Maziku-Winston Smith
JF-Expert Member
- May 17, 2015
- 296
- 167
Habari zenu wanajamvi,
Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.
Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.
Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.
Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?
Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.
Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.
Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.
Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?