Balozi wa Marekani: Demokrasia inabidi iangalie mazingira ya nchi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,016
9,884
Katika mkutano wa wadau wa Demokrasia ulioandaliwa na TCD, Balozi wa Marekani Nchini Tanzania, Michael Battle amesema demokrasia sio lazima ifanane kwa kila nchi, lazima kila demokrasia izingatie mazingira yake.

Amesema demokrasia ya Tanzania, inabidi izingatie mazingira ya Tanzania, ifanane na Tanzania.

Aidha ameisifu Tanzania kuwa imekuwa ikipiga hatua vizuri, na wao (Wamarekani) wataendelea kuwa washirika wa Tanzania ili kusaidia kukuza demokrasia nchini.

Marekani ni moja kati ya wadau waliofadhili mkutano wa demokrasia wa mwaka huu, ambao kwa mwaka huu mgeni rasmi ni rais wa Zanzibar, Hussein Ally Mwinyi
 
Kwahiyo sasa Democrasia itategemea nchi na nchi. Sasa ufahamu unaanza kuwarudi. Lazima waanze kuona wananchi wanataka nini sio kulazimishana
 
Hilo dongo kwa RC. Maprotestanti Wamewasambaratisha wakatoliki na vibaraka wao Afrika Magharibi sasa wanawaambia wakatoliki wasijione kuwa wana stronghold huku Mashariki.

mfaransa anapigwa chini Francophone zote mdogo mdogo, walianza Rwanda, wakaja Burundi sasa wanafagia fagia kati hapo na magharibi.
 
Siwanasemaga kwamba sisi Africa ni maskini mbona hawataki kuondoka??
 
Watakuja wale wa kusema Balozi kanunuliwa na Lumumba

Kwani Ww Unaona Aliyoyaongea Huyo Balozi Ni Ya Kweli? Huyo Balozi Ni Kunguru,. Tupe Mifano Hai Ya Hatua Za Kweli Zilizopigwa Na Tanzania Kidemokrasia ? Hakuna Kilichotekelezwa Zaidi Ya Ahadi Zinazopigwa Danadana Tangu Na Tangu.
 
Hilo dongo kwa RC. Maprotestanti Wamewasambaratisha wakatoliki na vibaraka wao Afrika Magharibi sasa wanawaambia wakatoliki wasijione kuwa wana stronghold huku Mashariki.

mfaransa anapigwa chini Francophone zote mdogo mdogo, walianza Rwanda, wakaja Burundi sasa wanafagia fagia kati hapo na magharibi.
Kumbe we bibi ni mweupe hivo kichwani
 
Hilo dongo kwa RC. Maprotestanti Wamewasambaratisha wakatoliki na vibaraka wao Afrika Magharibi sasa wanawaambia wakatoliki wasijione kuwa wana stronghold huku Mashariki.

mfaransa anapigwa chini Francophone zote mdogo mdogo, walianza Rwanda, wakaja Burundi sasa wanafagia fagia kati hapo na magharibi.

Kikongwe punguza kunywa mataputapu sa umeandika upuuzi gani huu.
 
Wazungu hawaaminiki sana imefika mahala tujiulize kwanini tusifiwe vitu ambavyo havina ukweli? Maana nyinyi hata kama mnakufa ila wao wanapata maslahi hawawezi zungumza lolote mfano nchi ya congo, ila pia kama hawapati wanachotaka hatakama nchi haina mizozo watawavuruga mfano Libya. Tukitegeme kufikiliwa hatuta endelea yani Balozi wa nchi kubwa duniani usimame nakusema ustawi wa democrasia unakua katika inchi ambayo vyama vingine, vimepokwa wabunge wake wote na chama tawala halafu tulivyo wapumbavu tunafulahia, bila kusimama wenyewe tusitalajie kuna atakaetusimamia na tukaendelea.
 
Back
Top Bottom