"Bambo" apata ajali mbaya



Wasanii wenzake na Bambo wakiwa na sura za majonzi mara walipofika hospitalini kumwona mwenzao Dickson Samson Makwaya a.k.a Bambo aliyelazwa kitandani.


Picha ya dereva wa pikipiki waliyopata nayo ajali alfajiri ya leo.

Picha ya Bambo

View attachment 32055

dah pole sana kijan..sema kwa kuangilia tu unaweza kusema dereva wa pikipiki hakuvaa element nzito za pikipiki...lakni ajali haina kinga...poleni sana

 
Pole sana Bambo. MUNGU atakuponya tu. ila barabara zetu ni hatari kwa yeyeto hata waenda kwa miguu nyakati za jioni ni hatari tupu hasa maeneo ya mijini. Bora vijengwe vivuko ya juuu kwenye junction za barabara. Madereva nao jamani muwe makini sana. Tujali utu na Ubinadamu zaidi ya maslahi. Mwenyezi MUNGU akuponye Bambo tutakumiss sana kwenye segment ya Magumashi ya Ze comedy ya Channel five. pole sana.
 
Jamani Bambo, pole sana! mungu akuponye haraka.

WanaJF, bado kuna tatizo kubwa na madereva wetu pamoja na miundo mbinu yetu, tena kubwa sana. Pikipiki hazijaanzia bongo jamani, kuna nchi nyingi sana kama Indonesia, Vietnam, Cambodia, South Korea, Japan na Malaysia usafiri wa pikipiki ni wa kawaida kabisa kama baiskeli mjini Shy au Tabora, lakini huwezi kukutana na ajali kila wakati.
1) Tatizo mojawapo ni madereva wetu kutojali watumiaji wengine wa barabara.
2) Jingine ni miundo mbinu yetu ni too stressful at all the time, unakuta mtu anatoka mwenge kuelekea posta anatumia zaidi ya saa moja hadi mbili.
3) Tatizo lingine watumiaje wengi wa pikipiki wanatumia hivi vifaa wakidhani ndo solution na ruhusa ya kuvunja sheria za barabarani, ndo kupenya penya kila sehemu bila kujali usumbufu unaowasababishia watumiaje wengine wa barabara, matokeo yake unakuta dereva mwingine kakomaa na upande anakoenda hapo ndo ajali kama hii inatokea.
4) Watumiaji wengi wa pikipiki hawajali wala hawana muda wa kuvaa helmet huenda sababu ya joto au kudharau sheria ambazo nazo ni chanzo cha rushwa.

Solutions:
1) Watumiaje wa pikipiki tujitahidi kukumbuka kuvaa helmet wakati tutumiapo pikipiki.
2) Tufuatane sheria kwa usalama wetu pamoja na usalama wa watumiaji wengine wa barabara.
3) Sawa, ajali haina kinga lakini wakati mwingine tunakuwa na haraka mno kiasi cha kukera watumiaji wengine wa barabara, maoni yangu watu tuheshimiane tunapotumia barabara, wote tunayo haki ya kutumia, kuishi na kufurahia kila kilichopo anapotokea mwingine anajifanya anaharaka ndo mwanzo ajali.
 
Aliumia kichwa ambapo kapata mtikisiko kidogo kwenye ubongo pamoja na kuvunjika mfupa wa paja la kulia.
Ameshafanyiwa operation kwenye hospitali ya mifupa ya MOI ambapo amewekewa chuma kwenye paja la kulia.
Anaendelea vizuri hapo MOI.
Mungu ampe quick recovery na abariki kazi nzito ya madokta na manesi waliomhudumia.
 
Tatizo hawa madereva wa boda boda siyo madereva wala awana lessen watatumaliza jamani polisi wanakamata kesho wapi bara barani halafu siku hizo boda boda zimefungwa muziki police wanaangalia tu
 
Bambi poli sani!
Ulikuw unakwendi wapi?
Usiku woti wajamini
Poli sana Bambi, Mungu atakusaidii!!
 
duh! kweli madereva wetu ni aibu mimi sijawahi kumuoana bambo live na natamani nikutane naye hata siku moja nyie mnamgog na kutaka kumuua? duh! yani usanii wa bongo kweli ni sifuri , bambo hana hata gari jamani
 
duh! kweli madereva wetu ni aibu mimi sijawahi kumuoana bambo live na natamani nikutane naye hata siku moja nyie mnamgog na kutaka kumuua? duh! yani usanii wa bongo kweli ni sifuri , bambo hana hata gari jamani

Usanii wa bongo ni sifa tu mkuu. Pesa hakuna.
 
duh! kweli madereva wetu ni aibu mimi sijawahi kumuoana bambo live na natamani nikutane naye hata siku moja nyie mnamgog na kutaka kumuua? duh! yani usanii wa bongo kweli ni sifuri , bambo hana hata gari jamani
Bambo Mungu ndie mpangaji wa kila kitu.Nakuombea upone na urejee kwenye harakati zako kama mwanzo.Kuhusu gari si lazima awe nalo muda wote mtu!Hapo utasikia ni mikono ya watu!Kumbe ndio ahadi aliopangiwa.Inasikitisha Bambo wetu!Pole! pole! pole sana.
 
duh! Kweli madereva wetu ni aibu mimi sijawahi kumuoana bambo live na natamani nikutane naye hata siku moja nyie mnamgog na kutaka kumuua? Duh! Yani usanii wa bongo kweli ni sifuri , bambo hana hata gari jamani
tanzania ya leo kuwa na gari ni anasa ndugu yangu.gari unanunua japani usd 2800,ushuru huku bongo unakuwa usd 3800.kwa hali hiyo utaweza kumili gari kweli?bambo hana gari,kwa kuwa kwa tz yetu,kuwa na gari ni anasa.
 
Kwani unadhani wanapenda kupanda hizo TOYO tatizo Bongo gari bado ni anasa, wewe fikiria kistarlet tu bila millioni 6 bado haujakimiliki. boda boda zitatumaliza sana na kusababishiwa ulemavu wa viungo kwa jamii pana ya Tanzania.
na ile lami ya kigogo inavotia wazimu hao waendesha pkipki ndo kabisaaaa
 
pole Bambo nafkiri huko utapata tiba muafaka, maana huku kwetu ukipelekwa hospitalini afu ikajulikana ni ajali ya pikipiki jiandae lazima ukatwe mguu hawana mda wa kupoteza
 
Ajali za pikipiki kweli zimefikia kiwango cha kutisha.Shuhudia pikipiki wrecks inje ya vituo vya polisi hapa inchini na inchi jirani.Hali ni mbaya hadi baadhi hospitali zimetenga special wards kwa majeruhi wa pikipiki(bodaboda wards).Serekali lazima ichukue hatua madhubuti ku regulate sector hii.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom