Bakora hazimjengi mtoto kinidhamu

Bakora hazimjengi mtoto kinidhamu

Habari zenu wanajamvi,

Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.

Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.

Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.

Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?
Kama kawaida yetu dunia ya wajuaji hii. Bwana Mungu Muumba kasema mtoto asinyimwe kiboko wewe ni nani hasa wa kupinga...
 
Bakora zinawajenga watoto maana hata kama mtoto alikuwa hataki kufanya Jambo Fulani la kumjenga ila akikumbuka fimbo lazima afanye.
Mfano. Una mtoto nyumbani ni mchafu sana hataki kuoga , umejaribu kumuelimisha bado hataki, ila pale unapoanza kutumia bakora mtoto lazima atayatafuta Maji yako wapi mwisho wa siku anazoea.

KWA mazingira haya fimbo zinakuwa zimemsaidia sana na zimemjenga
Ni kweli kabisa.Nina kabinti kangu 5yrs Sasa alikuwa na tabia Kila akivua nguo anatupa chini hapo kamerudi shule hapa utakuta soksi pale Sweta pale sketi,nimefundisha kwa mdomo weeee siku yake nikampa bakora zake, siku hizi yeye ndio msemaji wa familia,utasikia wewe dada weka nguo pale kwenye Tenga mama atakuchapa wewe?
Fimbo haikwepi kwa mtoto sema tu kwa kiasi na iwepo interval sio Kila siku achapwe.
 
Kati ya kitu wazazi walikosea ni kuto wachapa watoto wao
Watoto wa sikuhizi wana majibu mabaya sababu ya malezi mabaya
Nina jirani yangu ana mtoto wa kike ana miaka 10 yupo STD 5,anasoma English medium ndio hao wakutochapwa anavyolelewa utasema yai la tausi wa pale magogoni...siku hiyo mama yake kajifanye amchape mtoto kapokonya fimbo na kumrudishia mama yake viboko huku anamuuliza Kama hunipendi kwa nini ulinizaa na maneno ya shit kibao na vizungu vyao,mama yake anajifanya kapanic nikajisemea moyoni hukumchapa at early stage uje umchape keshakomaa..kifupi ilikuwa ni tukio la aibu Sana...Nilitamani nimshike yule mtoto nimnyuke fimbo uwezo sikuwa nao tu....
WITO watoto wetu wa kiswahili ni wagumu Sana sijui wenzetu wazungu ila tujitahidi tu kuwanyoosha mpaka tutapoishia tuwe tumesimama kwenye nafasi zetu
 
Muleta mada atakuwa miongoni mwa wale walio brainwashed na wanaharakati wa haki za mtoto, hawa ndo wamechangia kushuka kwa maadili ya watoto nyumbani na mashuleni.

Kwa kila baya MTU alifanyalo lazima aadhibiwe kwalo ili kujenga nidhamu na kumrejesha katika njia sahihi. Lakini pia naomba nieleweke, so kila kosa lazima mtoto aadhibiwe kwa viboko, kuna mambo mengine anahitaji kukanywa tu. Lakini tusitake ku- legitimize kuwa kutumia adhabu za viboko ni ukatili

Sent from my TECNO F3 using JamiiForums mobile app
 
Habari zenu wanajamvi,

Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.

Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.

Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.

Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?


Kwanza ujue kwamba kila mtoto au watoto wanamalezi tofauti na tabia tofauti...kunawatoto niwapole mpaka mzazi anaogopa kunawatoto ni watundu mpaka kero kwa kila mgeni aingiaye katikannyumba hiyo..kunawatoto wanaiga mambo kwa watoto wengine..all in all ni mzazu mwenye akili tumamu tu ndio anajua anataka mtoto wake aweje...nakukumbusha mtoto yake ni fimbo...
Yaani mtoto lazima ajue kama nikifanya hivi nitachapwa au kunajambo linanikuta..ni fimbo tu ndio inamfanya mtoto awe na nidham..
 
Habari zenu wanajamvi,

Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.

Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.

Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.

Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?
Usimnyime mtoto bakora, Maandiko Matakatifu yameagiza hivyo.
Hata hivyo, inaonyesha KAMA binadamu tulio wengi huwa tuna roho mbaya kwa watoto, especially pale inapotokea kuwa siyo wa kuzaa sisi wenyewe. Kutokana na hali hii, inaonyesha kuwa mara nyingi binadamu unaweza ukamkuta anamchapa mtoto kwa prejudices zake tu na si kwa sababu za msingi, na pale inapotokea kuwa anazo sababu za msingi za kufanya hivyo, mapigo yake yanakuwa mazito mno na ambayo hayaendani kabisa na kosa husika la mtoto, na hapa ndiyo uharibifu unapotokea.

Ni fimbo iliyomwangukia mtoto kutokana na upendo tu na kwa uwiano sahihi kulingana na kosa alilofanya, ndiyo iliyo na matokeao chanya kwa mtoto husika, tofauti na hivyo fimbo kwa mtoto lazima iwe na madhara makubwa, tena sana tu!
 
Habari zenu wanajamvi,

Binafsi nimekuwa nikiwaona wazazi wengi wakiwachapa bakora watoto wao kama njia ya kuwatia nidhamu na nimekuwa nikisikitishwa sana na hii tabia kwani binafsi siamini kama bakora zinamjenga mtoto kinidhamu.

Badala ya kutumia bakora kumtia mtoto nidhamu jiulize kwanza je huyu mtoto anao uwezo wa kuwaza na kuwazua ikiwa anao basi mweleze kwa maneno ya kumjenga, usimpige bakora wala na kitu chochote.

Na kama hana uwezo wa kuwaza na kuwazua basi mwekee vizuizi vitakavyomfanya asiweze kuharibikiwa.

Je wewe una mtazamo gani juu ya bakora?
Usitufokee.

Kila mmoja ana namna yake ya kumrekebisha tabia mtoto wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom