Barabara mbovu Dar mjini nani alaumiwe?

Barabara mbovu Dar mjini nani alaumiwe?

bcsolution

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
394
Reaction score
177
Habari wanajamii, hivi kuendelea kwa mvua kunyesha na barabara nyinyi za mjini kuharibika nani alaumiwe? Wahusika wako wapi? Wanasubiri nini? Leo asubuhi nimevunja kitu chini ya gari yangu hata sijui kitu gani maana nimekwepa mashimo mpaka mengine yakawa hayakwepeki, kodi tunalipa.

Sasa wanashindwa kuweka hata vifusi tupite kama lami imewashinda? Kwani walikuwa hawajui kama mvua zipo? hawakuweka fungu la kurekebisha roads, pale round about karibu na dtv kuna shimo limezibwa na taka pale, mi naona bora iwe hivo mashimo yote tujaze taka tu ndo solution au kwa kuwa wao wana malandcruiser sie vi corola.
 
huu mji umekuwa kero kupita maelezo. angalia uhuru rd, lindi st, india st, huwez kuamini kama zinapita at the heart of the busiest, large-GDP-share, locality in tz.
 
Barabara kama vitu vingine vinavyolipiwa pesa kujengwa au kununuliwa, ni lazima vinakuwa na 'lifespan'.

Kwa Tanzania kichekesho kinakuja pale Kilomita moja inapogharimu Sh. 1b lakini barabara inadumu kwa msimu mmoja tu! Maana hata hizo za molam huwa zinadumu walau misimu miwili.
Cha kusikitisha zaidi ni pale unapoenda kwa majirani kama Rwanda, Kenya, Zambia nk, wao utakuta barabara imegharimu 600m lakini inadumu walau miaka 10! (Refer mradi wa Arusha - Namanga - Athi River).

Ndio maana kiuchumi wanasema kudaiwa sio vibaya lakini nchi zinazodaiwa trillion 40 zimefanya maendeleo makubwa na sustainable tofauti na viinimacho vyetu.
Nini kifanyike... sijui!
 
Wahamishie wizara zote dodoma tupate nafasi ya kuzikarabati.

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Kuna uwezekano mkubwa rangi za NJANO na KIJANI zikahusika.........

7.jpg
 
Nimetoka juzi Dar....Yani ni kinyaaa.....Jiji ni chafuu....Mtaa wa congo barabara zote zimejaa maji na tope....

Mm sijajua uzuri wa DSM upo wapi....
 
Nimetoka juzi Dar....Yani ni kinyaaa.....Jiji ni chafuu....Mtaa wa congo barabara zote zimejaa maji na tope....

Mm sijajua uzuri wa DSM upo wapi....

Uzuri wa dar upo kwenye uchafu...
 
Ukitokea hidery plaza, oryx shell kabla ya kukutana na barabara kubwa ya kuingia posta mpya pale kuna mashimo miaka nenda rudi hata kabla ya mvua nilishijiuliza maswali mengi sana bila yakupata majibu. Au ile barabara sio ya jiji.!!!!
 
Ukitokea hidery plaza, oryx shell kabla ya kukutana na barabara kubwa ya kuingia posta mpya pale kuna mashimo miaka nenda rudi hata kabla ya mvua nilishijiuliza maswali mengi sana bila yakupata majibu. Au ile barabara sio ya jiji.!!!!

hili eneo watu wamejivua akili wanapita wrong side (rong saiti) kwa sasa. kama unaendesha pale uwe makini coz left side hapapitiki
 
Huh? Bongo siku hizi Nyu Yoki, watu wana mahela kibao, sasa ubovu wa barabara utoke wapi?

Acha hizo wewe....bongo tambarareeeeeeee
 
viongozi wa mamlaka husika hawawezi kujenga barabara zidumu wao wanataka barabara ikijengwa kesho wapige hela huo ni uozo waoo..ona kinondoni road ilivyojengwa ona mwai kibaki ona barabara za makumbusho yaani aibu sanaaa hawa washenzi wana harinu tu magari yetu gadamnnnn kula malankaaaaa ths gvt
 
Barabara kama vitu vingine vinavyolipiwa pesa kujengwa au kununuliwa, ni lazima vinakuwa na 'lifespan'.
Kwa Tanzania kichekesho kinakuja pale Kilomita moja inapogharimu Sh. 1b lakini barabara inadumu kwa msimu mmoja tu! Maana hata hizo za molam huwa zinadumu walau misimu miwili.
Cha kusikitisha zaidi ni pale unapoenda kwa majirani kama Rwanda, Kenya, Zambia nk, wao utakuta barabara imegharimu 600m lakini inadumu walau miaka 10! (Refer mradi wa Arusha - Namanga - Athi River).
Ndio maana kiuchumi wanasema kudaiwa sio vibaya lakini nchi zinazodaiwa trillion 40 zimefanya maendeleo makubwa na sustainable tofauti na viinimacho vyetu.
Nini kifanyike... sijui!
banner.png


getresource.axd

5741955315_1968b94d34_b.jpg

1338622620-nairobithika-superhighway-gets-road-markings_1215526.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom