Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 19,151
- 50,176
Poleni kwa hustling and bustling za mjini Dar.
Kuna hii "day trip" ya kwenda Bagamoyo unaweza kwenda na kujifunza vitu mbalimbali. Sio mbali sana, ni kilometa 70 kasoro kutokea Ubungo, na unaweza kwenda kwa usafiri wako (karibia masaa mawili kutokea Ubungo) au ukaenda kwa usafiri wa umma (magari ya kuunga ila jumla nauli haifiki elfu 5 hadi unafika).
Bagamoyo ni moja ya mji wa kihistoria uliopo Mkoa wa Pwani, ambako utajifunza mengi sana kuhusu utumwa, dini ya kikristo, ukoroni, maisha ya kale n.k
Wakazi wa Bagamoyo wanajishughulisha sana sana na biashara ya uvuvi na uuzaji wa samaki kutoka Bahari ya Hindi.
Wapo wachache wanajishughulisha na mambo ya utalii (mfano kutembeza wageni & arts), uvunaji wa chumvi (kwa evaporation), kilimo cha mazao na biashara ndogo ndogo.
1. Kanisa la Kale
Hapa utakutana na kanisa la kwanza kabisa Tanzania. Ambalo ndani yake utajifunza historia nyingi sana. Pia kuna jumba la makumbusho ya kale pembeni yake. Utajifunza mengi pia. Kiingilio kanisani ni Bure ila jumba la makumbusho ni Elfu 2. Hafu nje kuna vijana wa kukutembeza utampa tip ata elfu 5.
2. Soko la Samaki
Kuna soko kubwa la Samaki ambapo utakutana na wauzaji na wanunuzi mbalimbali. Kama unaweza kununua itakua poa tu.
3. Ngome ya Wajerumani
Ni sehemu ambayo Wajerumani waliitumia kama base yao ya kijeshi miaka ya 1880s. Hapa ukiwa na mwenyeji oana mbwembwe atatianutapenda.
4. Vyuo mbalimbali.
Kama unaweza utavisit vyuo kama SAUT (Marian University College), Chuo cha Sanaa, Branch ya MUHAS, Ifakara Health Institute, Kaole Agriculture Inst etc. Unaweza ulizia ata admission kwaajili ya mdogo/mwanao.
5. Fukwe
Kuna fukwe nzuri na kubwa ambapo pia utaona shughuli mbalimbali za uvuvi. Fukwe zao ni bure na hazina viingilio.
Kuhusu malazi, Bagamoyo ina lodge za bei ya kawaida lakini pale mji mkongwe kuna hotels za kitalii na cottage za kishua ambazo kulala inazidi ata laki 1 kwenda juu.
Ukitaka kuona mji vizuri, tumia usafiri wa baiskeli au pikipiki kwasababu utaona mengi zaidi na utafaidi.
Sehemu zingine unaweza visit:
1. Snake Park (Kuna aina mbalimbali ya nyoka, wanyama (zoo), michezo mbalimbali ya watoto na wakubwa. Ipo Kaole road, karibia Kilometa 5 kutokea mjini Bagamoyo.
2. Empire Sport Bar Kanywe bia.
3. Kaole Ruins kwa picha na more history.
4. Poa Poa Restaurant kale Pizza.
Picha nyingine:
Kuna hii "day trip" ya kwenda Bagamoyo unaweza kwenda na kujifunza vitu mbalimbali. Sio mbali sana, ni kilometa 70 kasoro kutokea Ubungo, na unaweza kwenda kwa usafiri wako (karibia masaa mawili kutokea Ubungo) au ukaenda kwa usafiri wa umma (magari ya kuunga ila jumla nauli haifiki elfu 5 hadi unafika).
Bagamoyo ni moja ya mji wa kihistoria uliopo Mkoa wa Pwani, ambako utajifunza mengi sana kuhusu utumwa, dini ya kikristo, ukoroni, maisha ya kale n.k
Wakazi wa Bagamoyo wanajishughulisha sana sana na biashara ya uvuvi na uuzaji wa samaki kutoka Bahari ya Hindi.
Wapo wachache wanajishughulisha na mambo ya utalii (mfano kutembeza wageni & arts), uvunaji wa chumvi (kwa evaporation), kilimo cha mazao na biashara ndogo ndogo.
1. Kanisa la Kale
Hapa utakutana na kanisa la kwanza kabisa Tanzania. Ambalo ndani yake utajifunza historia nyingi sana. Pia kuna jumba la makumbusho ya kale pembeni yake. Utajifunza mengi pia. Kiingilio kanisani ni Bure ila jumba la makumbusho ni Elfu 2. Hafu nje kuna vijana wa kukutembeza utampa tip ata elfu 5.
2. Soko la Samaki
Kuna soko kubwa la Samaki ambapo utakutana na wauzaji na wanunuzi mbalimbali. Kama unaweza kununua itakua poa tu.
3. Ngome ya Wajerumani
Ni sehemu ambayo Wajerumani waliitumia kama base yao ya kijeshi miaka ya 1880s. Hapa ukiwa na mwenyeji oana mbwembwe atatianutapenda.
4. Vyuo mbalimbali.
Kama unaweza utavisit vyuo kama SAUT (Marian University College), Chuo cha Sanaa, Branch ya MUHAS, Ifakara Health Institute, Kaole Agriculture Inst etc. Unaweza ulizia ata admission kwaajili ya mdogo/mwanao.
5. Fukwe
Kuna fukwe nzuri na kubwa ambapo pia utaona shughuli mbalimbali za uvuvi. Fukwe zao ni bure na hazina viingilio.
Kuhusu malazi, Bagamoyo ina lodge za bei ya kawaida lakini pale mji mkongwe kuna hotels za kitalii na cottage za kishua ambazo kulala inazidi ata laki 1 kwenda juu.
Ukitaka kuona mji vizuri, tumia usafiri wa baiskeli au pikipiki kwasababu utaona mengi zaidi na utafaidi.
Sehemu zingine unaweza visit:
1. Snake Park (Kuna aina mbalimbali ya nyoka, wanyama (zoo), michezo mbalimbali ya watoto na wakubwa. Ipo Kaole road, karibia Kilometa 5 kutokea mjini Bagamoyo.
2. Empire Sport Bar Kanywe bia.
3. Kaole Ruins kwa picha na more history.
4. Poa Poa Restaurant kale Pizza.
Picha nyingine: