Baba vijacho na mama vijacho 2023 tukutane hapa

Baba vijacho na mama vijacho 2023 tukutane hapa

Kuna wadau watafanya jamaa aidha asuse na kuukimbia uzi ama lah furaha yake ikabatilishwa.

Wadau wameshikilia bango utungwaji mimba.

Wanaume wengi wana hili la kutojua mimba inatungwa wakati gani(mwanamke akiwa siku gani kwenye mzunguko wake).

Kuna dogo ni mwanachuo hakua hata anajua nini maana ya menstruation cycle, dem wake kumwambia yupo kweny siku zake dogo akaona ni kitu cha ajabu mno. Anabwabwaja asijue kina maana gani, kwa ubwabwajaji wa dogo alikua ilikua akicheza rafu kwa dem yeyote hawezi chomoa akibambikiwa kibendi.

Hivi vitu si vya wanawake pekee, tujifunze jama.
Hebu niacheni kidogo jana ndio nimeombwa lazima tukaanze clinic wote mana ndio anataka aanze hilo sio tatizo kabisaa mimi kwenda ila nikienda tatizo ni ....[emoji23][emoji23][emoji23]nadhani mshajua sasa kupokea majibu nahisi kuharisha hata nikutwe fresh nakuwa hoi bin taaban
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Asante mungu baba mwezi huu wa 5 tayri tumebahatika kupata mtoto wa kike.
Hakika ni mrembo haswa mama na mtoto wanaendelea vzr.Mungu tusaidie mrembo wetu awe na afya njema kwa miaka yote.
Hongera sna ndugu
 
Jamani tule vizuri watoto wakue vizuri
20230519_184939.jpg
 
Nakumbuka niliwahi kuwa katika chombo cha usafiri kuna mada kama hizi za uzazi zikawa zinazungumzwa kuna mtu wa makamo tu akaropoka mi sioni faida ya watoto.

Nikamwambia acha kutupunga wewe ungekuwa huna sahizi yawezekana ungekuwa unaloga tu huko upate akapanic sana raia wote wakamvaa ilikuwa kimya safari nzima.

Hongereni vijacho...
 
Dah it was so pain...13/6..walizaliwa wakiwa na miezi 6 na week 3..ndo maana ikawa ngumu kusurvive..wa kiume 1 kg akafariki kesho yake wa kike 900 gm ye kapigania maisha week nzima

Pole kwa changamoto kiongozi
 
Back
Top Bottom