Kuna kitu nadhani Wakristo wengi hawakijui. BAKWATA:
1) Sio chombo cha kila Muislam
2) BAKWATA, kama ilivyo KKKT au TEC, au chama cha waendesha baiskeli wa Shinyanga, is a non profit, non governmental organisation.
Kwa hiyo support ya Serikali kwa Waislamu wa Tanzania haiwezi kuwa inapitia exclusively through BAKWATA. Serikali inataka Waislamu waji organize under the BAKWATA umbrella, kitu ambacho Waislam wengi wanakipinga. Ukimwambia muumini wa kwa Kakobe au wa Mama Rwakatare apokee support ya serikali kupitia KKKT (Walutheri) au TEC ( Wakatoliki) atakwambia over my dead body! Sio kila Mkristo ni Mkatoliki!
Sheikh Mkuu wa BAKWATA, kwa mfano, hatakiwi kutangaza sikukuu ya Kitaifa ya kumaliza Ramadhani kwa sababu sio Waislam wote wana subscribe to BAKWATA na hana mamlaka hayo kisheria. Hapo ndio unazaa wa kina Sheikh Ponda na Sheikh Basalleh wa Msikiti wa Mtambani, Msikiti wa Idrissa... extremist clerics though they are lakini wana haki ya kusema, again, mbele ya msajili wa non-profits za Tanzania, BAKWATA haina uzito na haki za kisheria kuzidi Chama cha Waendesha Baiskeli wa Temeke!
Sasa kwa nini BAKWATA ipokee support ya serikali kwa niaba ya Waislamu wote?