Barakoa 😷 Kujilinda na COVID-19 zauzwa Tshs. 2000 na Bila kuivaa huingii lango la Hospitali kwenda kupata matibabu

Je ni lazima wagonjwa wanunue mask kutoka kwao?
Sehemu nyingi nchi zingine sasa hivi ni lazima kuvaa mask au kufunika mdomo na pua kwa njia yoyote ya kitambaa hili kupata uduma. Kama mtu hana mask maalum, wanatumia kilemba, kitambaa chochote kufunika pua na mdomo.

Kwahio ni muhimu kuruhusu raia watumie kitambaa chochote kuziba pua na mdomo hili kupunguza usumbufu. Kanga za zamani mtu anaweza kutumia kukata na kukunja mara tatu akafunika mdomo na pua kama hana hela ya kununua mask. Muhimu ni kuhakikisha kitambaa ni kisafi.

Tuache uvivu wa kufikiri kwamba kila kitu hatuwezi au hakiwezekani. Kuna mitambala mibovu majumbani mengine mnatumia kupigia deki lakini mnashindwa kutumia kuziba midomo na pua kujikinga na hili janga.

Huu ugonjwa upo na uamaliza watu. Ni muhimu kuchukua hatua mapema kuliko kusubiri hapo baadae hali ikiwa mbaya.
.... hongera ndg umetoa elimu njema Sana nazani wahusika wakilifanyia kazi inaweza saidia sana....lengo kuu ni kuondoa maambukizi mapya na kuendana na hali ya vipato vya wananchi.....
 
Balakoa zinatengenezeka, kama kweli unahitaji kuvaa na kujilinda, si lazima ununue.
Ukiwa na lesso ukaikunja vizuri na rubber band zako tayari balakoa.
Wale akina mama wa kiislam hawahitaji ziada tena, lile vazi tosha kabisa.
Hiyo ya massa manne ni kwa wale wanaohisi imezidiwa jasho mate nk
 
Kama inatakiwa kuvaliwa kwa masaa 8 tu,ina maana kwa siku mtu unatakiwa utumie Barakoa 2 hasa kwa sisi tunaokwenda kwenye mihangaiko ya kutafuta pesa,hiyo ina maana tayari ni 4,000.00...!!
Mkuu acha kupotosha!
 
Balakoa zinatengenezeka, kama kweli unahitaji kuvaa na kujilinda, si lazima ununue.
Ukiwa na lesso ukaikunja vizuri na rubber band zako tayari balakoa.
Wale akina mama wa kiislam hawahitaji ziada tena, lile vazi tosha kabisa.
Hiyo ya massa manne ni kwa wale wanaohisi imezidiwa jasho mate nk
aisee hii ni mpya ...nimepata sasa kutoka kwako
 
Pesa za kununua ndege tungepata barakoa hadi tukazikimbia
....nikweli lakini kwasasa ndege tulikwisha nunua hata tukisema tuuze ili tupate pesa ya barakoa hatuwezi kupata mteja....nazani tuanze na vilivyopo (1) wabunge wapunguze posho na mishahara yao iyo pesa isaidie kununua barakoa (2) mh: rais waziri mkuu na mawaziri wote wapunguze mishahara yao isaidie kununua barakoa (3) wakuu wote wa idara wakuu wa mikoa na wilaya makatibu na watendaji wote wapunguze mishahara na posho iyo pesa isaidie kununua barakoa (4) ruzuku ya vyama vya siasa vyote ipunguzwe nusu ikasaidie kuwalipia wananchi umeme na maji katika kipindi hiki kigumu cha mapambano ya covid-19
 
Kama inatakiwa kuvaliwa kwa masaa 8 tu,ina maana kwa siku mtu unatakiwa utumie Barakoa 2 hasa kwa sisi tunaokwenda kwenye mihangaiko ya kutafuta pesa,hiyo ina maana tayari ni 4,000.00...!!
Kuna barakoa za aina tofauti Kuna zile ambazo unavaa na kuzifua yaani kuzifanyia usafi( reusable mask) na hizo za muda mfupi ( disposable mask) na Bei hazifanani,ukiona huwezi ya 2000 unaangalia uwezo wako ili mradi kupunguza maambukizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.... hongera ndg umetoa elimu njema Sana nazani wahusika wakilifanyia kazi inaweza saidia sana....lengo kuu ni kuondoa maambukizi mapya na kuendana na hali ya vipato vya wananchi.....
Kusema kweli inasikitisha sana kuona tunaleteana usumbu kwenye jambo hatari kama hili. Ushahidi gani tunataka hili tuchukue hatua mapema?

Kuna nchi zilidharau sasa hivi wanakiona cha moto. Sisi tumshukuru Mwenyezi Mungu mpaka sasa hali ni salama kwahio ni muhimu kuanza kujikinga sasa hivi.
Juzi nilileta mada hapa kuomba rais aweke sheria ya mda watu wavae mask wakiwa kwenye miangaiko ya kila siku na kama hawataki wakae ndani. Kuna wapuuzi walinishambulia kwamba nataka niuze mask, hivi kweli kwa akili yetu ndogo kuna kitu gani kwenye mask kinamlazimisha mtu anunue kama hana uwezo kama si uvivu wa kufikiri? Mitambala yote ndani ya nyumba, kanga zote hizo na vilemba mtu anashindwa kutumia kuziba mdomo na pua anapotoka nje kuokoa maisha yake na wengine?

Tujikinge, tuoshe mikono mara kwa mara kuokoa maisha yetu ndugu zangu. Janga hili alichagui maskini wala tajiri. Tusisubiri misaada ya mask kutoka nje, wao wenyewe hawana za kutosha. Tutumie vitu tulivyokua navyo majumbani kwetu.
 
aisee hii ni mpya ...nimepata sasa kutoka kwako

kama umefanya kazi maabara ndiyo maana huwa hazitumiki kuzuia harufu wala kemikali. hutumika mara nyingi kwenye vumbi, kitaalamu vumbi lina particulates. CORONA hubebwa na particulates au droplets ambazo kwenye kitambaa hazipiti.
Hakikisha kitambaa chako hakina matundu.
 
Mungu wetu yu anatupenda sotee....wenye pesa mnunue hzo balakoa tusiokuwa na pesa tuamini tu Mungu yu pamoja nasi sote anatupenda sanaa...
 
Balakoa zinatengenezeka, kama kweli unahitaji kuvaa na kujilinda, si lazima ununue.
Ukiwa na lesso ukaikunja vizuri na rubber band zako tayari balakoa.
Wale akina mama wa kiislam hawahitaji ziada tena, lile vazi tosha kabisa.
Hiyo ya massa manne ni kwa wale wanaohisi imezidiwa jasho mate nk
Mkuu sema wewe. Akili zetu zimeshikwa na mchina mpaka tunashindwa kutafuta mbinu mbadala kwenye mambo madogo sana. Kila mtu analalamika bei kama wamelazimishwa kununua.
 
Hapana kwenye barakoa tusingewaza hio kitu kwanza kwenye afya msisitizo huwa dawa zaidi kisha vifaa vingine vinafatia, just imagine nchi kama marekani inafikia hatua ya kuteka barakoa za nchi nyingine. Je walizonazo hazitoshi?maskini sie tusingeweza
Hapo ndipo tungekuwa na huduma nzuri hata barakoa zingekuwa za kutosha kwa wakati fulani.
 
Ugonjwa wa Corona Virus au Covid-19 inazidi kuleta madhara na kusababisha vifo mbali mbali duniani na hapa nchini.

Bila shaka nchi yetu ndo miongoni mwao nchi chache barani Afrika ambazo zimechukua tahadhari kadhaa bila kufungia wananchi wake ndani (Lockdown) na kuacha wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji huku wakihadhari.

Kutokana na hali kuonekana kuanza kuwa mbaya kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotangazwa kwa sasa, Hospitali na vituo vya afya zimeanza kutoruhusu wagonjwa kuingia Getini la Hospitali bila kuwa wamevaa Barakoa. Hili ni jambo la kupongezwa na la maana sana kujilinda na maabukizi.

Hata hivyo, hali ya barakoa moja kuuzwa Tshs 2000 imekuwa kidogo changamoto kwa wagonjwa hasa walala hoi. Je hakuna uwezekano bei ikapungua angalau ikauzwa kwa rejareja tshs 500? Kwa kweli hili nalo ni janga.

Hakuna mtu anayependa kuugua huu ugonjwa au kuambukiza wengine huu ugonjwa. Sasa kama vifaa vya kujikinga vitakuwa bei ghali je wananchi wa hali ya chini watamudu?

Tunakoelekea, itakuwa kwamba huwezi ingia sokoni bila kuvaa barakoa nalo ni jambo jema sana na kama watendaji wanaliona mapema na kianze maana masikini nako japokuwa tunanawa mikono basi watu tuvae na barakoa kujilinda kikamilifu. Iwe lazima kwa muuzaji na mteja kuvaa barakoa.

Barakoa inashauliwa kuvalia kwa masaa 4 mfululizo na baada ya hapo itolewe na mtu avae nyingine. Je kama zitakuwa zinauzwa Aghali je wananchi watamudu?

Leo hii pale St. Joseph Hospital Mjini moshi, kuna watu walikuwa wamekwama kuingia mlangoni mwa geti la hospitali kwa kukosa 2000 ya barakoa.

Si kila aende hospitali anaumwa, wengine huwapelekea chakula ndugu zao wagonjwa waliolazwa. Sasa kama mtu alikuwa amejiandaa na nauli halafu anakuta stop getini ya kotoingia bila kuvaa barakoa hapo huwa mtihani.

Kama mama amempeleka mtoto kwenye matibabu, hapa inamlazimu kununua barakoa Mbili : ya kwake (mama) na mtoto pia.Kwa hali hiyo mama atagharamia sh 4000. Hii gharama hakuitegemea kabisa!

My takes.

Barakoa zigawe bure au zipungue bei na zivaliwe na kila mtu sehemu ya mkusanyiko.

Kwa sasa si muda wa Hospitali na maeneo ya public ya mkusanyiko kufanya biashara za hizi Barakoa kama ilivyo kwenye Hospitali ya St. Joseph Mjini Moshi. Wazitoe kama huduma na kama inagalimu basi zitolewe kwa bei nafuu sana.
1.umeandika kanakwamba ni utaratibu wa hospitali zote nchini kumbe ni kwenye hiyo hospitali ya Moshi pekee (tena ya mtakatifu-siyo ya umma)

2.barakoa ni vyema zivaliwe na wagonjwa tu au kama na wengine basi kwenye maeneo hatarishi

3.usiione watu wajinga kusema msivae barakoa hovyohovyo kwani endapo mkiamua wote mvae itakuwa kama fashion na si kinga tena na ndo tutapukutika kama kuku wenye kideli maana umakini utakosekana pia itakuwa ngumu kutofautisha wagonjwa na wasio wagonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom