Kula ya hao wanaoshusha nadhani ukiigawa unapata milo mitatu yako yani asubuhi mchana na jioni yeye ndio anapiga mlo m 1..wana pulling si ya kawaida Hapa niko pembeni ya hardware kubwa sana washusha cement ni Njemba 4 tu and in 1hr washapukutisha mzigo wa lori zima uko store..
Juu ya lori anapanda m1 wa kuwabebesha wenzake chini wanaokimbiza store watatu..mchaka mchaka wake mama ukiwaangalia unachoka wewe badala ya wao.
Watu wanao ingiza hela nyingi kwanza wengi hawana elimu,halafu wanapokaa pamoja wanajazana pumba kwa story zisizo na maendeleo so ni ngumu sana wao kuendelea,ukizungukwa na wajinga akili yako itakua hivyo hivyo.
Sio hao tu..kuna madereva boda boda,nao ni wanafanya kazi katika mazingira magumu ila Laki per day ni ya kugusa tu kwa mchapa kazi kweli ila maisha yao ndio mimi nachoka...
Japo sio wote maana nilishawahi enda nyumbani kwa boda boda mmoja Nilijihisi naona mazingaombwe sio kwa nyumba ile na vitu vle,nikiri tu wazi kipindi kile jamaa alinipiga gap kubwa sana.
.
Wanaume wafanya kazi Ngumu Akili zao wengi wameziacha kijijini kwao,,wamekuja mjini na Miili tu.