Wong Fei
JF-Expert Member
- Apr 13, 2016
- 5,509
- 7,263
Pole sana. Ila sijakuelewa hapaWandugu nimekuja humu kuomba ushauri kwa hili swala linalonisumbua.
Ni muda sasa umepita tangu kuachana na mume wangu nililokuwa naishi nalo baada ya mzozo wa hapa na pale.
Wazazi wakatuita kusuluisha lakini baba mkwe akakomalia hataki kuona tukirudiana huku akitoa sababu ambazo hazina msingi wa maana, wazazi wangu kuona vile wakaamsha popo tukaondoka na mimi nikaelekea kwangu.
Sasa ni muda baba mkwe amekuwa akinilaghai anataka tuanzishe uhusiano na baadae ikiwezekana tuanze kuishi pamoja, mkewe alifariki katika ajali ya gari miaka 7 iliyopita.
Wanajamii hii kitu ndo kwanza naisikia kutoka kwa huyu Baba naona sio kawaida. Nikamshtaki kwenye ukoo au?
''Ni muda sasa umepita tangu kuachana na mum wangu nililokuwa naishi nalo baada ya mzozo w hapa na pale''.
Nisaidie ndugu maana kuachana kupo hata mm pia huwa nahuzunika sana nikisikia wanandoa wameachana. Najua mapenz yanauma lkn sijafurahishwa na haya maneno. Umeyaandika km una kisasi moyoni.
Sawa umeshaachana na huyo mume wako lkn ukithubutu kutembea na baba mkwe ni aibu sana, utadharaulika na kila mtu na kukuona ww haufai kuwa mke. Km unataka kuolewa tafuta mtu mwingine not your father in law
