Kweli sasa Spika amekuwa laughing stock....
Sikumbuki ni gazeti gani, kati ya MTANZANIA na Mwananchi, waliandika Dau alikwenda, badala ya kusema kuhusu Malima aliyoyasema Bungeni, alianza kujitetea kuhusu ununuzi wa maghala kwa Quality Group, na kusema kwamba walioandika THISDAY na KULIKONI walimuonea, kwani utaratibu ulifuatwa. Akaulizwa, Malima alikuita kuwa shahidi wake, ama kuja kujisafisha? akasema yy anajaribu kuonyesha mfano wa jinsi Mengi anavyotumia vyombo vyake vibaya, akaulizwa sasa kesi ni MALIMA KUSEMA ITV INATUMIA DAKIKA MBILI KWA RAIS NA WAZIRI MKUU WAKATI MENGI ANATUMIA DAKIKA KUMI, kuna uhusiano gani na NSSF KUNUNUA MAGHALA? hayo ndio maelezo ya DAU sawa na alivyokwenda Mke wa Mahalu aliyesema mume wake kaonewa na THISDAY Kwa kumsingizia kuwa ameiba pesa wakati serikali imemrudisha tu nyumbani aje kupangiwa kazi nyingine. (ILIKUA KABLA YA KUFIKISHWA MAHAKAMANI)