KERO Barua ya wazi kwa Shabiby bus

KERO Barua ya wazi kwa Shabiby bus

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Zogoo da khama

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2013
Posts
638
Reaction score
607
Naleta kwenu lalamiko langu kama ifuatavyo:

Mnamo tarehe 4. 12. 2025 majira ya saa 1:40 usiku nilifika kituo cha mabus Mbezi Magufuri terminal kutuma bahasha kwenda ofisi ya Tanesco Dodoma, nilipokelewa na mhudumu wenu na kupewa ref ya mzigo no SSB 961 AKZ baada ya kufanya malipo, jambo la kushangaza na kusikitisha hadi sasa tarehe 15 Dec bahasha haijafika na haijulikani ilipo, nimejitahidi kufuatilia bila majibu, jambo la kusikitisha ni wahudumu wenu hapo Dodoma hawana kauli nzuri, hawapokei simu, ukibahatika kupiga wanakublock.
Je huo ndio utendaji wenu wa kazi?

Dodoma wanasema niitafute mwenyewe je, mnataka nifanye ukaguzi kwenye mabus yenu?
Nilikuwa mteja wenu mzuri sana, kwa kusafirisha mizigo na kama abiria lakini kwa hili na kauli za watendaji wenu yatosha.

No za simu na majina ya wote nilikuwa nawaliana nao kuhusu udhembe na upotevu wa document yangu ninazo hata huyo wa Dodoma mwenye kauli chafu
 
Naleta kwenu lalamiko langu kama ifuatavyo:
Mnamo tarehe 4. 12. 2025 majira ya saa 1:40 usiku nilifika kituo cha mabus Mbezi Magufuri terminal kutuma bahasha kwenda ofisi ya Tanesco Dodoma, nilipokelewa na mhudumu wenu na kupewa ref ya mzigo no SSB 961 AKZ baada ya kufanya malipo, jambo la kushangaza na kusikitisha hadi sasa tarehe 15 Dec bahasha haijafika na haijulikani ilipo, nimejitahidi kufuatilia bila majibu, jambo la kusikitisha ni wahudumu wenu hapo Dodoma hawana kauli nzuri, hawapokei simu, ukibahatika kupiga wanakublock.
Je huo ndio utendaji wenu wa kazi?
Dodoma wanasema niitafute mwenyewe je, mnataka nifanye ukaguzi kwenye mabus yenu?
Nilikuwa mteja wenu mzuri sana, kwa kusafirisha mizigo na kama abiria lakini kwa hili na kauli za watendaji wenu yatosha. No za simu na majina ya wote nilikuwa nawaliana nao kuhusu udhembe na upotevu wa document yangu ninazo hata huyo wa Dodoma mwenye kauli chafu
Kondoa ujinga huu watanzania komaeni kuwaondoa CCM. Nchi imeshakuwa kama kisiwa cha wahuni na watu hawajali. Nchi nyingine kuna sekta zinazohusika na kusikiliza malalamiko ya wateja na kuamua kwa haki. Hawa unaweza kuwapeleka mahakamani lakini kupata haki inaweza kuwa hati hati na ikachukuwa muda mrefu bila kusahau gharama. Anyways jaribu hivyo hivyo kwenda kudai haki yako....
 
Bila sisi Watanzania kubadilika na kuchukua hatua hakuna ambacho tutafanya zaidi ya maumivu moyoni!

Kama unayo risiti na mzigo wako umepotea,Tafuta Mwanasheria waburuze mahakamani,hiyo risiti ndiyo ushahidi wenyewe!

Kama hiyo Barua ilikuwa muhimu maana yake wamekukwamisha na kukupotezea muda,Hapo itabidi wakulipe fidia ya kukupotezea muda!,Wapeleke mahakamani hao Wapumbavu Ili angalau wanaweza kuacha uzembe,Haya mambo ya Kuwa kila Jambo tunalalamika sidhani kama yatatusaidia!
 
Huwa kuna makosa ya kibinadamu yanatokea kwenye hizi shughuli, changamoto kubwa huwa ni hawa wafanyakazi wengi wanaowekwa kwenye hizi ofisi hawana skills za kutatua hizo changamoto ndogo ndogo au kubwa, utawaona wabaya Shabiby ila shida ni wahudumu na uwezo wao wa kutatua shida umeishia hapo.
 
Ulijichanganya kutuma mzigo huko, kama wapo rafu kwa abiria wao wataweza kutunza mzigo usioongea... Unaweza kupanda hili gari ukajutia safari.
 
Huwa kuna makosa ya kibinadamu yanatokea kwenye hizi shughuli, changamoto kubwa huwa ni hawa wafanyakazi wengi wanaowekwa kwenye hizi ofisi hawana skills za kutatua hizo changamoto ndogo ndogo au kubwa, utawaona wabaya Shabiby ila shida ni wahudumu na uwezo wao wa kutatua shida umeishia hapo.
Huduma zao za usafiri hazipo vizuri, ukitaka kuchukia safari panda hili gari.
 
Naleta kwenu lalamiko langu kama ifuatavyo:

Mnamo tarehe 4. 12. 2025 majira ya saa 1:40 usiku nilifika kituo cha mabus Mbezi Magufuri terminal kutuma bahasha kwenda ofisi ya Tanesco Dodoma, nilipokelewa na mhudumu wenu na kupewa ref ya mzigo no SSB 961 AKZ baada ya kufanya malipo, jambo la kushangaza na kusikitisha hadi sasa tarehe 15 Dec bahasha haijafika na haijulikani ilipo, nimejitahidi kufuatilia bila majibu, jambo la kusikitisha ni wahudumu wenu hapo Dodoma hawana kauli nzuri, hawapokei simu, ukibahatika kupiga wanakublock.
Je huo ndio utendaji wenu wa kazi?

Dodoma wanasema niitafute mwenyewe je, mnataka nifanye ukaguzi kwenye mabus yenu?
Nilikuwa mteja wenu mzuri sana, kwa kusafirisha mizigo na kama abiria lakini kwa hili na kauli za watendaji wenu yatosha.

No za simu na majina ya wote nilikuwa nawaliana nao kuhusu udhembe na upotevu wa document yangu ninazo hata huyo wa Dodoma mwenye kauli chafu
Wafungulie kesi mkuu.
 
Naleta kwenu lalamiko langu kama ifuatavyo:

Mnamo tarehe 4. 12. 2025 majira ya saa 1:40 usiku nilifika kituo cha mabus Mbezi Magufuri terminal kutuma bahasha kwenda ofisi ya Tanesco Dodoma, nilipokelewa na mhudumu wenu na kupewa ref ya mzigo no SSB 961 AKZ baada ya kufanya malipo, jambo la kushangaza na kusikitisha hadi sasa tarehe 15 Dec bahasha haijafika na haijulikani ilipo, nimejitahidi kufuatilia bila majibu, jambo la kusikitisha ni wahudumu wenu hapo Dodoma hawana kauli nzuri, hawapokei simu, ukibahatika kupiga wanakublock.
Je huo ndio utendaji wenu wa kazi?

Dodoma wanasema niitafute mwenyewe je, mnataka nifanye ukaguzi kwenye mabus yenu?
Nilikuwa mteja wenu mzuri sana, kwa kusafirisha mizigo na kama abiria lakini kwa hili na kauli za watendaji wenu yatosha.

No za simu na majina ya wote nilikuwa nawaliana nao kuhusu udhembe na upotevu wa document yangu ninazo hata huyo wa Dodoma mwenye kauli chafu
Next time tumia EMS mkuu hasa kwa nyaraka ambazo ni sensitive. Watu wa mabasi usiwaamini sana.

Kuna huyu jamaa anajiita USIRI naona anajitahidi kwenye kusafirisha vifurushi
 
Huwa kuna makosa ya kibinadamu yanatokea kwenye hizi shughuli, changamoto kubwa huwa ni hawa wafanyakazi wengi wanaowekwa kwenye hizi ofisi hawana skills za kutatua hizo changamoto ndogo ndogo au kubwa, utawaona wabaya Shabiby ila shida ni wahudumu na uwezo wao wa kutatua shida umeishia hapo.
Watumishi wa kwenye makampuni ya maBus wengi viburi na Wana nyodo sana......na hii ndio kawaida ya watanzania wengi wakiwa kwenye nafasi za kazi
 
No za simu na majina ya wote nilikuwa nawaliana nao kuhusu udhembe na upotevu wa document yangu ninazo hata huyo wa Dodoma mwenye kauli chafu

Wallah sikutaka kwenda nje ya mada wala sio kwamba uzi mzima nimeona neno UDHEMBE lakini nimecheka nisiwe muongo

Pole, nadhani wahusika watasoma na kufanyia kazi
 
Gari gani nzuri zaidi kwa Dar Dodoma siku hizi mkuu?

Mara ya mwisho nilienda na BM nikarudi na Shabiby
Hawa ABC wamelinda jina lao hawana mpinzani, ila watakupitisha kwenye hotel zao za ghali. Bora kupanda Esther ila sio shabiby😀
 
Huduma katika haya ma bus ya mikoani, kampuni nyingi bado hazijaweza kutoa kiwango kinachostahili, na kinachowafelisha wanachukua watu ambao hawana weledi kutokana na malipo madogo, matokeo yake ndo hayo. Nlishawai safirisha Taa kutoka Dsm to Mbeya na kampuni moja ya bus, kufika mbeya taa 9 zimevunjika kumbe kwenye kupakia mizigo waliweka mizigo mingine juu yake , na nliwaambia pale ofsini kwao wakati nalipia ule mzigo kuwa zile ni taa na kwenye box kwa nje nikaandika KIOO kama taadhari ili katika kupanga mizigo wapange kwa uangalifu lakini bado wakafanya huo uzembe. Nlirudi ofisini kudai fidia majibu yao ndo yalinichosha. Walisema mzigo wenye vitu vya kuvunjika wanasafirisha kwa dhamana ya mteja hivyo hawahusiki na uharibifu wowote

Note: Taa moja ilikua inagharimu 70k × 9 = 630k ikawa imepotea kirahisi hivo
 
Hawa ABC wamelinda jina lao hawana mpinzani, ila watakupitisha kwenye hotel zao za ghali. Bora kupanda Esther ila sio shabiby😀
Esther hata kwa mawe siitaki, kama mara 3 hivi Esther kwenda Rombo reporting time saa 9 alfajiri bus inaondoka saa 1:15 asubuhi, chaaa
 
Wallah sikutaka kwenda nje ya mada wala sio kwamba uzi mzima nimeona neno UDHEMBE lakini nimecheka nisiwe muongo

Pole, nadhani wahusika watasoma na kufanyia kazi
Ndio hicho tuu ulichoona, ila lengo umelielewa?
 
Back
Top Bottom