Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,202
Reaction score
99,941
Baba, si ulisema tuna majirani wema sana? Na kwamba nyumba yetu ina utulivu, tena wewe na wanao yaani kaka zangu na dada zangu tunapendana sana? Mbona sasa huyu Jirani yetu baba Kagoma juzi alitufokea na tena akatufokea sana tu, huu ni ujirani gani?

Namkumbuka Mama nanihii juzi alivyotoka kuuza vitumbua vyake kule ughaibuni kaja akataka kutudhulumu dishi letu la maji na maji yake akidai dishi lote na maji yake ni vya kwake?

Huyu Babu yake Musa-Vani juzi niliwakuta kilabuni yeye, yule mtoto wa Kunyata na jirani mwingine wakikuteta tena wakisema wanataka waanzishe mto wao wenyewe, ati wasiwe na wanashirikiana na sisi, baba naona kama vile maadaui wanaongezeka kuliko marafiki.

Leo wakati natoka shule nikapitia kule kwa Mwalimu wa Kizungu, nikamkuta anaangalia Luninga huku taarifa lukuki zikitamalaki kuwa eti, kaka zangu na dada zangu nusura wadunfane leo walipokuwa kwenye darasa lao la tuisheni kule Arusha, Baba; nionavyo mimi maadui wanaongezeka kuliko marafiki.

Nilipokuwa pale chini ya mti wakati nasubiri kuchota maji nikajiliwa na wazo la kuwahesabu hawa waliokuwa marafiki, ndugu na jamaa zetu ambao baba wewe mwenyewe pamoja na akina babu mlidiriki kuwakaribisha hadi chumbani kule ambako hawakuruhusiwa kuingia, mmmhhh baba sikuamini kuwa haha pale Kaunga eti nao wana watoto wa baba yao mdogo anaitwa Mama wa 23 eti nao pia hawatutaki!!!

Baba, nakuomba sana aamka usingizini tutengeneze njia zetu, kama tutashindwa kabisa kupatana na majirani hawa basi heri tunoe mapanga yetu kungali na muda wa kufanya hivyo.

Waslaam Kitinda mimba wako, safarini Shinyanga
 
Majirani walipoambiwa shamba letu (ardhi) haliwahusu, ndio chuki hizi unazoziona zikaanza.
Walizidisha chuki siku yule mbuni mkubwa (air force one) alipotua uani kwetu. Wivu ukawazidi eti kwa nini hakutua kwao.
Tujijue na kujitegemea sasa, majirani wa karibu hatuna.
 
Baba, si ulisema tuna majirani wema sana? Na kwamba nyumba yetu ina utulivu, tena wewe na wanao yaani kaka zangu na dada zangu tunapendana sana? Mbona sasa huyu Jirani yetu baba Kagoma juzi alitufokea na tena akatufokea sana tu, huu ni ujirani gani?

Namkumbuka Mama nanihii juzi alivyotoka kuuza vitumbua vyake kule ughaibuni kaja akataka kutudhulumu dishi letu la maji na maji yake akidai dishi lote na maji yake ni vya kwake?

Huyu Babu yake Musa-Vani juzi niliwakuta kilabuni yeye, yule mtoto wa Kunyata na jirani mwingine wakikuteta tena wakisema wanataka waanzishe mto wao wenyewe, ati wasiwe na wanashirikiana na sisi, baba naona kama vile maadaui wanaongezeka kuliko marafiki.

Leo wakati natoka shule nikapitia kule kwa Mwalimu wa Kizungu, nikamkuta anaangalia Luninga huku taarifa lukuki zikitamalaki kuwa eti, kaka zangu na dada zangu nusura wadunfane leo walipokuwa kwenye darasa lao la tuisheni kule Arusha, Baba; nionavyo mimi maadui wanaongezeka kuliko marafiki.

Nilipokuwa pale chini ya mti wakati nasubiri kuchota maji nikajiliwa na wazo la kuwahesabu hawa waliokuwa marafiki, ndugu na jamaa zetu ambao baba wewe mwenyewe pamoja na akina babu mlidiriki kuwakaribisha hadi chumbani kule ambako hawakuruhusiwa kuingia, mmmhhh baba sikuamini kuwa haha pale Kaunga eti nao wana watoto wa baba yao mdogo anaitwa Mama wa 23 eti nao pia hawatutaki!!!

Baba, nakuomba sana aamka usingizini tutengeneze njia zetu, kama tutashindwa kabisa kupatana na majirani hawa basi heri tunoe mapanga yetu kungali na muda wa kufanya hivyo.

Waslaam Kitinda mimba wako, safarini Shinyanga

Waganga wa kienyeji wanatufitinisha na majirani zetu, tayari lamli zimepigwa na Baba yetu ameshikwa uchawi, pia Baba ye uaponzwa sana kihelehe kama cha dada zetu wanaopachikwa mimba wakingali mashuleni.
 
Waganga wa kienyeji wanatufitinisha na majirani zetu, tayari lamli zimepigwa na Baba yetu ameshikwa uchawi, pia Baba ye anaponzwa sana na kihelehe chake cha kuwa kama cha dada zetu wanao jipitishapitsha kwa viwembe na kujikuta wamepachikwa mimba wakingali mashuleni.
 
Waganga wa kienyeji wanatufitinisha na majirani zetu, tayari lamli zimepigwa na Baba yetu ameshikwa uchawi, pia Baba ye uaponzwa sana kihelehe kama cha dada zetu wanaopachikwa mimba wakingali mashuleni.

Baba mwingine huyu hapa wa ukoo wa akina mama wa 23,alipita ana kiu tukamkirimu kwa maji ya kunywa na hifadhi ajikinge na jua,tuka muona kama mwanafamilia mwenzetu.Lakini kumbe mjasiri aachi asili,baba juzi ulisema watu kama hawa warudi kwao mbona unawaacha wanaendelea kutuporomoshea matusi?Baba turuhusu hata sisi wanao tujichukulie hatua mkononi tuwageuze bucha maana uzuri DNA ya mama wa 23 ni kali sana haisumbui kuwajua wanaukoo wake waliojazana kwenye kaya yetu baba
 
Mimi nilihisi kuwa urafiki wenu utasambaratika baada ya kuwakaribisha wale watosi na wahitu kwenye kijiwe chenu.
 
hahahhahaaa baba yetu ni mchawi? Duh kweli inauma sana kuona wanawe tunatengwa, ukweli ni kwamba hatuna tena rafiki wala jirani
Ukiona hivyo ujue wamegundua baba yetu ni mchawi, huoni tuna mashamba, maji,maziwa na asali lakini wanae tumekondeana wanaonenepa ni watu wa ukoo mwingine..!?, Sisi anatulisha unga wa sembe tu..
 
sisi wenyewe kwa wenyewe tumeanza kugombana baba yuko kimya. tukianguka na kuumia baba haji kutujulia hali tunaambiwa tu kwamba eti alisafiri wala hataki kuaga... baba amegeuka ombaomba mpaka watoto wenzetu wanatucheka.....
 
Hahahahaa sio kweli kuwa baba na kiherehere pengine baba yetu ni mkarimu kupitiliza na mdomo kukosa breki lakini kwakua huyu ndie baba yetu hatuna budi kusimama upande wake, japo majirani wanamweka uchi, sie watoto tujitahidi kumfunika baba wengine wasiione aibu yake.......
Waganga wa kienyeji wanatufitinisha na majirani zetu, tayari lamli zimepigwa na Baba yetu ameshikwa uchawi, pia Baba ye uaponzwa sana kihelehe kama cha dada zetu wanaopachikwa mimba wakingali mashuleni.
 
Pamoja na hayo, lakini kiwe kweli ndio chanzo cha kutengwa na majirani? hapana, kuna lililojificha hapa, baba tuweke wazi wanao, tunaaibika, hasa hiki kilimo cha UNGA kilichoshamiri sasa ndio hofu yangu kubwa
baba asije kuwa alipola mke ndio tukazaliwa sie....
 
Twende kwa nani kusema pale baba anapotukosea heshima? baba anaposhindwa majukumu yake ya kifamili tukimbilie kwa nani sie? Amka usingizini baba
sisi wenyewe kwa wenyewe tumeanza kugombana baba yuko kimya. tukianguka na kuumia baba haji kutujulia hali tunaambiwa tu kwamba eti alisafiri wala hataki kuaga... baba amegeuka ombaomba mpaka watoto wenzetu wanatucheka.....
 
Baba familia yako tu umeshindwa kuitunza, ona tunavyo chukiana ndani ya hii nyumba, unashindwa hata kumzuia kaka kunichomea kibanda changu cha wana kondoo...?
Baba boma lako limechafuka Baba, hebu ona na bamdogo nae anavyo Pinda na kushadadia tupigwe wakati tukiwa kwenye arakati ya kutafuta uongozi bora wenye amani na maendeleo katika familia yetu...!
Baba hebu toa lile tabasamu nililolizoea na uweke ndita usoni kama marehemu Babu labda naweza kuhisi kweli uko serious na hii familia, maana nahisi kama unataka kututoa kafara!!!!!!!
 
Pamoja na hayo, lakini kiwe kweli ndio chanzo cha kutengwa na majirani? hapana, kuna lililojificha hapa, baba tuweke wazi wanao, tunaaibika, hasa hiki kilimo cha UNGA kilichoshamiri sasa ndio hofu yangu kubwa

yawezekana hiki kilimo chetu cha sasa wanchofanya rafiki zake baba anaokunywa nao kahawa...
 
Hahahahaaa Elli you are so creative! Big up! Hii lugha iliyotumika hata jirani hawezi kuistukia kw urahisi! Manake tunamueleza baba mapungufu yake bila kumuadhiri kwa majirani! Na hata wachangiaji wote wamezingatia.....
 
Back
Top Bottom