Bakora hazimjengi mtoto kinidhamu

Bakora hazimjengi mtoto kinidhamu

No wonder watoto wa siku hizi matatizo matupu kama wazazi mko hivi.
Hata vitabu vya dini vinaruhusu bakora kwa watoto.
Ndiyo maana wakoloni walikuwa wanawachapa bakora babu zetu ili wawe watiifu?
 
Kuna adhabu mbadala unaweza kumnyima kitu akipendacho sana kama adhabu mfano kama anapenda sana mkate na blueband MPE mkate mkavu
Mkuu hii adhabu ya kumnyima mtoto vyakula ni mbaya zaidi ya bakora.
 
Mtoa mada angalia busara zako ztakukosesha malezi bora..!!!

M nnavojua jua nidham Na tabia ya mtoto hujengwa mtoto anapokuwa Na umri Usiozd miaka mitano hadi sita( mlio soma psychology hamta nipinga)..

Kimsing huu ndio umr ambao mtoto anakuwa Na hurka ya kujarb kfanya kla kinacho wezekana maana ndio umri anaojifunza mazngira kw kias kikubwa..

Hivyo katka umri huu sidhan Kama mtoto anakiwa Na utambz Na upeo mkbwa wa kurekebishwa pind anapokosea kwa ktumia maneno Tu Kama unavodai mtoa mada..!!!

Unatakiwa kumkanya Na kumuonya kwa njia itakayo mtia uoga Ili asrudie.....HIYO UNAYOSEMA UTAITUMIA BAADA YA KUSHINDA KUMNYOOSHA KATKA UMRI NILIO UTAJA HAPO JUU..!!
Mimi namchapa mtoto wangu mara chache sana, lakini mara nyingi natumia maneno. Na anafahamu ni wakati gani nimekasirika na ninamaanisha hasa ninachosema. Neno langu moja ni zaidi ya fimbo za mama yake (ambaye anapenda sana kupiga). Hapa simaanishi kwamba watoto waachwe tu wafanye yale wanayojisikia kufanya.

Ninavyopendelea mimi ni kujenga hatua za makanyo kiasi kwamba mtoto anaelewa uzito wa kila hatua pale anapokuwa anafanya makosa. Hata jicho linatosha kumkumbusha mtoto kwamba hapa nimeshaharibu, na adhabu inaweza ikanijia any time. baada ya hapo ni maneno, haya nayo yana ngazi zake, na "tone" inaweza kumpa picha.

Kama alikuwa anaharibu au kuchezea kitu, unaweza kwenda kukitoa kitu hicho au kumtoa yeye, na "utoaji" huo ukiunganisha na maneno inaweza pia kumpa picha mtoto ni kiwango gani haujapendezwa na hilo.

Fimbo au corporal punishment inatakiwa iwe ya mwisho. Nakubaliana na kuwepo kwa option hii ili mtoto anapotaka kufanya kosa afikirie uwezekano wa kutandikwa, jambo ambalo linaweza kusaidia kupunguza "tendency" yake ya kufanya kosa husika.

Tatizo ni kwamba wazazi wengine wanaona kuwa hii ndiyo "the only option" wanayoijua na kuitumia, kwa kosa lolote afanyalo mtoto. Matokeo yake mtoto akishaizoea hali hiyo basi anakuwa nunda maana hakuna adhabu ya kutisha zaidi anayoihofia. Ikifikia hatua hii ndio unakuta wazazi/walezi wanakuwa desperate na kuamua kutumia visu, moto, kunyima chakula, etc baada ya kuona hata fimbo hazifanyi kazi...na ikifikia hatua hiyo, mimi na wewe tunawaita WAKATILI tunapoona matukio hayo yakitangazwa kwenye vyombo vya habari. Tukumbuke kuwa most of the time, inakuwa process hadi kufika hapo.
 
Kuwa uyaone nilidhani ni magorofa na magari kumbe ni maisha na asiyefunzwa na mamaye ulimwengu utamfunza wewe acha tu kumchapa akija uraiani huku awazingue wananzengo wamtie adabu
 
Kama unategemea bakora kumjenga mtoto kitabia basi unakosea kwa sababu bakora ni kama short-term measure tu ya kumuadabisha lakini kumbuka huyo mtoto atakuwa mkubwa huko baadae nani atamchapa akikosea?



Akiwa mkubwa maamuzi ni yake, wewe kama mzazi umesha play part yako ya kumfunza. Unaweza usimchape na bado akaishia kuwa na tabia zisizopendeza, je utaendelea kutumia theory yako ya utoto kumfundisha na wewe?
Samaki mkunje .......angali mbichi. Kiboko muhimu, kinavyomuuma inamkaa akilini kwamba jambo fulani halifai na hatorudia, tofauti na hadithi hadithi za mdomoni tu.
 
Ndiyo maana wakoloni walikuwa wanawachapa bakora babu zetu ili wawe watiifu?

Ukoloni ulikuwa unyanyasaji, kumchapa mtu mzima sio. Ndommaana hata huyo mtoto utamchapa, itafika age fulani huwezi kumchapa tena.
 
Mleta mada wewe mwenyewe umeleta hoja ambayo huna uhakika nayo. Ulipaswa kuja na fact inayoeleza madhara ya kupiga na matokeo chanya ya kutokupiga.
Nadhani huelewi ulichoandika na athari zake ktk malezi!

Kwanza nikuhakikishie,fimbo inarekebisha si kwa mtoto tu,hata mtu mzma km ww,natamani hapa ungekuwa karibu nikutandike bakora 3 za nguvu kwa huu utumbo ulioandika siku nyingine usingerudia.

Fimbo kwa mtoto ni muhimu mno! Kuna makosa huwa tunafanya wakati wa kutoa hii adhabu bora kabisa ktk malezi.
Mfano mtoto ameenda shule akiwa na begi la shule na limejaa mahitaji yake,anatoka shule anapita kucheza mpira wa sox mitaani,anapotoka anaacha begi,hapo anaweza kutunga hata uongo kuwa ameporwa.

Hapo unakuwa na wajibu wa kumchapa ili kumsaidia mambo mawili.
(1)awe makini
(2)asiwe muongo

Hapo unakata fimbo nzurii,kisha unamuita ndani chumbani unamfungia humo,unamchapa akuambie ukweli na atakuambia,hapo unamuongeza adhabu ya kukudanganya,unamuacha ndani unaenda kukata fimbo nyingine,hapo unamtisha tu na unamwambia akitoka usimuone akijifuta machozi. Na inabidi ale kiapo cha kutorudia kosa km hilo. Mtoto usimchape mbele ya watu..! Fimbo ni muhimu sana ktk malezi..
 
Bakora zinasaidia sana iwapo mtoto ataadhibiwa kwa kiwango anachostahili kulingana na umri...
 
Bakora hazilipi na ni uonevu wa hali ya juu.

Wanaosema ni vitabu vya dini ndio vinafundisha wanieleze wapi mitume wetu walichapwa bakora.
BAKORA KWA MTANZANIA MUHIMU ILA KILA KITU KWA KIASI.PIMA KOSA NA ADHABU
Tumkumbuke Gandhi na mbinu aliyotumia kufikia malengo yake.

Kama mwanao akivunja chombo nyumbani unamchapa,je wewe ulishawahi kuchapwa kazini kwako uliposababisha hasara kama hiyo!!?:

Mengi tunafanya bila kutafakari wala kujielewa,wengi wamechapwa vya kutosha lakini ndio hao hao wamekuwa majambazi nk
 
Bakora bwana nikichocheo cha mtoto kua na nidhamu tena kwa kiasi kikubwa sana !! Wewe leta uleaji Wa kizungu hapa kwa mtoto wako ujute !!!
 
Bakora kwa mtoto no saw a maana hats maandiko matakatifu ya mungu yanasema usimnyime mtoto mapigo
 
Bakora inatengeneza nidhamu yamtoto ila sio kila kosa linatibiwa kwabakora...!
**mtoto anaelimishwa naikitokea anakariri makosa yake ktk swala moja, unamuadhibu kwaupole alaf wamweleza tena kosa lake**
Nahii inasaidia endapo baba namama watalifanya kwapamoja ie baba akipiga mtoto, mama amkumbatie mtoto nakumliwaza kwakumwambia alichokikosea, na mama akimpiga mtoto, baba amchukue nakumliwaza nakumwambia kosa lake ililomfanya aadhibiwe.

Kinyume chake ikiwa kila kosa afanyalo mtoto akaadhibiwa namzazi mmoja, naakakosa kimbilio kwamzazi mwengine hii itamjengeq kiburi huyo mtoto.

::::adhabu hujenga nidham kwahoja yakuwa nidhamu walizo nazo kizazi cha miaka ya 90's, nacha watoto wamiaka ya elfu2 nitofauti sana::::
 
Bakora zinawajenga watoto maana hata kama mtoto alikuwa hataki kufanya Jambo Fulani la kumjenga ila akikumbuka fimbo lazima afanye.
Mfano. Una mtoto nyumbani ni mchafu sana hataki kuoga , umejaribu kumuelimisha bado hataki, ila pale unapoanza kutumia bakora mtoto lazima atayatafuta Maji yako wapi mwisho wa siku anazoea.

KWA mazingira haya fimbo zinakuwa zimemsaidia sana na zimemjenga
 
Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.mzazi usipomchapa nyumbani akija shule akakosa nidhamu tutamchapa na adhabu tutampa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom