Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Hivi mara baada ya babu kufa, hakutuachia mrithi? nakumbuka marehemu babu alikua na wazee wenzie waliokuwa na maono kama yake, twaweza kwenda kuwaona hao?

baba kawa mkorofi kaota mapembe baada ya kumrithi babu hataki kusikia la mtu hata la marafiki wa babu amelewa ubaba hadi mila na desturi alizoachiwa na babu kazifungia kwenye kibuyu na kutupa baharini kila anachofanya kimekuwa adui kwa watoto na majirani
 
Baba, si ulisema tuna majirani wema sana? Na kwamba nyumba yetu ina utulivu, tena wewe na wanao yaani kaka zangu na dada zangu tunapendana sana? Mbona sasa huyu Jirani yetu baba Kagoma juzi alitufokea na tena akatufokea sana tu, huu ni ujirani gani?

Namkumbuka Mama nanihii juzi alivyotoka kuuza vitumbua vyake kule ughaibuni kaja akataka kutudhulumu dishi letu la maji na maji yake akidai dishi lote na maji yake ni vya kwake?

Huyu Babu yake Musa-Vani juzi niliwakuta kilabuni yeye, yule mtoto wa Kunyata na jirani mwingine wakikuteta tena wakisema wanataka waanzishe mto wao wenyewe, ati wasiwe na wanashirikiana na sisi, baba naona kama vile maadaui wanaongezeka kuliko marafiki.

Leo wakati natoka shule nikapitia kule kwa Mwalimu wa Kizungu, nikamkuta anaangalia Luninga huku taarifa lukuki zikitamalaki kuwa eti, kaka zangu na dada zangu nusura wadunfane leo walipokuwa kwenye darasa lao la tuisheni kule Arusha, Baba; nionavyo mimi maadui wanaongezeka kuliko marafiki.

Nilipokuwa pale chini ya mti wakati nasubiri kuchota maji nikajiliwa na wazo la kuwahesabu hawa waliokuwa marafiki, ndugu na jamaa zetu ambao baba wewe mwenyewe pamoja na akina babu mlidiriki kuwakaribisha hadi chumbani kule ambako hawakuruhusiwa kuingia, mmmhhh baba sikuamini kuwa haha pale Kaunga eti nao wana watoto wa baba yao mdogo anaitwa Mama wa 23 eti nao pia hawatutaki!!!

Baba, nakuomba sana aamka usingizini tutengeneze njia zetu, kama tutashindwa kabisa kupatana na majirani hawa basi heri tunoe mapanga yetu kungali na muda wa kufanya hivyo.

Waslaam Kitinda mimba wako, safarini Shinyanga
Na Babu naye aliwakaribisha Mjairani wote akawasomesha na wengine akawa vyumba vya uwaani waishi bila kupa kodi nab walipo jiweza akawapa uraia. aaa jamanii Babu alifika hadi kwenda kuwagomboa walipo 'Ganda !! mmmh leo hii eti wanatusengenya na kupwagaa sijui Baba umewakosaniii? alafu majirani wanatutangazia mabaya kwa wegeni.
 
baba kawa mkorofi kaota mapembe baada ya kumrithi babu hataki kusikia la mtu hata la marafiki wa babu amelewa ubaba hadi mila na desturi alizoachiwa na babu kazifungia kwenye kibuyu na kutupa baharini kila anachofanya kimekuwa adui kwa watoto na majirani
huyu huyu baba etu Mpendwa!!! Kama ni kweli basi kazi tunayo na safari bado ni ndefu maana tutamalizaje safari yetu pasipo kuwa na majirani???
 
Halafu baba jana majirani wamekutana kwenye ile klabu yenu ya ujirani, wewe hawajakuita eti wanaona umewageuka na huaminiki. Sisi wanao sasa tunaogopa hata kuwatembelea majirani, hasa wale wa kule kwa mzee kimbau mbau kwani hapa kwetu tumewafukuza
 
Halafu baba jana majirani wamekutana kwenye ile klabu yenu ya ujirani, wewe hawajakuita eti wanaona umewageuka na huaminiki. Sisi wanao sasa tunaogopa hata kuwatembelea majirani, hasa wale wa kule kwa mzee kimbau mbau kwani hapa kwetu tumewafukuza
hahahahaaa nilikua sijaiona hii mkuu, kwani baba ana amslahi gani na hawa watu?? nauliza tu
 
Back
Top Bottom