Napenda sana majirani wa aina hii

Chief Kumbyambya

JF-Expert Member
Jun 16, 2022
541
1,682
Aiseeeee habari za leo wazee.........

Huyu jirani yangu ana watoto wawili mmoja yuko darasa la tano mwingine yuko darasa la pili, ni mdada wa makamo shughuli yake kuu ni kupika vitafunwa asubuhi na kuzungusha Kwa wateja wake. Shughuli zake zingine sizijui na huwa sizifwatilii kabisa.

Hawa watoto wake ni wanagombanaga vibaya mnoo, kama mnavyojua watoto wa kiume wakifwatana wanakuwaga na mtiti ni balaa.

Sasa bwana huyu mkubwa huwa anamtandikaga sana huyu mdogo japokuwa haka kadogo kana hasira hatari ila ndiyo hivyo kwakuwa ni kadogo huwa kanapewa sana kichapo na kaka yake na marayingi nikiwakuta wanagombana huwa namkoa makwenzi huyu mkubwa maana anamdundaga sana sana huyu mdogo wake.

Juzi jumamosi asubuhi wakati mama yao kaenda kuzungusha vitafunwa huko madogo wakaanza kugombana tena wanagombana nje nikatoka kama kawaida nikamkoa makwenzi yule mkubwa akaanza kulia, ile analia mama yao akaja kuulizwa nini dogo akasema huyu anko kanipiga, nikamweleza mama yao kuwa huyu mkubwa anampigaga sana huyu mdogo hivyo nilikuwa namuonya watakuja kuumizana hawa.

Ebwana yule dada si akaanza kuniwashia moto.... Akasema usije kumpiga mtoto wangu hata mmoja na hata hata ukiwakuta wanauana waache usinipigie wanangu Babu weee... Tena komaa.

Duuu mbele za majirani nikakaa kimya ila wakamuonya kuwa kauli yake sio nzuri yeye akakomaa niàcheni watu tukasema poa.

Sasa jana wakati kaenda kuzungusha vitafunywa huko huku madogo wakaanza kukung'utana Mimi nipo zangu nje nafua nikawaacha kama siwaoni, mdogo kapigwa kalia weeee kaka mtu akajua ameshinda sasa kaka mtu akajisahau kumbe dogo kaenda ndani kabeba kisu kamvizia kaka yake kamdomeka kisu cha jicho tena kilizama kabisaa dogo akaanza kupiga makelele pale uso mzima umejaa damu tupu.

Majirani wengine hawakuwepo Mimi na jirani mmoja ni mdada alikuwa kalala ila Kwa Yale makelele ikabidi aamke kutoka tu anakutana na hicho kisanga anataka kwenda kumuhudumia yule dogo nikampga mkwara rudi ndanii.. unakumbuka mama yao juzi alisemaje? Demu akakumbuka akarudi ndani Mimi huyo naendelea kufua majinzi yangu pale huku naendelea kuburudika na kilio cha uchungu toka kwa yule dogo.

Mama yao anarudi anakuta dogo anagalagala chini damu uso mzima na kisu bado kimetulia palepale jichoni alafu mjuba nipo pale kimyaa naendelea kuanika nguo zangu... Yule dada akaanza kupiga makelele pale huku akilia ananilaumu eti Kwa nini watoto wanaumizana vile alafu nipo hata sishtuki na sijachukua hatua yoyote!!!

Kwa kauli aliyonitolea juzi kuhusu wanae nikasema hapa nikimjibu naweza nikatwa na hasira nikamtia ngumi buure, sikumjibu kitu,.. nikamkata jicho eeweeeeee.... Nikaaendelea kuanika nguo zangu akazidi kulia yule dada anashindwa kile kisu akitoeje pale jichoni, nikamkata tena jicho kali saaana nikamalizia kuanika nguo zangu nikaingia geto nikaoga nikatoka namkuta bado analia akiomba msaada nikamkata tena jicho la kibandidu mbaya mbovu nikaamsha zangu kuelekea mtaani.

Jana toka nilivyotoka geto pale sikurudi kabisa huwa sipendagi sana makelele ya kipuuzi puuzi. Nilienda zangu lodge nikaita manzi flani nikaagiza valeur kubwa na kitimoto kilo moja na nusu tukapiga tukafanya yetu muda huu ndo naamka ndiyo nikakumbuka kile kisanga cha Jana pale geto nikacheka saaana hahahahahaha.

Haya maisha hayahitaji mpuuzi mmoja akupigie makelele ya hovyo hovyo tu.
 
Chief naomba kwanza nikwambie wewe ni mpumbavu mmoja mkubwq sana!

Kwahiyo maneno ya mama yao kwa situation hiyo yana uzito gani,,,kweli unashindwa kuchanganua mambo nakuona ni msaada upi ulihitajika kwa huyo malaika wa mungu?

Halafu unaona fahari kuongea huo upuuzi kuwa ulienda sijui wapi na kupata kinywaji na dem wako!

Ovyo kabisa!
 
Una roho mbaya sana wewe jamaa,
Bila shaka huna mtoto,

Kwanza ulikosea toka mwanzo kua unampiga yule mtoto mkubwa,ungewaelimisha tu kua wapendane na wasipigane kwani wao ni ndugu,kama wasingekusikia ungemtaarifu Mama yao kuliko kuwapiga,

Hata kama Mama yao alikukataza kuingilia ugomvi wa watoto wake ila kitendo cha mmoja kumchoma kisu mwenzake ulitakiwa utoe msaada kwa huruma ya huyo mtoto na sio kwa kufuata maneno ya yule Mama,huyo mtoto ni mtoto wa taifa ndio maana hata kumuua mtoto wako ni kosa la jinai,hata kujiua ni kosa la jinai,

Umekosea sana,kama mtoto kaharibiwa jicho,sio tu hasara kwa huyo Mtoto na Mama yake bali ni hasara kwa taifa pia,kumbuka watoto ndio taifa la kesho,

Mungu akusaidie kukupunguzia hiyo roho mbaya na roho ya visasi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom