, karakana za kubadilisha magari ili yaweze kutumia gesi asilia kama nishati zipo tatu tu Tanzania nzima. Hivyo, kwa kipindi hichi kifupi cha changamoto ya uhaba wa mafuta, tukifuata njia hii kwa magari yote, hatutaweza kuitekeleza. Kazi tunayopaswa kuifanya kabla ya kufuata njia hii ni kujenga vituo vingi vya kujaza gesi asilia katika kila wilaya nchini Tanzania, pamoja na kujenga karakana za kutosha za kubadilisha magari ya petroli na dizeli ili yaweze kutumia gesi asilia.

Lakini hata hivyo, tunaiomba Serikali iendelee kusisitiza matumizi ya gesi asilia kwenye magari, pamoja na kuweka sera wezeshi, kutoa mikopo, na ruzuku ili kuwawezesha Watanzania kutumia gesi asilia kwenye magari yao pale inapobidi kufanya hivyo.
 
Hilo lingeweza kuleta tija pale ambapo tungekuwa na viongozi "Waadilifu" na sio hawa "Wabadhilifu!"

Ukiwaruhusu hawa viongozi "wabadhirifu" mithili ya "Panya" eti kuanza kuingilia akiba ya "Dhahabu".
Hautakawia kusikia nako wameikausha Hazina yote tena kwa muda mfupi sana.

Tunaishi na kuongozwa na Mafisi ...elewa hilo!
 
Kwa mujibu wa mikataba, dhahabu yetu sio inauzwa nje tu na si humu ndani?

Yaani wawekazaji kwenye migodi ya dhahabu, mikataba yao si inawaruhusu wauze kwa dola moja kwa moja nje na hawalazimika kuleta dola hapa nchini?
Ngoja waje watu wa sekta ya madini walifafanue hili vizuri. Watu wa madini tunawahitaji huku mtolee ufafanunuzi juu ya hili ili umma upate kuelewa.
 
Hilo lingeweza kuleta tija pale ambapo tungekuwa na viongozi "Waadilifu" na sio hawa "Wabadhilifu!"

Ukiwaruhusu hawa viongozi "wabadhirifu" mithili ya "Panya" eti kuanza kuingilia akiba ya "Dhahabu".
Hautakawia kusikia nako wameikausha Hazina yote tena kwa muda mfupi sana.

Tunaishi na kuongozwa na Mafisi ...elewa hilo!
Mkuu hujaeleza kwa kina.
 
Upungufu wa mafuta vituoni unahusiana na utaratibu wa kukokotoa bei kila mwisho wa mwezi.
Wafanyabiashara wakijua bei itapanda wanasubiria bila kuchukua na kuuza mzigo ambao tayari wameshanunua kwa bei ya jumla.
Ni vizuri bei iamuliwe na soko, serikali iingilie tu pale inapobidi.
Bei za mafuta zimetangazwa, vipi waliokua hawauzi wamenza kuuza??
 
Back
Top Bottom