Zesh
JF-Expert Member
- Apr 27, 2017
- 15,381
- 24,979
Nunueni barakoa za kitambaa ambazo zinafulika. Ukiwa nazo mbili au tatu zinatosha. Unafua na kubadilisha kila siku..na bei yake ndo hiyo hiyo elfu mbiliUgonjwa wa Corona Virus au Covid-19 inazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa nchini.
Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani (Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari.
Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.
Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500? Kwa kweli hili nalo ni janga.
Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?
Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona mapema na kianze maana masikini nako japokuwa tunanawa mikono basi watu tuvae na barakoa kujilinda kikamilifu. Iwe lazima kwa muuzaji na mteja kuvaa barakoa.
Barakoa inashauliwa kuvalia kwa masaa 4 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu avae nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?
Leo hii pale St. Joseph Hospital Mjini moshi, kuna watu walikuwa wamekwama kuingia mlangoni mwa geti la hospitali kwa kukosa 2000 ya barakoa.
Si kila aende hospitali anaumwa, wengine huwapelekea chakula ndugu zao wagonjwa waliolazwa. Sasa kama mtu alikuwa amejiandaa na nauli halafu anakuta stop getini ya kotoingia bila kuvaa barakoa hapo huwa mtihani.
Kama mama amempeleka mtoto kwenye matibabu, hapa inamlazimu kununua barakoa Mbili : ya kwake (mama) na mtoto pia.Kwa hali hiyo mama atagharamia sh 4000. Hii gharama hakuitegemea kabisa!
My takes.
Barakoa zigawe bure au zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.
Kwa sasa si muda wa Hospitali na maeneo ya public ya mkusanyiko kufanya biashara za hizi Barakoa kama ilivyo kwenye Hospitali ya St. Joseph Mjini Moshi. Wazitoe kama huduma na kama inagalimu basi zitolewe kwa bei nafuu sana.
Nchi gani wanagawa bure?Nchi ambazo Rais wao anajali wananchi hizi barakoa ni BUREEEEE
Marekani watu wameshauriwa wafunge hata vitambaa, mask watumie wahudumu wa afyaSijui kwanini Serikali isitumie ubabe kama ule wa Trump itaifishe vifaa vyote vya kujikinga na kuvigawa kwetu wahitaji
Wewe mbona haupo strict nyumban kwako?Nimeenda hospitali leo pale Mnazi Mmoja hakuna kuchekiwa wala nini zaidi ya kupuliziwa maji yenye dawa tu .
You'd think a hospital of all places wangekua strict ila waapi . Si Madokta wala manesi waliovaa hizo mask
Nyumbani kwangu ukiingia tu nguo unavulia mlangoni zinaenda kufuliwa nawewe unaenda kuogaWewe mbona haupo strict nyumban kwako?
Hapana kwenye barakoa tusingewaza hio kitu kwanza kwenye afya msisitizo huwa dawa zaidi kisha vifaa vingine vinafatia, just imagine nchi kama marekani inafikia hatua ya kuteka barakoa za nchi nyingine. Je walizonazo hazitoshi?maskini sie tusingeweza
Hizo barakoa za kutoa bure kwa watu takribani millioni 40 watazipata wapi?..barakoa zigawiwe bure kwa wananchi.
Hizo barakoa za kutoa bure kwa watu takribani millioni 40 watazipata wapi?
Sijui kwanini Serikali isitumie ubabe kama ule wa Trump itaifishe vifaa vyote vya kujikinga na kuvigawa kwetu wahitaji
Si ujibu swali langu kwanza? Ninyi hadi kwenye Corona mnalalamika! Pumbavu!!
1.umeandika kanakwamba ni utaratibu wa hospitali zote nchini kumbe ni kwenye hiyo hospitali ya Moshi pekee (tena ya mtakatifu-siyo ya umma)
2.barakoa ni vyema zivaliwe na wagonjwa tu au kama na wengine basi kwenye maeneo hatarishi
3.usiione watu wajinga kusema msivae barakoa hovyohovyo kwani endapo mkiamua wote mvae itakuwa kama fashion na si kinga tena na ndo tutapukutika kama kuku wenye kideli maana umakini utakosekana pia itakuwa ngumu kutofautisha wagonjwa na wasio wagonjwa
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna nyumbu wa Ufipa anaweza kuonhea chochote tofauti na Mbowe na akabaki salama? Nipo mfano...nyinyi kazi yenu ni kumuabudu na kuimba mapambio ya kumsifia Jiwe.
Kuna nyumbu wa Ufipa anaweza kuonhea chochote tofauti na Mbowe na akabaki salama? Nipo mfano.
Hofu nayo ni ugonjwa.Nimeenda hospitali leo pale Mnazi Mmoja hakuna kuchekiwa wala nini zaidi ya kupuliziwa maji yenye dawa tu .
You'd think a hospital of all places wangekua strict ila waapi . Si Madokta wala manesi waliovaa hizo mask
Jibu swali langu dogo, acha ku disgrace...ccm kila mtu anadukuliwa.
..bado viongozi wenu wana mawazo ya kikatili ya enzi za ukomunisti.
Serikali Ina viwanda 4999Ugonjwa wa Corona Virus au Covid-19 unazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa nchini.
Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani (Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari. Hili ni jambo ambalo sisi watanzania tunalipongeza sana tena sana.
Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.
Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500 au tsh 1000.
Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?
Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona basi mapema lianze maana masokoni nako japokuwa tunanawa mikono hatuko salama 100%.Basi watu tuvae barakoa kujilinda kikamilifu na iwe lazima kwa muuzaji na mteja wote tuvae barakoa.
Inasemekana barakoa moja inashauliwa kuvalia kwa masaa 4 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu avae nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?
Si kila anende hospitali anaumwa, wengine huwapelekea chakula ndugu zao wagonjwa waliolazwa. Sasa kama mtu alikuwa amejiandaa na nauli halafu anakuta stop getini ya kotoingia bila kuvaa barakoa hapo huwa mtihani.
Kama mama amempeleka mtoto kwenye matibabu, hapa inamlazimu kununua barakoa Mbili : ya kwake (mama) na mtoto pia.Kwa hali hiyo mama atagharamia sh 4000.
My takes.
Barakoa zigawe bure au zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.
Kwa sasa si muda wa Hospitali na maeneo ya public ya mkusanyiko kufanya biashara za hizi Barako. Wazitoe kama huduma na kama inagalimu basi zitolewe kwa bei nafuu sana.
Inasubiri mishemishe za uchaguziKwann isiwe free ?
Miisaada ya kupambana na corona inakazi gani?