hizo taarifa za kusikitisha, pole mwanakwetu. La Bambo limevuma kutokana na umaarufu wake. Japo nahisi, kwa siku hiyo inawezekana ajali zilikuwa kadhaa, na majeraha makubwa zaidi. Ni tatizo kubwa zaidi ya inavyodhaniwa. Kukosekana kwa mkakati maalumu kulidhibiti, je, ni kwa sababu tumejenga utamaduni wa kushtushwa na idadi ya majeruhi kwa tukio au? Je chanzo ni vyombo vyenyewe, madereva, abiria, wamiliki, mfumo wa sheria, miundombinu au wasimamizi na watekelezaji wa sheria.!? Tunatakiwa kulishughulikia.