dazipozi
JF-Expert Member
- Nov 5, 2011
- 1,137
- 106
Nauchukia mziki wa bongo, nachukia media nyingi za bongo. Maswali mengi yatajijenga vichwani mwenu, kujiuliza kwanini nimeamua kuandika waraka huu kwenu; Mapresenter njaa. Labda nianze na hadithi fupi. Nilipoanza mziki mwaka 2009, sikuwa na wazo la kufanya mziki ili uwe kama biashara kwangu. Lakini kwa wale waliosomea biashara wataelewa kiasi ambacho unawekeza, ndio mori inapozidi kupanda. Hamu y...a kutamani biashara yako izidi kukuwa hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu na mwenzangu Jafaryzo Baizo wakati tunaanza mziki tulichukulia kama ni jambo la kujiburudisha. Baada ya kufanya baadhi ya ngoma hata wazazi wakaturuhusu, wakathubutu; kutupa pesa ndogo ya kuingia studio, ikaongeza tamaa yetu ya kufanya vitu vikubwa zaidi ili tuweze kujitangaza. Sisi ni wanafunzi, Lakini tulijinyima tukafanya bonge moja ya video kutoka Kwetu studio. Nadiriki kusema ni kwa gharama zetu, kuanzia pesa tuliyomlipa Mussah, modals tuliowaleta. tulitoa mifukoni mwetu. Ni kiasi kikubwa tuliwekeza bila jasho na msaada kutoka kwa mtu yeyote. Siwezi kusema ni kiasi gani tulilipa lakini ni gharama kubwa kwetu. Nashukuru Mungu video ilitoka kwa wakati, hakukutokea tatizo la aina yeyote. Sasa dhumuni la barua hii, ni hapa. Tukiwa na video mkononi, Huku tukiwa na uhakika wa kufanya Interview, kama sio airtime ya kutosha katika station moja kubwa ya Tv. Tuliahidiwa na marafiki ambao si vyema nikawataja. Ambao wapo katika hiyo station. Nikisema marafiki ni marafiki wanaonifahamu vizuri na mimi ninawafahamu. Si urafiki ambao umeanza baada ya hizi kazi za muziki. Lakini cha kushangaza hakuna kitu, tumeambulia patupu. Amani sana kwa Tony Tbway Escaber kwa moyo wa huruma na uthubutu na wa kirafiki uliotufanyia japo kwa matatizo kidogo ya kiufundi ilisababisha video kutokwenda hewani. Huwa najiuliza zile video za kina P-square, STL, Keko, P-Unit na wale wengine wanaokuja kutuchukulia mamilioni ya pesa katika show kama Rick rossT/Sh Milioni 220, Ludacris na wengineo wengi hivi huwa wanalipia hizo mnazoziita promotion? Kwanini hamna huruma? Kwanini hamjiulizi mara mbili underground kama mimi, nimekufuata unipigie video yangu, niliyojinyima kula chipsi shuleni nikala sambusa; nimekufuata kwa ndala na suruali nyeusi iliyobadilika rangi matakoni na kuwa nyeupe, nitapata wapi laki moja au mbili ya kukupa ili uicheze video yangu? Nimetoa labda laki moja studio kutengeneza audio, nikatoa laki saba kutengeneza video, bado kuna hela za kuburn cd, Dv, hata nauli pia
.. sisi tuna kazi gani ya kupata hizo pesa? Ukikaa kwenye station tv za siku hizi video za kibongo hupigwa mara chache sana tofauti na za huko ghaibuni. Napenda nifahamu jamani hao pia wanatoa hizo pesa za promotion? Kama ni za wabongo utaona za Yule Yule msanii mmoja, video mbili ambazo ni nyimbo mbili tofauti. Inaniuma sana nikiona mnatukandamiza halafu mnasema underground wanasumbua sana. Hivi mmesahau kabla hujapata huo upresenter ulikuwa mtaani? Umeisahau ile njaa iliyotafuna utumbo wako hata ukadiriki kusema maisha ni magumu? Ukajaribu kuongea ongea kuangalia kama sauti yako inafaa kuwa mtangazaji? Japo ulisomea udaktari wa mifugo? Kiukweli inabidi tubadilike watanzania. Tuthamini kwanza vya kwetu ili na sisi tukapige show kubwa tukachota madolari nchini kwao. Tusiishie kupiga katika birthday party za pedeshee mmoja huko ughaibuni.Mx