MKANDAHARI
JF-Expert Member
- Apr 7, 2011
- 5,706
- 6,517
We shoga hatukutaki humu tenaUamuzi Wa Kama Kina Halima Mdee Wafukuzwe Au La BADO Haujatoka, Wajumbe Wa Baraza Kuu Ndo Wanaingia Kwenye Zoezi La Kupiga Kura Muda Huu
We shoga hatukutaki humu tenaUamuzi Wa Kama Kina Halima Mdee Wafukuzwe Au La BADO Haujatoka, Wajumbe Wa Baraza Kuu Ndo Wanaingia Kwenye Zoezi La Kupiga Kura Muda Huu
Salama yao kurudi ccm ingawa huko nako jiwe ndio alikuwa anagawa vyeo kwa mamluki nowadays wenye chama wamekazaKumbuka akina Komu na Selasini walihamia NCCR lakini Mambo yakawa magumu, na Kuna tetesi Selasini anaweza kurudi chadema. Pia kumbuka kwamba hata ACT tayari Kuna watu huko wamejipanga na Wana vyeo huwezi kwenda huko tu ukapewa nafasi na ukawa na usahwishi Kama ulio kuwa nao chadema.
Lengo lao ni Mshahara tu sio kufanya Siasa kwa maana ya kutetea Wananchi so watawezaIla wataweza siasa za ACT za kutokuikosoa serikali?.
Kikao kinapaswa kuketi baada ya mda ganiii, pindi kipatapo barua ya rufaa??Ndugu elewa kwamba walikata Rufaa kupinga kufukuzwa uanachama. Ndio maana ilibidi baraza kuu likae na kujadili Rufaa yao na baadae kutoa maamuzi.
Pole sana masalia ya Jiwe nenda kazikwe nae mnadhani mmejimilikisha Nchi hiiSerekali ikiwapakata sana hawa jamaa huwa wana nongwa sana, lazima wawekewe ukali kadogo,na hicho kikao ni cha nini sana?
Walifukuzwa walikata rufaaKumbe walikuwa hawajafukuzwa?!
Haa Maamuzi Yapo BayanaHayo ndio Maamuzi ya chama kila mtu apambane na hali yake
This is CHADEMA..Mungu zidi kukibariki hiki chama..HALIMA MDEE NA WENZAKE 18 WAFUKUZWA RASMI CHADEMA
Baraza Kuu la #CHADEMA limezitupilia mbali Rufaa za Halima Mdee na wenzake 18 wakipinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya chama hicho kwa kukubali kwenda kuapishwa na kuwa wabunge wa Viti Maalumu bila baraka za chama
======
UPDATE:
View attachment 2221145
Halima Mdee: Kilichofanyika ni Uhuni, hata Mbowe (Freeman) mwenyewe anajua
John Mrema: Baada ya uamuzi wa Baraza Kuu, Katibu Mkuu ataandika barua kumuarifu Spika kuwa suala lao limehitimishwa; tutamwachia spika afanye uamuzi kama alivyosema anasubiri Rufaa zao
=======
Matokeo ni kama ifuatavyo;
Kanda ya Victoria (Wajumbe 44)
-Wanaokubalia wavuliwe uwanachama 42
-Wasiokubali 1
-Wasiofungamana na Upande wowote 1
Jumla kura 44
Kanda ya Nyasa (Wajumbe 57)
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 57
-Wasiokubalina 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 57
Kanda ya Unguja (Wajumbe 22)
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 19
-Wasiokubali 1
-Wasifungamana na Upande wowote 1
Jumla ya Kura 22
Kanda ya Pemba 15
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 12
-Wasiokubali 1
-Wasifungamana na Upande wowote 2
Jumla ya Kura 15
Kanda ya Kusini 32
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 32
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 32
Kanda ya Pwani 47
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 45
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 2
Jumla ya Kura 47
Kanda ya Kati 44
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 44
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 44
Kanda ya Serengeti Wajumbe 41
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 41
-Wasiokubalina 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 41
Kanda ya Magharib Wajumbe 37
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 37
Wasiokubali 0
Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 37
Kanda ya Kaskazini Wajumbe 61
-Wanaokubali wavuliwe uanachama 61
-Wasiokubali 0
-Wasifungamana na Upande wowote 0
Jumla ya Kura 61
Kura 352 zimekubaliana na Kamati Kuu na kura 5 ndo zimepingana na maamuzi ya Kamati Kuu
WatavaaAsa yale magwanda watapeleka wapi 😂😂😂
Nyuma ya nondo alienda baada ya zaidi ya nusu mwaka toka hao mabinti wakate rufaa yaooo. Pia mwenyekiti hakwenda na office ya chademaC kamati kuu ikikaa ilichelewa kukaa sababu mwenyekit alikua nyuma ya nondo gaidi
😁😄😃😀Mzilankende, JoboWalivuna walichopanda walikuwa wanapewa kiburi na mwendazake na Ndugai leo wako wapi?
Walifukuzwa lakini wakakata rufaaKumbe walikuwa hawajafukuzwa?!
Walikata rufaaKwani hawakuwa wamefukuzwa hawa?
Hapo Ndiyo Nyani Katema Bungo Halafu Siyo Msimu Wa MaembeBaada ya hapo nini kinafuata?
Hata wakienda mahakamani ni kusogeza muda tu,ni bora kukaa pembeni kuheshimu maamuzi ya chama.Labda kuna siku wakasamehewa kabla ya 2025 wakajipanga upya kuwania nafasi za uongozi.Watamkuta Kibatala kwenye geti la Kisutu.
Yaani mwenyekiti atoke kuongea na mkuu wa muhimili uliojichimbia zaidi then eti mahakama?Acha kupanikiii. Mahakama inazingatia sheria. Hivyo lazima katiba ya chadema ichukuliwe na kisha isomwe ilikubaini kama kama haki inafuatwa kwa mjibu wa katiba ya chadema. Na muache kupaniki kabisaa
Acheni kuwakandamiza kwa kuwatishia wanasheria wenu kandamizi dhidi ya akinamama. Kwenda mahakamani ni haki yao. Acheni kuwatisha, etiwatulie mbeleni mtawasamehe kwa kosa lipi mpaka waombe msamahaa. Tunataka sheria ichunguze na itoe hakiiiHata wakienda mahakamani ni kusogeza muda tu,ni bora kukaa pembeni kuheshimu maamuzi ya chama.Labda kuna siku wakasamehewa kabla ya 2025 wakajipanga upya kuwania nafasi za uongozi.
Lakini pammoja na hayo wamekitumikia chama,na kupitia vikwazo vingi,kusweka ndani mara kwa mara na kufunguliwa kesi za kubumba.