tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Abubakar Zubeir amesema Baraza Kuu ya Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) itaendelea kusimamia maslahi ya Nchi ambapo ametoa wito kwa watanzania kuendelea kuwa wazalendo na Taifa lao pamoja na kuilinda amani.
Mufti ameeleza hayo leo wakati akizungumza na baadhi ya viongozi wa dini na serikali wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Njombe ambapo pia amesema miongoni mwa kazi ya BAKWATA ni pamoja na kuhimiza watu kuilinda amani na kuwa wazalendo na taifa tofauti na wengine wanavyodhani kuwa Baraza hilo linatumiwa na serikali.
Soma pia: Mufti Abubakar Zubeir: BAKWATA si vibaraka wa serikali
"Tunazungumza sana swala la amani na uzalendo kwasababu tunaijua nchi ilivyo sasa akili ya watu wengine wanafikiri labda sisi ni vibaraka yani serikali inatutumia nendeni huko mkaseme hivi, a a sisi hatutumiwi na serikali tunajua umuhimu wa kutengeneza jamii ambayo inajua umuhimu wa kuwa mzalendo katika nchi yako" amesema Sheikh Mkuu wa Tanzania Abubakar Zubeir
Mufti ameeleza hayo leo wakati akizungumza na baadhi ya viongozi wa dini na serikali wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Njombe ambapo pia amesema miongoni mwa kazi ya BAKWATA ni pamoja na kuhimiza watu kuilinda amani na kuwa wazalendo na taifa tofauti na wengine wanavyodhani kuwa Baraza hilo linatumiwa na serikali.
Soma pia: Mufti Abubakar Zubeir: BAKWATA si vibaraka wa serikali
"Tunazungumza sana swala la amani na uzalendo kwasababu tunaijua nchi ilivyo sasa akili ya watu wengine wanafikiri labda sisi ni vibaraka yani serikali inatutumia nendeni huko mkaseme hivi, a a sisi hatutumiwi na serikali tunajua umuhimu wa kutengeneza jamii ambayo inajua umuhimu wa kuwa mzalendo katika nchi yako" amesema Sheikh Mkuu wa Tanzania Abubakar Zubeir