KERO Barabara ya maili Moja mpaka Chalinze ni Kero kubwa

KERO Barabara ya maili Moja mpaka Chalinze ni Kero kubwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bird Watcher

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2013
Posts
4,496
Reaction score
9,275
Wakuu hi barabara tunasubiri Nini Kuitanua? Niliona kafulila kamfurusha Mbia ambaye alitaka Kufanya huu mradi na Serikali Kwa mode PPI ajenge halafu a impose Toll fee,

Baada ya Kuongea vile hajarudi Tena kutoa way forward

Barabara imekuwa kero Kubwa sana Kwa wasafiri Yani Foleni ya Kufa mtu

Ni kweli serikali inashindwa Kuona Kuwa hii barabara Iko overloaded

Soma Pia:Kafulila: Tumemkataa mbia barabara ya kulipia Kibaha -Chalinze kwa maslahi mapana ya nchi yetu

Soma Pia: GE2025 - Samia: Usanifu wa barabara njia 6 ya Maili moja- Chalinze unaendelea
 
Serikali ipi? Hii hii yenye akili za kina Samia?
 
Wakuu hi barabara tunasubiri Nini Kuitanua? Niliona kafulila kamfurusha Mbia ambaye alitaka Kufanya huu mradi na Serikali Kwa mode PPI ajenge halafu a impose Toll fee,

Baada ya Kuongea vile hajarudi Tena kutoa way forward

Barabara imekuwa kero Kubwa sana Kwa wasafiri Yani Foleni ya Kufa mtu

Ni kweli serikali inashindwa Kuona Kuwa hii barabara Iko overloaded
Ujenzi ungeshaanza tangu 2023 Ila redio mbao zinasema maswala ys % ndio yanachelewesha
 
Kuna nyingine kutoka Singida kwenda Arusha, kipande cha njia panda Singida hadi Babati, barabara imejaa mashimo ya kushangaza utadhani si ya lami! Imegeuka kuwa kero na aibu kwa nchi kuwa na barabara mbovu kiasi kile!
 
Aisee unaweza tumia masaa 6 kutoka Mbezi hadi Moro hivi hivi
 
Kuna makampuni ya kichina yakipewa kandarasi ya kujenga barabara ujenzi wake unakuwa tofauti na wachina wengine. Barabara za makampuni mengine zinabomoka haraka na makampuni mengine hazibomoki haraka walau miaka kumi zinadumu ila wengine miaka kumi haifiki barabara hutatapakaa viraka vitupu na zingine hata kuweka viraka haiwezekani. Linganisha makampuni ya kichina ya SIETCO na CHICO, haya makampuni yanatofautiana sana kujenga barabara. Ipo kampuni nyingine ya CGC, hizi kampuni za kichina hujenga barabara kwa bajeti wanazozijua wao kwa kilometa walizopewa kujenga. Hapa utakuta kilometa alizojenga mmoja wao barabara inakuwa imara kwa miaka mingi na mwingine kilometa alizojenga hazidumu muda mrefu, lami inamemenyuka na kuwa mashimo. Ujenzi hutofautiana kampuni na kampuni. Mwingine akipewa tenda anafukua na kuondoa udongo wa juu na kuweka mwingine kwa matabaka huku mwingine yeye hushindilia udongo alioukuta na kuongeza tabaka moja juujuu kisha lami, huyu ndiye barabara anazojenga hubomoka baada ya miaka michache
 
Kuna nyingine kutoka Singida kwenda Arusha kipande cha njia panda Singida hadi Babati barabara imejaa mashimo ya kushangaza utadhani si ya lami. Imegeuka kuwa kero na aibu nchi kuwa na barabara mbovu kiasi kile
Mkuu bora hiyo ina mashimo lakini unatembea . Hiko kipande cha maili moja to chalinze folen yake ni hatari, hasa wakati wa jioni. Yani unatoka mkoani mapema sana alfajiri unategemea saa 12 ufike magufuli, lakini unakuja kuingia saa 3 usiku
 
NIWAKATI WA KUPAMBANIA KATIBA MPYA. KATIBA AMBAYO ITAKAYOWAPA WANANCHI NGUVU YA KUWAWAJIBISHA VIONGOZI WAZEMBE. ITAFIKA WAKATI, HAO VIONGOZI WATAKUWA HAWATAKI KUCHAGULIWA KWA KUHOFIA KUWAJIBISHWA NI TOFAUTI NA SASA WANAGOMBANIA NA TENA WENGINE WANAJITABIRIA HATA KABLA YA UCHAGUZI KUFIKA. TUSIJE TUKAFANYA MAKOSA KAMA TULIOYAFANYA HUKO NYUMA, TUTAJUTA.
 
Back
Top Bottom